Barabara ya Mwendokasi kutoka Maktaba hadi Tegeta kuanza kujengwa, Ubungo Kimara kufumuliwa

Barabara ya Mwendokasi kutoka Maktaba hadi Tegeta kuanza kujengwa, Ubungo Kimara kufumuliwa

Kabla ya nyingine ubungo Hadi kimara ,si wange endelea kibaha mpaka mlandizi ,mdogo mdogo mpaka chalinze,kunatisha ajali kila siku,Barabara mbovu magari mengi
Halafu matochi kibao ni kama hawapendi mpite hizo 6 line.
Nauliza tu kauli ya mkandarasi anakuja kipande cha moro chalinze njia mpya ataanza lini.
 
Hiyo ya Ubungo-Kimara njia 8 imekaa vizuri sana

Ina maana hapo itakuwa njia 8 Ubungo mpaka Kibaha

Nashauri serikali wasiishie tu Ubungo wajenge tena njia 8 kutoka Ubungo hadi Kivukoni (Hapo itakuwa ni njia 8 kutoka Kivukoni hadi Kibaha)

Nimeona manufaa ya njia 8 ukipita barabara ya Kimara hadi Kibaha hakuna foreni kabisa siku hizi
 
Hiyo ya Ubungo-Kimara njia 8 imekaa vizuri sana

Ina maana hapo itakuwa njia 8 Ubungo mpaka Kibaha

Nashauri serikali wasiishie tu Ubungo wajenge tena njia 8 kutoka Ubungo hadi Kivukoni (Hapo itakuwa ni njia 8 kutoka Kivukoni hadi Kibaha)

Nimeona manufaa ya njia 8 ukipita barabara ya Kimara hadi Kibaha hakuna foreni kabisa siku hizi
Bomoa bomoa itakuwa sio ya kitoto

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Barabara za mabasi ya mwendo kasi haziwezi kuwa suluhisho la foleni ya magari dar , ni very short term project na baada ya miaka kadhaa mbele tutakuja kuvunja tena hizi barabara na kujenga kile ambacho first world wanafanya .
Public roads zinatakiwa ziboreshwe na sio ku priotize category fulani ya usafiri kama tunavozipa kipaumbele mwendokasi.
Wenzetu Kenya hili wameliweza .
 
Kwa ufupi sana

Serikali ya Tanzania kupitia Tanroads leo 30 Juni 2023 inasaini Mikata Minne ya ujenzi wa miundombinu ya Usafiri wa haraka wa Mabasi (BRT) awamu ya nne.

Inaanza kujenga barabara ya Magari yaendayo haraka kutoka Katikati ya Mji (Maktaba) hadi Tegeta, ambayo itajengwa na Wakandarasi wawili. Mmoja kutoka Maktaba kadi Morocco na mwingine kutoka Morocco hadi Tegeta ikiwemo ujenzi Madaraja.

Pia Serikali imesaini Mkataba wa upanuzi wa barabara ya Morogoro kutoka Ubungo hadi Kimara kuwa ya njia nane kutoka Njia sita za sasa.

Pia inasaini Mkataba wa barabara Vikawe kutoka Mapinga hadi kuunganisha barabara ya Dar Morogoro na ile ya Dar Bagamoyo

Ipo hivi:

1. Mkataba wa kwanza ni Km 13 kutoka Maktaba hadi Mwenge then inakata Kona hadi Ubungo kupitia barabara ya Sam Njuma

2. Mkataba wa pili ni Ujenzi wa barabara ya Mwendokasi kutoka Mwenge hadi Tegeta km 15. 63.

3. Mkataba wa tatu ni kwamba pale Mbuyuni kutajengwa kituo, Simu 200 patajengwa kituo na Kivukoni Terminal watajenga kituo hizi ni Depot. Zitajengwa na Mkandarasi mmoja.

4. Upanuzi wa Barabara Ubungo hadi Kimara kuwa ya Njia nane badala njia 6 za sasa

5. Mkataba mwingine ni barabara kiwango cha lami kutoka TAMCO Vikawe Mapinga km 23 na sehemu ya Pili Pangani hadi Mapinga km 13.59

Stay tuned


=====
View attachment 2674688
Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Mohamed Besta leo tarehe 30 Juni 2023, akisaini mkataba kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkandarasi kutoka Kampuni ya China Geo – Engineering Corporation ya China kwa ajili Ujenzi wa Miundombinu ya barabara yenye urefu wa Km. 13.5 kuanzia Maktaba ya Taifa mpaka Mwenge ikijumuisha kipande cha Barabara ya Sam Nujoma kutoka Mwenge mpaka Ubungo.

Mkataba pia unahusisha upanuzi wa Daraja la Selander, Uenzi wa Vituo Vikuu Viwili vya Mabasi, Vituo vya Kawaida vya Mabasi Ishirini (20) na Vituo Mlisho (Feeder Station) kumi (10).

Mkataba huu ni wa gharama ya Shilingi 174,380,157,323.00, na umepangwa kukamilika katika muda wa miezi 18.
View attachment 2674690View attachment 2674691
Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Mohamed Besta leo tarehe 30 Juni 2023 akisaini mkataba kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ya barabara yenye Urefu wa Km 15.63 kuanzia Mwenge mpaka Tegeta.

Mkataba huu pia unahusisha upanuzi wa Madaraja matatu, (Mlalakuwa, Kawe na Tegeta), Ujenzi wa Vituo Vikuu vya Mabasi, Vituo vya Kawaida vya Mabasi Kumi na Tisa (19) na Vituo Mlisho (feeder station) Vitano (5).

Mkandarasi aliyeshinda kutekeleza mradi huo ni Kampuni ya Shandong Luqiao Group Co., Ltd kutoka China kwa gharama ya Shilingi 193,855,936,443.00, Ujenzi umepangwa kukamilika katika muda wa miezi 18.
View attachment 2674694View attachment 2674695View attachment 2674696
Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Geofrey Kasekenya akishuhudia Utiaji Saini wa Mikataba Minne ikiwemo Ujenzi wa Karakana (Depot) Mbili na Kituo Kikuu cha mabasi kimoja.

Mikataba hiyo imesainiwa leo tarehe 30 Juni 2023 na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Mohamed Besta kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar- es Salaam.

Mkandarasi aliyeshinda tuzo ya Ujenzi huo Kampuni ya China Communications Construction Company Ltd kutoka China kwa gharama ya Shilingi 60,984,151,987.18, Ujenzi umepangwa kukamilika katika muda wa miezi 18.
View attachment 2674700View attachment 2674701
Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Geofrey Kasekenya akishuhudia utiaji saini wa mikataba minne ikiwemo Ujenzi wa Karakana (Depot) Mbili na Kituo Kikuu cha mabasi kimoja.

Mikataba hiyo imesainiwa leo tarehe 30 Juni 2023 na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Mohamed Besta kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar- es Salaam.

Mkandarasi aliyeshinda tuzo ya Ujenzi huo Kampuni ya China Communications Construction Company Ltd kutoka China kwa gharama ya Shilingi 60,984,151,987.18. Ujenzi umepangwa kukamilika katika muda wa miezi 18.
View attachment 2674702View attachment 2674703
Serikali kupitia TANROADS imesaini mkataba wa Uenzi wa Barabara ya TAMCO – Vikawe hadi Mapinga kwa kiwango cha lami, sehemu ya Pangani hadi Mapinga (Km 13.59).

Mkataba huo umesaini leo tarehe 30 Juni 2023 katika ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar- es Salaam na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Mohamed Besta kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya.

Taarifa ya Mtendaji Mkuu TANROADS imesema aliyeshinda tuzo ya utekelezaji wa mradi huo ni Kampuni ya Kings Builders Ltd ya Tanzania, Mradi utajengwa kwa gharama ya Shilingi TZS 17,859,098,225.00, Muda wa utekelezaji wa mradi ni Miezi 12.

Barabara hiyo ina jumla ya km 22, inaanzia katika Mji wa Kibaha ambapo ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani inakwenda hadi Mapinga katika Wilaya ya Bagamoyo

Aidha Barabara hiyo ni kiungo muhimu kati ya barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Kilimanjaro, Arusha na Tanga kupitia Bagamoyo.

Hata hivyo Mhandisi Mohamed Besta ameeleza kuwa kwa kutambua umuhimu wa barabara hiyo serikali ilielekeza kuanza Ujenzi wa Sehemu ya Kwanza yenye urefu wa km 8.41. Ujenzi ulianza mnamo mwaka 2013/14 na maendeleo ya mradi yamefikia asilimia 40%.
View attachment 2674706
Tuna shindwa nn kutrain watu wetu rather kutegemea nje
 
Kabla ya nyingine ubungo Hadi kimara ,si wange endelea kibaha mpaka mlandizi ,mdogo mdogo mpaka chalinze,kunatisha ajali kila siku,Barabara mbovu magari mengi
kweli kabisa. Kibaha-chalinze ni eneo hatarishi sana.

Pia, kwa mwenendo wa BRT ya sasa, ni bora serikali itafute mwendeshaji binafsi wa BRT, mwekezaji wa ndani kama mwanzoni ilivyokuwa maxcom walipoinstall hata ile mitambo na wakaanzisha malipo ya kadi. Waliopo sasa wamefeli sana, kazi imewashinda. Ikiwa kimara -kivukoni-moroko-gerezani imewashinda hivi. Njia zingine za tegeta, mbagala, gongo la mboto zikianza wataweza?
 
Mama hii miradi yako ni heavy, tuliona hapa bwana yule akitujengea kibarabra cha cha pale Mwenge kwa kuwakamua pesa zao wabunge.

Leo umeamuwa mama. Jioneeni"




Jamani hii ni mi Dirham ya Dubai nini?

Yes ni mambo ya DP, Baada ya kununua bandari wamesema hawataki foleni kabisa kontenna zao zinatakiwa zipite kwa kasi ambayo hata TRA hawataona zimepitia wapi.
 
Hiyo ya Ubungo-Kimara njia 8 imekaa vizuri sana

Ina maana hapo itakuwa njia 8 Ubungo mpaka Kibaha

Nashauri serikali wasiishie tu Ubungo wajenge tena njia 8 kutoka Ubungo hadi Kivukoni (Hapo itakuwa ni njia 8 kutoka Kivukoni hadi Kibaha)

Nimeona manufaa ya njia 8 ukipita barabara ya Kimara hadi Kibaha hakuna foreni kabisa siku hizi
Hiyo sahau haitakaa iwezekane, hv huoni tuu Barabara ya mwendokasi ilivyopita pale kisutu mpaka kuja kutokea huku Posta ya zamani kwa kuforce, Sasa hizo njia SITA zitapita wap mpaka kivukoni
 
Barabara za mabasi ya mwendo kasi haziwezi kuwa suluhisho la foleni ya magari dar , ni very short term project na baada ya miaka kadhaa mbele tutakuja kuvunja tena hizi barabara na kujenga kile ambacho first world wanafanya .
Public roads zinatakiwa ziboreshwe na sio ku priotize category fulani ya usafiri kama tunavozipa kipaumbele mwendokasi.
Wenzetu Kenya hili wameliweza .
Hakuna mji wenye foleni mbaya kama Nairobi hapa east Africa...wenyew wanatamani hata wawe na mwendokasi....
Kuna muda ukifika pamoja na barabara zao pana cbd ya Nairobi haifikiki kabisa...

BRT ni solution nzr tu....na baadae wanawwza fikiria kuweka trams kwenye hizo njia za mwendokasi....

Nairobi wanaifata marekani ambako miji yake ina foleni hatari...Dar inaifata Europe ambao miji yao ina brt, trams na subways na siku hiz hadi baiskeli kabisa...na actually Europe iko vzr kimaendeleo kuliko us

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Hakuna mji wenye foleni mbaya kama Nairobi hapa east Africa...wenyew wanatamani hata wawe na mwendokasi....
Kuna muda ukifika pamoja na barabara zao pana cbd ya Nairobi haifikiki kabisa...

BRT ni solution nzr tu....na baadae wanawwza fikiria kuweka trams kwenye hizo njia za mwendokasi....

Nairobi wanaifata marekani ambako miji yake ina foleni hatari...Dar inaifata Europe ambao miji yao ina brt, trams na subways na siku hiz hadi baiskeli kabisa...na actually Europe iko vzr kimaendeleo kuliko us

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Hoja yangu sio kupinga barabara za brt , bali namaanisha barabara hizo sio suluhisho la foleni mjini hapa , Nairobi ina foleni kwa sababu mji wa wenyewe ni mdogo ililinganisha na dar na huwezi kulinganisha infrastructures za Kenha na Tanroad .
Hizi barabara baada ya miaka 10 tutakuja kuvunja tena! amini nakwambia.
 
Back
Top Bottom