Bashe: Rais Samia ametoa Sh700 milioni ujenzi skimu ya Usense mkoani Katavi yenye urefu wa 7.5km

Bashe: Rais Samia ametoa Sh700 milioni ujenzi skimu ya Usense mkoani Katavi yenye urefu wa 7.5km

Bashe pc

  • Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia ametoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.
    Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia metoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.

Bashe ameyasema hayo leo Oktoba 3 alipotembelea skimu hiyo, akisema wameweka mkakati ambao utamlinda mkulima, lengo ni kuhakikisha wakulima wananufaika kupitia shughuli zao za kilimo.

"Ni dhambi kuwaletea matumaini ambayo hayapo. Utaratibu uko hivi, nimempa Mhandisi siku 45 zabuni iwe imetangazwa ,watafanya michakato yao kumpata mkandarasi kwa hiyo hii skimu hii yenye wakulima 250 haitaanza kujengwa leo itachukua muda.

“Ninaamini msimu huu hata ukianza skimu haitakuwa imejengwa kwa sababu miujiza ilikuwepo wakati wa mtume Muhammad na Yesu, siku hizi hakuna miujiza," amesema Bashe na kusisitiza lazima taratibu ziwepo kufanikisha ujenzi.

Ameongeza skimu hiyo itajengwa mfereji mkuu ambao utakuwa na kilomita nane na mifereji mitano ambayo itakuwa na kilimota 7.5 kwa hiyo wakulima hao wasubiri lakini amewahakikishia zabuni itatangazwa ndani ya siku 45 na mkandarasi lazima apatikane.

"Nataka kupata majibu katika kipindi kifupi kwamba mkandarasi tayari amepatikana na taratibu zote zinaendelea vizuri, tunataka kila kitu kiwe sawa ili Waziri aje kuzindua ujenzi wa skimu hii. Serikali itawekeza fedha hizo milioni 700 ili kujenga hii skimu ya Usense maana yake lazima fedhazirudi ili tukawekeze sehemu zingine.

"Bahati mbaya miradi mingi ya umwagiliaji ambayo imewekezwa imekosa ufanisi kwa sababu viongozi wanaopewa kuisimamia wengi wanakuwa wabadhirifu kwa sababu fedha zinazochangwa zinanaishia kwenye vikao," amesema.

Bashe pcc
Pia, ametoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kuhakikisha wakulima waliosajiriwa kwenye skimu hiyo wanapimiwa maeneo yao na kupewa hati ya umiliki wa mashamba, kila mtu awe na hati ya umiliki wa shamba lake ili wawe na uhakika ndiyo wawe na uchungu.

Kwa upande mwingine, Bashe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa Kuendeleza Umwagiliaji, hivyo wakulima wa kilimo cha umwagiliaj watapewa elimu kuhusu mfuko huo, ambapo wakivuna mazao kuna mchango ambao watautoa kuchangia.

"Mkulima asilazimishwe kulipa fedha kama hajalipa kiingilio cha kujisajili, mnaweza mkakubaliana mkulima akivuna kama ni asilimia 2.5 au tatu mpige mahesabu kwa gunia za mpunga halafu zile gunia zinahifadhiwa kwenye ghala la pamoja," amefafanua Bashe.


KAZI IENDELEE
Soma hyo
244568317_555200182229340_6751137530076851751_n.jpeg
 
kwani hata kama ni kodi zenu akiusema hizo naenda kutanulia dubai utamwambia nini akisema hizo napeleka shuleni utamwambia nini? kaidhinisha ziende huko kwahiyo usikatae kuwa ametoa kwani unafikiri yeye atatoa kwenye mshahara wake? acheni ulimbukeni
Soma hyoooooo
IMG-20211006-WA0004.jpeg
 
Fedha ya serikali au fedha ya Hangaya
 

Bashe pc

  • Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia ametoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.
    Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia metoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.

Bashe ameyasema hayo leo Oktoba 3 alipotembelea skimu hiyo, akisema wameweka mkakati ambao utamlinda mkulima, lengo ni kuhakikisha wakulima wananufaika kupitia shughuli zao za kilimo.

"Ni dhambi kuwaletea matumaini ambayo hayapo. Utaratibu uko hivi, nimempa Mhandisi siku 45 zabuni iwe imetangazwa ,watafanya michakato yao kumpata mkandarasi kwa hiyo hii skimu hii yenye wakulima 250 haitaanza kujengwa leo itachukua muda.

“Ninaamini msimu huu hata ukianza skimu haitakuwa imejengwa kwa sababu miujiza ilikuwepo wakati wa mtume Muhammad na Yesu, siku hizi hakuna miujiza," amesema Bashe na kusisitiza lazima taratibu ziwepo kufanikisha ujenzi.

Ameongeza skimu hiyo itajengwa mfereji mkuu ambao utakuwa na kilomita nane na mifereji mitano ambayo itakuwa na kilimota 7.5 kwa hiyo wakulima hao wasubiri lakini amewahakikishia zabuni itatangazwa ndani ya siku 45 na mkandarasi lazima apatikane.

"Nataka kupata majibu katika kipindi kifupi kwamba mkandarasi tayari amepatikana na taratibu zote zinaendelea vizuri, tunataka kila kitu kiwe sawa ili Waziri aje kuzindua ujenzi wa skimu hii. Serikali itawekeza fedha hizo milioni 700 ili kujenga hii skimu ya Usense maana yake lazima fedhazirudi ili tukawekeze sehemu zingine.

"Bahati mbaya miradi mingi ya umwagiliaji ambayo imewekezwa imekosa ufanisi kwa sababu viongozi wanaopewa kuisimamia wengi wanakuwa wabadhirifu kwa sababu fedha zinazochangwa zinanaishia kwenye vikao," amesema.

Bashe pcc
Pia, ametoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kuhakikisha wakulima waliosajiriwa kwenye skimu hiyo wanapimiwa maeneo yao na kupewa hati ya umiliki wa mashamba, kila mtu awe na hati ya umiliki wa shamba lake ili wawe na uhakika ndiyo wawe na uchungu.

Kwa upande mwingine, Bashe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa Kuendeleza Umwagiliaji, hivyo wakulima wa kilimo cha umwagiliaj watapewa elimu kuhusu mfuko huo, ambapo wakivuna mazao kuna mchango ambao watautoa kuchangia.

"Mkulima asilazimishwe kulipa fedha kama hajalipa kiingilio cha kujisajili, mnaweza mkakubaliana mkulima akivuna kama ni asilimia 2.5 au tatu mpige mahesabu kwa gunia za mpunga halafu zile gunia zinahifadhiwa kwenye ghala la pamoja," amefafanua Bashe.


KAZI IENDELEE
Ni serikali ndiyo imetoa fedha hizo, na wala siyo Rais SSH. Toka awamu ya kwanza mpaka ile ya nne hatujawahi kusikia kila kitu kikifanywa na serikali kina kuwa "attributed" na mtu.

Ulimbukeni huu ulianzishwa kipindi cha awamu wa tano chini ya JPM. Sasa naona imeshakuwa ni kasumba tayari, kila kitu sasa ni Mama kafanya.

Wana CCM waache mara moja tabia hii mbaya na ya kijinga. Ebu watumie ofisi zetu za ubalozi zilizopo ughaibuni wapate kujifunza kitu.

Wachungu ili wapate kuona kama marais wa nchi za nje nao pia wanafanyiwa upuuzi kama huu pale endapo Rais anapokuwa akitimiza majukumu yake ya kila siku ya kikatiba [emoji51][emoji51][emoji51]
 
mmeshaanza mambo yenu yale....Sema serikali imetoa shilingi kadhaa kwa ajili ya 1,2,3...unaposema Rais fulanu ametoa mnatupa ukakasi kidogo.
Kwani wewe unaposikia neno Rais Samia unaelewa nini?
 
huyo mama amepata wapi hizo pesa wakati mshahara wake sio mkubwa kiasi hicho??
Hivi kwanini bavicha wengi ni mbumbumbu kiasi hiki?

Kwani wewe unaposikia neno "Rais Samia" unaelewa nini hasa?

"Rais Samia" ni taasisi hivyo usilinganishe na mtu binafsi kama unavyomtaja bibi yako au babu yako.
 
Nashangaa mtoa mada...Unamanisha Rais anamihela ameanza kugawa kama alivokua akifanya JPM?..kumbe hela za Umma viongozi wenu hujitwalia na kuzifany zao sio??
Rais ni tasisi,

Hebu kuweni na akili basi
 
Hivi kwanini bavicha wengi ni mbumbumbu kiasi hiki?

Kwani wewe unaposikia neno "Rais Samia" unaelewa nini hasa?

"Rais Samia" ni taasisi hivyo usilinganishe na mtu binafsi kama unavyomtaja bibi yako au babu yako.
Anatolea wapi pesa??
Nyoosha maelezo.
 
Hongera raisi Samia kwa kuonesha uzalendo na upendo wa kweli kwa nchi yako. Wenye akili zilizo huru tunauona mchango wako uliotukuka ndani ya taifa letu, japo kuna wale ambao akili zao hazipo huru (yan wamezikabizi kwa viongozi wao) wanajifanya hawaoni unachokifanya.

Wengi wao wanajua fika kuwa viongozi wao wamekaa bungeni zaidi ya miaka 10 hadi 15, bila hata kuacha alama ya kuchimba japo visima viwili vitatu kwa wapiga kura wao nk.
Sasa mbona huku kibamba tunakunywa maji ya miferejini mpaka leo while hili jimbo lilikua chini ya upinzani zaidi ya miaka 10
 

Bashe pc

  • Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia ametoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.
    Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Rais Samia metoa Sh700 milioni kwa ajili ya ujenzi wa skimu ya Usense na kuboresha uzalishaji wa zao la mpunga linalolimwa katika skimu hiyo iliyopo Kata ya Uruwira Wilaya ya Mpanda mkoani Katavi.

Bashe ameyasema hayo leo Oktoba 3 alipotembelea skimu hiyo, akisema wameweka mkakati ambao utamlinda mkulima, lengo ni kuhakikisha wakulima wananufaika kupitia shughuli zao za kilimo.

"Ni dhambi kuwaletea matumaini ambayo hayapo. Utaratibu uko hivi, nimempa Mhandisi siku 45 zabuni iwe imetangazwa ,watafanya michakato yao kumpata mkandarasi kwa hiyo hii skimu hii yenye wakulima 250 haitaanza kujengwa leo itachukua muda.

“Ninaamini msimu huu hata ukianza skimu haitakuwa imejengwa kwa sababu miujiza ilikuwepo wakati wa mtume Muhammad na Yesu, siku hizi hakuna miujiza," amesema Bashe na kusisitiza lazima taratibu ziwepo kufanikisha ujenzi.

Ameongeza skimu hiyo itajengwa mfereji mkuu ambao utakuwa na kilomita nane na mifereji mitano ambayo itakuwa na kilimota 7.5 kwa hiyo wakulima hao wasubiri lakini amewahakikishia zabuni itatangazwa ndani ya siku 45 na mkandarasi lazima apatikane.

"Nataka kupata majibu katika kipindi kifupi kwamba mkandarasi tayari amepatikana na taratibu zote zinaendelea vizuri, tunataka kila kitu kiwe sawa ili Waziri aje kuzindua ujenzi wa skimu hii. Serikali itawekeza fedha hizo milioni 700 ili kujenga hii skimu ya Usense maana yake lazima fedhazirudi ili tukawekeze sehemu zingine.

"Bahati mbaya miradi mingi ya umwagiliaji ambayo imewekezwa imekosa ufanisi kwa sababu viongozi wanaopewa kuisimamia wengi wanakuwa wabadhirifu kwa sababu fedha zinazochangwa zinanaishia kwenye vikao," amesema.

Bashe pcc
Pia, ametoa maagizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kuhakikisha wakulima waliosajiriwa kwenye skimu hiyo wanapimiwa maeneo yao na kupewa hati ya umiliki wa mashamba, kila mtu awe na hati ya umiliki wa shamba lake ili wawe na uhakika ndiyo wawe na uchungu.

Kwa upande mwingine, Bashe amesema Serikali imeanzisha Mfuko wa Kuendeleza Umwagiliaji, hivyo wakulima wa kilimo cha umwagiliaj watapewa elimu kuhusu mfuko huo, ambapo wakivuna mazao kuna mchango ambao watautoa kuchangia.

"Mkulima asilazimishwe kulipa fedha kama hajalipa kiingilio cha kujisajili, mnaweza mkakubaliana mkulima akivuna kama ni asilimia 2.5 au tatu mpige mahesabu kwa gunia za mpunga halafu zile gunia zinahifadhiwa kwenye ghala la pamoja," amefafanua Bashe.


KAZI IENDELEE

Sasa naanza kumwelewa former CAG Prof Assad,huu ujinga sijui utaisha lini.Hizi ni kodi zetu ambazo zitatakiwa kuidhinishwa na Bunge.

Mh Rais Samia Suluhu hizi fedha kazitoa wapi !.
 
Back
Top Bottom