Baba achinjwa na familia yake akidaiwa kuwa kikwazo cha kutumia mali za familia

mda mwingine bora kumalizana hapahapa duniani,yaani bora kuvunja chungu haki mahakamani ngumu kupatikana
 
Mkuu kuna muda huwa una mawazo mazuri sana
 
Soma habari za mauaji hata humu JF uone mikoa inayoongoza ni Mara, Mwanza na Shinyanga. Lini ulisikia mtu Tanga kaua mzazi sijui mtoto wake
 

Wengi wenu mnamatatizo ya Akili na upeo mdogo wa kufikiri. Sema watu wanafiki watabisha au wataona haya/aibu kulisema Jambo Hilo.

Ninaushahidi wa kutosha juu ya Jambo Hilo. Sema sio site wapo wachache wanaojielewa.
Ola wengi wenu ni macherema.

Hasira za kijinga,
Kutokujiamini na ubabe usio na kichwa wala miguu.
Imani za kichawi na ushirikina ninyi ndio nambari moja.

Lazima mubadilike bhana.

Soma hapa👇🏽👇🏽
 
Hiyo sentensi ya mwisho imenichekesha sana
 
Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza linawashikilia watu watano akiwemo Mkazi wa Kijiji cha Kiliwi wilayani Kwimba, Hoka Mazuri (48) na wanaye wawili kwa tuhuma kumuua mumewe, Mange Washa (49)...

Daaah sisi wazazi tuombee sana hawa watoto wetu, hao walishidwa tu kuelewa uyo mzee wao alikuwa akiwatunzia wao hao hao watoto izo mali!! Ila watoto na mama wamekosa maarifa! R.I.P

Hawa wauza bange, gongo, mirungi wangeachana nao tuu maana life ni gumu na mkuu kasema tule kwa urefu wa kamba.... sasa kamba zao zinaruhusu kulq hapo[emoji1353]

Police, takukuru kama kweli mpo siriazi na hii inchi anzeni na zile behewa za SGR,
 
Kwakuwa ni Mwanza basi utalaumiwa umaskini ila ingetokea Kilimanjaro ambapo ni nadra mauaji kutokea hapa makelele yangekuwa mengi.

Ukweli ni kwamba Mwanza na Shinyanga ndipo wanaongoza kwa mauaji si wanawake si wanaume, hatua zakupambana na hiyo zichukuliwe either kielimu kwa jamii au kiroho.

Too much stereotype kwa Kilimanjaro hasa wanawake wakati hawana shida kama huko kanda ya ziwa
 
Mkiambiwa mkitaka kuoa mushirikishe wazazi mnajifanya wajanja mnataka pisi kali matokeo yake ndo hayo.
 
Khaaaaah
 
Watu watano akiwemo mama na watoto wake wawili wanaodaiwa kuhusika katika mauaji ya baba yao mzazi mkazi wa Kijiji cha Kiliwi wilayani Kwimba mkoani Mwanza, Mange Washa (49) wamepandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza na kusomewa shtaka la mauaji.

Waliopandishwa kizimbani leo Jumatano Disemba 14, 2022 katika mahakama ya Wilaya ya Kwimba ni Hoka Mazuri (48) ambaye ni mke wa marehemu pamoja na watoto wake wawili Masunga Mange na Paskali Mange. Wengine ni wanaume wawili wanaodaiwa kulipwa Sh800, 000 na wanafamilia hao kutekeleza mauaji hayo ni Shija Masalu (28) na Makoye Lusana (53) ambaye ni mshtakiwa namba moja katika kesi hiyo ya Jinai namba 12/2022.

Akisoma shtaka linalowakabili mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya hiyo, Ndeko Dastan, Mwendesha mashtaka wa Serikali, Robert Mwanakatwe amesema Disemba Mosi mwaka huu washtakiwa hao walimuua, Mange Washa kwa kumkata kichwa akiwa amelala nyumbani kwake kisha kutenganisha kichwa na kiwiliwili chake. "Washtakiwa wote mnashtakiwa kutenda kosa hilo la mauaji kinyume na kifungu namba 196 na 197 cha Kanuni ya Adhabu marekebisho ya mwaka 2022, mauaji ambayo mnadaiwa kuyatekeleza huko Kiliwi tarafa ya Bupamwa wilayani Kwimba," amesema. Baada ya kuwasomea shtaka hilo ameomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa kwa sababu upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Ndeko Dastan ameahirisha kesi hiyo hadi Disemba 28,2022 itakapoitwa kwa ajili ya kutajwa tena. "Washtakiwa mtaendelea kukaa rumande hadi hapo kesi itakapoitwa tena kwa ajili ya kutajwa, shtaka linalowakabili halina dhamana," amesema Hakimu Dastan
Washtakiwa hao wanadaiwa kupanga njama na kutekeleza mauaji ya mwanaume huyo waliyemtuhumu kuwanyima uhuru wa kutumia mali za nyumbani kwao, Disemba Mosi mwaka huu kabla ya kukamatwa Disemba 5, mwaka huu kwa hatua zaidi za kisheria.

Source: Gazeti la Mwananchi la Disemba 14, 2022.
 
Hii inazidi kutujuza kuwa kina mama ni wabinafsi tofauti na jamii inavyoamini na kuwatwisha wanaume lawama kila kukicha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…