Baraza Jipya la Mawaziri 2020: Hizi ndizo kasoro kuu 3 ninazoziona

Baraza Jipya la Mawaziri 2020: Hizi ndizo kasoro kuu 3 ninazoziona

Waislamu bwana shida tupu.Ungejua hata kwamba Rais hakuwa na mawazo ya udini wala unzanzibari alipokuwa ana-zoom kutafuta mawaziri! I believe he was more interested in professionalism.Be positive,mawazo hasi hayatawafikisha popote,mtajiletea visukari na pressure bure wakati mwenzenu hata hayuko huko.
Kwa taarifa yako you are very wrong what you believe is wrong uteuzi umefanywa kidini purposefully
 
Rais Mkristo
Makamu wa Rais Muislam
Waziri mkuu Muislam
Jaji Mkuu anaemuapisha Rais Muislam
Mkuu wa majeshi Muislamu
Mkuu wa polisi Muislamu
Mkuu wa uhamiaji Muislamu
Mkuu Magereza Muislamu
mkuu wa zimamoto Muislamu
Mkuu wa takukuru Muislamu
 
Haya ya kawaida,nakumbuka kipindi Cha kikwete Kuna mbunge alishawahi kumtuhumu rais ni mbaguzi wa kidini, anajaza waislamu kwenye teuzi zake,mussa zungu akatoa takwimu za mawaziri,naibu waziri wakuu wa mikoa na wilaya na makatibu wakuu ikaonekana mbunge anachoongea hata hakijui maana bado wakristo walikuwa wengi zaidi ya waislamu.tumuache rais achague watu anaoamini watamsaidia katika kufikia malengo yake ya kuwaletea maendeleo wananchi
 
Mimi ni mwislam, ila alieleta mada hii ni Mjinga, unastahili tu kuelimishwa huenda ukaeleimika, ukaondokana na ujinga. Kwa hiyo ulitaka rais achague baraza la mawaziri lenye wakristo 50% na waislam 50%?. Kwa hiyo achague tu kukuridhisha wewe kwa idadi hiyo hata kama watendaji husika hawawezi kazi.......
Utakuwa ni wale waislamu ambao hamjitambui mlioishia kusoma juzuu na kuimba kaswida
Kilichofanyika kwenye uteuzi huu ni ubagudhi wa hali ya juu kwa ndugu zetu waislamu sio kweli katika nchi hii eti hakuna mtanzania muislamu anayeweza kuwa waziri
Wewe Kama ni kweli muislamu utakuwa mpuudhi flani
 
Kwa taarifa yako you are very wrong what you believe is wrong uteuzi umefanywa kidini purposefully
Mna shida kweli kweli,yaani mmejaa ushari tu.Anyway hebu be realistic,hivi akiteua kidini anapata faida gani?Nipe advantages moja,mbili,tatu au hata zaidi.
 
Mna shida kweli kweli,yaani mmejaa ushari tu.Anyway hebu be realistic,hivi akiteua kidini anapata faida gani?Nipe advantages moja,mbili,tatu au hata zaidi.
Embu Google kitu kinaitwa social inclusion ndio utaelewa faida zake
 
Embu Google kitu kinaitwa social inclusion ndio utaelewa faida zake
Shida tupu.Hata hivyo,mbona kuna viongozi wengi tu Waislamu,tena wakubwa,akiwemo Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.Acheni figisu figisu zisizo na maana.Na kama hajaona Waislamu wanaofaa,àfanyeje achukue tu kwa kuwa ni Waislamu?Au je kama hao wanaofaa hawajaingia kwenye radar yake?Narudia tena Waislamu kueni positive,itawapa heshima zaidi.
 
Debate ya waziri gani katoka wapi na ni wa dini gani utaikuta kwenye sh**hole countries tu. Hivi umeshawahi kusikia Wamarekani au Waingereza, kwa mfano, wakijadili secretary gani katoka upande gani wa nchi na ni wa dini gani? Jibu sote tunalijua; hawajadili huu upuuzi, kwa sababu hauna tija kwa taifa!
huelewi the big picture
 
Ofcourse wewe ni muislamu mwenye siasa kali kama zile za alshabaab,ISIS na Boko Haram.
Na pengine wewe ni member wao na uliwahi kusumbua huko Kibiti kabla ya kukimbilia Msumbiji.
Imani ya mtu ni matendo yake.
Mtu anaweza kuwa Joshua ama John lakini ni alshabaab kama wewe na ndugu yako Ruyagwa.
Anaweza pia kuwa Seif lakini ni kafiri kama mnavyopenda kuwaita.
Au wanaweza kuwa mapagani nk.
Sasa imani zao umezitambuaje?
Kwa kuangalia majina???
Hell No!upo wrong sana.
Baraza la mawaziri Zanzibar hakuna hata mmoja mwenye jina la kigalatia lakini watu kimya,ni kwa sababu huko ni siasa na sio sehemu ya kufanyia ibada.
So long as hawabughudhiwi wanaposali basi hata mmoja asipopewa ni sawa tu.
Likewise kwa huku Tanganyika.
Wanasiasa hawana dini,ukinyimwa uhuru wa kuabudu lalamika lakini sio kwenye hili la siasa.
Magu simkubali kwa mengi lakini hili la kuwathibiti alshabaab wa Kibiti namnyooshea mikono.
Na kwa hili pia la kutojali ujinga ujinga wa Udini na ukanda
Kijana hueleweki sijui umekunywa wanzuki wewe duu!!!.
Zanzibar ni nchi yenye waislamu wakazi zaidi ya 98%. Ile ni nchi yenye serikali na mamlaka. Unataka wewe ukawe Waziri nenda ukawe Mzanzibar. Kisha wewe ni mtu wa ajabu. Unashabikia udini na ukanda? Hivi chuoni mambo yanavyoharibika kwa majirani zetu???
 
Heshima yako mkuu
Loftins,

AHADI YA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE KWA WAISLAM 1962

Haiwezekani kuielewa ahadi ya Nyerere katika haki na usawa kwa raia wote kama alivyoahidi wakati wa kudai uhuru, hadi usome hotuba yake aliyoitoa tarehe 10 Desemba, 1962 katika Bunge wakati Tanganyika inakua jamhuri.

Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.

Nyerere alikuwa na haya ya kusema:

‘’Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.’’

Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema kwa Waislam.

Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.

Bila shaka Nyerere alisema maneno haya akitambua mchango mkubwa wa Waislam wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nyerere alisema maneno haya akijua kuwa ingawa yeye alikuwa Rais Mkatoliki lakini Waislam kwa nia ya kuleta umoja wa Watanganyika chini ya TANU na kupigania uhuru hawakusita kumuunga mkono kwa dhati.

Na siku alipoacha uongozi baada ya kutawala kwa robo karne Mwalimu Nyerere katika hotuba yake maarufu ya kuaga aliyotoa Diamond Jubilee Hall alikuwa na haya ya kusema:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.

Sasa nipo katika hali ya kufurahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.

Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.

Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''

Huyu ndiye Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alivyoeleza tatizo la Waislam na jinsi alivyolitatua.

Yapo mengi ambayo yangewezwa kuelezwa kuhusu ukweli wa kauli hii lakini tutosheke na haya.

Leo Waislam wanatatazika na idadi yao katika Baraza la Mawaziri lililo na Waislam 3 dhidi ya Wakristo 20.

Picha ya kwanza kulia ni Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi mwaka wa 1962.

Picha ya pili ni Mshume Kiyate na Julius Nyerere 1964 na picha ya tatu ni kulia Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Iddi Faiz Mafungo wakiwa Dodoma 1956.
Screenshot_20201207-063029.jpg
Screenshot_20201207-063727.jpg
Screenshot_20201207-063855.jpg
 
Duh ukizungumzia MaDED, maDAS , wakurugenzi wa mashirika ya umma, makatibu wakuu, Wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya Huko Waislamu idadi yao ni chache sana pia.

Kiufupi utawala huu unanuka udini ajabu

Huko Zanzibar kuna wakisto wangapi kwenye baraza la mawaziri la Hussein Mwinyi? Siungi mkono Uteuzi wa mawaziri wa JIWE usiozingatia umoja wa nchi yetu; haingii akilini kwa wilaya moja ya IRAMBA kutoa mawaziri watatu as if hakuna wananchi toka sehemu zingine za nchi wanaostahili kuteuliwa!!!
 
Huwa mnaungana pamoja na kuteteana kwenye maslahi ya watu wa dini yenu.

Nahisi ningeishia kutaja wanawake na wazanzibar peke yake mgeunga mkono hoja, ila kitendo cha kutaja kuhusu umuhimu wa kuwepo kwa notable inclusiveness ya waislamu kwenye baraza mmeona hii mada haijakaa sawa hahaha

Kemeeni teuzi za udini, nchi hii ni yetu sote

Lakini tutaendelea kulisema hili maana halijakaa sawa
Ukiwa unaanzisha thread kama hizi usiweke mihemko, hauna uthibitisho wowote wa kusema wakristo wataungana, kama unao hebu weka ushahidi hapa.

Hii tabia ya kuangalia dini za watu kila mara likitajwa Baraza la Mawaziri ni kudumaza akili, mna stuck hapo every year as if mliambiwa waislamu msipokuwepo kwenye hilo Baraza la Mawaziri mtauzwa utumwani, mara mseme nchi ya wakatoliki etc.. siku zote aliwazalo mjinga......!!

Haya mawazo yenu ya kichovu yanachangia kwa kiasi kikubwa sana kurudisha nyuma harakati za kulikomboa hili taifa, miaka yote hamjiamini ni kulalamika tu, serikali ikifanya unyama wake kwa raia siku zote haiangalii dini zao, wala rangi, au kabila; simply wanapiga wote tu, amkeni usingizini.

Na hii tabia ya kuwa mfia dini nayo inachangia sana kudumaza akili za wengi, hizo dini zimeletwa na waarabu na wazungu, wewe umepokea tu, jiongeze utoke kwenye hiyo mental slavery uliyomo.

Kule juu kabisa umejibiwa vizuri sana na Mama Amon, sijaona popote ulipo react, naamini umeona hoja zake umezisoma na kuzielewa vizuri ukaamua kufunga mdomo.

Na ukiona umefungwa mdomo na hoja za mwingine maana yake hoja zako ni dhaifu, hivyo kistaarabu unatakiwa ujifunze kwa mawazo ya wengine, sio kuchagua hoja dhaifu na kuzijibu ili ku-justify ulichokiandika hapa ni sawa, ila ukweli ni wrong sio sahihi, mawazo yako ni mgando.

NB. Huu uzi nimeuona muda mrefu ila sikuwa interested kuuchangia kwa sababu haya mambo ya dini kwangu sio mpenzi kiivyo, yanadumaza akili tu; mpaka nilipoiona hiyo comment yako hapo juu ndio nikajua una udhaifu kichwani, unahitaji kuamshwa usingizini, siku zote naiangalia roho yangu na matendo yangu zaidi.
 
Huko Zanzibar kuna wakisto wangapi kwenye baraza la mawaziri la Hussein Mwinyi? Siungi mkono Uteuzi wa mawaziri wa JIWE usiozingatia umoja wa nchi yetu; haingii akilini kwa wilaya moja ya IRAMBA kutoa mawaziri watatu as if hakuna wananchi toka sehemu zingine za nchi wanaostahili kuteuliwa!!!
Sijawahi kupiga kura kuchagua mwakilishi, wala shehia wala raisi wazanzibar. Hilo swali linawafaa wazanzibari zaidi
 
Ukiwa unaanzisha thread kama hizi usiweke mihemko, hauna uthibitisho wowote wa kusema wakristo wataungana, kama unao hebu weka ushahidi hapa.

Hii tabia ya kuangalia dini za watu kila mara likitajwa Baraza la Mawaziri ni kudumaza akili, mna stuck hapo every year as if mliambiwa waislamu msipokuwepo kwenye hilo Baraza la Mawaziri mtauzwa utumwani, mara mseme nchi ya wakatoliki etc.. siku zote aliwazalo mjinga......!!

Haya mawazo yenu ya kichovu yanachangia kwa kiasi kikubwa sana kurudisha nyuma harakati za kulikomboa hili taifa, miaka yote hamjiamini ni kulalamika tu, serikali ikifanya unyama wake kwa raia siku zote haiangalii dini zao, wala rangi, au kabila; simply wanapiga wote tu, amkeni usingizini.

Na hii tabia ya kuwa mfia dini nayo inachangia sana kudumaza akili za wengi, hizo dini zimeletwa na waarabu na wazungu, wewe umepokea tu, jiongeze utoke kwenye hiyo mental slavery uliyomo.

Kule juu kabisa umejibiwa vizuri sana na Mama Amon, sijaona popote ulipo react, naamini umeona hoja zake umezisoma na kuzielewa vizuri ukaamua kufunga mdomo.

Na ukiona umefungwa mdomo na hoja za mwingine maana yake hoja zako ni dhaifu, hivyo kistaarabu unatakiwa ujifunze kwa mawazo ya wengine, sio kuchagua hoja dhaifu na kuzijibu ili ku-justify ulichokiandika hapa ni sawa, ila ukweli ni wrong sio sahihi, mawazo yako ni mgando.

NB. Huu uzi nimeuona muda mrefu ila sikuwa interested kuuchangia kwa sababu haya mambo ya dini kwangu sio mpenzi kiivyo, yanadumaza akili tu; mpaka nilipoiona hiyo comment yako hapo juu ndio nikajua una udhaifu kichwani, unahitaji kuamshwa usingizini, siku zote naiangalia roho yangu na matendo yangu zaidi.
Nahisi umerukia mada, ingekuwa ni vyema ukarudia kusoma mada husika, kisha ukasoma post uliyoiquote ambayo nilikuwa namjibu yule bibie uone muktadha mzima wa hiyo post.

Kama huoni tatizo kuwa na waislamu 3 ndani ya baraza la mawaziri la watu 23 huewezi kuelewa mada hii.

Na kama huoni tatizo watu kulaani teuzi zilizokaa kikanda au kikabila lakini watu haohao ambao hulaani mambo hayo hawaoni tatizo teuzi zilizokaa kidini na huwa wanafumba macho kama ni nothing pindi teuzi hizo zikifanywa, basi huwezi elewa jibu nililomjibu huyo uliyeniquote nikimjibu.

Ukitaka kuelewa vizuri geuza role, uwe na raisi Muislamu aunde baraza la mawaziri 23 lenye wakiristo 3 tu kisha lete mrejesho hapa hizo shutuma, lawama, miguno kutoka kila kona ya nchi!

Inawezekana vipi kwenye baraza la mawaziri lenye watu 23 liwe na waislamu 3 tu ina maana katika nchi hii hakuna waislamu wa kutosha wenye vigezo hadi hiyo tochi ya uteuzi iwe inamulikia watu wa imani moja tu?

Mimi nilitegemea muupige vita udini kwa vitendo, sasa mnashambulia watu wanaoukemea udini huo kwa kuonyesha kuwa kuna kila dalili za udini katika teuzi!
 
Back
Top Bottom