Baada ya tukio la Japan, Vyombo vya dola vifanye mapitio ya kiusalama mikutano ya barabarani

Baada ya tukio la Japan, Vyombo vya dola vifanye mapitio ya kiusalama mikutano ya barabarani

Matukio yanapotokea kama ni mabaya ndio huwa tunajaribu kukosoa na hii ni kawaida ya binadamu kusema laiti ingekuwa hivi

Rais wetu aliefariki alikuwa na ulinzi wa hali ya juu ingawa mpaka leo hatujui ilikuwa inatumika shilling ngapi kumlinda kwa ule ulinzi lakini pamoja na helicopters juu na makomandoo mpaka wenye manati ili hata jolowe akikatishwa ashushwe kimya kimya bila kumbughudhi Rais

Ila aliondoka nae siku yake ilipofika
Kama siku ikifika hata wewe unaweza kufa kifala ila ni kifo tu haijalishi unalindwa Vipi

Japan wana sheria ngumu sana za bunduki na hiyo ilikuwa ni ya kutengeneza locally tu
Na hapo hata walinzi hawakutegemea kwa kuamini amani iliyopo na pia mda wake ulishafika na ikawa sababu
Kwahiyo wewe ungekua mfanya maamuzi ya mwisho,ungeamua ulinzi wa viongozi uondolewe kabisa,kwasababu siku ikifika,kifo hakizuiliki.. sindiyo?
 
Kwahiyo wewe ungekua mfanya maamuzi ya mwisho,ungeamua ulinzi wa viongozi uondolewe kabisa,kwasababu siku ikifika,kifo hakizuiliki.. sindiyo?

Umeelewa vibaya sana kama una mawazo hayo ya kunilisha
Ulinzi ni muhimu na sijasema uondolewe
Hata mimi Nina silaha ya kujihami ingawa najua ipo siku nitakufa
 
kuuwawa kwa kupigwa risasi Abe kwenye mkutano wa hadhara ni salam kwa viongozi wote duniani kuwa maamuzi na kauli zao za kibabe wanapokuwa madarakani hazimfurahishi kila raia na wapo raia wanaotamani kuwaua wakipata nafasi.

Hii ina maana hata Rais akimaliza muda wake bado hayuko salama kuna watu wanamuwinda wamuue kwa kuchukizwa na mambo aliyofanya akiwa madarakani. Kumuua si lazima kwa risasi hata kumuwekea sumu tu kwenye msosi!!

Swali ni je watu wangapi wana vinyongo na viongozi wetu wasiopenda nchi yetu kuagana na umaskini huku wao wakionekana kula bata za kiwango cha juu na kuwakaripia raia?

mfano wa kauli mbaya na hatari kwa raia maskini wenye hasira ya ukosefu wa ajira na mahitaji muhimu ni "kama hutaki mikopo au tozo hamia Burundi"!!, "watu wenye akili za kawaida", "hiyo mbona ni pesa ya mboga tu"

Kiongozi mtenda mema kwa watu wake huwa hakuna raia wa kumuwinda mf Magu alicheza ngoma na raia wake waliompenda.
 
Back
Top Bottom