Bado sijaelewa jambo moja: Hivi tunataka kuendesha SGR sambamba na reli ya zamani?

Bado sijaelewa jambo moja: Hivi tunataka kuendesha SGR sambamba na reli ya zamani?

Kuna kila dalili kwamba SGR itakapokamilika bado tutakuwa na reli ya zamani ikitoa huduma. Hapo mwanzo nilifikiri kwamba reli ya zamani itaendelea kutoa huduma kwa matawi ya Tabora - Mpanda, na labda Dar -es Salaam kwenda Tanga, Moshi na Arusha, ambako sijasikia lolote juu ya kuwepo kwa SGR.

Lakini kila habari zinapotolewa, sisikii hili likiwekwa wazi. Ninasikia tu kuhusu SGR sambamba na reli ya zamani, na manunuzi yakifanywa kwa ajili ya reli zote mbili.

Kwa nini tuendelee kuhudumia na kuwekeza kwenye reli zote mbili? Ni kupanua wigo wa huduma katika bei, kwamba SGR iwe kwa mabwana na reli ya zamani watwana?

Ninachelea kwamba uwepo wa SGR utafanya reli ya zamani iendeshwe kwa hasara iwapo tutaendelea kuitumia. Nilidhani labda SGR ikikamilika reli ya zamani itauzwa kama vyuma chakavu.

Labda ni ule uswahili wetu tu wa kiafrika, tunaendelea kutaka kumiliki vitu vya zamani, tunashindwa kuvitupa hata kama tumenunua kitu kipya mbadala
Na kwa kweli sijui kama utapata jibu kutoka kwa wahusika kueleza haya uliyoweka hapa.

Kama kutakuwepo na ushindani kati ya hizi reli mbili kuendeshwa kwa pamoja, maana yake ni kwamba hapatakuwepo na ufanisi katika zote mbili, kwa sababu hakuna pato litakaloweza kupatikana kufanikisha uendeshaji wa zote mbili kwa pamoja.

Na kama ulivyoelezea vizuri kabisa, juhudi za kuimarisha 'meter gauge' zingehamishiwa kwenye hayo maeneo ambako bado hapajawa na mipango ya kujenga SGR, ili reli hiyo ifanye kazi vizuri zaidi katika maeneo hayo.

Haya tunayoyaona sasa hivi ni kama kuchanganyikiwa, na kutotoa uamzi wa moja kwa moja kifanyike kitu gani. Kuchanganyikiwa huku kunachagizwa na wafadhiri toka nje, kama WB wanaoendelea kutoa vipesa mjinga kwa hiyo reli ya zamani. Hapa wahusika bado wana mirija yao, na hawataki kuiachia wakati pesa hiyo bado inatiririka.
 
Kuna kila dalili kwamba SGR itakapokamilika bado tutakuwa na reli ya zamani ikitoa huduma. Hapo mwanzo nilifikiri kwamba reli ya zamani itaendelea kutoa huduma kwa matawi ya Tabora - Mpanda, na labda Dar -es Salaam kwenda Tanga, Moshi na Arusha, ambako sijasikia lolote juu ya kuwepo kwa SGR.

Lakini kila habari zinapotolewa, sisikii hili likiwekwa wazi. Ninasikia tu kuhusu SGR sambamba na reli ya zamani, na manunuzi yakifanywa kwa ajili ya reli zote mbili.

Kwa nini tuendelee kuhudumia na kuwekeza kwenye reli zote mbili? Ni kupanua wigo wa huduma katika bei, kwamba SGR iwe kwa mabwana na reli ya zamani watwana?

Ninachelea kwamba uwepo wa SGR utafanya reli ya zamani iendeshwe kwa hasara iwapo tutaendelea kuitumia. Nilidhani labda SGR ikikamilika reli ya zamani itauzwa kama vyuma chakavu.

Labda ni ule uswahili wetu tu wa kiafrika, tunaendelea kutaka kumiliki vitu vya zamani, tunashindwa kuvitupa hata kama tumenunua kitu kipya mbadala
Kwani hauoni vitu vya zamani vinaozea store na kama vingeuzwa serikali ingepata kipato.
 
Kwani hauoni vitu vya zamani vinaozea store na kama vingeuzwa serikali ingepata kipato.
Tatizo ni kwamba serikali haina chombo cha kuuza vitu vya zamani. Zamani tulikuwa na kitu kinaitwa State Trade Company (STC), na GAPEX ndio waliuwa kampuni za serikali za kufanya biashara ndani na nje, wakaziua
 
Kumbe unalilia nini!?
Aaah, kumbe ulidhani nalia, mie silii, nimeuliza swali tu, tutaendesha SGR na reli ya zamani kwa pamoja? Sasa kama una jibu eleza, kama huna acha kujibu maswali ambayo hayajaulizwa au kurukia conclusions
 
Najua ndivyo wengi wanafikiri, lakini amini nakuambia, usidhani ukiwaleta Chadema au ACT sijui basi hiyo ndio dawa ya maendeleo. Binadamu ni wale wale, wawe CCM, Chadema au ACT hata TLP. Niambie ni nchi gani duniani imepiga hata kubwa ya maendeleo kwa kuwa tu walibadilisha chama tawala. Zambia? Kenya? USA? Uingereza? Brazil? Malawi?

NI kawaida kudhani mchezaji alie benchi atafanya vizuri zaidi, lakini huwezi hata siku moja kuwa na huo uhakika. Inaweza itokee, inaweza isitokee.

Ndio maana siku zote nimesema, siri ya kuifanya angalau Tanznia iendelee, sio lazima Chadema wachukue nchi, bali ni kufanya vyama vya upinzani viwe na wabunge wengi kwa pamoja, ikiwezekana kuliko hata idadi ya wabunge wa CCM

Mie nilisema raisi atakaekuja kuwa mzalendo wa kweli wa Tanzania mwenye kuitakia maendeleo Tanzania ni yule atakaeimarisha upinzani nchini, sio anaeimarisha Chama chake dhidi ya upinzani. Na kwa hili nawakosoa wote waliokuwa maraisi tangu mfumo wa vyama vingi uanze - Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na hata Samia. Wote wameiangusha sana nchi hii na hakuna mzalendo wa kweli kati yao. Porojo tu zimewajaa lakini sio wazalendo hawa wote, wapigania tonge kwa sababu ni wapigania vyama vyao badala ya nchi yao.

Kama Samia angenisikiliza, ningemwambia kama kweli una uchungu na hii nchi, wapaishe wapinzani, wafanye wawe popular na kuheshimika nchini, wafanye waogopwe na chama chako mara mia zaidi ya ilivyo sasa. Mwinyi kule Zanzibar ana idea kidogo, lakini bado yuko very mediocre
Wewe ni mpumbavu Tu aliingia Magufuli MTU mmoja tulisahau maji kukata, umeme kukata, barabara tuliziona.

Shwain

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Wewe ni mpumbavu Tu aliingia Magufuli MTU mmoja tulisahau maji kukata, umeme kukata, barabara tuliziona.

Shwain

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Sawa. Mie ni mpumbavu. Hongera basi wewe mwerevu ulienizidi. Lakini bado Magufuli amekufa kama alivyokuwa akiua wengine. Alikowapeleka ndiko alikoenda. Huo ndio ukweli ambao werevu kama wewe wanapaswa kuelewa na kumsahau kwa sababu hatarudi ili mnufaike kwa kupendelewa na kuumizwa kwa watu wengine kama mlivyokuwa mmezoea
 
Aaah, kumbe ulidhani nalia, mie silii, nimeuliza swali tu, tutaendesha SGR na reli ya zamani kwa pamoja? Sasa kama una jibu eleza, kama huna acha kujibu maswali ambayo hayajaulizwa au kurukia conclusions
Kama unaona reli ya zamani inafanyiwa ukarabati mkubwa na kununuliwa mabehewa,Hilo linakua swali la msingi kweli!?
 
Binafsi naona ni tija kuoperate reli zote sambamba. Reli iliyopo ni nzima inafanya kazi, ni cheaper kuoperate na inaongeza transit capacity, itaendelea kuissupport SGR mpaka iwe fully operational, inaweka uingiliano/compatibility na reli zingine mf TAZARA pia ni backup ikitokea tatizo kwenye SGR. Sababu zipo nyingi kuendelea kuwa nayo.
Kabla ya kuandika hayo, fahamu haya.
1. Gharama za kuendesha reli ya zamani ni kubwa kuliko faida itokanayo na mapato yake.

2. Faida ya SGR itaanza kuonekana pale tu ubebaji wa mizigo utakapokuwa mkubwa kufikia uwezo wake wa juu. (Wataalamu wanasema hilo lengo huenda likafikiwa miaka 20 ijayo ikiwa mazingira ya uchukuzi wa mizigo yatazidi kuwa bora zaidi ya sasa)

3. Matumizi ya reli ya zamani kusafirisha mzigo na abiria yako chini kuliko uwezo wake (Underutilized).

4. Lengo la kujenga SGR ni ili kuchukua nafasi ya reli ya zamani.

5. SGR inajengwa kwa pesa za mikopo, na ili kuweza kulipa huo mkopo kwa wakati, ni lazima SGR kuwezeshwa kutumika kwa ufanisi wote.
 
Ndio utajua hakuna viongozi pale, kitu kama mabehewa hata kutoa maelezo ya maana kwamba ni kwa ajiri ya treni ya zamani na sio SGR wameshindwa,ilikuwa ni kitu kidogo sana kueleza ukweli kuhusu yale mabehewa lakini nafikiri hata waowenyewe hawaelewi tofauti au wanafikiri kila mtu fala kama wao kama yule aliyesema juzi vitu vimepanda bei kwa ajiri ya Ukraine
Kama ulishindwa kuelewa utofauti wa yale mabehewa hata kabla hawajatoa maelezo yao basi we jihesabu sio fala tu bali ni bonge la fala..[emoji6], huo ndo ukweli mchungu unless otherwise uwe unachangamsha genge tu.
 
Ingekuwa busara reli ya zamani wangeiweka katika standard za SGR.

Tungenunua mabehewa aina 1 tu sio sasa tunapambana na vitu viwili vitakavyotushida.
 
Inabidi uwe na akili za mwenda wazimu kudhani kwamba kuna kiongozi yeyote wa Tanzania ataongoza nchi bila kukiuka katiba ya Tanzania; si Mwinyi, si Mkapa, si Kiwete, Si Magufuli, si Samia si yule atakaekuja
Duh!
hili nalo ni sehemu ya mada hii nzuri?
Sidhani kama nitawalaumu kwa hilo. Hata mie ningefanya hivyo hivyo katika positions zao. Hiyo ndio reality.
Na hili?

Inasikitisha sana!
 
Kama unaona reli ya zamani inafanyiwa ukarabati mkubwa na kununuliwa mabehewa,Hilo linakua swali la msingi kweli!?
Linakuwa swali la msingi kwa sababu natarajia ufikirie zaidi ya swali. Linakuwa kama rhetoric question kwa ajili ya kukufanya ufikirie kitu unachofanya, kwamba kina walakini. Ni sawa na mtu unaaga kwenda mahali, unataka kuzamia South, na mtu anakuuliza hivi umeamua kwenda South kweli? That is a figurative question.

Kwa hiyo basi, ili nikuonyeshe mbali ya swali langu ni kwamba ninachouliza ni kwamba what is the point ya kuwa na SGR na reli ya zamani at the same time, hasa ukiangalia operational costs. Kwa nini hatukuchagua one or the other? Kuna upembuzi makini umefanywa kuangalia cons and pros za ku run reli zote mbili, ambazo literally zinaenda destination zile zile?

In fact, siku zote nimefikiria kwamba tuna-maintain reli ya zamani kwa mipango ya baadae kuifanya iwe track ya pili ya SGR ili treni ziwe zina run unidirectional, yaani SGR ya kwenda na SGR ya kurudi. Kwa hiyo nilitarajia majibu around that context
 
Linakuwa swali la msingi kwa sababu natarajia ufikirie zaidi ya swali. Linakuwa kama rhetoric question kwa ajili ya kukufanya ufikirie kitu unachofanya, kwamba kina walakini. Ni sawa na mtu unaaga kwenda mahali, unataka kuzamia South, na mtu anakuuliza hivi umeamua kwenda South kweli? That is a figurative question.

Kwa hiyo basi, ili nikuonyeshe mbali ya swali langu ni kwamba ninachouliza ni kwamba what is the point ya kuwa na SGR na reli ya zamani at the same time, hasa ukiangalia operational costs. Kwa nini hatukuchagua one or the other? Kuna upembuzi makini umefanywa kuangalia cons and pros za ku run reli zote mbili, ambazo literally zinaenda destination zile zile?

In fact, siku zote nimefikiria kwamba tuna-maintain reli ya zamani kwa mipango ya baadae kuifanya iwe track ya pili ya SGR ili treni ziwe zina run unidirectional, yaani SGR ya kwenda na SGR ya kurudi. Kwa hiyo nilitarajia majibu around that context
Brazil na India wanazo zote na zinafanya kazi pamoja,hiyo mgr sisi tunaoenda tabora miaka na miaka tunajua usumbufu wa ukifika station flani mnakaa kusubiri aidha treni ya abiria au mizigo ifike mlipo mupishane,aidha tunafanya upanuzi na kuongeza efficiency ya bandari ya dar na kujenga bmoyo,sgr peke yake haitoshi kwa namna shughuli za kiuchumi zinavyokua kwa nchi tunazozihudumia kupitia bandari
 
Duh!
hili nalo ni sehemu ya mada hii nzuri?

Na hili?

Inasikitisha sana!
Mkuu, nimeshakuambia, you need to be realistic. Kwa nini tu-pretend maraisi wetu wamemuwa wakiongoza kwa kufuata katika kama walivyoapa? Ndio maana nikasema kama unafikiri hivyo basi wewe ni mwenda wazimu, au huijui katiba yetu.

La pili, unafikiri kwa nini hawa kina Masanja wa TRC, kina Mwigulu Nchemba, wanaishia kuonekana wanaongea mambo tofauti na raisi nyakati fulani fulani? Kwa nini wanakuwa kama wana uwoga fulani kuongea ukweli wote kama wanavyoulewa? Ni kwa sababu wanaogopa kuongea kitu ambacho waswahili wanasema "watashushuliwa na raisi". Samia ni mtu wa vijembe sana, kama hujui basi hujui kusoma watu. Labda ni silka ya Wazanzibar, lakini kuna watu hiyo tabia inawakera.

Unakumbuka Raisi Samia alichomfanyia Prof. Mkenda? Sasa that set a precedent ya uoga kwa wateule wote wa raisi Samia. Hawako confident tena kueleza kile wanachoelewa ili Samia asije kuwaumbua kama alivyomfanyia Prof. Mkenda. Niliandika humu JF, kwamba Samia alikuwa very unwise kwa jinsi alivyo react kwenye kauli ya Prof. Mkenda, na nilitamani she could be bigger (wiser) than that. Ndio maana hata mimi, kwa jinsi ambavyo sasa nimemsoma Samia, nasema ningefanya hivyo hivyo, kwa sababu alternative ni nini, kuachia ngazi? Kwa hiyo, sometimes all you need is to realistic. Msome Samia, mwelewe, na caress her ego, as long as hufanyi madhambi.
 
Ni sawa na uwepo wa mwendokasi na daladala za kawaida hapo mjini Dar
 
Najua ndivyo wengi wanafikiri, lakini amini nakuambia, usidhani ukiwaleta Chadema au ACT sijui basi hiyo ndio dawa ya maendeleo. Binadamu ni wale wale, wawe CCM, Chadema au ACT hata TLP. Niambie ni nchi gani duniani imepiga hata kubwa ya maendeleo kwa kuwa tu walibadilisha chama tawala. Zambia? Kenya? USA? Uingereza? Brazil? Malawi?
siamini kuwa wewe huoni tofauti ya sisi na CCM yetu, na wao na vyama mbalimbali vilivyoweza kushika madaraka.
Umateka uliowekwa na CCM, kwamba huwezi kamwe kuwaondoa madarakani umekuzima akili kabisa?
 
Ni sawa na uwepo wa mwendokasi na daladala za kawaida hapo mjini Dar
Hapana, si sawa, kwa sababu ukiondoa daladala kwa kuwa una mwendo kasi huwezi kukidhi demand ya usafiri Dar, na hata zote kwa pamoja bado hazikidhi
 
Back
Top Bottom