Bado sijaelewa jambo moja: Hivi tunataka kuendesha SGR sambamba na reli ya zamani?

Bado sijaelewa jambo moja: Hivi tunataka kuendesha SGR sambamba na reli ya zamani?

sasa

Sasa Mkuu haya Mabehewa na Vichwa vya Treni si wamekubali wenyewe kwamba ni Used? ama hivi havikununuliwa walipewa?
Hapana, walinunua hawakupewa, na watu wanasema bei waliyonunulia iko juu mno. Kulingana na maelezo yao, vilikuwa kwa ajili ya SGR, lakini inaonekana vimeenda reli ya zamani
 
Hapana, walinunua hawakupewa, na watu wanasema bei waliyonunulia iko juu mno. Kulingana na maelezo yao, vilikuwa kwa ajili ya SGR, lakini inaonekana vimeenda reli ya zamani

dah
SGR mpaka reli ya zamani? spandi treni aisee. Kwanza nikiangalia Maisha wanayoishi wale wanaofanya chanting ( wale wanaobadili njia ) umeona walivyo? taabani wakati wale ni watu Muhimu sana yaan wamechokaaa huku hawa wengine wanakula kiyoyozi ndani ya Bombadia..

kwa hiyo itabidi wanunue Mengine ili kutuliza hili sekeseke ama ndo imeisha hiyo. aisee inatia hasira
 
Mmezoea cheweing gum nyie, wenzenu wa zamani walizoea matobolwa - waulize watu wa Tabora watakuambia utamu wa matobolwa kulinganisha na hizo cheweing gum zenu!
The power of FAKE ID..!! Unajiandikia tu huku hujui kuwa unayemjibu ni baba yako au yupo sawa naye
 
Kuna kila dalili kwamba SGR itakapokamilika bado tutakuwa na reli ya zamani ikitoa huduma. Hapo mwanzo nilifikiri kwamba reli ya zamani itaendelea kutoa huduma kwa matawi ya Tabora - Mpanda, na labda Dar -es Salaam kwenda Tanga, Moshi na Arusha, ambako sijasikia lolote juu ya kuwepo kwa SGR.

Lakini kila habari zinapotolewa, sisikii hili likiwekwa wazi. Ninasikia tu kuhusu SGR sambamba na reli ya zamani, na manunuzi yakifanywa kwa ajili ya reli zote mbili.

Kwa nini tuendelee kuhudumia na kuwekeza kwenye reli zote mbili? Ni kupanua wigo wa huduma katika bei, kwamba SGR iwe kwa mabwana na reli ya zamani watwana?

Ninachelea kwamba uwepo wa SGR utafanya reli ya zamani iendeshwe kwa hasara iwapo tutaendelea kuitumia. Nilidhani labda SGR ikikamilika reli ya zamani itauzwa kama vyuma chakavu.

Labda ni ule uswahili wetu tu wa kiafrika, tunaendelea kutaka kumiliki vitu vya zamani, tunashindwa kuvitupa hata kama tumenunua kitu kipya mbadala
Shida kubwa tuliyo nayo hatuna mipango ya muda mrefu inayoeleweka na iliyo wazi mfano reli zitakuwaje miaka 50 ijayo, miji itakuwaje, nk.

Kwa hiyo mambo yanafanyika kuendana na utashi wa kiongozi aliepo. Ndio maana tunashukuru rais kufanya hili na lile - inakuwa kama hisani badala ya jukumu la kutekeleza mipango iliyo wazi na inayoeleweka. Na kwa hili ilani ya chama sioni kama itakupa jibu, haina maelezo yanayoeleweka na mipango ya muda mrefu....
 
Shida kubwa tuliyo nayo hatuna mipango ya muda mrefu inayoeleweka na iliyo wazi mfano reli zitakuwaje miaka 50 ijayo, miji itakuwaje, nk.

Kwa hiyo mambo yanafanyika kuendana na utashi wa kiongozi aliepo. Ndio maana tunashukuru rais kufanya hili na lile - inakuwa kama hisani badala ya jukumu la kutekeleza mipango iliyo wazi na inayoeleweka. Na kwa hili ilani ya chama sioni kama itakupa jibu, haina maelezo yanayoeleweka na mipango ya muda mrefu....
Lakini reli siku zote ni kitu cha muda mrefu, hatutegemei muundo wa reli utabadilika katika miaka 50 ijayo kwamba wote tuende kwenye bullet trains. Kwa hiyo hakuna baya juu ya hili la SGR kuwa mpango wa muda mrefu, ila ni huu mkoroganyo kidogo wa mabehewa na SGR Vs reli ya zamani
 
Sasa kama reli iliyopo ni nzima inafanya kazi, ni cheaper ku-operate, kwa nini tukaamua kujenga SGR kwa mabilioni ya fedha badala ya kuimarisha hiyo iliyo nzima?
Tukitazama nchi kama Afrika ya kusini, India, na Brazil n.k nao pia walikuwa na na hii hii MGR na hawakuitelekeza waliendelea nayo kwa sababu ilisupport reli mpya zao.

India wakaenda mbali zaidi kujenga hadi Broad gauge ambayo ni kubwa zaidi kwa hiyo ya SGR (1435mm) ambayo ni 1676mm, kwahiyo wanayo meter gauge (1000mm), standard gauge (1435mm) pia hiyo Broad gauge (1676mm) na zinapiga kazi.

Afrika ya kusini wao wana standard gauge, meter gauge na cape gauge (1067mm) ambayo kama hiyo ya TAZARA iliongezeka 67mm tu kutoka katika ile Meter gauge kwahiyo inategemea na nyinyi wahusika mmejipanga vipi kuendesha reli zote mlizonazo kwa faida.

Sera bora, uendeshaji timamu, uongozi imara na mipango dhabiti inawezekana, Je wao watayaona hayo?
 
Nchi mpaka huu mfumo wa kijani
Ukitoka labda mambo yanaweza kaa
Sawa

Ova
Najua ndivyo wengi wanafikiri, lakini amini nakuambia, usidhani ukiwaleta Chadema au ACT sijui basi hiyo ndio dawa ya maendeleo. Binadamu ni wale wale, wawe CCM, Chadema au ACT hata TLP. Niambie ni nchi gani duniani imepiga hata kubwa ya maendeleo kwa kuwa tu walibadilisha chama tawala. Zambia? Kenya? USA? Uingereza? Brazil? Malawi?

NI kawaida kudhani mchezaji alie benchi atafanya vizuri zaidi, lakini huwezi hata siku moja kuwa na huo uhakika. Inaweza itokee, inaweza isitokee.

Ndio maana siku zote nimesema, siri ya kuifanya angalau Tanznia iendelee, sio lazima Chadema wachukue nchi, bali ni kufanya vyama vya upinzani viwe na wabunge wengi kwa pamoja, ikiwezekana kuliko hata idadi ya wabunge wa CCM

Mie nilisema raisi atakaekuja kuwa mzalendo wa kweli wa Tanzania mwenye kuitakia maendeleo Tanzania ni yule atakaeimarisha upinzani nchini, sio anaeimarisha Chama chake dhidi ya upinzani. Na kwa hili nawakosoa wote waliokuwa maraisi tangu mfumo wa vyama vingi uanze - Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na hata Samia. Wote wameiangusha sana nchi hii na hakuna mzalendo wa kweli kati yao. Porojo tu zimewajaa lakini sio wazalendo hawa wote, wapigania tonge kwa sababu ni wapigania vyama vyao badala ya nchi yao.

Kama Samia angenisikiliza, ningemwambia kama kweli una uchungu na hii nchi, wapaishe wapinzani, wafanye wawe popular na kuheshimika nchini, wafanye waogopwe na chama chako mara mia zaidi ya ilivyo sasa. Mwinyi kule Zanzibar ana idea kidogo, lakini bado yuko very mediocre
 
Tukitazama nchi kama Afrika ya kusini, India, na Brazil n.k nao pia walikuwa na na hii hii MGR na hawakuitelekeza waliendelea nayo kwa sababu ilisupport reli mpya zao.

India wakaenda mbali zaidi kujenga hadi Broad gauge ambayo ni kubwa zaidi kwa hiyo ya SGR (1435mm) ambayo ni 1676mm, kwahiyo wanayo meter gauge (1000mm), standard gauge (1435mm) pia hiyo Broad gauge (1676mm) na zinapiga kazi.
Mkuu, hebu labda utufahamishe nini hasa faida ya kuwa na hizo reli zenye ukubwa tofauti, kama unavyosema India. Inawasaidia nini kuwa na reli SGR 1435 na hiyo ya 1676?

Halafu ndio utufahamishe sasa kwa nini tuwe na SGR na hii ya zamani, au hasara ya kuwa na SGR peke yake itakuwa nini, hasa ikiwa zote SGR na hiyo ya zamani zote nzinaenda sehemu zile zile, Mwanza na Kigoma
 
I
Lakini reli siku zote ni kitu cha muda mrefu, hatutegemei muundo wa reli utabadilika katika miaka 50 ijayo kwamba wote tuende kwenye bullet trains. Kwa hiyo hakuna baya juu ya hili la SGR kuwa mpango wa muda mrefu, ila ni huu mkoroganyo kidogo wa mabehewa na SGR Vs reli ya zamani
Inatakiwa uwe mpango wa muda mrefu, ila hawana ndio maana hatuelewi...kwa nini reli ya kaskazini isiendelezwe wakati kuna abiria na mrundikano wa malori ya mizigo namanga? Sasa akiibuka rais flani anaweza kusema napo pajengwe SGR!! Haya yanatakiwa kuwepo kwenye mipango ya muda mrefu inayoeleweka!!!
 
Inatakiwa uwe mpango wa muda mrefu, ila hawana ndio maana hatuelewi...kwa nini reli ya kaskazini isiendelezwe wakati kuna abiria na mrundikano wa malori ya mizigo namanga? Sasa akiibuka rais flani anaweza kusema napo pajengwe SGR!! Haya yanatakiwa kuwepo kwenye mipango ya muda mrefu inayoeleweka!!!
Mkuu, jambo jingine nikukumbushe, reli haipaswi kujengwa hata siku moja kwa lengo la kuhudumia abiria. Abiria ni sehemu ndogo sana ya mapato ya reli na inapaswa kuwa huduma tu, ambayo mara nyingi inabidi iwe subsidized na mapato ya huduma ya mizigo. Hatuna uchumi wa kupeleka SGR kaskazini kwa ajili ya abiria kama factor kubwa.

Kama SGR itashindwa kuingiza faida kutokana na mizigo kwa kuwa bado wasafirishaji watapenda kutumia malori badala ya SGR, basi itakufa kabla haijaanza. Na hilo ndio linaua TAZARA

Leo nikiwa Mkurugenzi wa TAZARA, nitamwambia Samia niwekee bandari kavu Mbeya kwa ajili ya Malawi, Zambia, na DRC, na hata Zimbabwe, nitakuonyesha how I can transform TAZARA. Yaani ukiagiza mzigo nje, unaweza kuu-clear Mbeya, na unafanya kuwa lazima mizigo yote ya Malawi, DRC na Zambia kuwa cleared Mbeya. Unachotakiwa kufanya ni fast tracking ya mzigo toka bandari ya Dar kwenda Mbeya - straight from Dar to Mbeya kwa treni ya Tazara, ufike within two days ya kupakiwa Dar.

Tazizo wanasiasa wa CCM ndio wamiliki wa malori ya mizigo. Ukija na huo mpango watakuua.
 
Hata mie ndivyo nilivyoelewa mwanzoni; SGR ingeanza na mabehewa ya zamani, kulingana na Samia. Lakini sasa naona mabehewa ya zamani ni ya reli ya zamani, kitu ambacho naona ni kama jambo jipya

Something is not adding up na hakuna aliye jasiri kusema ukweli
Kwa hiyo sgr imeanza na hujaona mabehewa ya zamani!?
 
Kwa hiyo sgr imeanza na hujaona mabehewa ya zamani!?
SGR imeanza? Mie sijui kwa kweli. Ila najua Samia alisema SGR itaanza na mabehewa ya zamani kabla ya mapya kukamilishwa kutengenezwa. kitu ambacho nimesema hapo juu was bad planning. Plan ilitakiwa by the time unamaliza SGR kwa ajili ya kuanza operation order ya kwanza ya mabehewa iwe tayari imekamilishwa. Tunaita synchronization in project implementation
 
SGR imeanza? Mie sijui kwa kweli. Ila najua Samia alisema SGR itaanza na mabehewa ya zamani kabla ya mapya kukamilishwa kutengenezwa. kitu ambacho nimesema hapo juu was bad planning. Plan ilitakiwa by the time unamaliza SGR kwa ajili ya kuanza operation order ya kwanza ya mabehewa iwe tayari imekamilishwa. Tunaita synchronization in project implementation
Hela ya kununua mapya' unayo!?
 
Hela ya kununua mapya' unayo!?
Aaah bwana, huko unaenda gizani na unaturudisha nyuma. Tangu mwanzo order ilitolewa kuagiza mabehewa mapya na ya zamani, hilo halina ubishi. Kuna wakati tatizo lilikuwa kuona kwamba design ya mabehewa yaliyosemwa ni mapya ni ya kizamani, na ikafafanuliwa kuwa ni kweli ni ya kizamani kwa sababu sio mapya. Mabehewa mapya mengi yanakuja kama train set, sio behewa moja moja.
 
Aaah bwana, huko unaenda gizani na unaturudisha nyuma. Tangu mwanzo order ilitolewa kuagiza mabehewa mapya na ya zamani, hilo halina ubishi. Kuna wakati tatizo lilikuwa kuona kwamba design ya mabehewa yaliyosemwa ni mapya ni ya kizamani, na ikafafanuliwa kuwa ni kweli ni ya kizamani kwa sababu sio mapya. Mabehewa mapya mengi yanakuja kama train set, sio behewa moja moja.
Wamesema tutaanzia makuukuu,shida nini!?
 
Back
Top Bottom