Benki ya Dunia yaitangaza Tanzania kuingia rasmi katika orodha ya Nchi zilizo katika uchumi wa kati

Benki ya Dunia yaitangaza Tanzania kuingia rasmi katika orodha ya Nchi zilizo katika uchumi wa kati

Bado hatujafika uchumi wa kati wenyewe unaoanzia $4000 per capita na kitu.
Kwa pamoja, tukitimiza wajibu wetu, hakika tutafika kwa sababu Serikali iliyoko madarakani inawekeza na kuimarisha mazingira ya kukuza uchumi wa viwanda.

Uchumi wa Viwanda ndio utatufikisha kwenye kundi la Nchi zenye Uchumi wa Kipato cha Kati (MIC).

Ili kufanikisha hilo:
• viwanda vinahitaji malighafi (kilimo, mifugo, uvuvi, madini, nk);.
• Ili Sekta hizo zizalishe malighafi za kutosheleza mahitaji ya matumizi ya bdani, viwanda, na mauzo ya nje ya nchi, lazima kuwepo miundo mbinu bora na imara (usafiri ardhini, majini na angani, maji, nishati).
• Kumudu uendeshaji na ukarabati (Operations & Maintenance) wa miundo mbinu hiyo, kunahitaji rasmaliwatu yenye uwezo na ujuzi;
• Kuipata rasmaliwatu wa aina hiyo kunahitajika huduma bora za jamii (elimu na afya).

Mwisho wa yote ni Siasa safi na Uongozi Bora.
 
Choo cha walimu huko masasi
2444028_IMG_20200630_091115.jpeg
 
''The world’s Middle Income Countries (MICs) are a diverse group by size, population, and income level. They are defined as lower middle-income economies - those with a GNI per capita between $1,006 and $3,955; and upper middle-income economies - those with a GNI per capita between $3,956 and $12,235 (2018). Middle income countries are home to 75% of the world’s population and 62% of the world’s poor. At the same time, MICs represent about one third of global GDP and are major engines of global growth.''

Hiyo ni kauli ya WB fuata hii link:Overview

Sasa na wewe omba msamaha kwa upotoshaji wako kama nilivyokwambia hapo awali kwa uongo wa wazi na kukejeli jitihada za Awamu ya 5.
Na hapa omba msamaha kwa upotoshaji. JPM data ni za miaka 3
Dah! We jamaa unachosha kishenzi!! Hivi ulinielewa pale nilipokuambia:-
Mbaya zaidi, watu wanazungumzia issues za 2019/2020 wewe unaleta maelezo y 2016/2017 halafu bado unasema nimeleta data za kupika wakati ni wewe mwenyewe ndie umeleta irrelevant data!!
Watu wanazungumzia ripoti ya leo ya WB, wewe unaleta ripoti ambayo ilikuwa updated November mwaka jana!!
WB2.png


Ripoti niliyokuwekea ndio current ripoti, na ndiyo inayotumiwa hata na serikali:-

WB3.png


Yaani pamoja na ku-bold nikidhani unaelewa unachoki-bold lakini bado unaishia kuweka the very same irrelevant data!!

In short, umeshindwa kujibu maswali niliyokuuliza!!!
 
Uliwaaminisha members kwamba datas zilikuwa za miaka 5 ya JPM wakati huo ulikuwa ni uongo. Pia ukakiri kwamba ulikuwa unaangalia miaka mitano mitano wakati data za miaka 2 ya JPM bado hazijaingia. Sasa unaweza kukiri kwamba ulikuwa unapotosha?
Jibu maswali niliyokuuliza wewe!!

Hivi hujisikii aibu unaweka link wakati ulichoandika ni tofauti na kilichopo kwenye link uliyoweka mwenyewe?! Yaani kuna kila dalili hata usomaji wa fiscal year hujui!

Narudia, kama data za miaka 2 hazijaangizwa, how come GNI ya sasa ionekane imefika 1036+ wakati GNI ya mwaka 2018 ni 1020?!

Jibu hayo maswali!!!
 
We jamaa bhana! Nimekuambia taja hizo figures unazosema ni za kupika, lakini umeshindwa!

Na nimekuhoji kama data za 2019 hazipo, how come tena WB waseme TZ imeingia kwenye LM wakati data za 2018 ni 1020?

Jibu kwanza hayo maswali manake hayo maelezo yako hapo juu ni irrelevant!

Mbaya zaidi, watu wanazungumzia issues za 2019/2020 wewe unaleta maelezo y 2016/2017 halafu bado unasema nimeleta data za kupika wakati ni wewe mwenyewe ndie umeleta irrelevant data!!

Taarifa ya World Bank ni hii hapa:-
View attachment 1494786

Haya unavyoiona imefanana na hicho ulichoandika?! Unaweza kuweka screenshot na link ya hicho ulichoandika? Angalia haya maelezo yako:- Unaweza kusema hizo figures zako zipo sehemu gani kwenye hiyo screenshot?

Halafu eti unadai uchumi wake umeanzia mwaka 2016/2017... sasa hiyo 2016/2017, 2017/2018, 2018/2019 GNI ilikuwa ngapi kama sio 970 wakati alikuta 980?!
Sasa BBC ndio source yako unayoiamini? Ina maana wenyewe WB ambao ndio wanatoa hizo data huwaamini? Au ndio kiwango cha darasa la pili?
 
Khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee Datas hicho ni kiswa-english. Nimemfukuza mpotoshaji amekwenda kuchimba dawa. Amekalia upotoshaji na uzandiki tu.
Acha kujifurahisha wewe! Eti umenifukuza wakati nimekuumbua mchana kweupe!! Maswli niliyokuuliza YOTE, umeshindwa kujibu, na umebaki eti data zangu fake! Nimekupa changamoto utaje hizo data fake, UMESHINDWA KUJIBU!

Lakini wakati unadai hayo, wewe ndo umeweka maelezo ya UONGO, or else, weka screenshot na link ya haya maelezo yako hapa chini:-
those with a GNI per capita between $1,006 and $3,955; and upper middle-income economies - those with a GNI per capita between $3,956 and $12,235 (2018). Middle income countries are home to 75% of the world’s population and 62% of the world’s poor. At the same time, MICs represent about one third of global GDP and are major engines of global growth.''
 
Tanzania tupo $ 1,063.Bado sana kufikia Uchumi wenyewe wa kati .Uchumi wa kati ule wenyewe unaanzia $4,046

Na watalazimisha tuko uchumi wa kati 2025!! Dona kantri masikini!! Uchumi wa kati si nchi zinazozungumzia maji safi na salama, matundu ya vyoo, madawati na nyumba za waalimu!!
 
Kwanza unaelewa maana ya ,,wastani'' tulifundishwa kuanzia Shule ya msingi jinsi ya kutafuta Wastani isitoshe nilifikiri Benki ya Dunia wapo upande wenu akina Zito Kabwe &Co. kwa nini msiwaulize hilo swali?
 
Kwa takwimu hizo, ni ushahidi tosha kwamba JPM amevuruga uchumi, na JK was far better compared to JPM.

Taarifa hiyo ya Benki ya Dunia inasema kwamba:- Kwa maana nyingine, hatimae ndo tumefika kwenye $1036+!!'

Ukiangalia WB Secondary Data, unakutana na hii kitu (GNI per capita by Atlas Method).
View attachment 1494559

Kumbe, 2015 GNI Per Capita by Atlas Method ilikuwa $980. Kwa maana nyingine, kwa miaka 5 mzima, JPM alikuwa anahangaika kuivusha GNI per capita from $980 to $1036... a difference of ONLY $54.

Kinyume chake, GNI Per capita in 2010 ilikuwa kama ifuatavyo:-
View attachment 1494564

Utaona hapo, in 2010 GNI per capita ilikuwa $720, na kwa maana nyingine, GNI per capita ilipanda from $720 in 2010 to $980 in 2015! Yaani ilipanda kwa $260, wakati miaka 5 ya JPM imepanda around $54+!

On top of that, mwaka 2005 GNI per capita ilikuwa $500, na kwa maana nyingine, miaka yake 5 ya kwanza, Mzee wa Msoga alipandisha GNI per capita from $500 in 2005 to $720 in 2010... yaani $220 wakati JPM miaka 5 yake ya kwanza inaonesha kapandisha for less than $100.

View attachment 1494576

Ama kweli mtaji mkubwa JPM ni Jeshi Kubwa la Wajinga lililopo nyuma yake! And JPM anafanikiwa haya kwa sababu ile ile niliyowahi kuitaja siku za nyuma: Tanzania is full of people with average mind, and many more below the average!

Khaaa yaani umefanya haya yote na kuyaandika ili rahisi aonekane hajafanya chochote umejumuisha na matatizo mengine yaliyotokea katikati ambayo yamesababisha uchumi wa nchi mbalimbali kushuka kwa kasi wakati wa JK hakukuwa na corona sisi na corona tumefikia hapo kubalini vya nyumbani jamani
 
Khaaa yaani umefanya haya yote na kuyaandika ili rahisi aonekane hajafanya chochote umejumuisha na matatizo mengine yaliyotokea katikati ambayo yamesababisha uchumi wa nchi mbalimbali kushuka kwa kasi wakati wa JK hakukuwa na corona sisi na corona tumefikia hapo kubalini vya nyumbani jamani

Rais *
 
Sasa BBC ndio source yako unayoiamini? Ina maana wenyewe WB ambao ndio wanatoa hizo data huwaamini? Au ndio kiwango cha darasa la pili?
Look at you?! Hivi unaona kweli wewe?! Yaani hiyo screenshot kuwa na layout nyekundu ndo umeona BBC?! Hivi hushangai screenshot nimetoa hadi address bar ili uone source ni ipi?! Matokeo yake unaanza kashifa, sasa anayeonesha kiwango cha darasa la pili sijui nani!!!

Na kwa jinsi mlivyo nyie watu, huo ndo mwanzo wa kutaka kuanza kumwaga matusi!
 
Acha kujifurahisha wewe! Eti umenifukuza wakati nimekuumbua mchana kweupe!! Maswli niliyokuuliza YOTE, umeshindwa kujibu, na umebaki eti data zangu fake! Nimekupa changamoto utaje hizo data fake, UMESHINDWA KUJIBU!

Lakini wakati unadai hayo, wewe ndo umeweka maelezo ya UONGO, or else, weka screenshot na link ya haya maelezo yako hapa chini:-

Sasa uliponiumbua ni wapi? Ukisoma hiyo clip ya WB ambayo ume-quote mwisho wameandika mwaka 2018 na wamesema kabisa hiyo GNI inakoma wapi? Sasa nikakuuliza ndio level ya darasa la 2? Sasa umeniumbua wapi?
 
Khaaa yaani umefanya haya yote na kuyaandika ili rahisi aonekane hajafanya chochote umejumuisha na matatizo mengine yaliyotokea katikati ambayo yamesababisha uchumi wa nchi mbalimbali kushuka kwa kasi wakati wa JK hakukuwa na corona sisi na corona tumefikia hapo kubalini vya nyumbani jamani
Duh! Ina maana hiyo 2016/2017 ambayo GNI ilikuwa 970 kulikuwa na corona?! Na hiyo 2017/2018 kulikuwa na corona?
 
TANZANIA YAINGIA UCHUMI WA KATI KABLA YA LENGO LA DIRA YA TAIFA YA 2025.

Leo 21:15pm 01/07/2020

Kwa kadiri ya vigezo vya Benki ya Dunia uchumi wa kati una matabaka mawili makubwa. La kwanza ni lile la uchumi wa kati wa ngazi ya chini na la pili ni uchumi wa kati wa ngazi ya juu,

Kabla ya Rais Magufuli kuingia madarakani Mwaka 2015 Tanzania ilikuwa katika uchumi wa chini,chini ya hayo matabaka mawili niliyoyataja hapo juu,Sasa ukiwa Katika Uchumi wa chini kabisa lengo linapaswa kuwa kuelekea uchumi wa kati wa ngazi ya chini,hii ni hatua moja kutoka katika uchumi wa chini,

Baada ya kufikia uchumi wa kati wa ngazi ya chini ndipo tunapaswa kuelekea uchumi wa kati wa ngazi ya juu,Kufikia uchumi wa kati wa ngazi ya juu sio mwisho wa safari ya kwenda juu katika ngazi za uchumi kwa nchi.Ngazi inayofuata baada ya kufikia uchumi wa kati wa ngazi ya juu ni ile ya uchumi wa kipato cha juu.

Lower Middle income ama Uchumi wa kipato cha kati,ni sawa na kusema umepata shamba la kulima,trekta lipo na mvua inanyesha,Sasa tunatarajia utalima,utapanda mahindi au mpunga,utavuna utauza na utapata kipato kitakachokuwezesha kutumiza mahitaji yako na ziada,

Hapa tunaangalia miundo mbinu itayowezesha Mwananchi mmoja mmoja kupata kipato kitachomwezesha kula mlo kamili na kuweka hela ya akiba,Key word kwa hapa ni miundo mbinu itatotupeleka kwenye tokeo chanya.

Maendeleo ya vitu au watu ndiyo yanayopelekea kipato cha mtu kutosheleza mahitaji yale ya muhimu na ziada,Mfano Ujenzi wa Bwawa la Umeme la Rufiji litalofagilia njia ya Ujenzi wa Viwanda vingi kutokana na uwepo wa nishati ya Umeme ya kutosha,

Hatimaye kuzalisha ajira na kuinua biashara kutokana na bidhaa tutazozalisha na kuingiza fedha ya kigeni na kuongeza mzunguko wa pesa na kumfikia kila mwananchi hivyo kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja,

Maendeleo ya vitu tunamaanisha uwepo wa miundombinu ya kufanikisha maendeleo, kama vile barabara na madaraja, reli, viwanja vya ndege na ndege, meli , vivuko, vituo vya afya, zahanati, hospitali, shule, walimu, na hata mifumo ya elimu isiyo malipo, Maendeleo haya ya vitu yatabaki kuwa ni uwekezaji muhimu kwa maendeleo ya watu.

Kipato ni mojawapo tuu ya vigezo vinavyotumika. Tabia nyingine za uchumi wa kati ni pamoja na maendeleo ya uchumi na teknologia, miundombinu, maendeleo ya viwanda, elimu, uwekezaji na kadhalika vilivyo juu ya uchumi wa chini lakini chini ya uchumi wa kipato cha juu.

Hivyo ni muhimu kwa wadau wote kuelewa njozi za kuelekea uchumi wa kati maana yake ni nini na tunatoka na kwenda wapi. Haya yasipofahamika tutakuwa tunasafiri kutoka na kwenda tusikopafahamu.

Kipato Cha mfukoni ni mchango wa mtu binafsi kwa nchi yake.Serikali inamtandikia miundo mbinu sahihi mwananchi, Kisha mwananchi kwa nafasi yake anachakarika kujiongezea kipato (Serikali haina uwezo wa kumfikia mwananchi mmoja mmoja na kumuwekea elfu kumi mfukoni kila siku).

Baada ya kipato cha mfukoni kuongezeka, kinachofuata ni mchango wa mwananchi kwa serikali yake;
1)Kulipa Kodi nyingi zaidi.
2) Kuajiri watu wengine wengi zaidi ambao nao watalipa Kodi.
3) Kuwekeza zaidi kutokana na serikali kuongeza ubora wa miundo mbinu ya kumwezesha huyu mwananchi azidi kuongeza kipato chake kutokana na Kodi inayokusanya kwake (it is a circle).

Jambo la msingi ni kuwa na jicho la kuiona hiyo miundo mbinu ambayo serikali inaitandika kama reli ya wananchi kupita kufanya shughuli zao za kuongeza kipato.

Swali na msingi la kujiuliza hapa, nini hujakifanyi mpaka kipato chako Cha mfukoni hakiongezeki!!!??.

This is lower Middle income after that we will come to Upper Middle income,Kwenye lower Middle Income ianaangalia vigezo vinne,

1-Uwezo wa nchi kupunguza umasikini kwa watu wake.
2-Uwezo wa nchi kukopesheka.
3-Uwezo wa nchi katika kupambana na maradhi kwa maana ya miundo mbinu ya afya kama hospitali,Madaktari na dawa.
4-Uwezo wa nchi katika kukidhi masuala ya elimu na kuondoa ujinga.

Kitakwimu kinachotakiwa ni kuongeza vipato ili wastani wa sasa uweze kupanda. Ni muhimu kuelewa kuwa wastani unakusanya mapato ya watu wote na kugawanya kwa idadi yao.

Bila shaka wapo wenye vipato vikubwa sana, vya kati na vidogo sana. Ili kufikia wastani wa juu wa vipato inabidi kuongeza vipato kwa kasi kubwa hata mnyonge,masikini awe na kipato cha kutimiza mahitaji yake na ongezeko la kipato liwe zaidi ya idadi ya watu.

Kiini cha uchumi wa kati ni kujali maslahi ya watu walio na vipato vidogo,Rais John Magufuli ametembea na wanyonge wenye vipato vidogo kwa miaka mitano ya muhula wake wa kwanza wa Urais kuongeza vipato vyao sambamba na vile vya wenye vipato vya kati na vya juu.

Mh Rais John Magufuli ana kipaji cha kuona sungura na bata kwa wakati mmoja,kiuongozi ana uwezo wa kumwona tajiri na masikini kwa wakati mmoja na wote wakapata haki sawa,kwa kuwajengea miundo mbinu wezeshi kwa kila mmoja kuweza kujipatia kipato,

Hii ni dhana kongwe ya kimtazamo iliyojengeka kifalsafa. Ni uwezo wa mwanadamu katika taswira moja kuwaona viumbe wawili wenye kufanana,Hivyo, inahusu uwezo wa kuliona jambo hilo hilo katika sura tofauti.

Maendeleo ya vitu au watu ndiyo yanayopelekea kipato cha mtu kutosheleza mahitaji yale ya muhimu na ziada,

Maendeleo ya vitu tunamaanisha uwepo wa miundombinu ya kufanikisha maendeleo, kama vile barabara na madaraja, reli, viwanja vya ndege na ndege, meli , vivuko, vituo vya afya, zahanati, hospitali, shule, walimu, na hata mifumo ya elimu isiyo malipo, Maendeleo haya ya vitu yatabaki kuwa ni uwekezaji muhimu kwa maendeleo ya watu.

Lower Middle income ni sawa na kusema umepata shamba,trekta na maji yanatiririka masaa ishirini na Sasa tunatarajia utapanda hata miwa na magimbi ukishindwa kabisa kujiongeza kupanda mahindi au mpunga ili uweze kujipatia kipato,

Hapa tunaangalia miundo mbinu itayowezesha Mwananchi mmoja mmoja kupata kipato kitachomwezesha kula mlo kamili na kuweka hela ya akiba,Key word kwa hapa ni miundo mbinu itatotupeleka kwenye tokeo chanya.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master's in Leadership and Management.

-Research; Assessing Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Data za watawala wa ccm hizo. Hazina ukweli wowote.
Hawajui madhara ya kudanganya kama sisi ni kipato cha kati kwa kupeleka madocuments ya KUBUMBA.

Kuanzia leo misaada ya nchi masikini tunakosa , tukitaka mkopo basi tunapigwa interest ile win win situation wala hakuna kuangalia nyani usoni maana nyie si matajiri wa kipato cha kati.

Yaani tumetoka chini ya dola moja mpaka dola 3 na ushee kwa siku!! Hongereni sana WADANGANYIKA.
 
Back
Top Bottom