Bado kuna wazazi wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili

Bado kuna wazazi wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili

Naamini umeona mengi, kufikia kuandika hivi Basi ni wazi Kuna maana kubwa nyuma ya hii, na Mimi nikijaaliwa uhai na uzazi salama nitaifikisha idadi ya watoto 6 uliotamani kuwa nao
Aisee, sita? Well, kama uzazi upo na hauna complications, una uwezo wa kulea na kusomesha ni sawa kabisa.
 
Sio jambo zuri kuzaa ikiwa mtoto wako tayari kaisha pevuka, ila kuna muda inabidi iwe hivyo
Mfano:- mtu nimezaa nikiwa na miaka 18 (ilikuwa bahati mbaya na sikutaka abortion) baada ya hapo nikasema sasa nahitaji kurekebisha makosa, nikaamua kutulia kuanza kuandaa life langu kwanza (nikarudi school) ndio nije nizae tena hapo nakuja kusema sasa nahitaji mtoto wa pili nina miaka 35 mtoto wa kwanza kaisha vunja ungo tayari. Unazania nini kitatokea kwa kizazi hiki
Katika 200 cases, issue ya namna hii ni moja au mbili tu baaas
 
Inategemea na mazingira na familia yako ikoje.
Ndugu Marehemu Mengi alipoona hana wajukuu akaaamua kutafuta wajukuu yeye mwenyewe. They are now 6/ 7 years old.
Nilitamani kuandika jambo kuhusiana na hili, sema tu kwa mila za kiafrika marehemu hapaswi kusema. R.I.P mzee wetu Mengi
 
Lakini watoto wa uzeeni ndio huwafariji wazee baada ya wakubwa wote kuanza maisha yao na isitoshe siku hizi utamaduni wa kuwaachia wazee wajukuu wawalee ni kama unakufa, kheri hiyo kidogo inawaondolea upweke ndani ya nyumba
Wazee wanapaswa kupata faraja kanisani/misikitini kwa kuungama mienendo yao ya ujanani huku wakijiandaa na pumziko la milele.
 
Mimi nilizaliwa kijijini.

Kaka yangu wa kwanza kazaa mtoto ambaye ni mkubwa kwangu.

Bro ana miaka 70.
Dingi naye yupo....

Sisi watoto wa mwisho ndio tunamsaidia sasa hivi.
Yalikuwa maisha ya kijijini lakini kila mtu anafanya jambo kutokana na mazingira yaliyopo kwa muda flani.

Kwa hali ya maisha ya sasa ni kazi sana kuzaa watoto wengi
Ninakuunga mkono hiyo statement ya mwisho
 
Hao wazee wa namna hiyo mara nyingi huwa hawako responsible, anatafuta kabinti ambako hakajielewi anaishia kukapa mimba. Kunabaki mwendelezo wa mizinga ya hapa na pale kutoka kwa watoto wake wakubwa, hadi anatengeneza migogoro kwenye familia..
Tena ni migogoro mikubwa sana kaka mkubwa
 
Tuseme alizaa mtoto akiwa na miaka 18.

Sasa akiwa na miaka 40 binti ana miaka 22, sawa wote wanazaa sioni ubaya hapo.

Mmh hesabu yenyewe sijui nimepata.
Kama alizaa akiwa na miaka 18, alikuwa wapi miaka yote mingine 22 akashindwa kuongeza watoto wengine mpaka anakuja kuzaa mtoto wa pili akiwa na miaka 40?
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu Watanzania;

Bado kuna watu wazima wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili.

View attachment 1667340

Siku ya sherehe ya mwaka mpya nilikutana na dada mmoja anaitwa Veronica (hili sio jina lake halisi) ambaye nilimaliza naye shule ya msingi mwaka 1999.

Huyu dada nilikwisha kutana naye mwezi kama wa August maeneo ya Banana Ukonga huku Dar. Kwa kuwa tulikuwa hatujaonana miaka takribani 15 tulipiga story nyingi sana za zamani.

Sasa nilipokutana naye tena Ijumaa ya tarehe 01 January 2020 huku Kivule ninapokaa (kwa maana aliniambia anakaa Kata moja na mimi) nilimuona anaongozana na binti mdogo wa miaka kama 9 hivi.

Tena huyo binti wamefanana kweli kweli. Basi tulipoonana tulisalimiana tena kwa furaha sana. Baada ya story kadhaa nikamuuliza, huyu ndio mtoto wako wa kwanza? Akakataa. Akasema hapana, huyu sio mtoto wangu.

View attachment 1667350

Huyu ni mdogo wangu wa mwisho. Mtoto wangu ameenda kwa baba yake kusalimia atarudi shule zikifunguliwa. Sema ndio rafiki yake mkubwa sana huyu (mdogo wake wa mwisho) kwa maana wamepishana mwaka mmoja tu.

Mimi sikuwa na jambo lingine la kumwambia zaidi tu ya kumpa hongera lakini nikawa ninajisemea tu kimoyomoyo "ina maana haya masuala ya mtoto na mama kuzaa kwa pamoja bado yanaendelea katika karne hii ya 21?"

Hii issue nilikuwa ninaiona tu kwa wazee wa zamani ambapo unakuta mtu unakutambulisha "huyu ndio baba yangu mdogo/shangazi yangu tumbo moja na baba" au "huyu ndio mama yangu mdogo tumbo moja na mama" lakini ukijaribu kuwatazama actually wanalingana umri au wamepishana mwaka mmoja tu.

View attachment 1667352

Mimi ni moja kati ya watu wanaokerwa sana na lugha za hawa dada/mama zetu manesi lakini linapokuja suala la kukemea wamama/wababa wanaoendeleza utamaduni huu wa hovyo mimi ninawaunga mkono sana.

Kuna mtoto wa shangazi yangu mmoja yeye ni nurse huko Geita anakwambia mama mtu mzima wa design hii akija kujifungua (wanawafahamu sana kwa maana vijijini watu ni wachache) huwa wanawachamba kwa maneno na lugha chafu mbele ya waume zao.

Kuna mama mmoja aliwahi kufariki mwaka 2006 alipokuwa anajifungua wakati bado tunakaa kule Keko. Sasa wakati wa mazishi watu wamekusanyika na wageni wanataka kujua chanzo cha kifo chake ikawa sasa ni aibu kusema kuwa amekufa kwa sababu ya "complications" za uzazi ilhali binti yake mkubwa ana mtoto wa miaka 2 tayari.

View attachment 1667341

Mimi binafsi ninaona sio jambo la hekima wala busara kwa mama/baba kuendelea kuzaa watoto wengine wadogo ilhali wale "first born" wamekwisha kuwa wababa/wamama wanaokaribia ku-reproduce.

Sio vizuri mama kuonekana ana tumbo kubwa la ujauzito pindi wale "first borns" wanapokuwa wamepevuka akili.

Kwa maoni yako, ni sahihi mama na binti/mtoto kuendelea kuzaa kwa pamoja? Mtoto wa mwisho kulingana na mjukuu wa kwanza?

"HAPPY NEW YEAR 2021"

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya wadau
=====
Eti maadili wewe unajua maadili gani ?.Kuzaa ni kukosa maadili? Nchi inataka watu wewe unaongea upuuzi ? Mpaka binti anaolewa maana yake anakuwa anajua mama yake alifanya nini ndipo akazaliwa yeye sasa hapo ajabu kitu gani?. Usituletee tabia za huko kwenu ulaya. Afrika ambapo binti anazaa akiwa miaka14 anarudi shule anamaliza chuo kikuu anazaa wa pili halafu yule kwanza ameshapevuka na anaweza olewa na akazaa .Amka Afrika siyo Ulaya.Afrika unaweza kuwa na miaka 25 na bado unaye Baba Mdogo wa miaka 2.
 
Aisee, sita? Well, kama uzazi upo na hauna complications, una uwezo wa kulea na kusomesha ni sawa kabisa.
Idadi hiyo ikipungua Ni mmoja kwa jinsi navyopenda kuzaa watano nitawafikisha Mungu anipe nguvu tu,, swala la malezi nalo naliwaza ila kama unaambiwa na mume nipe mbegu uwezo wa kulea upo, why not nisizae!!! Nitazaa tu,
 
ndio jamii zetu za kiafrika wengine tunazeeka mapema kwa kuwa huwa tunalazimika kupokea shikamoo za waliotuacha mbali kiumri yan jitu limekupita miaka kuanzia nane huko eti linakuamkia kisa baba yake mdogo au anko wake aaaaaah...... (tusichukulie kila kitu serious)[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu Watanzania;

Bado kuna watu wazima wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili.

View attachment 1667340

Siku ya sherehe ya mwaka mpya nilikutana na dada mmoja anaitwa Veronica (hili sio jina lake halisi) ambaye nilimaliza naye shule ya msingi mwaka 1999.

Huyu dada nilikwisha kutana naye mwezi kama wa August maeneo ya Banana Ukonga huku Dar. Kwa kuwa tulikuwa hatujaonana miaka takribani 15 tulipiga story nyingi sana za zamani.

Sasa nilipokutana naye tena Ijumaa ya tarehe 01 January 2020 huku Kivule ninapokaa (kwa maana aliniambia anakaa Kata moja na mimi) nilimuona anaongozana na binti mdogo wa miaka kama 9 hivi.

Tena huyo binti wamefanana kweli kweli. Basi tulipoonana tulisalimiana tena kwa furaha sana. Baada ya story kadhaa nikamuuliza, huyu ndio mtoto wako wa kwanza? Akakataa. Akasema hapana, huyu sio mtoto wangu.

View attachment 1667350

Huyu ni mdogo wangu wa mwisho. Mtoto wangu ameenda kwa baba yake kusalimia atarudi shule zikifunguliwa. Sema ndio rafiki yake mkubwa sana huyu (mdogo wake wa mwisho) kwa maana wamepishana mwaka mmoja tu.

Mimi sikuwa na jambo lingine la kumwambia zaidi tu ya kumpa hongera lakini nikawa ninajisemea tu kimoyomoyo "ina maana haya masuala ya mtoto na mama kuzaa kwa pamoja bado yanaendelea katika karne hii ya 21?"

Hii issue nilikuwa ninaiona tu kwa wazee wa zamani ambapo unakuta mtu unakutambulisha "huyu ndio baba yangu mdogo/shangazi yangu tumbo moja na baba" au "huyu ndio mama yangu mdogo tumbo moja na mama" lakini ukijaribu kuwatazama actually wanalingana umri au wamepishana mwaka mmoja tu.

View attachment 1667352

Mimi ni moja kati ya watu wanaokerwa sana na lugha za hawa dada/mama zetu manesi lakini linapokuja suala la kukemea wamama/wababa wanaoendeleza utamaduni huu wa hovyo mimi ninawaunga mkono sana.

Kuna mtoto wa shangazi yangu mmoja yeye ni nurse huko Geita anakwambia mama mtu mzima wa design hii akija kujifungua (wanawafahamu sana kwa maana vijijini watu ni wachache) huwa wanawachamba kwa maneno na lugha chafu mbele ya waume zao.

Kuna mama mmoja aliwahi kufariki mwaka 2006 alipokuwa anajifungua wakati bado tunakaa kule Keko. Sasa wakati wa mazishi watu wamekusanyika na wageni wanataka kujua chanzo cha kifo chake ikawa sasa ni aibu kusema kuwa amekufa kwa sababu ya "complications" za uzazi ilhali binti yake mkubwa ana mtoto wa miaka 2 tayari.

View attachment 1667341

Mimi binafsi ninaona sio jambo la hekima wala busara kwa mama/baba kuendelea kuzaa watoto wengine wadogo ilhali wale "first born" wamekwisha kuwa wababa/wamama wanaokaribia ku-reproduce.

Sio vizuri mama kuonekana ana tumbo kubwa la ujauzito pindi wale "first borns" wanapokuwa wamepevuka akili.

Kwa maoni yako, ni sahihi mama na binti/mtoto kuendelea kuzaa kwa pamoja? Mtoto wa mwisho kulingana na mjukuu wa kwanza?

"HAPPY NEW YEAR 2021"

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya wadau
=====
Kwani katiba inasemaje?
 
Yani mimi nawashangaa jinsi mnavyoshangaa haya mambo.

Njoeni huku Tanga mjionee sasa haya mambo bila kuhadithiwa nawatembeza nyumba hadi nyumba.
 
Back
Top Bottom