Baraza Jipya la Mawaziri 2020: Hizi ndizo kasoro kuu 3 ninazoziona

Baraza Jipya la Mawaziri 2020: Hizi ndizo kasoro kuu 3 ninazoziona

Nahisi umerukia mada, ingekuwa ni vyema ukarudia kusoma mada husika, kisha ukasoma post uliyoiquote ambayo nilikuwa namjibu yule bibie uone muktadha mzima wa hiyo post.

Kama huoni tatizo kuwa na waislamu 3 ndani ya baraza la mawaziri la watu 23 huewezi kuelewa mada hii.

Na kama huoni tatizo watu kulaani teuzi zilizokaa kikanda au kikabila lakini watu haohao ambao hulaani mambo hayo hawaoni tatizo teuzi zilizokaa kidini na huwa wanafumba macho kama ni nothing pindi teuzi hizo zikifanywa, basi huwezi elewa jibu nililomjibu huyo uliyeniquote nikimjibu.

Ukitaka kuelewa vizuri geuza role, uwe na raisi Muislamu aunde baraza la mawaziri 23 lenye wakiristo 3 tu kisha lete mrejesho hapa hizo shutuma, lawama, miguno kutoka kila kona ya nchi!

Inawezekana vipi kwenye baraza la mawaziri lenye watu 23 liwe na waislamu 3 tu ina maana katika nchi hii hakuna waislamu wa kutosha wenye vigezo hadi hiyo tochi ya uteuzi iwe inamulikia watu wa imani moja tu?

Mimi nilitegemea muupige vita udini kwa vitendo, sasa mnashambulia watu wanaoukemea udini huo kwa kuonyesha kuwa kuna kila dalili za udini katika teuzi!
Wachana na hisia hit the target. Hujajibu hata point yangu moja unakimbia kimbia tu. Sikushangai ndio maana hata hoja za Mama Amon kule mwanzo hujajibu hata moja.

Bado niko pale pale siondoki, kuongelea haya mambo ya dini ni kupoteza muda bila sababu, binafsi sioni maana ya kuangalia watu kwa majina yao ili nianze kujiuliza kama huyu ni mwenzangu au sio.

Nimeshakwambia kule juu serikali ikifanya uhuni wake haiulizi dini ya mtu, unatakiwa umjue adui yako vizuri ili ujue namna ya kumshambulia, nyie naona miaka yote mnaruka ruka tu.

Kule Zanzibar Mwinyi katangaza Baraza lake la Mawaziri, asilimia kubwa ni waislamu, lakini sijamsikia mkristo yeyote au pagani akilalamikia hilo, HAKUNA.

Nyie wenyewe mko kimya kwenu mnaona ni sawa kwasababu kwa mtazamo wenu mnaona mmebebwa, miaka yote mnajiona dhaifu, mnaonewa, na hali hii ndio inawajengea tabia ya ubinafsi mnayotaka ienee kila mahali, na huu pia ni uthibitisho kwako wengine hayo mambo ya dini hatuna sababu ya kuyajadili, yanafupisha upeo wa fikra; if you think small you will remain small for life.

Halafu usinijibu issue yangu ya udini kwa kuchanganya na ukanda sijui ukabila, stick to the point, mimi najibu suala la udini pekee kwasababu huu ndio kama wimbo wenu wa taifa; wacha huo ukabila na ukanda wachangie wengine.

Mna tatizo la kisaikolojia. Siku nyingine mkija na hii hoja ya ajabu ajabu muwakumbuke na wapagani sababu nao hawana wakuwasemea.
 
Mimi ni mwislam, ila alieleta mada hii ni Mjinga, unastahili tu kuelimishwa huenda ukaeleimika, ukaondokana na ujinga. Kwa hiyo ulitaka rais achague baraza la mawaziri lenye wakristo 50% na waislam 50%?. Kwa hiyo achague tu kukuridhisha wewe kwa idadi hiyo hata kama watendaji husika hawawezi kazi.......
Watanzania ,watanganyika na wazanzibar wanakatishwa tamaa na baadhi ya wanasiasa na maamuzi yao, hivyo wanaamua kuachana na mambo ya kufatilia Siasa!

Niwakumbushe tu ndugu zangu, sukari tunayokorogea Hot beverage ni siasa, mafuta tunayoweka kwenye automobile ni siasa, beer na condom tunazotumia ni siasa!

Tusiache, tuendelee kujadili SIASA, siasa ni maisha.
 
Wachana na hisia hit the target. Hujajibu hata point yangu moja unakimbia kimbia tu. Sikushangai ndio maana hata hoja za Mama Amon kule mwanzo hujajibu hata moja.

Bado niko pale pale siondoki, kuongelea haya mambo ya dini ni kupoteza muda bila sababu, binafsi sioni maana ya kuangalia watu kwa majina yao ili nianze kujiuliza kama huyu ni mwenzangu au sio.

Nimeshakwambia kule juu serikali ikifanya uhuni wake haiulizi dini ya mtu, unatakiwa umjue adui yako vizuri ili ujue namna ya kumshambulia, nyie naona miaka yote mnaruka ruka tu.

Kule Zanzibar Mwinyi katangaza Baraza lake la Mawaziri, asilimia kubwa ni waislamu, lakini sijamsikia mkristo yeyote au pagani akilalamikia hilo, HAKUNA.

Nyie wenyewe mko kimya kwenu mnaona ni sawa kwasababu kwa mtazamo wenu mnaona mmebebwa, miaka yote mnajiona dhaifu, mnaonewa, na hali hii ndio inawajengea tabia ya ubinafsi mnayotaka ienee kila mahali, na huu pia ni uthibitisho kwako wengine hayo mambo ya dini hatuna sababu ya kuyajadili, yanafupisha upeo wa fikra; if you think small you will remain small for life.

Halafu usinijibu issue yangu ya udini kwa kuchanganya na ukanda sijui ukabila, stick to the point, mimi najibu suala la udini pekee kwasababu huu ndio kama wimbo wenu wa taifa; wacha huo ukabila na ukanda wachangie wengine.

Mna tatizo la kisaikolojia. Siku nyingine mkija na hii hoja ya ajabu ajabu muwakumbuke na wapagani sababu nao hawana wakuwasemea.
Umechelewa kufuatilia hii mada, Mama Amon alijibu kwenye page ya mbele zaidi ya hii mada, nikamjibu. Mods wakalichukua jibu lake kutoka page ya mbele alilojibia wakaliweka kwenye post ya pili ya page ya kwanza ya mada hii na pia baada ya jibu lake hilo nilifanya naye kadebate karefu kidogo tafuta hako ka mjadala kwenye page za mbele za nyuma za mada hii utaona

Kuhuzu Zanzibar ningefurahi pia kuona Mwinyi anaunda serikali inayoakisi demografia ya watu wa huko, Hata hivyo mimi nina interest zaidi na Serikali ya Muungano kwa Sababu serikali ya Muungano ndiyo serikali ya wote, ile ya Zanzibar ni ya Wazanzibari, sina hata haki ya kupiga kura huko kumchsgua shehia wala mwakilishi

Kuhusu Ukanda na Ukabila ni point ile ile tu ya demografia ya wajumbe waundao serikali, Kama ni halali kukemea sura ya ukabila kwenye uteuzi basi ni halali kutokubaiana na uteuzi wenye sura ya kidini

Kuhusu Waislamu kubebwa, ninatofautiana na wewe, infact Waislamu wamekuwa ni wachache kwenye fursa za utumishi wa kisiasa serikalini hii ilikuwa toka zamani, Hali iliboreka kidoogo wakati wa Kikwete, lakini Magufuli ndo kawasideline kupita kiasi, huyu kafanya too much mpaka aibu.

Kama hii nchi ni yetu sote tunategemea kuoba serikali yenye sura ya kitaifa kwa sababu watu wenye vigezo vya kushika nafasi mbalimbali wanapatikana katika watu wa imani zote.

Kuchagua watu wa imani moja kwa percentage ya kutisha kama alivyofanya Magufuli safari hii ni dalili za udini wa kutisha
 
Umechelewa kufuatilia hii mada, Mama Amon alijibu kwenye page ya mbele zaidi ya hii mada, nikamjibu. Mods wakalichukua jibu lake wakaliweka post ya pili lakini jibu lake lipo na tulifanya kadebate karefu kidogo naye baada ya post yake hiyo tafuta majibu utaona

Kuhuzu Zanzibar ningefurahi pia kuona Mwinyi anaunda serikali inayoakisi demografia ya watu wa huko, Hata hivyo mimi nina interest zaidi na Serikali ya Muungano kwa Sababu serikali ya Muungano ndiyo serikali ya wote, ile ya Zanzibar ni ya Wazanzibari, sina hata haki ya kupiga kura huko kumchsgua shehia wala mwakilishi

Kuhusu Ukanda na Ukabila ni point ile ile tu ya demografia ya wajumbe waundao serikali, Kama ni halali kukemea sura ya ukabila kwenye uteuzi basi ni halali kutokubaiana na uteuzi wenye sura ya kidini

Kuhusu Waislamu kubebwa, ninatofautiana na wewe, infact Waislamu wamekuwa ni wachache kwenye fursa za utumishi wa kisiasa serikalini hii ilikuwa toka zamani, Hali iliboreka kidoogo wakati wa Kikwete, lakini Magufuli ndo kawasideline kupita kiasi, huyu kafanya too much mpaka aibu.

Kama hii nchi ni yetu sote tunategemea kuoba serikali yenye sura ya kitaifa kwa sababu watu wenye vigezo vya kushika nafasi mbalimbali wanapatikana katika watu wa imani zote.

Kuchagua watu wa imani moja kwa percentage ya kutisha kama alivyofanya Magufuli safari hii ni dalili za udini wa kutisha
Magufuli anaonekana mbinafsi na wewe hapa unasema serikali ya Zanzibar haikuhusu, ni ya wazanzibari! hauna interest nayo; kwani ile Zanzibar haipo ndani ya JMT?

Ndio maana nimekwambia hoja yenu ya udini zaidi inasukumwa na tabia yenu ya ubinafsi, kwasababu hata wapagani nao wapo Tanzania lakini sijawahi kuwaona mkiwasemea nao kila mara mnapokuja na hoja zenu za udini.

Hebu wacheni kupoteza muda na haya mambo ya udini muelekeze akili na fikra zenu kwenye mambo makubwa zaidi hili taifa lisonge mbele kidemokrasia na kiuchumi.
 
Magufuli anaonekana mbinafsi na wewe hapa unasema serikali ya Zanzibar haikuhusu, hauna interest nayo; kwani ile Zanzibar haipo ndani ya JMT? ndio maana nimekwambia hoja yenu ya udini zaidi inasukumwa na tabia yenu ya ubinafsi, kwasababu hata wapagani nao wapo Tanzania lakini sijawahi kuwaona mkiwasemea nao kila mara mnapokuja na hoja zenu za udini.
Sasa ubinafsi upi kuhusu Zanzibar?

Sipigi kura kule kumchagua rais wao
Sina haki ya kugombea kule hata kuwa mjumbe wa shehia
Sina haki ya kuwa muwakilishi

Zanzibar nitaiongelea zaidi kwenye mambo ya muungano , lakini hayo mambo yao mengine sina Interest nayo kivile. Naweza kuongelea kwa sababu ya uhuru wa maoni lakini siwezi kuwashikia bango sana ishu zao kama ishu za Serikali ya JMT pindi ikizingua kupita maelezo

Kama unaona kuna jambo liliokukera namna Mwinyi alivyounda serikali yake huko Zanzibar basi nawe unaweza kuiandalia mada, lakini mimi binafsi nina Interest na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Magufuli kuliko Hussein Mwinyi, Maana Sijawahi kushiriki uchaguzi huko na sheria inanizuia kushiriki chaguzi za huko za SMZ
 
Loftins,

AHADI YA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE KWA WAISLAM 1962

Haiwezekani kuielewa ahadi ya Nyerere katika haki na usawa kwa raia wote kama alivyoahidi wakati wa kudai uhuru, hadi usome hotuba yake aliyoitoa tarehe 10 Desemba, 1962 katika Bunge wakati Tanganyika inakua jamhuri.

Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.

Nyerere alikuwa na haya ya kusema:

‘’Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.’’

Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema kwa Waislam.

Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.

Bila shaka Nyerere alisema maneno haya akitambua mchango mkubwa wa Waislam wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nyerere alisema maneno haya akijua kuwa ingawa yeye alikuwa Rais Mkatoliki lakini Waislam kwa nia ya kuleta umoja wa Watanganyika chini ya TANU na kupigania uhuru hawakusita kumuunga mkono kwa dhati.

Na siku alipoacha uongozi baada ya kutawala kwa robo karne Mwalimu Nyerere katika hotuba yake maarufu ya kuaga aliyotoa Diamond Jubilee Hall alikuwa na haya ya kusema:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.

Sasa nipo katika hali ya kufurahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.

Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.

Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''

Huyu ndiye Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alivyoeleza tatizo la Waislam na jinsi alivyolitatua.

Yapo mengi ambayo yangewezwa kuelezwa kuhusu ukweli wa kauli hii lakini tutosheke na haya.

Leo Waislam wanatatazika na idadi yao katika Baraza la Mawaziri lililo na Waislam 3 dhidi ya Wakristo 20.

Picha ya kwanza kulia ni Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi mwaka wa 1962.

Picha ya pili ni Mshume Kiyate na Julius Nyerere 1964 na picha ya tatu ni kulia Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Nyerere, Sheikh Mohamed Ramia na Iddi Faiz Mafungo wakiwa Dodoma 1956.View attachment 1644179View attachment 1644180View attachment 1644181
Mzee wangu umeandika vitu vingi sana embu hitimisha kwa kutueleza ulipendelea Rais ateue Mawaziri kwa kuzingatia imani zao?

Na kama ni hivyo kwani hawa Mawaziri wanakwenda kufanya kazi za Kanisa au Misikiti?

Swali la mwisho, una hakika gani kuwa hao unaowaita Wakristo na Waislamu wanafuata misingi na mafundisho ya imani zao? Wewe ni mtu wa zamani kidogo unafahamu mwanasiasa ni mtu wa aina gani.

Shirki! Shirki! Shirki!
 
Rais anateua baraza la Mawaziri kwa kushauriana na Makamu wa Rais na Waziri Mkuu. Hao wote ni Waislamu kwani wao hawakuliona hilo?

Ishu ya wanaweke wacha wakae nyumbani watulee.

Wazanzibar na wenyewe wana nchi yao. Anyway Mbarawa ameniumiza moyo kukosekana kwenye baraza la mawaziri.

Anyway today is Sunday take your Bible and go to your nearest church.
Nchi ipi au ile maamuzi yake yote yanaamuliwa tanganyika
 
Huko Zanzibar kuna wakisto wangapi kwenye baraza la mawaziri la Hussein Mwinyi? Siungi mkono Uteuzi wa mawaziri wa JIWE usiozingatia umoja wa nchi yetu; haingii akilini kwa wilaya moja ya IRAMBA kutoa mawaziri watatu as if hakuna wananchi toka sehemu zingine za nchi wanaostahili kuteuliwa!!!
Sasa kuna nani mwingine kwenye maCCM yaliyopo Bungeni anayeweza kuwa na elimu sawa au ya kumkaribia Kitila na Nchemba?
 
Hilo la wanawake lilikuwa wazi sana, wangetemwa wengi tu, mtazamo wa mzee kwa wanawake uko kipuuzi mno.
Kama Unalea binti nyumbani kwako ukileta habari ya kumfanya yeye ni special.. utampotezana kumharibia maisha..

Yeye ni binadamu aliyejaaliwa kuwa mwanamke.. kama anataka chochote maishani she has to put in equal work.. usitake uwaziri kisa wewe ni mwanamke.. upate uwaziri kwasababu unaweza.. kuliko wengine.
 
Rais angekuwa ni muislamu na akateua waislamu wakutosha (kama nusu tu ya baraza zima), leo jumapili makanisani zingesomwa nyaraka za maaskofu kuipinga serikali, mahubiri na maombi yangekuwa ni kuipinga serikali, wakristo wangeambiwa wafunge siku kadhaa dhidi ya uislamu kushamiri hapa Tz nk.

Viongozi wa kikristo nawajua vizuri.
Lini hili limetokea to support your claims!?
 
Uko sahihi, Ukitaka kuona wakiristo wakiungana kuteteana ni katika vitu kama hivi-Hapa watamtea Magufuli kwa nguvu zote kwa sababu analinda maslahi yao kwa vitendo na bila haya!

Hoja nzima maadamu nimetaja waislamu tu basi hawana haja ya kuona kuwa nimetetea wanawake na Wazanzibar

Nchi hii kuna udini wa kimyakimya wa ajabu sana, haya anayofanya Magufuli ni pembe tu imeanza kuchomoza ya kilichojificha chini
Full stop... wewe una ubinafsi unajificha nyuma ya Udini. Maana wenye dini kweli hawana husda wala Kijicho kama wewe.

Unachokiongea wewe ni shirki.. kujifanya kujua ya kesho wakati Mwenyezi Mungu amekupa leo uipokee na uishi.. tayari uko hapa na mwenzako Zanzibar-ASP nyie mshaona mabaya yote hata ambayo hayajatokea..

Huo ndio Uchawi na Ushirikina unaotajwa katika vitabu vya dini. Acheni kuuchafua uislamu kwa upotofu wenu.
 
Hayo uliyoandika yakitekelezwa na kuzoeleka yatakuja kuleta vurugu na kuvunja amani nchini. Watu wateuliwe kwa sifa zao za kiutendaji nidhamu na maadili kazini. Tusije muda rais kabla hajateua waziri Muft anaambiwa pendekeza waislam wanne wa kuingia baraza la mawaziri au askofu anaambiwa hivo. Ndugu tutaiharibu nchi.
 
KATIBA,SHERIA,KANUNI ZINASEMAJE KUHUSU BARAZA LA MAWAZIRI:?

Katiba yetu ibara ya 54 inasema Mawaziri watatokana na wabunge ila hakuna sifa za Udini,Ukanda, Jinsia, Hali ya Ulemavu, elimu nk


Kwa Mujibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 ibara ya 4(1) inasema kwamba " Shughuli zote za Mamlaka ya NCHI katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na Vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji,vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji HAKI na pia Vyombo viwili vyenye Mamlaka ya KUTUNGA sheria na kusimamia utekelezaji wa Umma.

ibara ya 4(2) imefafanua vyombuo viwili kuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na serikali ya Zanzibar, Vyombo viwili vya Itaoji haki ni Mahakama ya Jmahuri ya Muungano na Mahakama ya Zanziar na Vyombo viwili vya kutunga sheria ni Bunge la Muungano na Barazala la Wawakilishi.


ibara ya 4(3) inatajja mambo ya Muungano........

ibara ya 4(4) inasema kwamba "Kila chombo kitaundwa na kutekeleza majukumu yake kwa kufuata masharti mengine yaliyomo katika katiba hii.

Sasa kwa kuchangia huu mjadala wenye Hoja dhaifu 3 kuhusu baraza la Mawaziri kwamba
(i) Limejaa Wakristo wengi,
(ii) Kwamba hakuna Wazanzibar
(iii) Kwamba limejaa Wanaume na watu Ukanda wa Ziwa (Demographical variables)


Nilitegemea watu wanukuuu angalau Kifungu chochote cha Katiba/ sheria ambacho Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri atakuwa amekiuka au basi tuseme tunamhukumu kwa kutumia mazoea- mila/norms au maelekezo ya Chama kinachotawala.

HOJA kubwa inayotaka kujengwa ni ya UBAGUZI-DISCRIMINATION.

Katiba inasemaje?
Katiba yetu ibara ya 13(4-5) inapinga aina zote za ubaguzi bila kujali ni aina gani,iwe Dini,kabila,ukanda au Jinsia.

13(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa Kazi au shughuli yoyote ya madaraka ya Nchi
Ni nani anayesema kwamba amebaguliwa? UBAGUZI ndio HOJA kuu hapa; Kuna Mzanzibar anasema kwamba yeye ana haki ya kuwa Waziri ila amebaguliwa?

Kuna Mwanamke anayelalamika kuwa ameachwa kwa sababu ya Jinsia yake?
Kuna Mtu wa Mkoa wowote anayelalamika kwamba ameachwa kwa sababu ya Mahali alipozaliwa?

Ili kupata Majibu ya Maswali hayo, Katiba yetu ibara ya 35 (2) inasema kwamba Ofisi yeyote ya utumishi wa Umma itatatekelezwa kwa NIABA ya RAIS, yaani mwenye Ofisi nni Rais ila Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa MIKOA au Wilaya wanamsaidia tu, Rais huweka mtu ambaye akimwamgalia anajiona yeye,anaona mategemei yake.


Funga Kazi ni ibara ya 37 ambayo walioitunga waliona mbali,inasema kwamba " Rais halazimishwi kufuata ushauri wowote katika kufanya maamuzi yake---hata Bunge linaweza kushauri ila Rais habanwi wala halazimishwi kufuata huo ushauri, You knwo why? Ili kumpatia Rais uwanja mpana wa kutekeleza Katiba kwa minajili ya Haki,

Sasa basi, Sheria inasema kwamba " Yeyote anayeteuliwa na Rais is working for the PLEASURE of the President; yaani if the President is not pleased with you, He will dismiss you on that good moment/minute/second.


Kwa ufupi kabisa, hadi Juni 2021, kutakuwa na Wazanzibar zaidi ya 2 kwenye Baraza la Mawaziri, kutakuwa na Wanawake zaidi ya 5 kwenye Cabinet, na watu wa Mikoa/Kanda zingine zinazoona haijaingizwa kwa Cabinet; utauliza nimejuaje? Kila timu inakuwa na Wachezaji 11 uwanjani ila kunakuwa na reserve List in case of majeruhi, RED CARD, or whatever Mchezo lazima uendelee; hata Simba SC Juzi mliona akina KAGERE waliingia dakika ya 85

Pili, Ukiangalia Size ya Manaibu Mawaziri 23 ni idicator kwamba ni waiting list ya kuingia kwa cabinet ndani ya muda mfupi, Wazanzibar wapo 3, wanawake manaibu are 4,Mikoa na Kanda mbali mbali wapo wengi.

Tunachoweza kufanya kwa mujibu wa Katiba hii,ni kumwombea Rais na Washauri wake HEKIMA, BUSARA NA AFYA NJEMA ili Mungu mwenyewe awafunulie SIRI zake ambazo hata sisi hatuzijui. Ingekuwa Katiba yetu inasema Mawaziri LAZIMA wathibitishwe na BUNGE-WANANCHI, hapo wanaolalamika wangekuwa na HOJA za kutaka kuwe na mabadiliko, kwamba Bunge liwakatae baadhi ya Mawaiziri ili kuziba malalamiko yao, huo mlango haupo kabisa.

Labada Katiba yetu iseme kwamba kwenye Wizara 5 za Muungano, Kila Pande ya Muungano iwe na Uwakilishi ndani ya Baraza la Mawaziri na iseme kati ya Wizara atazounda Rais, 3 lazima 1/3 iwe ni Wanawake; hapo kutakuwa na Nguvu ya Kikatiba na itakuwa ni kufuata tu.
ILANI ya chama inasemaje?
 
Nikiangalia hili baraza la mawaziri, by all standards haliakisi sura ya Taifa na kwa hiyo halisaidii kwa namna yoyote kuimarisha umoja wa Kitaifa.

1. Hivi inawezekana vipi uje na baraza la Mawaziri la watu 23 lakini lenye Waislamu 3 tu?

Takwimu hizi ni 87% Wakiristo, na 13% Waislamu. Je, hii maana yake ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanaoweza kufanya kazi ya kuendesha serikali yetu katika nchi yetu more than 80% ni watu wa dini moja? Hili linaacha maswali mengi. Lakini haya sishangai, inaonyesha tu kuhusu ujeuri wa mamlaka za uteuzi, Waislamu hili suala wamelilamikia sana, Mwaka 2016 Sheikh Khalifa alilisemea, Kisha mwaka huu kwenye Waraka wa shura ya maimamu Sheikh Ponda alilisema.

Binafsi sioni kama ni weledi wa kiungozi kutoheshimu demography za nchi yako katika kuunda timu ya kufanya nayo kazi. Naiona kama ni udini wa dhahiri tu ambao unashuhudiwa na aina ya teuzi zilizofanyika toka muhula wa kwanza wa serikali hii!. Je, Waislamu wanapenda haya? - La hasha, lakini pamoja na hayo Wa kulaumiwa pia ni viongozi wao, hawajitambui, hawajielewi, wanapigana mishale wao kwa wao badala ya kusimama kwa sauti moja ya kuangalia maslahi ya watu wao. Angalau Sheikh Ponda anajitambua, aliliona hili.

2. Baraza la Mawaziri halina Waziri hata mmoja kutoka Zanzibar
Zipo wizara za muungano, hakuna waziri hata mmoja wa wizara hizo ambaye ni Mzanzibar. Ni yaleyale niliyoyasema kwenye nukta ya juu. Huwezi kuunda timu ya mambo ya nchi isiyozingatia demography za kitaifa. Kwa mfano Huwezi mathalani ukachukua watu kutoka Kanda moja ukaunda baraza la mawaziri halafu ukasema eti hawa vigezo vyao vinatosha, Well hata kama vinatosha je wao peke yao ndo wenye vigezo? . Lakini katika hili Wazanzibar wa CCM nao wajilaumu wenyewe, Wameamua kuitoa nchi yao kwa Tanganyika "iwasimamie" basi wacha nchi yao igeuzwe mkoa, yaani hata mawaziri kutoka kwao ni hiyari tena kama ilivyo mawaziri kutoka Mtwara, Mwanza au Tanga

3. Idadi ya Wanawake ni ndogo katika baraza zima la Mawaziri

Sijajua kama ilikuwa ni vision ya kitaifa au ni maono ya kiuongozi tu wa serikali za awamu ya tatu na nne. Lakini kuna kipindi tumewahi kuwaza 50/50. Japo kwa maoni yangu hiyo siyo hoja, lakini kwangu hoja ya msingi ilikuwa ni kuwa lazima katika vyombo vya mamlaka na maamuzi jinsia zote zionekane vizuri siyo kuwa na mfumo uliolalia upande mmoja kupita kiasi (mfumo dume), Sasa wanawake wa kutosha wapo, kwa nini baraza la mawaziri liwe na wanawake kiduchu sana kwenye hili baraza?

Kwa hiyo ukiniuliza kuhusu hili baraza nitakwambia kuwa:
a)
Hili baraza linanuka udini, ni as if Magufuli katuletea parokia ya Mtakatifu Joseph, haliakisi demography ya kitaifa ya kwamba nchi hii ina watu wengi wa imani zote hizi mbili. Nilitegemea kuona baraza lenye sura ya kitaifa, lakini naona baraza lenye sura ya Tanzania ya Kikristo zaidi

b) Hili ni baraza la Tanganyika, yawezekana vipi usiwe na baraza lenye waziri kamili hata mmoja Mzanzibar?

4) Ni baraza la Mfumo dume - Ratio ya akina mama katika baraza hilo siyo wakilishi, sioni ni kwa namna gani baraza hilo linasaidia kuondoa mfumo dume

Namshauri Magufuli atengue hilo baraza kabla ya kuliapisha. La sivyo litampa tabu kwenye kubalance force za kijamii za kitaifa.

Katika kipindi hiki ambapo jumuia ya kimataifa inamnyooshea kidole juu ya aina ya utawala wake, ingekuwa busara kujaribu kubalance force za ndani, ingemsaidia sana.

Ila akizidi kukataliwa ndani ya nchi na nje ya nchi, basi ajiandae kutumia miguvu zaidi kutawala katika kipindi hiki cha miaka mitano, kwa sababu kutakuwa na silent rejection ya utawala wake ndani ya nchi na hii itamsumbua sana!
Kumbuka Mh. rais kaweka wachapakazi tu, sasa uweke Waislam wengi nani atafanya kazi ikiwa kila muda inabidi atoke kazini aende msikitini au ajifiche chooni kusali swala 5? Mh. anapohitajika haonekani kisa anaswali tena wakati wa kazi...kuweni serious jamani. Mimi hapa naona ni wachapakazi tu na sioni dini.
 
KATIBA,SHERIA,KANUNI ZINASEMAJE KUHUSU BARAZA LA MAWAZIRI:?

Katiba yetu ibara ya 54 inasema Mawaziri watatokana na wabunge ila hakuna sifa za Udini,Ukanda, Jinsia, Hali ya Ulemavu, elimu nk


Kwa Mujibu wa Katiba ya Tanzania ya 1977 ibara ya 4(1) inasema kwamba " Shughuli zote za Mamlaka ya NCHI katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na Vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji,vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji HAKI na pia Vyombo viwili vyenye Mamlaka ya KUTUNGA sheria na kusimamia utekelezaji wa Umma.

ibara ya 4(2) imefafanua vyombuo viwili kuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na serikali ya Zanzibar, Vyombo viwili vya Itaoji haki ni Mahakama ya Jmahuri ya Muungano na Mahakama ya Zanziar na Vyombo viwili vya kutunga sheria ni Bunge la Muungano na Barazala la Wawakilishi.


ibara ya 4(3) inatajja mambo ya Muungano........

ibara ya 4(4) inasema kwamba "Kila chombo kitaundwa na kutekeleza majukumu yake kwa kufuata masharti mengine yaliyomo katika katiba hii.

Sasa kwa kuchangia huu mjadala wenye Hoja dhaifu 3 kuhusu baraza la Mawaziri kwamba
(i) Limejaa Wakristo wengi,
(ii) Kwamba hakuna Wazanzibar
(iii) Kwamba limejaa Wanaume na watu Ukanda wa Ziwa (Demographical variables)


Nilitegemea watu wanukuuu angalau Kifungu chochote cha Katiba/ sheria ambacho Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri atakuwa amekiuka au basi tuseme tunamhukumu kwa kutumia mazoea- mila/norms au maelekezo ya Chama kinachotawala.

HOJA kubwa inayotaka kujengwa ni ya UBAGUZI-DISCRIMINATION.

Katiba inasemaje?
Katiba yetu ibara ya 13(4-5) inapinga aina zote za ubaguzi bila kujali ni aina gani,iwe Dini,kabila,ukanda au Jinsia.

13(4) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa Kazi au shughuli yoyote ya madaraka ya Nchi
Ni nani anayesema kwamba amebaguliwa? UBAGUZI ndio HOJA kuu hapa; Kuna Mzanzibar anasema kwamba yeye ana haki ya kuwa Waziri ila amebaguliwa?

Kuna Mwanamke anayelalamika kuwa ameachwa kwa sababu ya Jinsia yake?
Kuna Mtu wa Mkoa wowote anayelalamika kwamba ameachwa kwa sababu ya Mahali alipozaliwa?

Ili kupata Majibu ya Maswali hayo, Katiba yetu ibara ya 35 (2) inasema kwamba Ofisi yeyote ya utumishi wa Umma itatatekelezwa kwa NIABA ya RAIS, yaani mwenye Ofisi nni Rais ila Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa MIKOA au Wilaya wanamsaidia tu, Rais huweka mtu ambaye akimwamgalia anajiona yeye,anaona mategemei yake.


Funga Kazi ni ibara ya 37 ambayo walioitunga waliona mbali,inasema kwamba " Rais halazimishwi kufuata ushauri wowote katika kufanya maamuzi yake---hata Bunge linaweza kushauri ila Rais habanwi wala halazimishwi kufuata huo ushauri, You knwo why? Ili kumpatia Rais uwanja mpana wa kutekeleza Katiba kwa minajili ya Haki,

Sasa basi, Sheria inasema kwamba " Yeyote anayeteuliwa na Rais is working for the PLEASURE of the President; yaani if the President is not pleased with you, He will dismiss you on that good moment/minute/second.


Kwa ufupi kabisa, hadi Juni 2021, kutakuwa na Wazanzibar zaidi ya 2 kwenye Baraza la Mawaziri, kutakuwa na Wanawake zaidi ya 5 kwenye Cabinet, na watu wa Mikoa/Kanda zingine zinazoona haijaingizwa kwa Cabinet; utauliza nimejuaje? Kila timu inakuwa na Wachezaji 11 uwanjani ila kunakuwa na reserve List in case of majeruhi, RED CARD, or whatever Mchezo lazima uendelee; hata Simba SC Juzi mliona akina KAGERE waliingia dakika ya 85

Pili, Ukiangalia Size ya Manaibu Mawaziri 23 ni idicator kwamba ni waiting list ya kuingia kwa cabinet ndani ya muda mfupi, Wazanzibar wapo 3, wanawake manaibu are 4,Mikoa na Kanda mbali mbali wapo wengi.

Tunachoweza kufanya kwa mujibu wa Katiba hii,ni kumwombea Rais na Washauri wake HEKIMA, BUSARA NA AFYA NJEMA ili Mungu mwenyewe awafunulie SIRI zake ambazo hata sisi hatuzijui. Ingekuwa Katiba yetu inasema Mawaziri LAZIMA wathibitishwe na BUNGE-WANANCHI, hapo wanaolalamika wangekuwa na HOJA za kutaka kuwe na mabadiliko, kwamba Bunge liwakatae baadhi ya Mawaiziri ili kuziba malalamiko yao, huo mlango haupo kabisa.

Labada Katiba yetu iseme kwamba kwenye Wizara 5 za Muungano, Kila Pande ya Muungano iwe na Uwakilishi ndani ya Baraza la Mawaziri na iseme kati ya Wizara atazounda Rais, 3 lazima 1/3 iwe ni Wanawake; hapo kutakuwa na Nguvu ya Kikatiba na itakuwa ni kufuata tu.
ILANI ya chama inasemaje?
Kwani marais waliyopita hawajaviona hivyo vifungu vya katiba? Mbona hatujakuwa tukisikia hizi kelele? Lisemwalo lipo na kama halipo laja.
 
Nawashangaa sana waislamu mnalalamika lalamika tu mnasahau kuwa top cream ya juu ya Serikali ni waislamu

Waziri mkuu muislam
Makamu wa Rais muislamu
Mkurugenzi wa usalama ni muislamu

Nenda kwa ma ded, ma das, wakuu wa wilaya na mikoa waislamu mbona wengi tu

Kipindi cha kikwete
Rais muislamu
Makamu muislamu
IGP (said mwema muislamu)
Mkurugenzi wa usalama ( othman muislamu)
Wakuu wa mshirika ya umma wengi walikuwa waislamu kina Ramadhani dau na wengine hukusikia wakristo wanalalamika you know why?

Hatumaindi vitu vidogo dogo kama hivi..

Nyinyi sasa kila kitu kwenu nongwa

Elimu Elimu Elimu
Nakazia
 
Back
Top Bottom