Walipofika wakataka kushusha maiti na kuondoka, ndipo alipowagomea na kuanza vurugu baadae maiti ikaenda kuhifadhiwa hospitali ya Polisi Kilwa Road.
Baba mzazi ana mashaka na kifo cha mwanae, anasema mwanae ameuawa kwa kuwa mwanae alisimamia ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake kufanya mauaji ya mfanyabiashara.
Baba mzazi anamuomba IGP Sirro kuunda tume kuchunguza kifo hiko. Anasema haiwezekani sero ya polisi kuwe na tambala!
Baba mzazi wa marehemu ni askari mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.
=====
"Nilipewa taarifa kuwa mwanao ameshikiliwa kwenye mahabusu ya Polisi, na Januari 22, 2022 nilipigiwa simu kuwa bahati mbaya mwanao amejinyonga, jambo ambalo lilinistua sana" Gaitan Mahembe, baba mzazi wa askari anayedaiwa kujinyonga Greyson Mahembe
"Polisi walifanya mambo haraka, wakaleta mwili hadi kwangu Segerea haraka walipofika wakawa wanasema shusha hapa, tukakataa nusura tupigane, tukawaambia mwili huu ukahifadhiwe kisha tuje hapa tuzungumze" Gaitan Mahembe, baba mzazi wa Greyson Mahembe, askari anayedaiwa kujinyonga
"Tuliwaambia askari waliouleta mwili, safari yetu ni ya Iringa lakini hatuwezi kuupokea hadi mtueleze, mwanangu ni afisa wa jeshi alitakiwa asindikizwe kijeshi na azikwe kijeshi kwanini halikufanyika hilo"Gaitan Mahembe, baba mzazi wa Greyson Mahembe, askari anayedaiwa kujinyonga
"Kama mwanangu alijinyonga wangeitwa ndugu upande wetu wakathibitishe au tungeoneshwa picha hata za kutoka jeshi la polisi zikionesha amejinyonga, au picha zozote kwenye vyombo vya habari. Hakuna hilo" Gaitan Mahembe, baba mzazi wa Greyson Mahembe, askari anayedaiwa kujinyonga
"Ndugu yetu aliitwa wakati marehemu alishapelekwa hospitali ya Ligula na akaoneshwa michubuko akielezwa ni ya kamba, kisha akaambiwa ni ya tambara la deki, hivi mahabusu ya jeshi kuna tambara la deki?" Gaitan Mahembe, baba mzazi wa Greyson Mahembe, askari anayedaiwa kujinyonga
"Mimi na familia yangu hatujaridhishwa, tunamuomba IGP alifafanue hili na ukweli uwekwe wazi. Hatuna kipato, hivyo tunaomba tupate mwanasheria wa kujitolea au wa serikali akatusaidia katika hili tutashukuru"Gaitan Mahembe,baba mzazi wa Greyson Mahembe,askari anayedaiwa kujinyonga
"Hakuna picha inayoonesha marehemu alijinyonga au ananing'inia, ukweli wake ndio uliomponza, marehemu alisema kwanini nihangaishwe wakati mimi nilitumwa? wakubwa wenyewe wapo, mimi nilikuwa ni mtekelezaji"Gaitan Mahembe, baba mzazi wa Greyson Mahembe, askari anayedaiwa kujinyonga
Polisi wengine ni shida sana. Subiri upate tatizo ndio utawajua vizuri polisi. Yaani sishangai kusikia haya yanayoendelea. Kuna wengine wana roho mbaya sana
Huyo kauliwa na mapolisi ili wamsingizie kesi, uhuni umerudi tena serikalini mama anaangaika na mambo ya kipumbaavu ya machifu na kuvaa ngozi, wakati nchini mambo yanaharibika.[emoji848]
Huyo kauliwa na mapolisi ili wamsingizie kesi ,uhuni umerudi tena serikalini mama ana angaika na mambo ya kipumbaavu vya machifu na kuvaa ngozi ,wakati nchini mambo yanaharibika
Baba mzazi ana mashaka na kifo cha mwanae, anasema mwanae ameuwawa kwa kuwa mwanae alisimamia ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake kufanya mauaji ya mfanyabiashara.
Baba mzazi anamuomba IGP Sirro kuunda tume kuchunguza kifo hiko. Anasema haiwezekani sero ya polisi kuwe na tambala
ASKARI ALIYESHTAKIWA KWA MAUAJI AJINYONGA MAHABUSU KWA TAMBALA LA KUDEKIA
ASP Greyson Mahembe ambaye ni Mrakibu Msaidizi wa Polisi anayedaiwa kujinyonga kwa tambala la kudekia akiwa mahabusu ya kituo cha Polisi Wilaya ya Mtwara, Mkoani Mtwara.
Greyson alikuwa miongoni mwa Maafisa wengine wa Polisi saba wanaotuhumiwa kuumua kijana Mussa Hamisi (25) ambaye ameuawa baada ya kudai fedha zake shilingi Milioni 33.7 ambazo Maafisa hao wanadaiwa kuzichukua kutoka kwa kijana huyo baada ya kumfanyia upekuzi, uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.