Bado kuna wazazi wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili

Naamini umeona mengi, kufikia kuandika hivi Basi ni wazi Kuna maana kubwa nyuma ya hii, na Mimi nikijaaliwa uhai na uzazi salama nitaifikisha idadi ya watoto 6 uliotamani kuwa nao
Aisee, sita? Well, kama uzazi upo na hauna complications, una uwezo wa kulea na kusomesha ni sawa kabisa.
 
Katika 200 cases, issue ya namna hii ni moja au mbili tu baaas
 
Inategemea na mazingira na familia yako ikoje.
Ndugu Marehemu Mengi alipoona hana wajukuu akaaamua kutafuta wajukuu yeye mwenyewe. They are now 6/ 7 years old.
Nilitamani kuandika jambo kuhusiana na hili, sema tu kwa mila za kiafrika marehemu hapaswi kusema. R.I.P mzee wetu Mengi
 
Lakini watoto wa uzeeni ndio huwafariji wazee baada ya wakubwa wote kuanza maisha yao na isitoshe siku hizi utamaduni wa kuwaachia wazee wajukuu wawalee ni kama unakufa, kheri hiyo kidogo inawaondolea upweke ndani ya nyumba
Wazee wanapaswa kupata faraja kanisani/misikitini kwa kuungama mienendo yao ya ujanani huku wakijiandaa na pumziko la milele.
 
Ninakuunga mkono hiyo statement ya mwisho
 
Hao wazee wa namna hiyo mara nyingi huwa hawako responsible, anatafuta kabinti ambako hakajielewi anaishia kukapa mimba. Kunabaki mwendelezo wa mizinga ya hapa na pale kutoka kwa watoto wake wakubwa, hadi anatengeneza migogoro kwenye familia..
Tena ni migogoro mikubwa sana kaka mkubwa
 
Tuseme alizaa mtoto akiwa na miaka 18.

Sasa akiwa na miaka 40 binti ana miaka 22, sawa wote wanazaa sioni ubaya hapo.

Mmh hesabu yenyewe sijui nimepata.
Kama alizaa akiwa na miaka 18, alikuwa wapi miaka yote mingine 22 akashindwa kuongeza watoto wengine mpaka anakuja kuzaa mtoto wa pili akiwa na miaka 40?
 
Eti maadili wewe unajua maadili gani ?.Kuzaa ni kukosa maadili? Nchi inataka watu wewe unaongea upuuzi ? Mpaka binti anaolewa maana yake anakuwa anajua mama yake alifanya nini ndipo akazaliwa yeye sasa hapo ajabu kitu gani?. Usituletee tabia za huko kwenu ulaya. Afrika ambapo binti anazaa akiwa miaka14 anarudi shule anamaliza chuo kikuu anazaa wa pili halafu yule kwanza ameshapevuka na anaweza olewa na akazaa .Amka Afrika siyo Ulaya.Afrika unaweza kuwa na miaka 25 na bado unaye Baba Mdogo wa miaka 2.
 
Aisee, sita? Well, kama uzazi upo na hauna complications, una uwezo wa kulea na kusomesha ni sawa kabisa.
Idadi hiyo ikipungua Ni mmoja kwa jinsi navyopenda kuzaa watano nitawafikisha Mungu anipe nguvu tu,, swala la malezi nalo naliwaza ila kama unaambiwa na mume nipe mbegu uwezo wa kulea upo, why not nisizae!!! Nitazaa tu,
 
ndio jamii zetu za kiafrika wengine tunazeeka mapema kwa kuwa huwa tunalazimika kupokea shikamoo za waliotuacha mbali kiumri yan jitu limekupita miaka kuanzia nane huko eti linakuamkia kisa baba yake mdogo au anko wake aaaaaah...... (tusichukulie kila kitu serious)[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwani katiba inasemaje?
 
Yani mimi nawashangaa jinsi mnavyoshangaa haya mambo.

Njoeni huku Tanga mjionee sasa haya mambo bila kuhadithiwa nawatembeza nyumba hadi nyumba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…