Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

..ukweli ni kwamba tulianzisha viwanda lakini tuliviendesha vibaya na kilichotuponza ni siasa za Ccm kuingilia utendaji.

..pia wapo viongozi ambao walimshauri Mwalimu Nyerere atafute wabia, na wawekezaji, ktk viwanda na mashiriki, lakini ushauri huo ulipingwa, na walioutoa waliitwa WASALITI wa Ujamaa.

..Kosa letu lilikuwa kuchelewa kubinafsisha tukajikuta tunafanya hivyo wakati viwanda vimekufa.

NB:

..Ubinafsishaji wa Tanzania Breweries ulipingwa sana. Watu walikasirika kwasababu aliyeuziwa ni KABURU.

..lakini wakati Breweries inabinafsishwa bia zilikuwa haba. Quality ya bia ilikuwa mbaya, wakati mwingine bia zilikuwa na uchafu. Kampuni ilikuwa imekwama ktk ujenzi wa kiwanda cha Mbeya.

..Tanzania Breweries ni moja ya makampuni ambayo yalibinafsishwa at the right time, to the right investor.
Ubinafsishaji wa Tanzania Breweries kwa kiasi kikubwa nawezakusem umefanikiwa.

Je, kuna ubinafsishaji mwingine wa viwanda uliofanikiwa kama wa TBL ?

Tuna mkwamo wa kitaifa aisee usikatae
 
Hivi ni baadhi tu ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere bahati Mbaya vingi ni magodauni na magofu vijana inawezekana mmesahau

1. TANGANYIKA PACKERS - usindikaji,upakiaji na usambazaji wa nyama ya ng'ombe. Kiwanda hiki kilikuwa Kawe na kingine mkoani Shinganya.
2. URAFIKI,Nguo 3.MWATEX, Nguo
4. KILTEX,Nguo
5. MUTEX, Nguo
6. POLYTEX- Nguo, vitenge
7. MOROGORO CANVAS - MAGUNIA, MATURUBAI
8. MOROGORO SHOES- VIATU
9. MOROGORO TANNERIES- NGOZI.
10. MWANZA TANNERIES- NGOZI.
11. BORA SHOES- UTENGENEZAJI WA VIATU.
12. KIBO MATCH FACTORY- Viberiti.
13. NATIONAL, MATSUSHITA, PHILLIPS- Utengenezaji wa batteries, radio na radio cassete.
14. PAMBA ENGINEERING- Uchongaji wa vipuri vya mashine za uchambuaji pamba.
15. SIDO - Shirika la kuhudumia viwanda vidogo
16. Kiwanda cha kubangua Korosho Mtwara
17.Viwanda vya kusindika na kubangua , Kahawa, Alizeti, Pareto, Karanga na Miwa. Morogogo/Kilimanjaro/Singida
18. Kiwanda cha vipuri vya mashine cha Mang'ula
19. Kiwanda cha vipuri za mashine cha Kilimanjaro
20. Kiwanda cha malori (kuunda mabasi na malori) cha Scania.
21. Kiwanda cha magari cha Nyumbu cha jeshi Kibaha.
22. TANALEC- kiwanda cha kutengeneza vifaa mbalimbali vya umeme.
23. Kiwanda cha karatasi cha Mgororo Mufindi mkoani Iringa.
24. Kiwanda cha kusindika na kusambaza maziwa cha UTEGI mkoani Mara.
25. Kiwanda cha usindikaji wa nafaka cha National Milling Corporation cha Dar-es-Salaam.
26. Tanga Steel Rolling Mill- vyuma, saruji na mabati.
27. Viwanda vya saruji vya Tembo Cement, Twiga Cement, Simba Cement pamoja na vile vya ALAF na GALCO.
28. Kiwanda cha zana za kilimo - UFI
29. Kiwanda cha madawa ya binadamu cha KPC - Keko Pharmaceutical Company.
30. Viwanda vya Bia vya Dar, Ndovu na Pilsner Arusha
31. Kiwanda cha Mvinyo Dodoma
32. Kiwanda cha matairi cha General Tyre kilichopo Arusha
33. Kiwanda cha katani cha Amboni mkoani Tanga.
34. TIPER - kiwanda cha kusafisha mafuta machafu, kusambaza mafuta ya dizeli, petrol na mafuta ya taa.j
Zote hizi ni White elephant , Misallocotion of resources
 
Ubinafsishaji wa Tanzania Breweries kwa kiasi kikubwa nawezakusem umefanikiwa.

Je, kuna ubinafsishaji mwingine wa viwanda uliofanikiwa kama wa TBL ?

Tuna mkwamo wa kitaifa aisee usikatae

..TBL walifanikiwa kwasababu hawakusubiri mpaka kiwanda kife.

..Wangekibinafsisha wakati kimekufa na kwa muwekezaji asiye na uwezo kiwanda kisingeweza kushindana na waagizaji toka nje.
 
..TBL walifanikiwa kwasababu hawakusubiri mpaka kiwanda kife.

..Wangekibinafsisha wakati kimekufa na kwa muwekezaji asiye na uwezo kiwanda kisingeweza kushindana na waagizaji toka nje.
TBL tayari ilikuwa mahututi iCU..
Enzi hizo ukitaka kreti 10 unatoa Kwanza rushwa halafu unasubiri wiki, then unapata kreti pungufu!!

Kilichosaidia pale ni kuibinafsisha Kwa mwekezaji mwenye uwezo mkubwa wa mtaji na uzoefu, SABMiller ya Afrika Kusini
 
Laana ya Viwanda vya Nyerere haitataucha huru mpaka ipatikane Katiba mpya na wahusika wote kuchukuliwa hatua stahiki kisheria na ku-reclaim vile viwanda hasa ambavyo havikufufuliwa vinatakiwa virudishwe tuanze upya. Hatuwezi kukubali kukaa kama Taifa mfu lisilokuwa na sheria wala taratibu lisilokuwa na mikakati ya maendeleo yenye vipindi maalum vya kujipima mafanikio yake.
 
Viwanda vya kukoboa na/ au kusaga nafaka (Nationa Milling) vilikuwepo angalau kimoja kila mkoa
Vilisaidia nini? watu walikuwa wanapanga foleni kununua unga na wengine kula unga wa yanga , monopoly ya National milling ndio iliua ushindani na kufanya watu kutegemea serikali kila kitu
 
Laana ya Viwanda vya Nyerere haitataucha huru mpaka ipatikane Katiba mpya na wahusika wote kuchukuliwa hatua stahiki kisheria na ku-reclaim vile viwanda hasa ambavyo havikufufuliwa vinatakiwa virudishwe tuanze upya. Hatuwezi kukubali kukaa kama Taifa mfu lisilokuwa na sheria wala taratibu lisilokuwa na mikakati ya maendeleo yenye vipindi maalum vya kujipima mafanikio yake.
Mawazo ya kijima haya, haturudi na hatutaki monopoly za serikali kumiliki viwanda mpaka vya viberiti na kumuona mfanyabiashara ni muhujumu uchumi
 
Ubinafsishaji wa Tanzania Breweries kwa kiasi kikubwa nawezakusem umefanikiwa.

Je, kuna ubinafsishaji mwingine wa viwanda uliofanikiwa kama wa TBL ?

Tuna mkwamo wa kitaifa aisee usikatae
Kila kitu kilifanikiwa, ilipunguza zigo la kutoa billions kama ruzuku kwa viwanda vibovu visivyo na faida yeyote, ilikuwa kama serikali ina flush pesa chooni kila mwaka
 
Kila kitu kilifanikiwa, ilipunguza zigo la kutoa billions kama ruzuku kwa viwanda vibovu visivyo na faida yeyote, ilikuwa kama serikali ina flush pesa chooni kila mwaka
Baada ya kuuzwa pesa zikawa zinaflashiwa matumboni !! Waliokuwa wanatakiwa kuuzwa ni wale walioshindwa kuviendesha viwanda sio kuviuza viwanda !! Je na nyumba za serikali zilizouzwa nazo zilikuwa ni mzigo kwa Serikali ??!!
 
Hapo ndipo kuna makosa makubwa kimtazamo wa sababu ya kuviuza, haikuwa eti ni kumnufaisha mnunuzi tu. Ni ili mnunuzi ahakikishe anavirekebisha viweze kuanza kuzalisha kwa manufaa ya Taifa, haswa kiteknologia. Sasa unapouza kiwanda cha serikali halafu hakuna kipengele kama hicho cha kuhakikisha kinabakia kuwa na manufaa kwa Taifa, then huo ni ubadhirifu wa mali ya umma.
Kitu kingine cha kuzingatia ni kwamba serikali yake ilitakiwa ijenge vipya vilivyo bora zaidi ndipo waviuze hivyo vilivyoundwa na Mwalimu, ili aonyeshe umahiri wake. Kama baba yako amejenga nyumba kwenye kiwanja cha familia ukaona si nzuri kipindi cha utu uzima wako, unatakiwa ujenge ya kwako iliyo bora zaidi na siyo kuibomoa aliyojenga Baba yako.
Leo hii ukiuliza fedha iliyopatikana kwa kuuza hivyo viwanda vyoote zimelinufaisha je Taifa kiuchumi haielezeki hata kidogo. Nina wasiwasi Mwalimu Nyerere alipata msongo wa mawazo kutokana na maamuzi haya ambao huenda ndiyo uliosababisha kifo chake. Hotuba ya Mwalimu Nyerere wakati wa kumteua inatosha kuthibisha hilo, it is beyond any reasonable doubt kwamba hili lilisababisha maumivu kwa Baba wa Taifa.
Ilikuwa ni muhimu maamuzi haya kujadiliwa kwa kina hata na Bunge. Vyuo vikuu tulikuwa navyo vilitakiwa vishirikishwe kufanya research ya nini kifanyike, vyuo kama UDSM, DIT, Arusha Tech, Sokoine University, Mzumbe, Chuo Cha Biashara DSM nk. walitakiwa wataalamu wapitie mkakati huo na kutoa ushauri. Unapokuwa kiongozi usiependa kushauriwa na unaishia kufanya maamuzi ya kubomoa uchumi wa nchi kiasi hicho, basi uwe tayari kushitakiwa kwa kosa la ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.
Kuna mtu amesema eti Baraza la Mawaziri halihusiki moja kwa moja kutokana na mfumo wetu. Kwanini basi hakuna hata mmoja wao aliyejiuzulu ili kujitoa kwenye huo ubadhirifu? Ina maana maadili ya uongozi hakuna.
Kitendo hicho kililirudisha Taifa miaka 40 nyuma kiuchumi.
Ni kweli Mwalimu aliumizwa sana na kuuzwa kiholela kwa viwanda vile na akawaambia mtabinafsisha hadi magereza na bado mambo yatakuwa magumu tu !! Kweli kiongozi yule na mawaziri wake walitakiwa washitakiwe kwa yale waliyoyafanya !!
 
Vingi alijiuzia mwenyewe na kugawana na ndugu na marafiki kule Kiwira makaa ya mawe ndio walikomba live wakanunua jumla bei ya kutupa ,yeye na Mramba,na mwanae bila aibu
 
Vilikufa kidogo kidogo kipindi cha Mwinyi, halafu Mkapa ndo akaja akavipiga nyundo vyote vilivyokuwa vinapumua bado katika awamu yake.
Baada ya vita vya Uganda,World Bank na IMF.walitaka Tanzania ifanye reform za uchumi.
Raisi Nyerere akakataa masharti hayo yaliosababisha Waziri wa Fedha Edwin Mtei na mshauri wa uchumi Professor Rweyemamu kujizulu.
Baada ya Mwalimu kugeuka mbogo na Raisi Reagan wa Marekani akageuka kiboko.IMF na World Bank wakasitisha mikopo au hata misaada na wakazionya taasisi nyingine za fedha za nchi za magharibi kutoisaidia Tanzania .
Katazo hilo tokea IMF,World Bank lilisabisha uchumi wetu kuyumba sana,kukosekana kwa pesa za kigeni.Viwanda vyetu vikashindwa kuagiza vipuri toka nje na kusababisha viwanda vyetu vizalishe chini kabisa ya kiwango.
Lakini nchi za Danmark,Norway,Sweden na Finland zikazidisha misaada mingi ya maendeleo lakini bado haikutosha kukwamua uchumi wetu.
 
Vilisaidia nini? watu walikuwa wanapanga foleni kununua unga na wengine kula unga wa yanga , monopoly ya National milling ndio iliua ushindani na kufanya watu kutegemea serikali kila kitu
Kibaya kilikuwa nini nini? Idea au utekelezaji? Wazo la viwanda haliwezi kuwa baya hata siku moja. Tatizo tunapenda muno hujuma; kuhujumu Serikali halafu tunaanza tena kuilalamikia. Kama havikusaidia kitu basi ujue kulikuwa na hujuma; wazo la kiwanda haliwezi kuwa baya au kushindwa kuzaa matunda hata siku moja, haiwezekani

Kwa upande wako unaonaje katika hili? Bora aliyekuja kuviuza, si ndiyo? Vipi baada ya kuuzwa vimesaidia zaidi kuzidi kabla ya kuuzwa kwake?
 
..TBL walifanikiwa kwasababu hawakusubiri mpaka kiwanda kife.

..Wangekibinafsisha wakati kimekufa na kwa muwekezaji asiye na uwezo kiwanda kisingeweza kushindana na waagizaji toka nje.
Vingine kama MWATEX na MUTEX vilikuwa vinafanya kazi ila vimebinafsishwa zaidi ya miaka ishirini lakini hamna kitu mpaka sasa
 
Mawazo ya kijima haya, haturudi na hatutaki monopoly za serikali kumiliki viwanda mpaka vya viberiti na kumuona mfanyabiashara ni muhujumu uchumi
Tunachohitaji ni waliovichukua wahakikishe vinazalisha na kuchochea maendeleo ya Teknologia nchini badala ya kuvitumia kama warehouse za kufichia bidhaa haramu. Nadhani sasa utakuwa umeelewa vizuri.
 
Back
Top Bottom