Baadhi ya watu wanajiuliza kwanini ''bwana yule'' hapati tena siri za Ikulu?

Baadhi ya watu wanajiuliza kwanini ''bwana yule'' hapati tena siri za Ikulu?

Kazi ya kigogo ni kufichua maovu na sio kufichua Siri.Maovu yasipokuwepo na kigogo hana dili tena.
 
Nimeona sehemu nyingi baadhi ya watu wakijadili kuhusu ''bwana yule'' huku wengine wakimbeza lakini wengine wakiuliza kimetokea nini kwa sasa ''bwana yule'' hapati tena siri za Ikulu...
Remember Mwanakijiji na kainzi!~!!!!
 
mama anatype mwwnyewe taarifa zake hampi secretary.inakuwa ngumu kuvuja.na akitangaza ni hapo kwa papo zege hailali
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Hebu usitoke nje ya mada, baki kwenye mada jadili hoja iliyoko mezani, ukisema huyo "bwana yule" haonekani kuwa na mrengo wa huyu wa sasa useme how, binafsi siamini kwanini siri zilizokuwa zinatoka wakati wa awamu ya tano ghafla zisitoke awamu ya sita, kwa move ipi aliyofanya huyu aliyepo madarakani kuzuia wakati anashindwa hata kwenye teuzi tu, anateua sasahivi badae anatengua.
Mkuu, yaani wewe huwa nakuelewaga Sana, najua kuwa wewe ni mpinzani na moyo wako unapenda mageuzi, cha ajabu ni Kwamba, unapenda zaidi kujadili hoja na sio ushabiki,

Sjui unakunywaga Ka soda kweli???

Embu agiza hapo then nitalipia
 
Hivi "muhishimiwa" Balozi Dr Bashiru ameanza kuchangia hoja kule bungeni? Sijamsikia.
 
Napenda niwasaidie kwa kuwaambia kuwa hakuna siri za Ikulu zilizozibitiwa ila wale waliokuwa wanatoa siri za Ikulu na kuzipeleka kwa ''bwana yule'' kwa sasa ndio hawa ambao wako madarakani. Kwa maana nyingine, kwa sasa ndio walioshika Ikulu/utawala moja kwa moja. Yaani sio tena watoa ushauri bali kwa sasa ni wabunifu na wasimamia utekelezaji.
kwahio kumbe ni internal job??
 
Sio kwamba utawala wa Samia umefanikiwa kuzuia siri za serikali zisimfikie Kigogo, issue ni kwamba wale waliokuwa wanavujisha hizo siri awamu iliyopita ndio marafiki wa Samia...
Kwa namna moja ama nyingine, lengo la kigogo Kwa mtizamo wake na wa Baadhi ya wengine, pengine ulikuwa ni zuri Sana,

Lakini lilikosa uzuri pale alipoonyesha kufurahi kwake na kuwa wa Kwanza kufahamu kuwa JPM hawezi kupona, hapo kulimuweka kwenye maswali mengi mno yasiyojibika vichwani mwa watu,

Angelikuwa super Man na mtu wa maana kama asingejiingiza kwenye kuugua na hata kufikia umauti wa aliyekuwa Raisi, na Kwa sababu hiyo, imekuwa ni vigumu Sana kuamini tu kuwa mwenda zake alifariki tu kawaida
 
Kwa namna moja ama nyingine, lengo la kigogo Kwa mtizamo wake na wa Baadhi ya wengine, pengine ulikuwa ni zuri Sana...
Labda yeye alikuwa muwazi tu katika kuonesha furaha yake. Lakini kwa yaliyotokea na yanayoendelea sasa, ni wazi kabisa watanzania wengi zaidi walifurahi (ukiacha mtoa mada hii, "mimi", mataga, na sukuma gang) na wengine labda walifurahi zaidi ya hata huyo 'chigogo'.
 
Imeunga unga andiko lako,it is simple logic utawala wowote ukibadilika the whole system inabadilika.haiwezekani tena kupata taarifa nyeti kwa muda huo mfupi.

Halafu jambo lingine Magufuli kwa muda aliokaa Ikulu tayari alikuwa na maadui ndani ya Serikali,Nje na ndani ya chama.Sasa Samia ndio kwanza ana miezi 3 hao maadaui amisha watengenezaje??
 
Nimeona sehemu nyingi baadhi ya watu wakijadili kuhusu ''bwana yule'' huku wengine wakimbeza lakini wengine wakiuliza kimetokea nini kwa sasa ''bwana yule'' hapati tena siri za Ikulu.

Kwa wasiojua vizuri wameenda mbali zaidi na kudai eti kwa sasa siri za Ikulu zimethibitiwa na uongozi mpya!

Napenda niwasaidie kwa kuwaambia kuwa hakuna siri za Ikulu zilizozibitiwa ila wale waliokuwa wanatoa siri za Ikulu na kuzipeleka kwa ''bwana yule'' kwa sasa ndio hawa ambao wako madarakani. Kwa maana nyingine, kwa sasa ndio walioshika Ikulu/utawala moja kwa moja. Yaani sio tena watoa ushauri bali kwa sasa ni wabunifu na wasimamia utekelezaji.

Biashara yao na ''bwana yule'' ya kumpa siri za Ikulu iliisha siku ambayo Rais Samia aliapishwa kuwa Rais wa Tanzania!

Haishangazi kuona kwa sasa ''bwana yule'' anawashambulia sana baadhi ya wale waliokuwa wanampa siri za Ikulu baada ya kugundua hawataki tena mahusiano naye. Yaani kwa sasa wamemalizana naye!

Nasikia kwa sasa wale wale waliokuwa wanampatia siri za Ikulu wana mpango wa ''kumnyamazisha'' ili huko mbeleni asije akatumia umaarufu waliomuwezesha wao wenyewe kuichafua serikali yao. Kibaya zaidi, wanamjua vizuri kwa maana kuwa, wanazijua nguvu zake na udhaifu wake(strengh and weakness) kwa sababu ndio walimuwezesha kupata umaarufu kwenye mitandao ya kijamii. Hata kupata kitambulisho cha ''blue tick'' ilikuwa ni jitihada za baadhi ya wale waliokuwa wanampatia siri za Ikulu.

Baada ya kukosa ushirikiano kwa sasa ''bwana yule'' anafanya jitihada za kuwa karibu na wenyeCHADEMA ili apate uungwaji mkono kwenye mitandao! Kwa wanaofahamu historia ya ''bwana yule'' watajua kuwa huko nyuma hakuwahi kuipenda/kuishabikia CHADEMA hasa hakumpenda Mwenyekiti Mbowe na aliwahi kumshambulia sana akidai mwizi wa pesa za chama.

Huko mwanzo, ''bwana yule'' alikuwa ni mwanaCCM lakini baadaye akawa ''mwanaACT-Wazalendo'' kabla ya ujio wa Maalim Seif na kundi lake! Wakongwe wa siasa nchini wanajua kuwa ACT-Wazalendo ni ''stepping stone'' kwa wanaCCM! Kwa maana nyingine, ACT-Wazalendo ni kama fimbo ya kuchapiana wanaCCM kwa wanaCCM!

Hasira za ''kutoswa'' zinamfanya aanze ''revenge'' kwa waliomtosa kwa kutumia ''platform'' za CHADEMA. ''bwana yule'' anajua bila kupata sapoti ya wanaCHADEMA hawezi kuendelea kuwa ''relevency'' kisiasa katika dunia ya mitandao!

Hoja iliyopo kwa sasa ni kujua kama ''kinyago'' walichokichonga walioko madarakani kwa sasa kitawatisha au watakiangamiza kabla hakijaanza kuleta madhara!
Mkuu MsemajiUkweli, umefanya analysis moja matata sana, kuna wakati na mimi nilikuwa najiuliza hivi, "Bwana yule" na haya mapenzi na CHADEMA yameanza anzaje? Kuna nini ameshaona amekikosa?

Muda utatufahamisha vizuri.
 
Sijaelewa.
Kwani lengo la Kigogo2014 kilikua Ni kutoa Siri za Ikulu ama kufichua mwovu ya Mtawala dhalimu.

Kama utawala wa Sasa unatenda mema Atafichua wema?

Nakuambia Hivi watu kama Kigogo huja kama utawala huminya haki za wananchi.

Watu kama Kigogo hupewa sapoti na watu wa mifumo kukosoa na kufichua uovu wa watawala wanapigana uhuru wa kutoa maoni.

Kwa huyo Mama karuhusu kukosolewa,Kigogo Hana kazi tena.
Mama akinyima uhuru Kigogo au Vigo wengine wataibuka tena.

Suala la kumnyamazisha hakina mashiko kwa sababu watu waaliomuona nuksi hawapo madarakani tena,na siku zinavyokwenda wanazidi kupoteza nguvu.mwisho wataishia kbs.
Kigogo alikuwa anakosoa au alikuwa anachafua? kwa sababu hakuna utawala ambao upo perfect ndio maana hata marais wote waliyopita kabla ya Magufuli walikuwa wanafanya makosa na walikuwepo wa kuwakosoa, kwahiyo kama kutoa siri za serikali kama alivyokuwa anafanya Kigogo ndio kukosoa basi tutegemee siri za serikali kuendelea kutoka maana hata sasa makosa yapo.
 
Ok nilidhani una udugu nawe, unajua kwenye uhalisia wa maisha sio kila kitu kitamgusa kila mtu pamoja huo utu na ubinadamu.
Nalijua hilo. Lakini watu wasio na utu ni wa kuwaweka mbali sana.

Mtu bila utu, hakuna tofauti na chatu.
 
Back
Top Bottom