Baraza Jipya la Mawaziri 2020: Hizi ndizo kasoro kuu 3 ninazoziona

Baraza Jipya la Mawaziri 2020: Hizi ndizo kasoro kuu 3 ninazoziona

Nahisi umerukia mada, ingekuwa ni vyema ukarudia kusoma mada husika, kisha ukasoma post uliyoiquote ambayo nilikuwa namjibu yule bibie uone muktadha mzima wa hiyo post.

Kama huoni tatizo kuwa na waislamu 3 ndani ya baraza la mawaziri la watu 23 huewezi kuelewa mada hii.

Na kama huoni tatizo watu kulaani teuzi zilizokaa kikanda au kikabila lakini watu haohao ambao hulaani mambo hayo hawaoni tatizo teuzi zilizokaa kidini na huwa wanafumba macho kama ni nothing pindi teuzi hizo zikifanywa, basi huwezi elewa jibu nililomjibu huyo uliyeniquote nikimjibu.

Ukitaka kuelewa vizuri geuza role, uwe na raisi Muislamu aunde baraza la mawaziri 23 lenye wakiristo 3 tu kisha lete mrejesho hapa hizo shutuma, lawama, miguno kutoka kila kona ya nchi!

Inawezekana vipi kwenye baraza la mawaziri lenye watu 23 liwe na waislamu 3 tu ina maana katika nchi hii hakuna waislamu wa kutosha wenye vigezo hadi hiyo tochi ya uteuzi iwe inamulikia watu wa imani moja tu?

Mimi nilitegemea muupige vita udini kwa vitendo, sasa mnashambulia watu wanaoukemea udini huo kwa kuonyesha kuwa kuna kila dalili za udini katika teuzi!
1. NI LINI UMEWASILIANA NA HAO MAWAZIRI KILA MMOJA KWA WAKATI WAKE WAKAKUONYESHA VYETI VYAO VYA UBATIZO?
 
KATIBA,SHERIA,KANUNI ZINASEMAJE KUHUSU BARAZA LA MAWAZIRI:?

Katiba yetu ibara ya 54 inasema Mawaziri watatokana na wabunge ila hakuna sifa za Udini,Ukanda, Jinsia, Hali ya Ulemavu, elimu nk


Kwa Mujibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 ibara ya 4(1) inasema kwamba " Shughuli zote za Mamlaka ya NCHI katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na Vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji,vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji HAKI na pia Vyombo viwili vyenye Mamlaka ya KUTUNGA sheria na kusimamia utekelezaji wa Umma.

ibara ya 4(2) imefafanua vyombuo viwili kuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na serikali ya Zanzibar, Vyombo viwili vya Itaoji haki ni Mahakama ya Jmahuri ya Muungano na Mahakama ya Zanziar na Vyombo viwili vya kutunga sheria ni Bunge la Muungano na Barazala la Wawakilishi.


ibara ya 4(3) inatajja mambo ya Muungano........

ibara ya 4(4) inasema kwamba "Kila chombo kitaundwa na kutekeleza majukumu yake kwa kufuata masharti mengine yaliyomo katika katiba hii.

Sasa kwa kuchangia huu mjadala wenye Hoja dhaifu 3 kuhusu baraza la Mawaziri kwamba
(i) Limejaa Wakristo wengi,
(ii) Kwamba hakuna Wazanzibar
(iii) Kwamba limejaa Wanaume na watu Ukanda wa Ziwa (Demographical variables)


Nilitegemea watu wanukuuu angalau Kifungu chochote cha Katiba/ sheria ambacho Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri atakuwa amekiuka au basi tuseme tunamhukumu kwa kutumia mazoea- mila/norms au maelekezo ya Chama kinachotawala.

HOJA kubwa inayotaka kujengwa ni ya UBAGUZI-DISCRIMINATION.

Katiba inasemaje?
Katiba yetu ibara ya 13(4-5) inapinga aina zote za ubaguzi bila kujali ni aina gani,iwe Dini,kabila,ukanda au Jinsia.

13(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa Kazi au shughuli yoyote ya madaraka ya Nchi
Ni nani anayesema kwamba amebaguliwa? UBAGUZI ndio HOJA kuu hapa; Kuna Mzanzibar anasema kwamba yeye ana haki ya kuwa Waziri ila amebaguliwa?

Kuna Mwanamke anayelalamika kuwa ameachwa kwa sababu ya Jinsia yake?
Kuna Mtu wa Mkoa wowote anayelalamika kwamba ameachwa kwa sababu ya Mahali alipozaliwa?

Ili kupata Majibu ya Maswali hayo, Katiba yetu ibara ya 35 (2) inasema kwamba Ofisi yeyote ya utumishi wa Umma itatatekelezwa kwa NIABA ya RAIS, yaani mwenye Ofisi nni Rais ila Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa MIKOA au Wilaya wanamsaidia tu, Rais huweka mtu ambaye akimwamgalia anajiona yeye,anaona mategemei yake.


Funga Kazi ni ibara ya 37 ambayo walioitunga waliona mbali,inasema kwamba " Rais halazimishwi kufuata ushauri wowote katika kufanya maamuzi yake---hata Bunge linaweza kushauri ila Rais habanwi wala halazimishwi kufuata huo ushauri, You knwo why? Ili kumpatia Rais uwanja mpana wa kutekeleza Katiba kwa minajili ya Haki,

Sasa basi, Sheria inasema kwamba " Yeyote anayeteuliwa na Rais is working for the PLEASURE of the President; yaani if the President is not pleased with you, He will dismiss you on that good moment/minute/second.


Kwa ufupi kabisa, hadi Juni 2021, kutakuwa na Wazanzibar zaidi ya 2 kwenye Baraza la Mawaziri, kutakuwa na Wanawake zaidi ya 5 kwenye Cabinet, na watu wa Mikoa/Kanda zingine zinazoona haijaingizwa kwa Cabinet; utauliza nimejuaje? Kila timu inakuwa na Wachezaji 11 uwanjani ila kunakuwa na reserve List in case of majeruhi, RED CARD, or whatever Mchezo lazima uendelee; hata Simba SC Juzi mliona akina KAGERE waliingia dakika ya 85

Pili, Ukiangalia Size ya Manaibu Mawaziri 23 ni idicator kwamba ni waiting list ya kuingia kwa cabinet ndani ya muda mfupi, Wazanzibar wapo 3, wanawake manaibu are 4,Mikoa na Kanda mbali mbali wapo wengi.

Tunachoweza kufanya kwa mujibu wa Katiba hii,ni kumwombea Rais na Washauri wake HEKIMA, BUSARA NA AFYA NJEMA ili Mungu mwenyewe awafunulie SIRI zake ambazo hata sisi hatuzijui. Ingekuwa Katiba yetu inasema Mawaziri LAZIMA wathibitishwe na BUNGE-WANANCHI, hapo wanaolalamika wangekuwa na HOJA za kutaka kuwe na mabadiliko, kwamba Bunge liwakatae baadhi ya Mawaiziri ili kuziba malalamiko yao, huo mlango haupo kabisa.

Labada Katiba yetu iseme kwamba kwenye Wizara 5 za Muungano, Kila Pande ya Muungano iwe na Uwakilishi ndani ya Baraza la Mawaziri na iseme kati ya Wizara atazounda Rais, 3 lazima 1/3 iwe ni Wanawake; hapo kutakuwa na Nguvu ya Kikatiba na itakuwa ni kufuata tu.
ILANI ya chama inasemaje?
Asante kwa uchambuzi mzuri. Jamani tuchapeni kazi tuiletee Nchi yetu maendeleo. Mhe.Lukuvi anataka watanzania wote tupate haki ya kumilki ardhi haijalishi sisi ni dini gani, kadhalika mawaziri na watendaji wote. Kuwepo waziri au kiongozi kutoka kabila, mkoa, dini yangu si hoja ya msingi ila ikitokea unashukuru!
 
HOJA kubwa inayotaka kujengwa ni ya UBAGUZI-DISCRIMINATION.

Katiba inasemaje?
Katiba yetu ibara ya 13(4-5) inapinga aina zote za ubaguzi bila kujali ni aina gani,iwe Dini,kabila,ukanda au Jinsia.

13(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa Kazi au shughuli yoyote ya madaraka ya Nchi
Nakubaliana nawe kuwa katiba inakataza aina zozote za ubaguzi; kwenye aina za ubaguzi ongeza Maoni ya kisiasa.
Kwa kuwa msingi wako ni kuwa katiba haijavunjwa, ni kweli ila ni vyema ukakemea vitendo vyote vya kibaguzi siyo kwa kuteua baraza tu.
Kifungu kidogo cha 5 cha ibara ya 13 ukikinukuu chote kinasema:
(5) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara hii

neno "kubagua" maana yake ni kutimiza haja, haki au mahitaji

mengineyo kwa watu mbalimbali kwa kuzingatia utaifa wao,

kabila, pahala walipotokea, maoni yao ya kisiasa, rangi, dini,

jinsia au hali yao ya maisha kwa namna ambayo watu wa aina

fulani wanafanywa au kuhesabiwa kuwa dhaifu au duni na

kuwekewa vikwazo au masharti ya vipingamizi ambapo watu wa

aina nyingine wanatendewa tofauti au wanapewa fursa au faida

iliyoko nje ya masharti au sifa za lazima, isipokuwa kwamba neno

"kubagua" halitafafanuliwa kwa namna ambayo itaizuia Serikali

kuchukua hatua za makusudi zenye lengo la kurekebisha

matatizo katika jamii.
Unsemaje kuhusu wale walionyimwa barabara kwa kuwa walichagua chama fulani?
 
Kumbuka Mh. rais kaweka wachapakazi tu, sasa uweke Waislam wengi nani atafanya kazi ikiwa kila muda inabidi atoke kazini aende msikitini au ajifiche chooni kusali swala 5? Mh. anapohitajika haonekani kisa anaswali tena wakati wa kazi...kuweni serious jamani. Mimi hapa naona ni wachapakazi tu na sioni dini.
Sipendi kuipuuza hoja au akili ya yeyote, isipokuwa kwa vile wewe umechupa mpaka katika kubeza kitu ambacho Waislamu wanakienzi , acha tu niseme wewe ni turd.
Kama Mwenyezi Mungu atanifadhili kwa kuniingiza katika Ufalme wake, ombi langu moja kwake ni kukipasua kichwa chako mbele yangu nione exactly ameweka nini ndani yake!
Kuna makumi ya nchi za Kiislamu zilizoendelea kwa 'light years' kuliko Tanzania ambazo husimamisha kazi 'hasa' kila wakati wa swala. Egypt ambayo inawajengea bwawa la umeme ni moja wapo. Nyingine ni Uturuki inayowajengea treni ya kisasa (Pengine hata hujui, mji ..a wewe) Ni akili fupi sana kufikiria dakika tano off, siyo uchapa kazi. In fact, kama wewe ni Msomi (sidhani hivyo, wewe ni riff raff tu) ungekwishasoma utafiti wa Wataalamu wakubwa (Wazungu, miungu yako) kuwa mfanyakazi anayepumzika muda baada ya muda, ndiye more productive na more creative (katazame kamusi au mwulize mtu maana ya matamko hayo).
 
Hayo uliyoandika yakitekelezwa na kuzoeleka yatakuja kuleta vurugu na kuvunja amani nchini. Watu wateuliwe kwa sifa zao za kiutendaji nidhamu na maadili kazini. Tusije muda rais kabla hajateua waziri Muft anaambiwa pendekeza waislam wanne wa kuingia baraza la mawaziri au askofu anaambiwa hivo. Ndugu tutaiharibu nchi.
Ni ajabu wenye sifa za utendaji, nidhamu na maadili kazini ikaonekana wengi wao sana wana sifa moja in common Wengi wao ni Wakiristo, Je hakuna waislamu wa kutosha wenye nidhamu, sifa za utendaji na maadili kazini?. Si bure teuzi hizi zinanuka Udini!, Huhitaji kuambiwa kuhusu udini, bali ukiuona unaujua, na mfano wa udini kwenye mambo ya kiserikali ni kwenye teuzi hizi za juzi za Magufuli
 
Asante sana Mama Amon kwa uchambuzi makini! Pamoja tujenge Nchi yetu!
Katika kujenga hitimisho la hoja yake katika uzi huu, Mama Amon kaandika kuwa haoni shida wateuliwa wote wa rais wakiwa kabila moja, mahali pengine kwenye uzi huuhuu alinijibu kuwa haoni tabu hata wakitoka famiia moja je unamuunga mkono katika hilo?
 
Ni ajabu wenye sifa za utendaji, nidhamu na maadili kazini ikaonekana wengi wao sana wana sifa moja in common Wengi wao ni Wakiristo, Je hakuna waislamu wa kutosha wenye nidhamu, sifa za utendaji na maadili kazini?. Si bure teuzi hizi zinanuka Udini!, Huhitaji kuambiwa kuhusu udini, bali ukiuona unaujua, na mfano wa udini kwenye mambo ya kiserikali ni kwenye teuzi hizi za juzi za Magufuli

Kuwa na dini sio kuwa mdini. Udini, ukabika, ukanda, etc vinathibitishwa kwa ushahidi. Sio tuhuma za rejareja kama hizi. Jenga hoja inayotusaidia kuona mambo kihivi:

1. Kuna kanuni ya uteuzi x mahali y

2. Uteuzi huu umevunja kanuni x kwa sababu P, Q, R, etc

3. Kwa hiyo kanuni x inevunjwa.

Huonekani kufikiri kiufundi namna hii.

Jiongeze
 
Eti
Kwani marais waliyopita hawajaviona hivyo vifungu vya katiba? Mbona hatujakuwa tukisikia hizi kelele? Lisemwalo lipo na kama halipo laja.

Eti LISEMWALO LIPO KAMA HALIPO LINAKUJA!

Umewahi kutafakari juu ya ujingishaji uliomo ktk methali hii?

Kama halipo linakuja kweli? Linakujaje na kutoka wapi?

Ukweli ni kwamba:

LISEMWALI AMA LIPO AU HALIPO, NA KAMA HALIPO HALIJI.

Acha kukariri mawazo ya wahenga feki.
 
Kuwa na dini sio kuwa mdini. Udini, ukabika, ukanda, etc vinathibitishwa kwa ushahidi. Sio tuhuma za rejareja kama hizi. Jenga hoja inayotusaidia kuona mambo kihivi:

1. Kuna kanuni ya uteuzi x mahali y

2. Uteuzi huu umevunja kanuni x kwa sababu P, Q, R, etc

3. Kwa hiyo kanuni x inevunjwa.

Huonekani kufikiri kiufundi namna hii.

Jiongeze
Mimi na wewe tunatofautiana kitu kimoja kidogo sana, wewe umejikita kwenye vigezo vyako vya uteuzi ulivyoviona vinafaa kuwa ndivyo vya kuzingatiwa bila kujali kingine chochote.

Mimi nakwenda mbele zaidi kwa kuvikubali vigezo vyako (i. e eimu, utayari, uzoefu etc) lakini on top of those nimeongeza kingine ambacho wewe hukitaki, mimi nimeongeza na kingine yaani "social inclussiveness" inayreflect demography ya Taifa.

Wewe social incusiveness unaona siyo muhimu sana ndiyo maana unaona kuwa so long as watu wana vigezo ulivyovitaja basi wateule wa rais hata wakiwa wa familia moja na yeye hilo siyo tatizo!

Mimi nasema hilo ni tatizo kubwa, na kwa muktadha huo hata kuteua watu wengi wa mrengo moja iwe wa kiimani, kidini, kijinsia etc wakati Population nzima katika hii nchi kuna watu wenye vigezo ulivyovisema naona siyo jambo sahihi.

Tunaweza kukubali kutokubaliana katika hilo, Mimi napenda serikali yenye watu wenye sifa na vigezo na iliyo inclusive. Watu hao wanapatikana nchini kutoka watu wa dini zote, kanda zote etc
 
Mimi na wewe tunatofautiana kitu kimoja kidogo sana, wewe umejikita kwenye vigezo vyako vya uteuzi ulivyoviona vinafaa kuwa ndivyo vya kuzingatiwa bila kujali kingine chochote.

Mimi nakwenda mbele zaidi kwa kuvikubai vigezo vyako (i. e eimu, utayari, uzoefu etc) lakini on top of those nimeongeza kingine ambacho wewe hukitaki, mimi nimeongeza na kingine yaani "social inclussiveness".

Wewe social incusiveness unaona siyo muhimu sana ndiyo maana unaona kuwa so long as watu wana vigezo uivyovitaja basi wateule wa rais hata wakiwa wa familia moja na yeye hilo siyo tatizo!

Mimi nasema ni tatizo kubwa, na kwa muktadha huo hata kuteua watu wengi wa mrengo moja iwe wa kiimani, kidini, kijinsia etc wakati Population nzima katika hii nchi kuna watu wenye vigezo ulivyovisema naona siyo jambo sahihi.

Tunaweza kukubali utokubaliana katika hilo, Mimi napenda serikali yenye watu wenye sifa na vigezo na iliyo inclusive. Watu hao wanapatikana nchini kutoka watu wa dini zote, kanda zote etc

Tunatofautiana hapa: Unasema "mimi nimeongeza." Mie nasema hapana, huna power right ya kuongeza vigezo vya uteuzi na kisha kuvitumia kufanya hukumu.

Anzisha mjadala wa kuongezwa kwa vigezo, jenga hoja ieleweke na kukubalika mpaka iwe rasmi ama ktk katiba au sheria. Then tumia msingi huo kukosoa.

Kwa sasa unachanganya sequence. Unahukumu kwankutumia sheria ambayo haijatungwa. Ni uchokozi usiovumilika.
 
Tunatofautiana hapa: Unasema "mimi nimeongeza." Mie nasema hapana, huna power right ya kuongeza vigezo vya uteuzi na kisha kuvitumia kufanya spinning.

Anzisha muadala ya kuongezwa kwa vigezo, jenga hoja ieleweke na kukubaliia mpaka iwe rasmi ama ktk katiba au sheria. Then tumia msingi huo kukosoa.

Kwa sasa unachanganya sequence. Unahukumu kwankutumia sheria ambayo haijatungwa. Ni uchokozi usiovumilika.

Ukiondoa kigezo cha ni lazima awe mbunge ndo awe waziri katiba haikufix vigezo vingine vyovyote vya nani awe waziri, Ni maamuzi ya raisi tu anayewateua ndo anaweka vigezo anavyovitaka na hatutangazii. Huenda vigezo alivyotumia Kikwete kupata mawaziri wake siyo hivyohivyo anavyotumia Magufuli, au vinaweza kuwepo some in common na some vikawa tofauti etc na hawatwambii, lakini ukiwa na akili timamu huwezi acha kuona Patterns fulanifulani

Sasa pattern tunayoiona kwa teuzi za Magufuli licha ya kigezo cha elimu tunaona watu waliolalia dini moja kwa sana (wewe unasema hilo siyo tatizo, lakini wengine tunaona siyo sawa kwa mujibu wa sababu tulizokwisha zieleza)

Nitakupa mfano, mwaka ya 1990's serikali ya Mkapa imewahi kuunda bodi ya Parole iiyojaa Wakiristu watupu, Waislamu walivyoguna akaivunja na kuiunda upya, alipoiunda upya ikawa very inclusive watu wakaridhika. Pale Mkapa alionyesha nini maana ya kuwa mtawala wa kitaifa na siyo kuwa na constricted mind

Kiufupi ni hivi:

Leadership is all about heuristics and the best heuristic is a leadership style that minimizes conflicts, brings a social harmony, enhance fairness and build an inclusive society, Nje ya hapo ni ubaguzi tu na kiburi cha mamlaka ambacho hakijengi mshikamano wa kitaifa kwa namna yoyote!
 
Hivi waziri akiwa wa dini flani wewe mwananchi wa kawaida ambaye uko dini ya huyo waziri unanufaika nini katika maisha yako ya kila siku? hebu tuanzie hapo kupata hayo manufaa kwa waziri akiwa wa dini yako

Mimi kwa mtazamo wangu nafikiri ni ufinyu wa kufikiri sana kwa mtu anayetoa hoja ya namna hii

Maadili ya uongozi ukataa ubaguzi wa dini,kabila,jinsia lengo kuu ni kuleta usawa na umoja wa kitaifa, lengo kuu ni tusihalalishe aliyosema botha
 

Attachments

  • Screenshot_20200518_071225.jpg
    Screenshot_20200518_071225.jpg
    78.1 KB · Views: 1
Ukabila ukanda udini uligawa taifa. Pia ni kinyume na maadili ya uongozi
 
Nikiangalia hili baraza la mawaziri, by all standards haliakisi sura ya Taifa na kwa hiyo halisaidii kwa namna yoyote kuimarisha umoja wa Kitaifa.

1. Hivi inawezekana vipi uje na baraza la Mawaziri la watu 23 lakini lenye Waislamu 3 tu?

Takwimu hizi ni 87% Wakiristo, na 13% Waislamu. Je, hii maana yake ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanaoweza kufanya kazi ya kuendesha serikali yetu katika nchi yetu more than 80% ni watu wa dini moja? Hili linaacha maswali mengi. Lakini haya sishangai, inaonyesha tu kuhusu ujeuri wa mamlaka za uteuzi, Waislamu hili suala wamelilamikia sana, Mwaka 2016 Sheikh Khalifa alilisemea, Kisha mwaka huu kwenye Waraka wa shura ya maimamu Sheikh Ponda alilisema.

Binafsi sioni kama ni weledi wa kiungozi kutoheshimu demography za nchi yako katika kuunda timu ya kufanya nayo kazi. Naiona kama ni udini wa dhahiri tu ambao unashuhudiwa na aina ya teuzi zilizofanyika toka muhula wa kwanza wa serikali hii!. Je, Waislamu wanapenda haya? - La hasha, lakini pamoja na hayo Wa kulaumiwa pia ni viongozi wao, hawajitambui, hawajielewi, wanapigana mishale wao kwa wao badala ya kusimama kwa sauti moja ya kuangalia maslahi ya watu wao. Angalau Sheikh Ponda anajitambua, aliliona hili.

2. Baraza la Mawaziri halina Waziri hata mmoja kutoka Zanzibar
Zipo wizara za muungano, hakuna waziri hata mmoja wa wizara hizo ambaye ni Mzanzibar. Ni yaleyale niliyoyasema kwenye nukta ya juu. Huwezi kuunda timu ya mambo ya nchi isiyozingatia demography za kitaifa. Kwa mfano Huwezi mathalani ukachukua watu kutoka Kanda moja ukaunda baraza la mawaziri halafu ukasema eti hawa vigezo vyao vinatosha, Well hata kama vinatosha je wao peke yao ndo wenye vigezo? . Lakini katika hili Wazanzibar wa CCM nao wajilaumu wenyewe, Wameamua kuitoa nchi yao kwa Tanganyika "iwasimamie" basi wacha nchi yao igeuzwe mkoa, yaani hata mawaziri kutoka kwao ni hiyari tena kama ilivyo mawaziri kutoka Mtwara, Mwanza au Tanga

3. Idadi ya Wanawake ni ndogo katika baraza zima la Mawaziri

Sijajua kama ilikuwa ni vision ya kitaifa au ni maono ya kiuongozi tu wa serikali za awamu ya tatu na nne. Lakini kuna kipindi tumewahi kuwaza 50/50. Japo kwa maoni yangu hiyo siyo hoja, lakini kwangu hoja ya msingi ilikuwa ni kuwa lazima katika vyombo vya mamlaka na maamuzi jinsia zote zionekane vizuri siyo kuwa na mfumo uliolalia upande mmoja kupita kiasi (mfumo dume), Sasa wanawake wa kutosha wapo, kwa nini baraza la mawaziri liwe na wanawake kiduchu sana kwenye hili baraza?

Kwa hiyo ukiniuliza kuhusu hili baraza nitakwambia kuwa:
a)
Hili baraza linanuka udini, ni as if Magufuli katuletea parokia ya Mtakatifu Joseph, haliakisi demography ya kitaifa ya kwamba nchi hii ina watu wengi wa imani zote hizi mbili. Nilitegemea kuona baraza lenye sura ya kitaifa, lakini naona baraza lenye sura ya Tanzania ya Kikristo zaidi

b) Hili ni baraza la Tanganyika, yawezekana vipi usiwe na baraza lenye waziri kamili hata mmoja Mzanzibar?

4) Ni baraza la Mfumo dume - Ratio ya akina mama katika baraza hilo siyo wakilishi, sioni ni kwa namna gani baraza hilo linasaidia kuondoa mfumo dume

Namshauri Magufuli atengue hilo baraza kabla ya kuliapisha. La sivyo litampa tabu kwenye kubalance force za kijamii za kitaifa.

Katika kipindi hiki ambapo jumuia ya kimataifa inamnyooshea kidole juu ya aina ya utawala wake, ingekuwa busara kujaribu kubalance force za ndani, ingemsaidia sana.

Ila akizidi kukataliwa ndani ya nchi na nje ya nchi, basi ajiandae kutumia miguvu zaidi kutawala katika kipindi hiki cha miaka mitano, kwa sababu kutakuwa na silent rejection ya utawala wake ndani ya nchi na hii itamsumbua sana!

Ila We jamaa unapata tabu sana. Lazima uandike kitu. Ninachoshangaa Ni how unapata hata muda. Kadiri ya maandiko yako yote humu , wew sio tu mpingaji bwabwaaaa wa JPM Bali pia Humtambui. Sasa unawezaje kumjudge kiongozi ambaye humtambui. Ila kwa akili yako fupi soma hoja za #2 za Mama Amon. Naona unapita tu kama huzioni Hivi Unapotoa vimajibu vyako vya ajabu.

Naomba tukuchangie tu nauli uende ubelgiji mana akili yako inazidi kuweuka. Nilienda Tz Mara moja. Nimeona changes nyingi njema. Sijui wewe mada zako unaandika Ukiwa chooni ubelgiji au kwenye Slums za Kenya.
 
Ila We jamaa unapata tabu sana. Lazima uandike kitu. Ninachoshangaa Ni how unapata hata muda. Kadiri ya maandiko yako yote humu , wew sio tu mpingaji bwabwaaaa wa JPM Bali pia Humtambui. Sasa unawezaje kumjudge kiongozi ambaye humtambui. Ila kwa akili yako fupi soma hoja za #2 za Mama Amon. Naona unapita tu kama huzioni Hivi Unapotoa vimajibu vyako vya ajabu.

Naomba tukuchangie tu nauli uende ubelgiji mana akili yako inazidi kuweuka. Nilienda Tz Mara moja. Nimeona changes nyingi njema. Sijui wewe mada zako unaandika Ukiwa chooni ubelgiji au kwenye Slums za Kenya.
lete mchango wa mawazo, acha matusi
 
Sasa kuna nani mwingine kwenye maCCM yaliyopo Bungeni anayeweza kuwa na elimu sawa au ya kumkaribia Kitila na Nchemba?
Kuwa Waziri kunahitaji zaidi ya elimu ya stashahada; kunahitaji pia busara na hekima!!! Sidhani kama hawa wanyiramba wote wana attributes hizo!!!! JIWE anataka walio kondooo!!!
 
Back
Top Bottom