Baada ya Ole Nasha kufariki ni wakati wa Mkataba wa bandari ya Bagamoyo kuwa wazi

Baada ya Ole Nasha kufariki ni wakati wa Mkataba wa bandari ya Bagamoyo kuwa wazi

Wewe level ya uelewa wako ni duni mno

Unachoongea na kilichoulizwa ni vitu viwili tofauti kabisa, unatoa vijikashifa vya kipumbavu kama ulivyo wewe
Wewe una level gani ya uelewa? Unataka kila mtu akubali kila uongo na uzushi unaozushwa kila akifa mtu basi huyo mtu kauliwa ili kina fulani wafanye ufisadi,je waliokufa wakati wa yule Bedui nao tusemeje? Usinipangie cha kuandika humu.
 
Natoa wito kwa wafuasi wa lile BEDUI lilokufa muacheni Mama afanye kazi badala ya kumzushia uongo kila kukicha,BEDUI keshakufa na harudi tena.
 
Hakuna, kuna mapandikizi ya TISS huko upinzani ili nchi ionekane ya kidemokrasia tuendelee kula hela za mabeberu!! Ni kama Mama anavyowazuga na ishu ya Covid ili tuendelee kutafuna mpunga wao kiulaini!! Mabeberu ni wepesi sana ukiamua kuishi nao kijanjajanja
Hivi tukiombiwa tuonyeshe list ya vifo vya corona takwimu ipi?
 
Waziri Ole Nasha ndiye aliyekuwa waziri ambaye kapewa majukumu ya ufuatiliaji wa mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo wenye makadirio ya thamani $10B. Watanzania wengi ni lazima tujiulize huyu waziri kijana kuondoka katika mazingira haya akiwa katikati ya mkataba mkubwa hivi.

Kwa kutoa Watanzania wasiwasi na kuzingatia tajari tulisha ambiwa kuna madudu mengi sana kwenye huu mkataba. Lakini China nayo imekuwa ikisema kusuhu kuwa na base za kijeshi kwenye bandari zao ni lazima mkataba uwe wazi ili Watanzania wote tujue tunaingia kwenye mkataba wa namna gani. Wakina Samia na Kikwete hawatakuwepo pale China ikipewa bandari kwa miaka 99 na bandari kuwa kama balozi hivyo China kufanya wanalotaka.

Pamoja na mambo ambayo hatuyajui ni

1. Kuna umuhimu gani wa kuwa na bandari tatu karibu ya Tanga, Dar na hii ya Bagamoyo
2. Bandari ya Bagamoyo watarudisha vipi uwekezaji wa $10B bila kuchukuwa mizigo ya bandari ya Dar!. Je itawezekana vipi hizi bandari mbili kuongeza mizogo kwa zote!?. Na bandari ya Dar kuna mtu anafikiri watapata tena mizigo ya kutoka China?.
3 Tujue China ni kama inatawala shaba kule Zambia ndiyo mjenzi wa Tazara Je mizigo ya Zambia itaendelea kupitia bandari ya Dar au Bagamoyo?

Ukiangalia vizuri hii bandari ya bagamoyo ni mradi wa watu wachache. Hivyo viwanda wanavyosema watajenga sio viwanda ni magodauni ya kuweka mizigo huo ndiyo ukweli. Hakuna kiwanda eti kinasubiri bandari kwasababu Tanzania tuna bandari na maeneo ya ujenzi sasa hivi. Lakini kuna pesa ya mafuta na bomba linaenda Tanga ni kwanini tusikuzi pale ambapo tayari tuna uhakika wa soko kubwa na pesa? Tanga kuna umbali gani???! na hii ingefanya bandari zote bado ziwe chini ya TPA. Hii bandari ya Bagamoyo haitakuwa ya TPA tujue hilo.

Msishangae mtoto wa Kikwete kualikwa China eti kwenye mafunzo na kuacha wabunge wengine wenye uzoefu. Hii yote ni mradi wa bandari na hawa Kikwetes tuwe nao makini sana. Vilevile tusiwaamini wapinzani kwenye hili China wanauwezo wa kuhonga mpaka upinzani. Kitu kimoja tu tunaomba ni uwazi mkataba wekeni hapa na sio kutudanganya kwa mambo ya kazi. Vilevile Ole Nasha kufariki ni kitu cha kujiuliza sana maana tunasikia alianza kupinga mambo mengine.
Mkataba huo utupiliwe mbali kabisa. Tanzania mama yetu tuilinde
 
Jaribu kuruhusu kichwa chako kufanya kazi! Bandari ni mizigo, asilimia kubwa ya mizigo ni kutoka China, hivi bandari zingine zitatoa mizigo wapi? Ile ya Bagamoyo itakuwa ya China!
Kwamba bandari tulizo nazo zishajitosheleza kiufanisi na mkubwa?
Hakuna haja ya zingine

Open your mind.

Magufuli aliwaamimisha kitu kimoja ki baya sana
 
Ukiona hata kiongozi wetu mkuu naye Yuko huko basi ujue lipo tatizo kubwa Sana Tena Sana kwa nchi hii
Hakuna mkataba ambao uko wazi na hautakuja kutokea!!..Furahia sasa unaweza kutoa maoni ukiwa huru tofauti na miaka 5 iliyopita!!..Ungekua unafurahia tu kama Ndondocha!!
 
Mi napata wakati mgumu hasa nikijaribu kuchungulia ambao hawapo kwenye zile nafasi ambao walikataa ile proposal ya awali.

Kamati ya majadiliano ilikuwa chini ya Prof. Kabudi wakati wajumbe wakiwa

1. Engineer Mfugale
2. Dkt. Chamuriho
3. Engineer Kakoko
4. Dkt Kilangi (Alikuwa mwanasheria mkuu wa serikali)

Ao wote hawapo leo kwenye zile nafasi na ukiangalia iyo list unaweza kuona kwanini ule mradi ulikataliwa sasa sijui wanasiasa watokaokuwa kwenye kamatu ya sasa ya mazungumzo.

Walikataa Bandari ya Bagamoyo kuendelezwa na kukubali International Airport kujengwa CHATO!!!! Ni sawa hiyo?
 
Tuache ujinga wa kuwa na dhana mbaya na kubeza kila linalofanywa na utawala uliopo na kutaka kuaminisha watu tena kwa nguvu kwamba eti ni Magufuli tu ndiye aliyekuwa na nia njema na nchi hii na kwamba wengine wote ni wapigaji tu,huko ni kumkufuru na kumkosea mwenyezi Mungu kwani mwenyezi Mungu kama aliweza kumuumba huyo Magufuli atashindwaje kuumba wengine kama yeye?
Binafsi naamini utendaji kazi wa Rais Samia ni wa makini na ni wenye lengo la kuleta manufaa kwa taifa na wananchi wake kwa ujumla hivyo sikubaliani na upuuzi wowote unaeletwa na mtu yeyote kwa sababu ya chuki zake binafsi.
Najua hivi sasa kuna vita kubwa inayoendelea baina ya makundi fulani fulani kwa sababu ya utashi wao binafsi tu na wengine wamekuwa wakipinga utawala wa Rais Samia lakini huwezi kuwasikia wakizisema wazi sababu zao(halisi) bali wao wamebaki tu kujificha kwenye box la "uzalendo".
Watu hawa ndio wamekuwa vinara wa kuzua uongo kila kukicha ili tu watimize kile wanachokusudia,
Watu hawa ni sawa na chui waliojivika ngozi ya kondoo,
Watu hawa ukiwatizama usoni wanajionesha tofauti na walichokificha ndani ya mioyo yao.
Hawa watu ni wanafiki na ni wabinafsi na ni watu hatari sana.
Cheki jizi hili
 
Kwamba bandari tulizo nazo zishajitosheleza kiufanisi na mkubwa?
Hakuna haja ya zingine

Open your mind.

Magufuli aliwaamimisha kitu kimoja ki baya sana
Magufuli alijua Bongo viazi mviringo wapo wengi sana ndio maana hata alipodai kuokota vichwa vya treni bandarini bado walishangilia, Bongo raha sana.😂😂😂
 
Back
Top Bottom