Baraza Kuu la Waislam Tanzania latoa tamko kuhusu Mahakama ya Kadhi na Katiba iliyopendekezwa

Status
Not open for further replies.
Tetere,
Baraza hili si BAKWATA...

Soma tena tamko kwa uangalifu...
Hayo mengine mie sina haja ya kuyasemea labda wengine watakujibu.

Mohammed, wewe waone hivyo hivyo unavyotaka kuwaona. Suala la mahakama ya kadhi ni kitendawili kuliko unavyodhani. Na BAKWATA wana SHUGHULIKIA kuhakikisha kuwa lengo halifikiwi. Tatizo liko hivi:
1. Lengo la mahakama ya kadhi haliko wazi
2. Nia haiko wazi
3. Mkakati na mipango ya kufikia lengo ni vurugu, dhaifu na imejaa rushwa
4. Waislam hawawezi kufikia lengo wakati kuna waislam wanaSHUGHULIKIA lengo lisifanikiwe kwa kula rushwa, kushibishwa matumbo yao na tamaa zao, kwa dhuluma!
 

Wanasiasa husema chochote wanapoomba kura. Ni jukumu letu wapiga kura kuchambua pumba na mchele. Kwa chaguzi za 1995, 2000, 2005, 2010, CCM haijateleza hata 10% ya iliyoyaahidi.
Hilo la mahakama ya kadhi ni moja kati ya mambo elfu moja ambayo hayajatekelezwa kwa wapiga kura.
 

Kuna muislamu yeyote aliyekosa haki yake kwa kukosekana kwa mahakama ya kadhi toka 1963 hadi sasa?
 
Kwani kuna dini au madhehebu gani ambayo imeomba mahakama ?!....kwa ajili ya kesi gani !?
Hii ni njia moja wapo ya kukimbia ukweli kuhusu kuanzisha Taasisi hii !
Hawa viumbe wa ajabu wanasumbuliwa na chuki tu, mahakama ya kadhi ni kwa ajili ya Waislam lakini kwao ni shida.
 
Kuna muislamu yeyote aliyekosa haki yake kwa kukosekana kwa mahakama ya kadhi toka 1963 hadi sasa?

Malalamiko ya Waislaamu kutaka wahukumiwe kwa mujibu wa Imani yao hujapatapo sikia ama mekufahamu sivyo....!?

Khasa kunako mas ala ya MIIRAATHI na NDOA....!?

Ndiyo wapo.
 
Malalamiko ya Waislaamu kutaka wahukumiwe kwa mujibu wa Imani yao hujapatapo sikia ama mekufahamu sivyo....!?

Khasa kunako mas ala ya MIIRAATHI na NDOA....!?

Ndiyo wapo.

kiukweli sijawahi kuyasikia... utanisamehe kwa hilo...
na ni kwa nini basi mambo yanahusu mirathi nk yanavyotamkwa kwenye sheria za kiislamu yasiwekwe kwenye sheria za kawaida za nchi. then ikatamkwa kuwa yatakuwa considered kwa waislamu tu?
 

Tetere,
Uungwana ni mtu kustahi fikra na mawazo ya mtu mwingine.

Ikiwa hizo ni fikra zako sawa na tusubiri tuone.
 
kiukweli sijawahi kuyasikia... utanisamehe kwa hilo...
na ni kwa nini basi mambo yanahusu mirathi nk yanavyotamkwa kwenye sheria za kiislamu yasiwekwe kwenye sheria za kawaida za nchi. then ikatamkwa kuwa yatakuwa considered kwa waislamu tu?

Tuko,
Hayo unayosema mbona yashajadiliwa sana?

Inaelekea wewe ni mgeni katika jambo hili.
Ikiwa hivyo ndivyo soma kwanza kisha ndiyo uingie katika mjadala huu.
 
kiukweli sijawahi kuyasikia... utanisamehe kwa hilo...
na ni kwa nini basi mambo yanahusu mirathi nk yanavyotamkwa kwenye sheria za kiislamu yasiwekwe kwenye sheria za kawaida za nchi. then ikatamkwa kuwa yatakuwa considered kwa waislamu tu?

Hii nchi haina uadilifu na Katiba ndo Msingi mkuu wa Utawala.

Sasa ushauri wako mzuri ila nami nashauri kuwa, wacha tuitie kunako hiyo Katiba ya Nchi kisha tutajaitungia hizo Sharia ndanimwe humo.

Kwani tatizo liwapi khasa kwa upande wa pili/ Wakristo maana yaonekana wao ndo wasoitaka dhaahir shaahir....!?

Kwani kuna nini huko/ humo hadi washupake nalo kiasi hiko....!?
 
Mohamed Saidi ni mtu mstaarabu sana,hana jazba anatoa darsa kwa lugha nzuri hata kwa mtu mkorofi.Tofauti na hawa panya road kina Ritz,THE BIG SHOW na kahtan!Mzee Mudi kwa nini sasa huwa huungani na sisi kwenye topic zingine kutupa busara zako?
 

Ajira za watu hizo, zitengenezeni hizo fursa wakuu
 

Wakristo tunataka fair play. ..
Mambo yetu hayapo kwenye gharama za serikali, kwa nini ya waislamu?
 
Mi nawakubalia muunde ila sitaki kabisa kodi yangu ihudumie mahakama hii, muwe mnawalipisha wanaofungua kesi. Huwezi tumia kodi ya mkristo kwa hili. Kamwe
 
sielewi hapa

Bora usielewe tu ni kuimizani kichwa tuu, nchi aina dini, watu wanalazimisha limahakama lao tuliendeshe sisi tusio wasilamu (taxes) ni upopo.

Endesheni wenyewe, tokeni vijiweni tafuteni mapoli jengeni misikiti huko, tafuteni vyanzo vingi vywa mapato, then anzeni.

Zanzibar ni nchi ya kisilamu kuendesha mahakama hiyo ni sawa.

Sipendi kusikia tena u.ji.nga huu hapa. tumechoka.
 
Wakristo tunataka fair play. ..
Mambo yetu hayapo kwenye gharama za serikali, kwa nini ya waislamu?

Hiyo Mahakama ilikuwepo tangu,
Suali ni je, nani aliiondosha....!?

Tuanze na hapo ndo penye KIINI, mangine yatatufika kirakhisi mno.

Ahsanta na tuendelee na Darsa.
 
Wakristo tunataka fair play. ..
Mambo yetu hayapo kwenye gharama za serikali, kwa nini ya waislamu?

Wakiona vipi waende zanzibar huku Tanganyika haiwezekani, walipa kodi wakuu Tanganyika ni wakristo ndio wengi kila sehemu za uzalishaji utawakuta wao.

Mbona roman Catholic wanayo wao ulna uendesha wao kwa kutumia canon law, na hawajawai kulialia.

Sipendi udini kweli kwenye utanganyika wangu, wote ni sawa.
 
Hiyo Mahakama ilikuwepo tangu,
Suali ni je, nani aliiondosha....!?

Tuanze na hapo ndo penye KIINI, mangine yatatufika kirakhisi mno.

Ahsanta na tuendelee na Darsa.

Wabara
Kama ilikuwepo kwenye sheria ni wazi kuwa iliwekwa na watunga sheria na iliondolewa na watunga sheria. Labda tujiulize sababu
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…