Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,984
- 19,288
Maandiko ni hadithi za kale tu, hazina ishu, kuna maandiko mengine yanaandika umuue jirani yako Kama ni mchawiHiyo ya three children a maximum ni kanuni yako uliyojitungia, hata ukisoma maandiko yote ya family planning hawajaweka limit ya idadi ya watoto.
Katika family planning unaelekezwa kuzaa watoto kwa utaratibu wa angalau kila baada ya miaka 2 au 3 ili mama apate muda mzuri wa kumtunza mtoto na yeye mwenyewe Afya yake iwe katika hali nzuri kabla ya kubeba ujauzito mwingine.
Pia inatoa fursa ya kujitathimini kiuchumi Kama unaweza kuongeza mtoto mwingine. Kwa hiyo Kama mtu atafuata utaratibu huo anaweza kuzaa hata watoto Saba.
Tatizo lako inawezekana hali yako ya kiuchumi inakulazimu uishie kuzaa watoto watatu, kwa hiyo unataka kugeneralize, au umekalili tu kuwa ukifuata uzazi wa mpango basi hutakiwi kuzidi watoto watatu.