Baba mzazi wa Askari Polisi anayedaiwa kujinyonga Mtwara adai kutoridhishwa na taarifa ya mwanae kujiua

Baba mzazi wa Askari Polisi anayedaiwa kujinyonga Mtwara adai kutoridhishwa na taarifa ya mwanae kujiua

Akiongea na Azam News, Baba mzazi wa askari aliyejinyonga anasema hajaridhishwa na taarifa za kifo cha mwanae!

Anasema alipigiwa simu na kuambiwa mwanao tumpeleke akazikwe wapi? Akawaambia mleteni nyumbani kwangu Tabata, Dar Ea Salaam.

Walipofika wakataka kushusha maiti na kuondoka, ndipo alipowagomea na kuanza vurugu baadae maiti ikaenda kuhifadhiwa hospitali ya polisi kilwa road.

Baba mzazi ana mashaka na kifo cha mwanae, anasema mwanae ameuwawa kwa kuwa mwanae alisimamia ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake kufanya mauaji ya mfanyabiashara.

Baba mzazi anamuomba IGP Sirro kuunda tume kuchunguza kifo hiko. Anasema haiwezekani sero ya polisi kuwe na tambala!

Baba mzazi wa marehemu ni askari mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.
Duh.
 
Akiongea na Azam News, Baba mzazi wa askari aliyejinyonga anasema hajaridhishwa na taarifa za kifo cha mwanae!

Anasema alipigiwa simu na kuambiwa mwanao tumpeleke akazikwe wapi? Akawaambia mleteni nyumbani kwangu Tabata, Dar Ea Salaam.

Walipofika wakataka kushusha maiti na kuondoka, ndipo alipowagomea na kuanza vurugu baadae maiti ikaenda kuhifadhiwa hospitali ya polisi kilwa road.

Baba mzazi ana mashaka na kifo cha mwanae, anasema mwanae ameuwawa kwa kuwa mwanae alisimamia ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake kufanya mauaji ya mfanyabiashara.

Baba mzazi anamuomba IGP Sirro kuunda tume kuchunguza kifo hiko. Anasema haiwezekani sero ya polisi kuwe na tambala!

Baba mzazi wa marehemu ni askari mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.
Wamemuuwa polisi wenzake kwenye ili kupindisha kesi, safari hii jamuhuri isifanye uzembe wa Kama kesi ya zombe ambapo kwa kujua kesi itakavyokuwa walimtorosha SADI aliyeamuliwakupiga risasi wafanyabiashara na kupora pesa, Askari aliyetubu na kueleza ukweli aliuwawa kabla ya ushaidi wake kupokelewa Kama kizibiti. So walipunguza nguvu ya mashaidi. Ndicho walichofanya hawa polisi wa kihuni, halafu polisi wanamdharau Sana mama, mbona yule baba aliyefariki masika mwaka Jana hawakumchezeachezea figisu, dharau mama wamezidi ukiwaachia waendelee kuuwa uwa raia wema, iko siku watajaribisha kwenu viongozi, oooh nyie wachekeeni
 
Hizi_kesi_za_kuchonga_wanapewa_wengi_sana_kuonewa._Serikali_dhalimu_hizi_zinapaswa_kuondolewa_...jpg
 
Yaani anaomba anayemtuhumu kuwa alimtuma kuua, kuunda kamati ya uchunguzi?!
Nyepesi nasikia, hao hao wakubwa wa juu walipoenda huko Mtwara kuwahoji askari walohusika, aliyejinyonga alisimamia ukweli kuhusu kila kitu kilichotokea. Nasikia walimwijia juu, na kumtisha saana. Askari huyo baada ya kutoka kuhojiwa alieleza kwao nyumbani kilichojiri kwamba katishwa saaana.

Japo baadae alipiga simu na kumwambia mama yake mambo si mabaya, na baada ya hapo wakapewa taarifa kajinyonga. Hili swala Rais aingilie kati tu, kama Kikwete alivyofanya na kuunda tume huru kwenye sakata lile la Zombe. Huyu Mkuu wetu wa jeshi la Polisi hakuna kitu.
 
Akomae nao ukweli utajulikana tuu!
Baba mzazi ana mashaka na kifo cha mwanae, anasema mwanae ameuwawa kwa kuwa mwanae alisimamia ukweli kuwa alitumwa na wakubwa wake kufanya mauaji ya mfanyabiashara.

Baba mzazi anamuomba IGP Sirro kuunda tume kuchunguza kifo hiko. Anasema haiwezekani sero ya polisi kuwe na tambala
 
Damu yako isinyamaze mpaka ijipatie kisasi kwa wale wote waliotoa uhai wako😭
ASKARI ALIYESHTAKIWA KWA MAUAJI AJINYONGA MAHABUSU KWA TAMBALA LA KUDEKIA



ASP Greyson Mahembe ambaye ni Mrakibu Msaidizi wa Polisi anayedaiwa kujinyonga kwa tambala la kudekia akiwa mahabusu ya kituo cha Polisi Wilaya ya Mtwara, Mkoani Mtwara. Greyson alikuwa miongoni mwa Maafisa wengine wa Polisi saba wanaotuhumiwa kuumua kijana Mussa Hamisi (25) ambaye ameuawa baada ya kudai fedha zake shilingi Milioni 33.7 ambazo Maafisa hao wanadaiwa kuzichukua kutoka kwa kijana huyo baada ya kumfanyia upekuzi, uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

Source : millard ayo
 
From my heart. Sipendi kabisa polisi. Sipendi kabisa magereza wanatamaa saaaana. Naishia hapo. Wanadhiki kama hawana ridhki. Siwapendi mno.

Haswa hao polisi wa mtwara, lindi, na masasi. Sijui nitukane vipi. Daaah.
 
Back
Top Bottom