Bado kuna wazazi wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili

Bado kuna wazazi wanaendelea kuzaa hata baada ya mtoto wao wa kwanza kuolewa? Mtoto wa mwisho analingana na mjukuu wa kwanza? Huku ni kukosa maadili

Je mwanaume kuzaa sambamba na kijana wake mkubwa wa kiume ni sawa?

Yaani baba na mwanae wote wananunua pampers kwa ajili ya watoto wao wachanga.
Sio sawa ndio maana nimetumia neno watoto nikimaanisha jinsia zote
 
Sijambo zuri na linasikitisha sana, ila kuna baadhi mazingira yanapelekea swala hilo, mfano kuna watu wanabakwa wakiwa wadogo miaka 16 anajifungua, anaenda shule baada ya hapo anaolewa unategemea mtoto atakaye mzaa apishane na wabinti yake?, kwa nyongeza umesema mambo ya zamani hata hivo mtu wa1 999, umemeliza shule wewe kwasasa unaesabika kama wa zanani usasa unaanzia 2015... [emoji23][emoji23]
 
Wanawake wenzetu wa Uganda na kando ya ziwa Victoria huko wanazaa hadi watoto 16, siyo huku mtu watoto 2 mama kachoka kachakaa.

Ndiyo mnapata sababu za kusema mama kazaa na binti kazaa.

Acheni wamama wazae, binafsi natamani ningezaa hata 6, kila mtoto ana furaha yake kwa mzazi.

Wamama zaeni watoto wengi ,kuna mwaka mtanikumbuka.
Kama wapo tumboni nikuwatoa tu walete baraka duniani.
 
As

Askari wa Miguu hili suala wengi hawaoni Kama Ni Upuuzi Mkubwa.. vitu Vingine Ni aibu Sana Fikiri una Miaka 25 umeoa halafu Mama Yako huyo na litumbo lake eti Ana mimba..... Dah Afrika tuna shida Sana...
Ndiyo mnatangulizana clinic wewe na mkeo na Baba &mama wote kuhudhulia clinic
 
Lakini watoto wa uzeeni ndio huwafariji wazee baada ya wakubwa wote kuanza maisha yao na isitoshe siku hizi utamaduni wa kuwaachia wazee wajukuu wawalee ni kama unakufa, kheri hiyo kidogo inawaondolea upweke ndani ya nyumba

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wewe kama kijana wa miaka 25 unajiskiaje kumuona eti mama yako ni mjamzito?
nitaona kawaida, as long as kaipata kwenye mahusiano halali ya ndoa, yenye kueleweka, halafu,

ukiona hadi nina umri huo halafu maza bado kawa na uwezo wa kushika ujauzito maana yake alinizaa mapema sana, hivyo atakuwa sio mzee bali mwanamama tu, nitaona freshi tu, mradi mahusiano yake yawe ya kueleweka
 
Na mimi namuunga mkono mzee wangu ntafyatua mpaka nifikie idadi ya watoto wake au nimzidi kabisa

Kwetu tupo watoto kumi na mbili saba wa kiume watano wa kike na wa mwisho alizaliwa mwaka 2008 you never know mzee anaweza akafanya yake tena maana Ng'ombe hazeeki maini.
Watoto wengi wa uzeeni huwa wanakuwa mataahira na wana uwezekano mkubwa wa kupata mtindio wa ubongo.

Ndio shida ya jamii ya watu wenye elimu kiduchu.

Mkizaa mataahira mnaanza kuisumbua serikali na jamii kwa ujumla. Mnatengeneza matatizo yanayoweza kuepukwa.

Atii ooh mie ntazaa mpaka tone la mwisho! SO WHAT? ni sifa?

Mbegu bora za watoto ni za ujanani! Sio unazaa mataahira ya uzeeni halafu unajisifu!
 
Watoto wengi wa uzeeni huwa wanakuwa mataahira na wana uwezekano mkubwa wa kupata mtindio wa ubongo.

Ndio shida ya jamii ya watu wenye elimu kiduchu.

Mkizaa mataahira mnaanza kuisumbua serikali na jamii kwa ujumla. Mnatengeneza matatizo yanayoweza kuepukwa.

Atii ooh mie ntazaa mpaka tone la mwisho! SO WHAT? ni sifa?

Mbegu bora za watoto ni za ujanani! Sio unazaa mataahira ya uzeeni halafu unajisifu!
Upo sahihi ni vizuri sana kuzaa ujanani angalu ukifika miaka 40-42 iwe mwisho.
 
Back
Top Bottom