Beatrice Mdogo wa Martha Mwaipaja aanika mabaya ya dada yake kwamba ana fedha nyingi lakini hamsaidii mama yake

Enh hongera, lakini huu ukweli 90 percent wengi usaidiwa na ma bro!
Ninae dada yangu ndio mkubwa kwetu. Anamsaidia sana mama tena bila kukumbushwa au kulazimishwa. Kiufupi ana msaada hata kwa sisi wadogo zake..sio mchoyo. Hata kama anacho kidogo atakugaia hicho hicho. Aishi maisha marefu dada yangu.
 
Huyo -Beatrice Kama anatoa nyimbo anapata Views mil 7 je yeye binafsi hawezi kumuhudumia mama yake ?

Na kuhusu Martha kununulia watu Magari na kuwafungulia biashara je haifai?

Katika sadaka zinazoleta nguvu huwa ni zile unawapa watu kitu kikubwa ambao hawana uhusiano na wewe wowote .

Hivyo Martha katika utohaji yupo sahihi.

Ni vizuri huyo ndugu yake angeangalia anakwama wapi na ajaribu kujiwekeza kimkakati ili afanikiwe.
 
 

Attachments

  • IMG_20241217_101658.jpg
    70.2 KB · Views: 4
  • IMG_20241217_101650.jpg
    77.5 KB · Views: 4
  • IMG_20241217_101642.jpg
    78.4 KB · Views: 2
  • IMG_20241217_101633.jpg
    82.5 KB · Views: 2
Hao manabii waongo wanawagombanisha tu; naamini mtu anateseka sababu ya matendo yake, wamcheki huyo Mama na history Yale, mara nyingi huwa wachawi
 
Hizo sadaka unazosema ni za kishirikina, uwape magari na kuwafungulia biashara watu baki wakati nyumbani kwako kunafuka moshi, ukiumwa na kuzidiwa ndugu zako ndio wa kwanza kukuhudumia na kukufulia chupi. Mama yako hata baiskeli hana.

Fungua akiri wewe, huo ndio utajiri ambao unayeyukaga gafla tu pindi ukikosea masharti.
 
Beatrice analalamika dada yake hamsaidii mama yao, malalamiko yake hayajagusa sana dada yake kumsaidia yeye.

Kama ni kweli hamsaidii mama yake, hilo ni tatizo na Beatrice yupo sawa kulalamika na kilia.

Tumekuwa tukifunzwa tangu utotoni, ibada njema inaanzia nyumbani. Mama yako hawezi kuwa na matatizo ukaacha kuyatatua ukaenda kutatua ya jirani halafu tuseme upo sahihi. Wewe utakuwa ni mwendawazimu tu!
 
Nimeshangaa sana watu humu wanampika Beatrice na kumwambia aache kulilia pesa za dada yake wakati Beatrice analia dada yake anauwezo mkubwa ila hamsaidii mama yake mzazi.

Kama Beatrice anasema ukweli (sidhani kama anaweza kudanganya katika hili) basi Martha ana tatizo au kuna tatizo sehemu.
 
Kama Martha
Mdogo wa Martha Mwaipaja aanika mabaya ya dada yake akidai kuwa Martha Mwaipaja ana fedha nyingi sana lakini hamsaidii mama yake vilevile akidai kuwa amejitenga na ndugu zake

Tazama Video hizi kwa utulivu

Kama Martha kagoma kumsaidia mama pambana dada ww ndo umsaidie mama sio lazimaa yeye
 
Nikajua ni pesa za urithi kumbe za Dada yake? hapo kuna shida mahali atafute zake hisani sio lazima, hapo mpaka usikie upande wa pili ndio utajua shida ilipo. Ila kusimama kujiliza eti usaidiwe kisa dada ako ana hela ni kujifedhehesha tuu, manake hao anaowalilia hapo hawatamsaidia lolote zaidi ya kujianika tu pasipo sababu ya msingi.
 
Kulea mtoto si kuwekeza kitegauchumi kwamba unawekeza ili baadaye aje akusaidie.

Mzazi unatakiwa kujiwekea mpango wako mwenyewe wa kujikimu na kushamiri bila ya kumtegemea mtoto.

Kwa sababu mtoto anaweza kufariki kabla yako.

Waacheni watoto waishi maisha yao wanavyotaka.

Waswahili walisema "Tenda wema uende zako, usingoje shukurani".

Tatizo watu wanaona kulea mtoto ni kama kuwekeza kwenye biashara, unalea mtoro ili aje kukusaidia baadaye.
 
Mama ambae alifukuzwa na mama yake, na mama ambae anatengwa na mwanae, ni mama ambae amezaa mtoto mbegu ya mama yake Mzazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…