Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

Baadhi ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambavyo ni magodauni na magofu

Hiyo haikuwa sababu toshelezi kuamua kuvitupa shimoni. Ni bora wangetafuta ushauri wa aliyevijenga kwanza pamoja na kupata ushauri wa waliofadhili ujenzi wake kuliko walichokifanya.

..Mwalimu Nyerere alikuwa anajadiliana na IMF, World Bank, na Paris Club [ nchi wakopeshaji wakubwa.]

..Mzee Mwinyi alipoingia aliendeleza mazungumzo na nchi na taasisi hizo kuhusu namna ya kutukopesha na kusamehe baadhi ya madeni.

..Majadiliano hayo ndiyo yaliyopendekeza zoezi la Ubinafsishaji. Baada ya hapo sheria ilijadiliwa BUNGENI na kupitishwa.

..Ubinafsishaji ulifanyika baada ya mashauriano, mazungumzo, na mijadala mipana na mikali wakati mwingine.
 
..Mwalimu Nyerere alikuwa anajadiliana na IMF, World Bank, na Paris Club [ nchi wakopeshaji wakubwa.]

..Mzee Mwinyi alipoingia aliendeleza mazungumzo na nchi na taasisi hizo kuhusu namna ya kutukopesha na kusamehe baadhi ya madeni.

..Majadiliano hayo ndiyo yaliyopendekeza zoezi la Ubinafsishaji. Baada ya hapo sheria ilijadiliwa BUNGENI na kupitishwa.

..Ubinafsishaji ulifanyika baada ya mashauriano, mazungumzo, na mijadala mipana na mikali wakati mwingine.
Sasa kwanini walishindwa kusimamia hilo zoezi liwe na Tija kwa Taifa? Badala yake wakalitumia kujinufaisha wao pamoja na familia zao? Inasaidiaje Taifa kuja kukiri baadaye kwamba hukulisimamia vyema hilo zoezi wakati ilikuwa ni wajibu kama Mkuu wa nchi? Na kwanini ukubali kuuwa vyoote kwa pamoja kipindi kimoja.Why not plan such a dangerous and unpredictable move in phases? Ili kujiridhisha baada ya kuchunguza katikati ya utekeleza kwamba uamuzi unafaa kuendelea au la? There is no excuses brother! That was a deadly mistake.
 
Hivi ni baadhi tu ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere bahati Mbaya vingi ni magodauni na magofu vijana inawezekana mmesahau

1. TANGANYIKA PACKERS - usindikaji,upakiaji na usambazaji wa nyama ya ng'ombe. Kiwanda hiki kilikuwa Kawe na kingine mkoani Shinganya.
2. URAFIKI,Nguo 3.MWATEX, Nguo
4. KILTEX,Nguo
5. MUTEX, Nguo
6. POLYTEX- Nguo, vitenge
7. MOROGORO CANVAS - MAGUNIA, MATURUBAI
8. MOROGORO SHOES- VIATU
9. MOROGORO TANNERIES- NGOZI.
10. MWANZA TANNERIES- NGOZI.
11. BORA SHOES- UTENGENEZAJI WA VIATU.
12. KIBO MATCH FACTORY- Viberiti.
13. NATIONAL, MATSUSHITA, PHILLIPS- Utengenezaji wa batteries, radio na radio cassete.
14. PAMBA ENGINEERING- Uchongaji wa vipuri vya mashine za uchambuaji pamba.
15. SIDO - Shirika la kuhudumia viwanda vidogo
16. Kiwanda cha kubangua Korosho Mtwara
17.Viwanda vya kusindika na kubangua , Kahawa, Alizeti, Pareto, Karanga na Miwa. Morogogo/Kilimanjaro/Singida
18. Kiwanda cha vipuri vya mashine cha Mang'ula
19. Kiwanda cha vipuri za mashine cha Kilimanjaro
20. Kiwanda cha malori (kuunda mabasi na malori) cha Scania.
21. Kiwanda cha magari cha Nyumbu cha jeshi Kibaha.
22. TANALEC- kiwanda cha kutengeneza vifaa mbalimbali vya umeme.
23. Kiwanda cha karatasi cha Mgororo Mufindi mkoani Iringa.
24. Kiwanda cha kusindika na kusambaza maziwa cha UTEGI mkoani Mara.
25. Kiwanda cha usindikaji wa nafaka cha National Milling Corporation cha Dar-es-Salaam.
26. Tanga Steel Rolling Mill- vyuma, saruji na mabati.
27. Viwanda vya saruji vya Tembo Cement, Twiga Cement, Simba Cement pamoja na vile vya ALAF na GALCO.
28. Kiwanda cha zana za kilimo - UFI
29. Kiwanda cha madawa ya binadamu cha KPC - Keko Pharmaceutical Company.
30. Viwanda vya Bia vya Dar, Ndovu na Pilsner Arusha
31. Kiwanda cha Mvinyo Dodoma
32. Kiwanda cha matairi cha General Tyre kilichopo Arusha
33. Kiwanda cha katani cha Amboni mkoani Tanga.
34. TIPER - kiwanda cha kusafisha mafuta machafu, kusambaza mafuta ya dizeli, petrol na mafuta ya taa.j
Jiwe yeye alijenga kiwanda kipi ati!?

Au kiwanda Cha Hawa mazuzu wanamtukana Samia na January kila kukicha!?

Mzee alikuwa msanii yule!
 
Sasa kwanini walishindwa kusimamia hilo zoezi liwe na Tija kwa Taifa? Badala yake wakalitumia kujinufaisha wao pamoja na familia zao? Inasaidiaje Taifa kuja kukiri baadaye kwamba hukulisimamia vyema hilo zoezi wakati ilikuwa ni wajibu kama Mkuu wa nchi? Na kwanini ukubali kuuwa vyoote kwa pamoja kipindi kimoja.Why not plan such a dangerous and unpredictable move in phases? Ili kujiridhisha baada ya kuchunguza katikati ya utekeleza kwamba uamuzi unafaa kuendelea au la? There is no excuses brother! That was a deadly mistake.

..kwanza sio kweli kwamba ubinafsishaji haukuwa na tija.

..pili sio kweli kwamba ubinafsishaji uliua viwanda.

..tatu zoezi lilifanyika kwa muda mrefu na kulikuwa na muda wa kutafakari, kushauriana, na kupima matokeo.

..kwa maoni yangu, ubinafshaji ulichelewa kufanyika, matokeo yake tukawa tunabinafsisha viwanda vilivyokufa.

..Zipo taarifa kwamba wataalamu toka SWEDEN waliishauri serikali ya awamu ya kwanza kuendesha viwanda kwa ubia ili kuviokoa lakini wazo hilo lilikataliwa.
 
Sahvi kuvirudisha shuguli maana
Wale importers wanaleta zengwe
Wanataka nchi iendele kuimport tu..

Ova
Nyie matahira simnasema mungu wenu alijenga viwanda elfu tatu na Mia kenda!!? Vipo wapi hili tuvione au kuviona mpka tuwe na jicho la kiroho
 
Mkuu Mkapa ndie alieuza NBC ikiwa ndio benki kubwa ya biashara.
Aliuza bank na majengo yake nchi nzima kwa bei ya kutupa,
Fedha kidogo iliyopatikana ndio iliyoanzisha NMB
Baba wa taifa alipinga sana lakini hakuwa na sauti tena, Mkapa allimweka mwenyewe, kibaya zaidi akawauzia makaburu ambao aliwapiga vita muda mrefu
NBC nakumbuka kama iliuzwa kwa billion 15 tu, na majengo yake yote.
 
Abood alikichukua kimoja hapo morogoro kwa ajili ya katani, baada ya muda kakigeuza kuwa godown la katani kutoka nje. Kuna siku nitamueleza mama samia hili, Magufuli aliwahi kumwambia huu ukweli abood. Natamani mama Samia nae amwambie ukweli huu. Mwingine aliyefanya ujinga huu ni Mo
Wapo wengi sana
Umesahau na kiwanda Cha MOPROCO
 
... Mkapa ndiye aliyekuja kuvigeuza magodown kwa kilichoitwa ubinafsishaji.
Yeye mwenyewe alikuwa analalamika kuwa wawekezaji wa ndani wanavililia halafu wakipewa wanavigeuza magodown. Wakinyang'anywa na vikapewa wawekezaji wa nje wanalalamika kuwa kwanini serikali haina uzalendo.
 
Hivi ni baadhi tu ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere bahati Mbaya vingi ni magodauni na magofu vijana inawezekana mmesahau

1. TANGANYIKA PACKERS - usindikaji,upakiaji na usambazaji wa nyama ya ng'ombe. Kiwanda hiki kilikuwa Kawe na kingine mkoani Shinganya.
2. URAFIKI,Nguo 3.MWATEX, Nguo
4. KILTEX,Nguo
5. MUTEX, Nguo
6. POLYTEX- Nguo, vitenge
7. MOROGORO CANVAS - MAGUNIA, MATURUBAI
8. MOROGORO SHOES- VIATU
9. MOROGORO TANNERIES- NGOZI.
10. MWANZA TANNERIES- NGOZI.
11. BORA SHOES- UTENGENEZAJI WA VIATU.
12. KIBO MATCH FACTORY- Viberiti.
13. NATIONAL, MATSUSHITA, PHILLIPS- Utengenezaji wa batteries, radio na radio cassete.
14. PAMBA ENGINEERING- Uchongaji wa vipuri vya mashine za uchambuaji pamba.
15. SIDO - Shirika la kuhudumia viwanda vidogo
16. Kiwanda cha kubangua Korosho Mtwara
17.Viwanda vya kusindika na kubangua , Kahawa, Alizeti, Pareto, Karanga na Miwa. Morogogo/Kilimanjaro/Singida
18. Kiwanda cha vipuri vya mashine cha Mang'ula
19. Kiwanda cha vipuri za mashine cha Kilimanjaro
20. Kiwanda cha malori (kuunda mabasi na malori) cha Scania.
21. Kiwanda cha magari cha Nyumbu cha jeshi Kibaha.
22. TANALEC- kiwanda cha kutengeneza vifaa mbalimbali vya umeme.
23. Kiwanda cha karatasi cha Mgororo Mufindi mkoani Iringa.
24. Kiwanda cha kusindika na kusambaza maziwa cha UTEGI mkoani Mara.
25. Kiwanda cha usindikaji wa nafaka cha National Milling Corporation cha Dar-es-Salaam.
26. Tanga Steel Rolling Mill- vyuma, saruji na mabati.
27. Viwanda vya saruji vya Tembo Cement, Twiga Cement, Simba Cement pamoja na vile vya ALAF na GALCO.
28. Kiwanda cha zana za kilimo - UFI
29. Kiwanda cha madawa ya binadamu cha KPC - Keko Pharmaceutical Company.
30. Viwanda vya Bia vya Dar, Ndovu na Pilsner Arusha
31. Kiwanda cha Mvinyo Dodoma
32. Kiwanda cha matairi cha General Tyre kilichopo Arusha
33. Kiwanda cha katani cha Amboni mkoani Tanga.
34. TIPER - kiwanda cha kusafisha mafuta machafu, kusambaza mafuta ya dizeli, petrol na mafuta ya taa.j
Mkapa aliviua vingi kwa kuviuza ovyoovyo na vingine kuwagawia wahuni.
Nakumbuka nyerere alishauri wabinafsishe viwanda vyenye kufanya vibaya tu ili vipate uwekezaji na ujuzi kutoka nje. Mabwanyenye na adui wa ujamaa wakataka vile vinavyofanya vizuri ndio wauziwe. Mkapa kwa ulevi tu akageuza nchi kuuza viwanda vyake vyote. Mabeberu wakanunua na kuvigeuza magodauni ya kuweka bidhaa kutoka viwanda vyao ng'ambo.
Hakika ilikua makosa makubwa yasiyo kifani kuhusu jitihada ya kujenga viwanda. Nakumbuka enzi hizo vijana wengi wakifanya kazi viwandani.
 
35. Zana za Kilimo Mbeya (ZZK) sijaiona hapo
36. Tancut Almasi - Iringa (Kiwanda cha kukata almasi)
37. National Milling Corporation (NMC) - kiwanda cha kusaga na kusindika nafaka
38. Kiwanda cha maziwa pale Ubungo Maziwa

Kuna vingine vingi tu ambavyo sisi ambao hatukuwepo enzi hizo tuliokuta masalia masalia tumeshavisahau.

Mwalimu kwa ujumla alianzisha mashirika takribani 600 (ila sio mashirika yote yalikuwa ni viwanda).
Kiwanda Cha nyavu nafkiri kinapakana na UFI.
DarBrews -Chibuku au siyo Cha Nyerere kile?
 
Kabla haujambebesha lawama Mh. Mkapa ni vyema ukaangalia sababu ambazo zilimfanya Mkapa kufikia hatua hiyo.

Iko hivi. Viwanda vingi havikuwa vinajiendesha kwa faida. Serikali ilikuwa ina vipa ruzuku ili viendelee kuwepo. Kuna sababu mbalimbali ambazo zilisababisha haya.
1. Management Mbovu. Wabongo tunajijua. Pamoja na kwamba Nyerere alijitahidi kusomesha watu na kuwapa nafasi..wengi walimuangusha.

2. Technolojia iliyopitwa na wakati. Baadhi ya viwanda alikuwa anapewa msaada...vilikuwa vimeshapitwa na wakati. Kumbe wale jamaa walikuwa wanatafuta sehemu ya kuvitupa. Wao wana move kwenye tech mpya ile ya zamani ndo wanawa wapa au kuwauzia. Hivyo ilikuwa gharama kubwa kuviendesha na havikuwa na ubora kama vya ulaya. Hivyo kufanya kutokuwa na ushindani katika soko. Maana una produce low quality at high cost.

So kipindi cha Mwinyi vingi ya hivyo viwanda vilifungwa. Hali ilikuwa mbaya sana. Watu walikaa nyumbani huku wakiendelea kulipwa mishahara.

Mkapa alipokea nchi ikiwa namna hiyo. Yaani una watu wako nyumbani wanalipwa mishahara. Una viwanda ambavyo havifanyi kazi na technolojia yake imepitwa na wakati.

Je utafanya nini.?

Mkapa aliamua kuvibinafsisha. Kwa sababu ni dhahiri serikali haiwezi kuendesha miradi ya kibiashara. Angali tu kwa mfano Mabasi ya Mwendo kasi, Angalia Tanesco etc..zote zinaendeshwa kwa ruzuku.

Sasa kwa nini uchukue gela ya walipa kodi uvipe viwanda visivyoingiza faida.?

Hivyo Mkapa akaamua kuvibinafsisisha. Ili private investors waendeshe na watoe ajira. Akawapunguza wafanyakazi kwa kuwalipa haki zao ili wasiendelee kula mishahara bila kazi.

Kuna tuhuma kwamba Mkapa aliuza viwanda kwa bei rahisi bei ya kutupa. Ukweli ni kwamba ingawa vilikuwa vinaitwa viwanda...havikuwa viwanda kiuhalisia. Mitambo yake mingi ilikuwa ya kizamani na haifanyi kazi. Hivyo Mkapa aliuza vyuma chakavu na majengo.

Baadhi ya walionunua walifanya vizuri..Viwanda kama TBL vinafanya vizuri hadi sasa. Ila baadhi ya walio nunua walivigeuza ma godown na wao ukiwauliza kwa nini hawakuviendeleza wana sababu zao.
Unasema kwamba General Tyre haikuwa na ubora?
Au Khanga ya urafiki haikuwa na ubora?
Aiseee....
 
Mkapa aliviua vingi kwa kuviuza ovyoovyo na vingine kuwagawia wahuni.
Nakumbuka nyerere alishauri wabinafsishe viwanda vyenye kufanya vibaya tu ili vipate uwekezaji na ujuzi kutoka nje. Mabwanyenye na adui wa ujamaa wakataka vile vinavyofanya vizuri ndio wauziwe. Mkapa kwa ulevi tu akageuza nchi kuuza viwanda vyake vyote. Mabeberu wakanunua na kuvigeuza magodauni ya kuweka bidhaa kutoka viwanda vyao ng'ambo.
Hakika ilikua makosa makubwa yasiyo kifani kuhusu jitihada ya kujenga viwanda. Nakumbuka enzi hizo vijana wengi wakifanya kazi viwandani.

..tujiulize ni viwanda vingapi vilikuwa vinafanya vizuri?

..kiwanda gani kilikuwa kinaendeshwa kwa faida na kinatoa gawio serikalini?

..pia tujiulize viwanda vingapi vilikuwa vinafanya vibaya na vimekuwa mzigo kwa serikali.

..mwisho, tujiulize kwa ujumla viwanda vilikuwa vinaendeshwa kwa faida? Vilikuwa vinatoa gawio serikalini? Au vilikuwa mzigo na vikitegemea ruzuku toka serikalini.
 
..tujiulize ni viwanda vingapi vilikuwa vinafanya vizuri?

..kiwanda gani kilikuwa kinaendeshwa kwa faida na kinatoa gawio serikalini?

..pia tujiulize viwanda vingapi vilikuwa vinafanya vibaya na vimekuwa mzigo kwa serikali.

..mwisho, tujiulize kwa ujumla viwanda vilikuwa vinaendeshwa kwa faida? Vilikuwa vinatoa gawio serikalini? Au vilikuwa mzigo na vikitegemea ruzuku toka serikalini.
Kuuliza kiwanda/viwanda gani vilikuwa vinatoa gawio au vinafanya vizuri haitoshi kusaidia km uamuzi wa kuviuza ulikuwa sahihi au la, nadhani walikosa hekima kujaribu kuona mbali hatua kwa hatua kuvipatia majibu changamoto zilizokuwa kiini cha kutofanya vizuri, vingi vilikuwa na matatizo ya mtaji, ujuzi na teknolojia..kwa rasilimali tulizo nazo, hasa madini..kupata majibu ya hayo matatu si vigumu kabisa.
Kwa kifupi waliamua vibaya, tena walikuwa na haraka na kosa lile lile ambalo hadi leo bado wanalirudia rudia kulifanya..mentality ya kudhani ndani ya serikali kuna majibu ya changamoto yoyote na hivyo kutohitaji majibu nje ya serikali..tabia hii haifai ni ya kukumbatia umaskini.
 
Kuuliza kiwanda/viwanda gani vilikuwa vinatoa gawio au vinafanya vizuri haitoshi kusaidia km uamuzi wa kuviuza ulikuwa sahihi au la, nadhani walikosa hekima kujaribu kuona mbali hatua kwa hatua kuvipatia majibu changamoto zilizokuwa kiini cha kutofanya vizuri, vingi vilikuwa na matatizo ya mtaji, ujuzi na teknolojia..kwa rasilimali tulizo nazo, hasa madini..kupata majibu ya hayo matatu si vigumu kabisa.
Kwa kifupi waliamua vibaya, tena walikuwa na haraka na kosa lile lile ambalo hadi leo bado wanalirudia rudia kulifanya..mentality ya kudhani ndani ya serikali kuna majibu ya changamoto yoyote na hivyo kutohitaji majibu nje ya serikali..tabia hii haifai ni ya kukumbatia umaskini.

..ubinafsishaji maana yake ni kufikabidhi viwanda kwa private sector huwezi kusema huko ni kutafuta majawabu serikalini.

..vijana hamjui nchi ilikuwa na hali gani kiuchumi, na matatizo ya fedha serikalini yalikuwa makubwa kiasi gani.

..Kwa kifupi nchi ilikuwa imekwama wakati Mwalimu Nyerere anang'atuka. Kulikuwa hakuna mahali tunaweza kupata fedha za kufufua hivyo viwanda. Nchi ilikuwa haikupesheki.

..Kujinusuru na nchi kuwa kama Zimbabwe au Sri Lanka tulilazimika kukubali masharti na maelekezo ya IMF, WB, na wakopeshaji wa Paris Club.


..Kwa hiyo ubinafsishaji ulitokana na sisi wenyewe kushindwa kuendesha uchumi wetu vibaya, hali iliyopelekea uzalishaji viwandani kuporomoka.

..Uamuzi wa kuviuza ulikuwa ni sahihi kwasababu tulikuwa hatuna uwezo wa kifedha kufufua viwanda vyetu.
 
..tujiulize ni viwanda vingapi vilikuwa vinafanya vizuri?

..kiwanda gani kilikuwa kinaendeshwa kwa faida na kinatoa gawio serikalini?

..pia tujiulize viwanda vingapi vilikuwa vinafanya vibaya na vimekuwa mzigo kwa serikali.

..mwisho, tujiulize kwa ujumla viwanda vilikuwa vinaendeshwa kwa faida? Vilikuwa vinatoa gawio serikalini? Au vilikuwa mzigo na vikitegemea ruzuku toka serikalini.
Hiyo siyo sababu ya uamauzi na utekelezaji hafifu namna ile bila kujali Taifa. Nikuulize swali, TANESCO ilikuwa inaliingizia nini Taifa? Kwanini hiyo hawakudhubutu basi kuibinafsisha?
 
Hivi ni baadhi tu ya Viwanda vya kimkakati alivyoanzisha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere bahati Mbaya vingi ni magodauni na magofu vijana inawezekana mmesahau

1. TANGANYIKA PACKERS - usindikaji,upakiaji na usambazaji wa nyama ya ng'ombe. Kiwanda hiki kilikuwa Kawe na kingine mkoani Shinganya.
2. URAFIKI,Nguo 3.MWATEX, Nguo
4. KILTEX,Nguo
5. MUTEX, Nguo
6. POLYTEX- Nguo, vitenge
7. MOROGORO CANVAS - MAGUNIA, MATURUBAI
8. MOROGORO SHOES- VIATU
9. MOROGORO TANNERIES- NGOZI.
10. MWANZA TANNERIES- NGOZI.
11. BORA SHOES- UTENGENEZAJI WA VIATU.
12. KIBO MATCH FACTORY- Viberiti.
13. NATIONAL, MATSUSHITA, PHILLIPS- Utengenezaji wa batteries, radio na radio cassete.
14. PAMBA ENGINEERING- Uchongaji wa vipuri vya mashine za uchambuaji pamba.
15. SIDO - Shirika la kuhudumia viwanda vidogo
16. Kiwanda cha kubangua Korosho Mtwara
17.Viwanda vya kusindika na kubangua , Kahawa, Alizeti, Pareto, Karanga na Miwa. Morogogo/Kilimanjaro/Singida
18. Kiwanda cha vipuri vya mashine cha Mang'ula
19. Kiwanda cha vipuri za mashine cha Kilimanjaro
20. Kiwanda cha malori (kuunda mabasi na malori) cha Scania.
21. Kiwanda cha magari cha Nyumbu cha jeshi Kibaha.
22. TANALEC- kiwanda cha kutengeneza vifaa mbalimbali vya umeme.
23. Kiwanda cha karatasi cha Mgororo Mufindi mkoani Iringa.
24. Kiwanda cha kusindika na kusambaza maziwa cha UTEGI mkoani Mara.
25. Kiwanda cha usindikaji wa nafaka cha National Milling Corporation cha Dar-es-Salaam.
26. Tanga Steel Rolling Mill- vyuma, saruji na mabati.
27. Viwanda vya saruji vya Tembo Cement, Twiga Cement, Simba Cement pamoja na vile vya ALAF na GALCO.
28. Kiwanda cha zana za kilimo - UFI
29. Kiwanda cha madawa ya binadamu cha KPC - Keko Pharmaceutical Company.
30. Viwanda vya Bia vya Dar, Ndovu na Pilsner Arusha
31. Kiwanda cha Mvinyo Dodoma
32. Kiwanda cha matairi cha General Tyre kilichopo Arusha
33. Kiwanda cha katani cha Amboni mkoani Tanga.
34. TIPER - kiwanda cha kusafisha mafuta machafu, kusambaza mafuta ya dizeli, petrol na mafuta ya taa.j
kwa vyovyote vile vitapaswa kurudishwa
 
Back
Top Bottom