Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Imani za za kijinga sana hizi, kinatabu kweli ndio kinafundisha hivyo?Alaaniwe atakaye ilaani Islael na Abarikiwe atayeibariki Islael...
Waungwana kuna mambo maishani huwa yanapotazamwa humuachia mtazamaji kila aina ya tafakuri kichwani mwake. Ndani ya miaka kadhaa ya hivi karibuni, kumezuka tabia ya watu kuitundika bendera ya Israel kwenye sehemu ya chini ya kioo cha ndani ya gari, kile ambacho dereva hukitumia kutazama magari yanayokuja kutokea nyuma ya gari.
Mwanzoni nilidhani ni mahaba binafsi ya mtu mmoja, lakini kadri siku zinavyokwenda ndivyo ambavyo mashabiki wa bendera hiyo maarufu duniani, walivyozidisha tabia hiyo.
Huwa najiuliza kama Waisrael na wao wanayo tabia ya kuitundika bendera ya Tanzania, katika sehemu ile ile ambayo sisi tunaitundika bendera yao ndani ya magari yetu. Huwa najaribu kujiuliza iwapo Mtanzania anayekatiza katika mitaa ya Jerusalem au Tel Aviv anaweze kukutana na gari ambalo ndani yake kuna bendera ya Tanzania imetundikwa, na muisrael akiendesha gari huku akiufurahia uwepo wa bendera yetu.
Haya ni mawazo yangu, kwani tabia hii imenifanya nijiulize iwapo upendo unaotoka mioyoni mwetu kuelekea kwa Waisrael, unaweza na wenyewe kuwa unathaminiwa na Waisrael bila ya sisi Watanzania kujua ni jinsi gani tunavyothaminiwa.
Netanyahu owes a hearty thanks to ISIS - Strenger than FictionMkuu ni kweli kabisa bendera ya Israel imepepea kwenye magari mengi lakini kumbuka Israel ni Taifa teule kama vitabu vitakatifu vinavoeleza wakati Tanzania au hispania ni mataifa ya kawaida
Mungu mbaguzi huyu! Waja wake kawapanga madaraja, ya mabwana na watwana sio? Amakweli dini ni kilevi, lazima uwe mlevi ndio ukubaliane na upuuzi huo.Nadhani ni namna ya watu kuonesha upendo kwa Mungu aliyejidhihirisha kupitia Taifa la Israel.
MATENDO YA MITUME 10:34,35 "...Mungu hana upendeleo bali katika kila Taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye "
Watu wanasoma matendo ya Mungu aliyoyafanya kupitia Israel, na Mungu amechagua Taifa mojawapo duniani ili kudhihirisha uwepo wake na nguvu zake.
Angeweza kuchagua Taifa lolote. Waisrael sio viumbe special tofauti na watu wengine, Muisrael asiyemwamini Yesu kama Bwana wake na Mwokozi wake ataenda jehanamu kama wasioamini wengine, kulingana na Biblia.
Hamna sababu ya msingi kulaumu mtu anayetumia uhuru wake kuelezea hisia zake pasipo kuhalifu sheria za nchi.
Huja sikia kama ubalozi wa Israel utafunguliwa tanzania au umeshafunguliwa, tangu kufungwa 1967.Waungwana kuna mambo maishani huwa yanapotazamwa humuachia mtazamaji kila aina ya tafakuri kichwani mwake. Ndani ya miaka kadhaa ya hivi karibuni, kumezuka tabia ya watu kuitundika bendera ya Israel kwenye sehemu ya chini ya kioo cha ndani ya gari, kile ambacho dereva hukitumia kutazama magari yanayokuja kutokea nyuma ya gari.
Mwanzoni nilidhani ni mahaba binafsi ya mtu mmoja, lakini kadri siku zinavyokwenda ndivyo ambavyo mashabiki wa bendera hiyo maarufu duniani, walivyozidisha tabia hiyo.
Huwa najiuliza kama Waisrael na wao wanayo tabia ya kuitundika bendera ya Tanzania, katika sehemu ile ile ambayo sisi tunaitundika bendera yao ndani ya magari yetu. Huwa najaribu kujiuliza iwapo Mtanzania anayekatiza katika mitaa ya Jerusalem au Tel Aviv anaweze kukutana na gari ambalo ndani yake kuna bendera ya Tanzania imetundikwa, na muisrael akiendesha gari huku akiufurahia uwepo wa bendera yetu.
Haya ni mawazo yangu, kwani tabia hii imenifanya nijiulize iwapo upendo unaotoka mioyoni mwetu kuelekea kwa Waisrael, unaweza na wenyewe kuwa unathaminiwa na Waisrael bila ya sisi Watanzania kujua ni jinsi gani tunavyothaminiwa.
Mungu ametumia Israel kufikia watu wa ulimwengu wote. GALATIA 3:28 "...Hapana myahudi wala myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. " Hakuna madaraja hapo, Muisraeli anayefanya dhambi ya ubaguzi atahukumiwa sawasawa na matendo yake, mkristo yeyote hapaswi kumchukia mtu yeyote na isitoshe Yesu mwenyewe alisema wapendeni adui zenu waombeeni wanaowaudhi... MATHAYO 5:44Mungu mbaguzi huyu! Waja wake kawapanga madaraja, ya mabwana na watwana sio? Amakweli dini ni kilevi, lazima uwe mlevi ndio ukubaliane na upuuzi huo.
Nalipenda mno neno "Israel" kuliko neno "Tanzania" maana neno Israel limeasisiwa na Mungu Mkuu
muumba wa mbingu na nchi; Mungu wa Ibrahimu; Mungu wa Isaka; Mungu wa Yakobo na baadae huyu ndiyo Israel; Maana ya jina lenyewe ni mshindi: Lakini neno Tanzania limeasisiwa na binadamu kwahiyo ni la kawaida tu. Hakuna nchi ya kusimama kupigana na Israel na ikashinda si Urusi,Marekani, Ujerumani wala China.
Fimbo ya enzi haitaondoka mikononi wa Yuda mpaka atakapokuja yeye mwenye kumiliki: Wafilisiti na Waarabu wote wanaifahamu vyema hii fimbo tokea enzi za Musa, Joshua na Daudi mwana wa Yese pia Mfalme wa Israel. Hii historia ilikuja kujirudia ule wa miaka ya 1962-1968-9 pale nchi takribani 9 za kiarabu ziliposalimu amri kwa taifa lenye watu wasiozidi milioni moja.
Mungu anabagua viumbe vyake?Wengine watakatifu,wengine si watakatifu,ubaguzi wa rangi wa wazi.
Nakubaliana na wewe kwamba kuna watu kama wewe ambao mnaikubali tabia yake ya ubabe wake huko mashariki ya Kati.Lakini pia ukubali kwamba kuna watu wanaiona Israel kama "taifa teule" na hapa kuna utata kwani ni zaidi ya Itikadi za kisiasa bali tunakwenda hadi kwenye Itikadi za kidini.
Kuna watu wanaodhani kwamba Waisrael ni wakristo (kwa maana ya asilimia) lakini waisrael kwa asili hawaamini kama Yesu ni Masihi Mpakwa mafuta wa Bwana Mungu Yehova. Ndiyo maana wakati kuna baadhi ya Wakristo wanakwenda Hija Israel waisrael wenyewe wanawashangaa na kuwaona kama ni watalii wa kawaida wanaokwenda kutalii maeneo ya Kihistoria yasiyo na mashiko ya Kiimani.
Kama ambavyo kuna mtizamo hasi kwamba Wapalestina wote ni waislam, wakati wapalestina wapo na wakristo na wao pia wanaporomoshewa mabomu na waisrael kama wanavyopromoshewa wenzao waislam kwenye nchi yao!!
Imani za kisasa ni zipi mkuu?Hizi imani za kishamba, taifa teule na sisi taifa letu ni la kawaida?
Nawakubali Israel kwa ubabe na msimamo, bhaaaas!