Bado kuna wanaobisha misiba ni mingi kuliko mwaka jana

Bado kuna wanaobisha misiba ni mingi kuliko mwaka jana

Si nia ya uzi huu kuorodhesha visa vya tanzia tangia kuondokewa bila ya kutarajia na mama yetu mpendwa mama mchungaji. Ikumbukwe kuwa majina ambayo yamekuwa yakiripotiwa ikiwamo humu jamvini ni yale yenye kuhusisha majina makubwa makubwa tu.

Hapa ninaangazia matukio ya juzi peke yake kutokea katika maeneo ya vijijini kuonyesha hali iko je:

Juzi katika mazingira tata kama yanazolingana na sababu za tanzia zinazowekwa humu jamvini siku za hivi karibuni, mkuu wa kituo cha polisi Nyakanazi (Biharamulo) naye katangulia mbele za haki.

Mtu mdogo huyo vijijini huko. Kufariki kwake hakukuonekana mahali popote.

Juzi hiyo hiyo maeneo karibu na mizani ya Nyakahura (Biharamulo) amefariki mtu njiani akipelekwa hospitali akiwa na matatizo ya kupumua.

Juzi hiyo hiyo huko Kahama (Shinyanga) ofisa halmashauri wa wilaya alifariki ghafla kwa matatizo kama hayo hayo ya kupumua.

Nani anawajua wadogo hawa huko madongo kuinama kiasi cha kufanya iwe habari ya kuripotiwa popote? Hii ikizingatiwa pia kuwa, hata kwa hao wakubwa juhudi za kudunisha matukio yao zimekuwa kubwa kwa kiasi tunachokiona?

Hebu basi hata tuweke japo sababu za vifo pembeni. Hata kujiuliza tu, hivi hii kasi ya vifo ni sawa sawa pia hamna?

Tumekuwa kama tuliopigwa upofu. Tunetekwa na shetani. Tumekuwa mawakala kamili na waaminifu wa shetani. Hatuoni wala hatusikii hadi pale mmoja mmoja litakapomfika peke yake mlangoni?

Nakumbuka kale kawimbo:

"nyoka huyo, nyoka huyo" (kibwagizo)
"Mwache apite" (kiitikio)

"nyoka huyo, nyoka huyo" (kibwagizo)
"Mwache apite" (kiitikio)

Hadi wote wanaangamia na nyoka wakiwa wakiitik ia acha apite.

Matukio ni mengi sana lakini ajabu ya Mussa pana kaupepo kengine siku za hivi karibuni ka kuona mtu au watu kufa ni jambo la kawaida. Hakuna kujali wala kufuatilia. Eti kuwa hata zamani watu walikuwa wanakufa.

Walikuwa wanakufa hivi?

Dalili kamili za kumtumikia shetani.

Enyi mnaodunisha vifo vya wengine ni vyema mkajitathimni:

"you could be in possession of the devil. Faithful agents of the devil himself".

Badilikeni jamani mnatia kinyaa.
5G, Chip na 666. Zina mahusiano makubwa sana.
Wanatakakutupeleka kwenye Chip ili maandiko ya 666 yatimie
 
5G, Chip na 666. Zina mahusiano makubwa sana.
Wanatakakutupeleka kwenye Chip ili maandiko ya 666 yatimie

Mkuu unadhani huko Uganda, Kenya na hata Uganda kasi ya vifo vya high profile individuals iko juu hivyo?

Sasa chip ya 5G inahusika Tanzania tu?
 
Uingereza ilipokuja Corona vifo vya magonjwa mengine navyo viliongezeka. Wamekuja kujua baadaye kuwa kumbe hata vingi vingine ilikuwa Corona.

Sina hakika kama umeielewa mada. Vifo vimeongezeka. Matatizo ya kupumua. Hakuna aliyesema ni Corona.

Haitushangazi vifo vimeongezeka? Haitushangazi ukisikia ni matatizo ya kupumua? Haitushangazi ni kwa nini ni siku za karibuni? Hatujali wala kuona kama hali sawa sawa.

Hatuoni kuwa kuna tatizo hadi litukute mlangoni. Kuna kitu halipo sawa.

Kama hatuoni hii ni serious tutakuwa watu wa ajabu mno.
Unaposema vifo vimeongezeka una maana kwamba kabla ya corona ulikuwa unafutilia idadi au hali ya vifo Tanzania kiasi cha kuweza kujua kuwa hivi sasa idadi ya vifo imeongezeka kuzidi baada ya kuingia kwa corona?

Mimi nafikiri kipimo kizuri ni kila mtu kuangalia eneo zima analoishi hali ikoje? je,maeneo tunayoishi kuna ongezeko la vifo kusiko kawaida?
 
Taarifa za huu ugonjwa ziwekwe wazi
 
I repeat, did you read your preceding comment that I had replied to?

Get back to your senses if you have any left with you, patsy. You had my promise - "you won't miss it!"

Miminika ....
OH! I was right... you've no confidence with your own argument, that's why you been beating around the bush instead of going directly to the point!
 
Mkuu tahadhari gani hizo ambazo yule RC alishindwa kuchukua? Kwa maneno yake alisema: "sijui ni sharti lipi sikuzingatia". Mwisho wa kumnukuu.
Kuzunguka hovyo hovyo na social distancing hakuzingatia.
 
Mkuu Kamundu , headline haiendani na main body, kwenye headline unazungumzia misiba mingi kuliko mwaka jana, hii ni issue ya data, subiri tufike mwisho wa mwaka, kisha tupate death toll ya mwaka jana compared na ya mwaka huu!.

Matangazo tuu ya vifo ndio mengi, ila jumla ni subiri mwisho wa mwaka, Wote wanaokufa kwa Corona walikuwa na issues zao za kiafya kabla, Corona ni kuwawahisha tuu.

Mzee Baba hajajificha, he is working from Ikulu ya Chato na kila siku tunamuona anapiga kazi kutokea pale unasema kajificha, kajificha vipi wakati pale ni kwake?!

P
Dah mkuu P naona unamtetea sana poti wako, lakini kiukweli amekula kona na nchi inakwenda tu.
 
uyo wa kahama sio kweli mkuu
Kafa kwa tatizo gani?
Anazikwa lini?
Nilisikia alipelekwa kituo cha afya kwema akazidiwa usiku huo huo akafa kwa tatizo la upumuaji japo tetesi za kitaa wanasema alikuwa mgonjwa wa dozi za hisani ya watu wa marekani ( mtaani kuna maneno sana)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tufanyeje tupate kupona?
Ikiwa twaambiwa tahadhari za msingi za kunawa na kuziba pua na midomo kwa barakoa nazo twazifuata
Una uhakika na ulichoandika? Mkuu mbona wengine hatupendi kabisa kutaja majina ya watu?

Kuhusiana na Kahama, ulizia halmashauri ya wilaya kitengo cha Ardhi watakwambia. Ila ikibidi nitakupa majina hata yote pia yakiwamo wa Nyakahura na Nyakanazi.

Acheni kuwa merchants of death.

Kama nyie haiwaumi sisi inatuuma sana. Mnakuwa wenzetu kama mnaishi sayari nyingine. Watu wa namna gani nyie?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uingereza ilipokuja Corona vifo vya magonjwa mengine navyo viliongezeka. Wamekuja kujua baadaye kuwa kumbe hata vingi vingine ilikuwa Corona.

Sina hakika kama umeielewa mada. Vifo vimeongezeka. Matatizo ya kupumua. Hakuna aliyesema ni Corona.

Haitushangazi vifo vimeongezeka? Haitushangazi ukisikia ni matatizo ya kupumua? Haitushangazi ni kwa nini ni siku za karibuni? Hatujali wala kuona kama hali sawa sawa.

Hatuoni kuwa kuna tatizo hadi litukute mlangoni. Kuna kitu halipo sawa.

Kama hatuoni hii ni serious tutakuwa watu wa ajabu mno.
Ungetaja hicho kisicho sawa ingekuwa msaada mkubwa sana.
Hakuna kificho watu wanakufa na kuugua sana tu, na tahadhari tunazoambiwa zinafanyiwa KAZI, tena wengi wanaoripotiwa kufa ni wale usiowatilia shaka kuwa wanachukua tahadhari.
Sasa tufanye nin?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo haya hakuna yanayokufikirisha?

1. Hawakuwahi kufa wakuu wa wilaya 2 ndani ya wiki 3.
2. Hawakuwahi kufa wabunge 3 ndani ya wiki 3.
3. Rais hakuwahi kubakia kwao kwa zaidi ya mwezi mzima.
4. Hatukuwahi kupata ugonjwa shughuli zote za shule zikastishwa.
5. Hatukuwahi kuwa na mazishi ya kusimamiwa na serikali.
6. Hatukuwahi kuwa na mazishi waombolezaji wasiozidi 10
7. Nk nk

Yote haya yanatokea katika kipindi hicho hicho.

Kweli haya huyaoni na ni jasiri wa kuulizana kama kuna jingine?

Sote tupo dunia hii hii au wengine mnatokea anga za juu?
Yote haya sababu ya covid19 hakuna swali, tunashuhudia kwenye jamii tunayoishi.
Nini kifanyike sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama benki zinavyofanya, unaweza pia kulinganisha Jan 2019 na Jan 2020 ama Q1 2019 na Q1 2020. Nakubaliana na wewe kuwa data zinahitajika. Otherwise ni umbeya tu.
Mkuu Kamundu , headline haiendani na main body, kwenye headline unazungumzia misiba mingi kuliko mwaka jana, hii ni issue ya data, subiri tufike mwisho wa mwaka, kisha tupate death toll ya mwaka jana compared na ya mwaka huu!.

Matangazo tuu ya vifo ndio mengi, ila jumla ni subiri mwisho wa mwaka, Wote wanaokufa kwa Corona walikuwa na issues zao za kiafya kabla, Corona ni kuwawahisha tuu.

Mzee Baba hajajificha, he is working from Ikulu ya Chato na kila siku tunamuona anapiga kazi kutokea pale unasema kajificha, kajificha vipi wakati pale ni kwake?!

P
 
Ungetaja hicho kisicho sawa ingekuwa msaada mkubwa sana.
Hakuna kificho watu wanakufa na kuugua sana tu, na tahadhari tunazoambiwa zinafanyiwa KAZI, tena wengi wanaoripotiwa kufa ni wale usiowatilia shaka kuwa wanachukua tahadhari.
Sasa tufanye nin?

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu cha kwanza ni elimu kuwa hivi ni vita vya taifa siyo vita vya mtu mmoja mmoja.

Mzee baba kule anatuangusha sana.

Maamuzi pale juu kwa mzee baba ni lazima yabadilike kulinusuru taifa hili.

Busara za marais wastaafu zinaweza saidia kumfunga huyu paka kengele. Watu hawawezi kuendelea kufa wakati wenye akili zao wakiangalia misukule ikitamalaki.
 
Back
Top Bottom