Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Bashungwa ametoa rai hiyo leo Novemba 13, 2024 Wilayani Karagwe Mkoani Kagera katika Kikao cha Baraza la Madiwani cha kujadili taarifa za robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/25 kilichohusisha Watendaji wa Halmashauri na Kata.
Ameitaka Halmashauri kufanya tathmini ya utoaji huduma wa Baraza hilo ili kujua changamoto zinazokwamisha utoaji wa haki kwa wakati na wanaohusika kukwamisha waweze kuchukuliwa hatua.
Bashungwa ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kujikita katika mipango miji na upimaji wa ardhi katika maeneo yanayoendelea kukua ili kuendana na uwekezaji unaofanywa na Serikali katika miundombinu ili kuepusha migogoro ya ardhi kwa wananchi.
Aidha, Bashungwa ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kuweka mipango mahsusi na kufanya kampeni endelevu ya utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ya vivuli pamoja na matunda ili kusaidia utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, Wallace Mashanda amewasisitiza Waheshimiwa Madiwani kuendelea na mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo yanayowazunguka kwa kuendelea kupanda miti kwa wingi.