Barakoa yawa vazi rasmi Ikulu

Barakoa yawa vazi rasmi Ikulu

Hawezi kufunga mipaka kwa sababu yeye na jiwe ni kitu kimoja....Hahahha

Na alipowaambia hivyo mkakenua memo yote nje.
mnadhani urais ni kelele!!!
20210511_113843.jpg
 
Mimi nitairoga maana hiyo si nia njema, lengo ni kututia hofu ili mwishowe walete chanjo kiulaini na kupiga mpunga huku wakituua taratibu, no way, anacheza ngoma asiyoijua inayopigwa na hayo mabeberu, au la wamemtisha akatishika, udhaifu kitu kibaya sana, tunarudi wnzi za Msoga sasa za Mr.Dhaifu
Mkuu chanjo zote ulizopata utotoni zimetengenezwa Tanzania?

Hofu unajitia mwenyewe kama utaruhusu iwe hivyo. swala la chanjo halina mjadala, sisi tupo tayari kwa maamuzi yeyote atakayochukua mama kwa sababu tumeipima dhamira yake na imeonekana kua NJEMA tofauti na mtangulizi wake. Maelfu ya watanzania wanasubiri chanjo ili waende KUHIJI.

Kaa kwa kutulia mama anafungua nchi wadogo zetu waliomaliza vyuo vikuu na sasa wanafanya kazi ya boda boda wapate ajira. ondoka katika kivuli cha mwendazake ishi katika uhalisia, zama zimebadilika. tushirikiane kumsapoti mama ili atufikishe salama.
 
Asalamaleko!

Mimi ninaishi Dar es salaam maeneo yenye kusongamana sana.

Watu ni wengi mno na wanapumuliana uso kwa uso kwa namna ambayo endapo kungekuwa na gonjwa la mlipuko basi wangekufa wote kama kuku wenye mdondo.

Huku sijasikia mtu yeyote aliyekufa kwa corona. Hakuna hata sisimizi aliyekufa.

Lakini tunaona Bibi Samia amejivika mibarakoa mikubwa usoni kama afisa-mazingira.

Ndio kusema kwamba, anajikinga na corona?

Halafu inaonekana corona inachagua mahali rasmi pa kupiga kambi. Kwa sasa corona imehamia ikulu!

Kama ambavyo dunia nzima imepata nafuu na maisha yameanza kurejea katika hali ya kawaida, kirusi huyu wa corona tunaambiwa amehamia India.

Kote kwingine duniani, corona amefifia na kufa makali, kakimbilia kwenda India kuweka makazi.

Huyu Kirusi ana akili sana. Sasa hivi hayupo Kariakoo wala Manzese wala Buza. Kakimbilia kwenda kujificha Ikulu.

Wow! What an intelligent virus! Anajua mahali pa kukaa. Anahama kule anahamia huku tena kwa ratiba rasmi kabisa.

Leo yupo Marekani, kesho anahamia South Africa, Kesho kutwa anahamia India. A very systematic virus!

Chanjo zinakuja lini?

Halafu pia lockdown itaanza lini?

Huyu kirusi akitoka magogoni akihamia hapa Kariakoo itakuwaje!?

Tunahitaji hatua madhubuti zichukuliwe mapema!

Kila mtu avae mabarakoa na kujitakasa mikono!

IMG_20210511_114001_584.JPG
 
Uko sahihi barakoa kwanza inasababisha Corona
sababu binadamu tunatoa hewa chafu tunapopumua NJE hiyo hewa chafu inaitwa carbon dioxide.Halafu tukivuta hewa ndani tunaingiza hewa safi ya oxygen,Sasa ukivaa barakoa haina matundu makubwa ya kutoa hewa chafu unapopumua hivyo haitoki yote sababu inashindwa kupenya kwenye matundu ya barakoa na ukivuta kuingiza ndani hewa safi ya oxygen nayo inakumbana na kizuizi cha barakoa inashindwa kupenya vizuri kuingia ndani

Matokeo yake inakutana ndani hapo na mabaki ya carbon dioxide ambayo imesalia kwa kushindwa kupita vizuri kwa hiyo inatengezwa hewa mpya ambayo ni muunganiko wa oxygen (o2) na carbon dioxide (co2) ambapo huzaliwa hewa mpya hataerishi kwa mapafu.Kimahesbu inakuwa hivi

oxygen +carbon dioxide=hewa mpya yenye muunganiko wa oxygen na carbon dioxide

o2+co2=co2

Hiyo hewa mpya unaivuta kuiingiza ndani ya mapafu matokeo yake unaanza kupata matatizo ya kupumua ambayo ndio corona yenyewe.Ndio maana nchi za wavaa barakoa Corona haaishi inazidi tu kuongezeka
Hahahaha...Dah, Hizi ndio akili za Mataga.
 
Urais si kelele, na wala sio kula mahindi barabarani na kugawa mapapai huku unawapiga fix Mataga kuwa ATCL inatengeneza faida ya 28bilion kumbe ni mwendo wa hasara kwa miaka yote 5, na cha ajabu Mataga wanaamini na kushangilia.
haya mwezi wa pili sasa yunataka kuona urais ni kitu gani.

mataga wana 5 ubaoni.
mama ana 0 ubaoni.
nyumbu wana 0 mkononi.
 
Hizi barakoa ni N95 maana tunaambiwa ni N95 type of mask ndio yenye uwezo wa kuzuia huyo kirusi asipenye hizi nyingine ni ubishoo tu wa kimarekani.
 
Tulio kwenye daladala na barakoa zetu😷😷😷 tujuane hapa
 
haya mwezi wa pili sasa yunataka kuona urais ni kitu gani.

mataga wana 5 ubaoni.
mama ana 0 ubaoni.
nyumbu wana 0 mkononi.
Kwa hiyo Mataga sasa ndio mmekuwa wapinzani wa serikali ya CCM?

Muda unaenda kasi sana aisee..
 
Uzi nyingine ndo maana zinakuwa na viewers wengi lakini comments chache.

Kwahy unataka lockdown?
 
Inafikirisha. Nadhani wameamua iwe, kufuata ya ugenini, kulala kichwa chini, miguu juu usiulize sababu, kwamba we fuata wanavyofanya wenyeji.
 
Kuepuka hii kadhia na kuwaepusha hawa wazee kuendelea kuteseka kisaikolojia, ni bora wote wenye miaka 61 na kuendelea walio na utayari wapokee chanjo! Not for virus but for psychological relief.
 
Kwa hiyo Mataga sasa ndio mmekuwa wapinzani wa serikali ya CCM?

Muda unaenda kasi sana aisee..
wala si ajabu,balaa ni pale nyumbu wanapohisi faraja jiwe kufariki[emoji1787][emoji1787][emoji1787].

unawaza adui yao alikuwa jiwe ama utawala wa ccm??[emoji23][emoji23]
poor arnimals.
 
Back
Top Bottom