Bashe: Rais Samia ametoa Sh700 milioni ujenzi skimu ya Usense mkoani Katavi yenye urefu wa 7.5km

Bashe: Rais Samia ametoa Sh700 milioni ujenzi skimu ya Usense mkoani Katavi yenye urefu wa 7.5km

Jambo zuri. Tukikazana na mipango ya kilimo cha umwagiliaji tutapiga hatua fulani. Maji tunayo mengi sana.
 
kwani hata kama ni kodi zenu akiusema hizo naenda kutanulia dubai utamwambia nini akisema hizo napeleka shuleni utamwambia nini? kaidhinisha ziende huko kwahiyo usikatae kuwa ametoa kwani unafikiri yeye atatoa kwenye mshahara wake? acheni ulimbukeni
Miradi ya amendeleo ya serikali inatekelezwa kwa mujibu wa sheria. siyo kwa matamko. Bajeti ikishapitishwa rais anapelekewa mswada wa sheria ya bajeti ili ausaini. Akishasaini ndo utekelezaji unaanza. Hivyo, huo mradi upo katika mpango wa serikali kupitia bajeti ya mwaka huu. kinachoenda kufanyika ni utekelezaji wa sheria.
 
Moja ya sababu inayoonesha kuna mwerevu fulani anayeongoza kundi la wajinga...
 
Majuzi hukusikia Rais atatoa pesa ya kujenga madarasa 15,000 hili vipi?

💪🏿💪🏿🙏🏿🙏🏿

Miradi ya amendeleo ya serikali inatekelezwa kwa mujibu wa sheria. siyo kwa matamko. Bajeti ikishapitishwa rais anapelekewa mswada wa sheria ya bajeti ili ausaini. Akishasaini ndo utekelezaji unaanza. Hivyo, huo mradi upo katika mpango wa serikali kupitia bajeti ya mwaka huu. kinachoenda kufanyika ni utekelezaji wa sheria.
 

Bashe pc

  • Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia ametoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.
    Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia metoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.

Bashe ameyasema hayo leo Oktoba 3 alipotembelea skimu hiyo, akisema wameweka mkakati ambao utamlinda mkulima, lengo ni kuhakikisha wakulima wananufaika kupitia shughuli zao za kilimo.

"Ni dhambi kuwaletea matumaini ambayo hayapo. Utaratibu uko hivi, nimempa Mhandisi siku 45 zabuni iwe imetangazwa ,watafanya michakato yao kumpata mkandarasi kwa hiyo hii skimu hii yenye wakulima 250 haitaanza kujengwa leo itachukua muda.

“Ninaamini msimu huu hata ukianza skimu haitakuwa imejengwa kwa sababu miujiza ilikuwepo wakati wa mtume Muhammad na Yesu, siku hizi hakuna miujiza," amesema Bashe na kusisitiza lazima taratibu ziwepo kufanikisha ujenzi.

Ameongeza skimu hiyo itajengwa mfereji mkuu ambao utakuwa na kilomita nane na mifereji mitano ambayo itakuwa na kilimota 7.5 kwa hiyo wakulima hao wasubiri lakini amewahakikishia zabuni itatangazwa ndani ya siku 45 na mkandarasi lazima apatikane.

"Nataka kupata majibu katika kipindi kifupi kwamba mkandarasi tayari amepatikana na taratibu zote zinaendelea vizuri, tunataka kila kitu kiwe sawa ili Waziri aje kuzindua ujenzi wa skimu hii. Serikali itawekeza fedha hizo milioni 700 ili kujenga hii skimu ya Usense maana yake lazima fedhazirudi ili tukawekeze sehemu zingine.

"Bahati mbaya miradi mingi ya umwagiliaji ambayo imewekezwa imekosa ufanisi kwa sababu viongozi wanaopewa kuisimamia wengi wanakuwa wabadhirifu kwa sababu fedha zinazochangwa zinanaishia kwenye vikao," amesema.

Bashe pcc
Pia, ametoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kuhakikisha wakulima waliosajiriwa kwenye skimu hiyo wanapimiwa maeneo yao na kupewa hati ya umiliki wa mashamba, kila mtu awe na hati ya umiliki wa shamba lake ili wawe na uhakika ndiyo wawe na uchungu.

Kwa upande mwingine, Bashe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa Kuendeleza Umwagiliaji, hivyo wakulima wa kilimo cha umwagiliaj watapewa elimu kuhusu mfuko huo, ambapo wakivuna mazao kuna mchango ambao watautoa kuchangia.

"Mkulima asilazimishwe kulipa fedha kama hajalipa kiingilio cha kujisajili, mnaweza mkakubaliana mkulima akivuna kama ni asilimia 2.5 au tatu mpige mahesabu kwa gunia za mpunga halafu zile gunia zinahifadhiwa kwenye ghala la pamoja," amefafanua Bashe.


KAZI IENDELEE
Duh safi sana.
Ni mshahara wake amezitoa hizi pesa au ameuza assets zake?
 

Bashe pc

  • Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia ametoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.
    Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia metoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.

Bashe ameyasema hayo leo Oktoba 3 alipotembelea skimu hiyo, akisema wameweka mkakati ambao utamlinda mkulima, lengo ni kuhakikisha wakulima wananufaika kupitia shughuli zao za kilimo.

"Ni dhambi kuwaletea matumaini ambayo hayapo. Utaratibu uko hivi, nimempa Mhandisi siku 45 zabuni iwe imetangazwa ,watafanya michakato yao kumpata mkandarasi kwa hiyo hii skimu hii yenye wakulima 250 haitaanza kujengwa leo itachukua muda.

“Ninaamini msimu huu hata ukianza skimu haitakuwa imejengwa kwa sababu miujiza ilikuwepo wakati wa mtume Muhammad na Yesu, siku hizi hakuna miujiza," amesema Bashe na kusisitiza lazima taratibu ziwepo kufanikisha ujenzi.

Ameongeza skimu hiyo itajengwa mfereji mkuu ambao utakuwa na kilomita nane na mifereji mitano ambayo itakuwa na kilimota 7.5 kwa hiyo wakulima hao wasubiri lakini amewahakikishia zabuni itatangazwa ndani ya siku 45 na mkandarasi lazima apatikane.

"Nataka kupata majibu katika kipindi kifupi kwamba mkandarasi tayari amepatikana na taratibu zote zinaendelea vizuri, tunataka kila kitu kiwe sawa ili Waziri aje kuzindua ujenzi wa skimu hii. Serikali itawekeza fedha hizo milioni 700 ili kujenga hii skimu ya Usense maana yake lazima fedhazirudi ili tukawekeze sehemu zingine.

"Bahati mbaya miradi mingi ya umwagiliaji ambayo imewekezwa imekosa ufanisi kwa sababu viongozi wanaopewa kuisimamia wengi wanakuwa wabadhirifu kwa sababu fedha zinazochangwa zinanaishia kwenye vikao," amesema.

Bashe pcc
Pia, ametoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kuhakikisha wakulima waliosajiriwa kwenye skimu hiyo wanapimiwa maeneo yao na kupewa hati ya umiliki wa mashamba, kila mtu awe na hati ya umiliki wa shamba lake ili wawe na uhakika ndiyo wawe na uchungu.

Kwa upande mwingine, Bashe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa Kuendeleza Umwagiliaji, hivyo wakulima wa kilimo cha umwagiliaj watapewa elimu kuhusu mfuko huo, ambapo wakivuna mazao kuna mchango ambao watautoa kuchangia.

"Mkulima asilazimishwe kulipa fedha kama hajalipa kiingilio cha kujisajili, mnaweza mkakubaliana mkulima akivuna kama ni asilimia 2.5 au tatu mpige mahesabu kwa gunia za mpunga halafu zile gunia zinahifadhiwa kwenye ghala la pamoja," amefafanua Bashe.


KAZI IENDELEE
Just kwa ulewa tuu

SAMIA anafanya biashara gani atoe helaa
Nimewaza tuuu😴😴😴😴
 
Back
Top Bottom