Bandari na DP World: Dkt. Slaa asema ni uuzaji wa Nchi. Adai Serikali iliyopo ina uhalali wa wasiwasi
Bandari ni suala la muungano kwa mujibu wa Katiba. Kuna DG wa Bandari wa Tanzania na huko Zanzibari kuna DG. Sasa anahoji huyo wa Zanzibar yupo kwa mujibu wa katiba ipi? Maana yake Zanzibar amekwapua madaraka na kuvunja katiba
Nice question,tusubirie majibu
 
Huyu Samia kwa mara ya kwanza nadiriki kusema ni kiongozi asiyefaa hata kidogo

Kwenye picha kubwa ni asilimia mia moja hajali chochote kuhusu Tanganyika mbaya zaidi wale waliomleta kwenye siasa za Tanganyika wanamuunga mkono kwasababu wanafaidika na maamuzi yake yanayohusisha ufisadi mkubwa ikiwemo kuuza nchi! Ukiuza bandari,ukiuza loliondo ukiruhusu madini yatoroshwe wewe umepiga mnada Tanganyika huna tofauti na muhujumu uchumi yule seth
Kuna genge moja hatari sana nyuma yake
 
Serikali ya awamu ya nne wakati inataka kutaifisha mashirika muhimu ikiwemo bandari, aliyetupa taarifa alifukuzwa kazi. Alitupa taarifa ya kutokubali kuyataifisha kutokana umuhimu wake kwa usalama wa Taifa.
Dkt. Slaa ameongelea mfano wa mbia katika kampuni ya mafuta wakati wa vita ya Uganda ambapo Tanzania ilikuwa inamiliki 51% katika kampuni hiyo huku mbia akiwa na 49% lakini aliweka ngumu kwasababu alidai mtu tunayepigana nae ni mbia wake pia hivyo. Slaa amedai kwa siku 5 vifaa havikuweza kuondoka kwasababu ya mafuta wakati nchi inaendelea kupigwa.
Hali ya hewa ya leo inasoma kivingine, hivi vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya kazi gani nchi inapouzwa mchana kweupeee tena na watu wawili kutoka nchi jirani
 
Back
Top Bottom