Baada ya Mwandishi Manyerere Jacton kueleza kinachoendelea Ngorongoro, sasa ndio naiamini Serikali, Wanahama kwa Hiyari

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi
Kunapotokea mgogoro wowote na kutokea sintofahamu yoyote inayowaweka wananchi kwenye njia panda, waamini lipi, kama kinachoendelea Ngorongoro, independent media ikiripoti hali halisi ya kinachoendelea, kitu hicho kinachoripotiwa huwa ndio ukweli halisi.

Asubuhi hii nilikuwa naangalia habari kwenye TV, tukapelekwa mubashara eneo la Ngorongoro na kushuhudia kwa macho yetu in real time kwa kuona hali halisi ya kinachoendelea Ngorongoro, licha ya kushuhudia wakazi wa Ngorongoro wakipanda kwenye mabasi tayari kuanza safari ya kuhama Ngorongoro kwa hiyari,
bado unakuwa huamini kama ni kweli wanahama kwa hiyari, nikimaanisha wanaweza kuwa wanahama kwa shinikizo fulani la kichinichini au enticement ya aina fulani, lakini baada ya kumuona mwandishi wa habari Legendari Manyerere Jacton ambaye ni an independent journalist, kama mimi nilivyo, tena huyu ni mwandishi mkongwe wa rika langu, tunaitana ma Comred, hivyo Leo baada ya kumuona Comred Manyerere Jacton ambaye pia ni member wetu humu jukwaani, akisema kinachoendelea Ngorongoro asubuhi hii, na kuona ni kuamini, sasa ndio naiamini serikali yangu kuwa wakazi wa Ngorongoro wanahama kwa hiyari, bila shinikizo lolote na bila ya vurugu zozote.

Manyerere akiwa Ngorongoro, ameeleza jinsi anavyoshudia wakazi wa familia 20 za mwanzo, huko Ngorongoro zinavyohamishwa kutoka Ngorongoro na kuhamishiwa Handeni mkoani Tanga.

Wananchi hao pia wamehojiwa na kuuthibisha uhiari wao na kueleza mategemeo yao. Manyerere ataandamana nao hadi mwisho wa safari yao

Kunapotokea sintofahamu yoyote kati ya serikali na jamii, ni vema sana kutumia an independent media na Kuwatumia independent journalists wanaaminika zaidi na jamii kuliko maofisa wa serikali.

Hivyo sasa nawaomba tuiaminie serikali yetu, wakazi wa Ngorongoro wanahama kwa hiyari hakuna kulazimishwa kokote wala shinikizo lolote.
Comred Manyerere Jackton , kwanza hongera sana kwa Mwandishi senior kuingia front na kuripoti live from eneo la tukio, wakati wengi wa ma senior wa levels zetu siku hizi, tunapenda kukaa desk na kutuma vijana. Ukipata muda, na huku jf, tupia tupia.

Paskali.
Update

Kuona ni kuamini, mkisikia maendeleo ya kweli, sasa ndio haya!.
P
 
Tusipende kusupport vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu kisa tunajipendekeza kupata vyeo kama I-dc, nk. Tuwe na huruma na utu jamani.
 
Tusipende kusupport vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu kisa tunajipendekeza kupata vyeo kama I-dc, nk. Tuwe na huruma na utu jamani.
hata wamaasai wanakiuka sheria kwa kung'ang'ania kuishi hifadhini kwani hilo eneo ni kwa ajili ya uhifadhi.ni lazima wananchi watii sheria vinginevyo hatua kali zichukuliwe zidi yao.muda wa kubembeleza haupo sababu waliishapewa nafasi na hawataki kuitumia.nn kinawalazimisha kukaa hifadhini wakati ardhi ni mali ya serikali na serikali inalitaka eneo lake kwa ajili ya uhifadhi.wapigwe tu. haki ni lazima ikaenda na wajibu.
 
Ngorongoro ule uchochezi wa watu wenye nia mbaya na nchi yetu ni moja ya vita ya kiuchumi dhidi ya jirani zetu ambao uchumi wao umejikita kwa wawekezaji ambapo huku kwetu tuna promote uwekezaji kwa kasi hivyo wanapata hofu fulani na kitu kingine hao wamasai wengi wao hao ng'ombe sio wakwao au wamechanganya na ng'ombe ambao wamiliki wengine wapo nchi jirani hata vijiji vya serengeti watu wa nchi jirani wanamiliki mifugo mingi sana kupitia ndugu zao kabila la wakurya ambao wapo huko na wilaya ya Serengeti na Tarime na kwa masai wapo huko na Ngorongoro,loliondo na maeneo mengineyo.Hiyo tunapofanya maamuzi kwa manufaa ya taifa letu halafu kikundi cha watu fulani kinataka kurudisha nyuma jitihada za serikali lazima watanzania tisimame na kukemea wenye interest binafsi badala ya kutanguliza utaifa kwanza.
 
Hata vijiji vya ujamaa ilikuwa sitaili kama hii, mwishoni, Kawawa(Rip) kaambiwa yeye ndiye alikosea jinsi ya kutekeleza. Sasa sijui akili yangu INAANZA kurudi nyuma au ni yako wewe!!!
 
Sasa Pascal Pascal Mayalla uhuru huu mliotumia kwenda kuwahoji wanaohama kwa hiyali kwanini pia msiutumie kwenda kuwahoji waliojerehuwa na Polise? Walionyimwa PF3 na wanakimbizana na Police? Au Uhuru wenu unataka kureport yale tu ambayo Serikali inapenda kuyasikia?
 
Paskali kama Paskali.
Tangu upate kura 1 mabandiko yako yamekuwa ya hovyo sana. Anyway hongera sana mkuu kwa kuutumia uhuru wako vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…