Bei ya kubadilisha dola leo ni Tsh 2418 kununua na Tsh 2442 kuuza. Je, hii ni dalili ya nini?

Mambo mawili yaweza kuwa sababu yakushuka kwa fx
1. Kwa Tz soko halipo huru hivyo serikali anaweza shusha kuleta panic kwenye soko while wakiwa na nia yakufanya watu wa deposit fx wamefungia kwenye locker
2. Mabadiliko ya sera na uchumi kubadilika upo uwezekano demand imeshuka while supply is high mnajuwa serikali imepiga marufuku matumiz ya fx kwenye malipo pia mauzo makubwa ya korosho,kahawa, maindi na dhahabu (BOP balance)
 
Na ndivyo ilitakiwa Serikali ifanye Toka Mwanzo,why ku koti bei za bidhaa na Huduma za ndani ya Nchi Kwa kutumia Dola badala ya Shilingi kama sheria inayotaka?

Mwisho usisahau kumiminika Kwa FDI na Kuongezeka Kwa exports.
 
At least shilingi inajututumua. We are strong economical lakini ni nini tunachouza mpaka tumefikia hatua ya kuimarisha shilingi kwa zaidi ya Tsh 200 ndani ya mwezi? Isije kuwa serikali ndo inauza dola zake kwa wingi Ili kuokoa shilingi.
Kuna msimu wa korosho huko Mtwara na Lindi, nayo tourism imefumuka vibaya sana.

Watalii KIA na ZNZ wafurika vya kutosha
 
At least shilingi inajututumua. We are strong economical lakini ni nini tunachouza mpaka tumefikia hatua ya kuimarisha shilingi kwa zaidi ya Tsh 200 ndani ya mwezi? Isije kuwa serikali ndo inauza dola zake kwa wingi Ili kuokoa shilingi.
Serikali ilizuia miamala ya bidhaa na Huduma za ndani ya Nchi kufanywa Kwa Dola.

Kuongezeka mara dufu Kwa Utalii,umepita Madini kuingiza forex,Royal tour impact

Kuongezeka mara dufu Kwa FDI,inakadiriwa kufikia $8bln

Kuongezeka Kwa mauzo ya bidhaa Nje ya Nchi yaliyochagizwa na uzalishaji wa mazao ya Kilimo kuongezeka sana eg Korosho,mahindi,kufuta,pareto na bidhaa za viwandani

Kupunguza uagizaji wa Baadhi ya bidhaa kutoka Nje ya Nchi Kwa sababu ya import-Substitute eg mbegu,Sukari,mbolea ,saruji nk.

Mwisho inflows za mikopo ya Kigeni ya serikali
 

Kama hatuwezi ku control spending, twafa mwanafyale. Maana tunachokusanya hakitoshi. Tuna mzigi mkubwa wa madeni.
Na bado tunaendelea kukopa. Kenya, Mozambique na nchi nyingine kadhaa ziliingia kwenye mtego huo na kupata tabu sana.
Mozambique walitegemea gas imewa kuwa haraka wakaanza kulipa. Ikachukua muda na kuna wanaojiita waasi wamechelewesha.
Kenya, bomba la mafuta lilipiga kona na kuja kwetu. Moja ya investemnt waliyokuwa wanaitegemea sana ili kuwezesha uchumi wakianza kulipa.
Hapa kwetu pia. Lazima tuwe na jitihada za makusudi kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Mkikaa viti vya mbele sio kunywa juice ya tende tu mkasahau kushauri na kusimamia namna nzuri za kuendesha uchumi
 
Tanzania Kwa asili ni Nchi ambayo ni conservative hayo hayawezi kutokea .

Mwisho bila hata Hilo Bomba la Uganda Bado Tanzania ingepata Mabomba mengine mfano majadiliano yanaendelea ya kujenga Mabomba ya gesi kutoka Tanzania Hadi Uganda, Kenya na Zambia.
 
Akomeshe vitendo vya wasiojulukana ili wananchi kwa ujumla wao wafurahie matunda ya kazi zake.
 
Kwani wahuni wakiingiza dola nchini kinyemela juna shida gani?
Inategemea na wingi wake.

Law of demand and supply ina apply.

Kipindi cha mavuno mengi ya mahindi, bei inashuka. Na mahindi yakipungua bei inapanda. Ndivyo ilivyo kwa dola.

Unapeleka dola sokoni, wafanya biashara wengi kariakoo wanazo, hawazigombanii. Lazima ushushe bei ya
kuuza.

Kuna siku dola ilikuwa wananunua 2,550 na wanauza 2,650 kwenye exchange office kama sijakosea. Lakini mimi niliuza kwa wafanya biashara kwa shs 2,700. Kuna jamaa aliuza 2,800. Hapo mahitaji yalikuwa makubwa. Kinyume chake inapelekea dola kushuka thamani.
 
Na USD zenyewe zinapatikana? Cash na bank transfers? Maana unaweza kuta rate ndogo ila ukifika unaambiwa hazipo
Saizi dollar hata elf 50 kama una account ya dollar NMB unapewa bila shida.......na kwa wanunuaji zipo hata kwenye bureau change unaweza kuta rate ya kuuza ni kiasi fulani,dollar ilivyo nyingi ukafika ndani ukanegotiate ukanunua kwa chini ya amount iliyokwenye bango
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…