Baba wenye 30s wenye mabinti teenagers njooni hapa (Huyu binti yangu nimpeleke Feza Girls au Makongo Sec?)

Changamo nayo kuona nayo ni kama umekuja kutueleza kuwa una binti wa miaka 15 na una uwezo wa kumsomesha feza,
Maana kila unachoambiwa unataka kila mtu akusuport mawazo yako, wewe una miaka 35 mtoto miaka 15 ni tofauti ya miaka 20 ambayo ni kubwa sanaaaa, ambapo watu wengi wako na tofauti hiyo na wazazi lakini tumefundishwa na tunawaheshimu wazazi, ina maaana wewe una matatizo katika ulezi wako kuna sehemu umeteleza.!
Jiulize kwanini ameenda kwa bibi heshima imeanza kurudi kuliko akiwa kwako.???
 
Watoto wa kike kunaumri ukifika Mambo huwa ovyo kabisa kunawale wanaojionesha kma wako alafu Kuna wa adabu mbele za watu lkn huko nje ni balaa

Kumuonesha mapenz mtotosana kupitiliza inawezapia kuwa sabbu kwa hatua aliofika ameshaharibu lakn hujachelewa muweke wazi kuwa ni binti na anatakiwa aweje kwa upendo kulingana na unavotaka awe mueleze mamayako kilakitu aongee nae kimaadili zaidi Kama mwanamke

Kuhus shule mtafutie boarding ambayo wakovzuri kitaaluma mtafute mwalimu wakike ambae Yuko vzuri mkabidhi kwake awe Kama mlezi na uwe karibu na uyo mwalimu kufatilia mienendo yake kinidhamu,

Nidhamu ikiwa ndogo hata uwezo darasani nao utapungua
 
Pia jinsi anavyokuona rafiki tumia hilo kumweleza kuhusu madhara ya mapenzi kwa umri mdogo.
Umuhimu wa kujitunza.

Expectation zako kwake

Mwambie jinsi wanaume walivyo waongo.
Etc etc

Itakaa zaidi kichwani mwake akiyasikia kutoka kwa mzazi kuliko akifunzwa na dunia

Mfundishe kujisimamia na kutoendana na ujinga wa makundi

Jua marafiki zake

Mkanye with reasons. Watoto wa siku hizi wana uelewa mpaka na wanahoji hivyo uwe na maelezo yaliyoshiba

Zaido ajue msimamo wako!!

Yaank ajue akimess wapi huna utani na ukimuadhibu uwe serious

Kumpeleka makongo au feza kama hujampa msingi mzuri nyumbani haitosaidoa sana.
 
Hivi mnaleaje watoto kufika hatua ya kubishana??!!🤔
Kwa nidhamu mpeleke makongo ingawa pia anaweza toka na tabia za ajabu zaidi ya alizonazo..
Mfuatilie huyo binti kwa ukaribu wazazi tusichoke kulea watoto wetu Jamani..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…