Baba wenye 30s wenye mabinti teenagers njooni hapa (Huyu binti yangu nimpeleke Feza Girls au Makongo Sec?)

Baba wenye 30s wenye mabinti teenagers njooni hapa (Huyu binti yangu nimpeleke Feza Girls au Makongo Sec?)

Mkuu kama hukuwahi kuwa na mtoto wa kike ukiwa teenager na sasa hivi upo in ur mid 30s and she is a teenager alie kwisha vunja ungo anaeishi kwenye social media generation huwezi kujua ugumu wake..

Nimesoma kitabu cha bondia Joe Frazier aliye zaliwa mwaka 1944 akampata mtoto wake wa kwanza binti Jackie Frazier ( ambae ni Judge na bondia mstaafu ) mwaka 1961 akiwa na miaka 16\17) kuhusu namna alivyo weza kudeal na malezi ya binti yake wakiwa na tofauti ndogo ya umri anasema ni rahisi sana mtoto anapokuwa bado hajabalehe lakini akiisha balehe ni ngumu sana na next to impossible ila kwake ilikuwa rahisi kwa sababu mtoto alipo fikisha umri wa balehe alimpeleka kwa mama yake mzazi.( mama wa mtoto )
Changamo nayo kuona nayo ni kama umekuja kutueleza kuwa una binti wa miaka 15 na una uwezo wa kumsomesha feza,
Maana kila unachoambiwa unataka kila mtu akusuport mawazo yako, wewe una miaka 35 mtoto miaka 15 ni tofauti ya miaka 20 ambayo ni kubwa sanaaaa, ambapo watu wengi wako na tofauti hiyo na wazazi lakini tumefundishwa na tunawaheshimu wazazi, ina maaana wewe una matatizo katika ulezi wako kuna sehemu umeteleza.!
Jiulize kwanini ameenda kwa bibi heshima imeanza kurudi kuliko akiwa kwako.???
 
Watoto wa kike kunaumri ukifika Mambo huwa ovyo kabisa kunawale wanaojionesha kma wako alafu Kuna wa adabu mbele za watu lkn huko nje ni balaa

Kumuonesha mapenz mtotosana kupitiliza inawezapia kuwa sabbu kwa hatua aliofika ameshaharibu lakn hujachelewa muweke wazi kuwa ni binti na anatakiwa aweje kwa upendo kulingana na unavotaka awe mueleze mamayako kilakitu aongee nae kimaadili zaidi Kama mwanamke

Kuhus shule mtafutie boarding ambayo wakovzuri kitaaluma mtafute mwalimu wakike ambae Yuko vzuri mkabidhi kwake awe Kama mlezi na uwe karibu na uyo mwalimu kufatilia mienendo yake kinidhamu,

Nidhamu ikiwa ndogo hata uwezo darasani nao utapungua
 
Pamoja sana kaka..
vitoto vya siku hizi ni sheedah . ukiwa mkali sana mtoto anaweza hata kuondoka nyumbani na usijue ameenda wapi.

So inabidi uwe Wise. Watoto wa siku hizi sio sawa na dada zetu wa miaka ya themanini/70 na mwanzoni mwa miaka ya 90.

Nilivyo kuwaga nikimuona video vixen Tunda alivyo haribikiwa halafu nikitazama cv ya baba ake mzazi Afande SabaSita nilikuwa nashangaa sana aisee na kuona kama mzee Sabasita anazingua .kumbe kuna umri binti akisha fika baadhi ya mambo huwezi kumzuia zaidi ya kumuachia Mungu. P funky kwa Kajala, baba ake Lulu, baba ake Wema, etc etc.

Mtoto wa kike alie balehe huwezi kumzuia kumiss behave ( kwa mfano kugongwa). Unacho weza kufanya ni :
1. Kumuwekea mazingira magumu sana ya kupata nafasi ya kugongwa. Yani hata akienda kugongwa basi awe amekulia timing ya hatari sana.


2. Kumchelewesha kuanza kugongwa. Badala ya kuanza kugongwa akiwa na miaka 13 basi at least aanze akiwa na miaka 17/18/19.

Ukiujua ukweli utakuweka huru
Pia jinsi anavyokuona rafiki tumia hilo kumweleza kuhusu madhara ya mapenzi kwa umri mdogo.
Umuhimu wa kujitunza.

Expectation zako kwake

Mwambie jinsi wanaume walivyo waongo.
Etc etc

Itakaa zaidi kichwani mwake akiyasikia kutoka kwa mzazi kuliko akifunzwa na dunia

Mfundishe kujisimamia na kutoendana na ujinga wa makundi

Jua marafiki zake

Mkanye with reasons. Watoto wa siku hizi wana uelewa mpaka na wanahoji hivyo uwe na maelezo yaliyoshiba

Zaido ajue msimamo wako!!

Yaank ajue akimess wapi huna utani na ukimuadhibu uwe serious

Kumpeleka makongo au feza kama hujampa msingi mzuri nyumbani haitosaidoa sana.
 
Hivi mnaleaje watoto kufika hatua ya kubishana??!!🤔
Kwa nidhamu mpeleke makongo ingawa pia anaweza toka na tabia za ajabu zaidi ya alizonazo..
Mfuatilie huyo binti kwa ukaribu wazazi tusichoke kulea watoto wetu Jamani..
 
Back
Top Bottom