Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Nitagombea Urais Upinzani ukinipa ridhaa

Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Nitagombea Urais Upinzani ukinipa ridhaa

Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa Tanzania na kada wa chama tawala cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa miongo mingi Bernard Membe anasema ikiwa vyama vya upinzani vitaungana na kumpa ridhaa ya kugombea nafasi ya Urais, basi atakuwa tayari kupambana na Rais John Magufuli katika uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Oktoba mwaka huu.

Membe amesifia sehemu ya utendaji kazi wa Magufuli, lakini ameyataja baadhi ya mambo ambayo anasema ikiwa hayatabadilishwa, basi yataitumbukiza nchi matatani. Katika mahojiano haya maalum na mwandishi wa BBC Sammy Awami kutoka nyumbani kwake, katika kijiji alichozaliwa Membe alianza kwa kutoa tathmini ya uongozi wa Rais Magufuli.



Chanzo: BBC

Hahahahaha wapinzani mjiandae tena, mmeletewa tena mtu, hahahaha, akishashindwa uchaguzi 2020, taaratibu atarejea CCM huku akiwa mpole na kuomba msamaha hahahaha, wapinzani wa Tanzania itawachukua muda sana kuuelewa huu mchezo!
 
Mkuu kuna kila dalili kuwa ww ni mzee, au kama ni kijana ni wale wavuvi wa kusoma. Hujaona kuwa chanzo ni BBC? Hata hivyo Membe ni tapeli wa kisiasa kama alivyo tapeli mwenzake Lowassa. Na iwapo wapinzani watampa nafasi tutawapa ukweli wao live bila kuuma maneno.
Muacheni Membe buana apeperushe bendera yenu wapinzani ili mshindwe vizuri, then Membe ataendelea kuwa wa kwetu
 
Rudi nyuma shetani


Wala siyo shetani wala nini!

Nakwambia mkimkataa Membe hali yenu ya matokeo ya Uchaguzi mtajuuta hamtoamini si tupo hapo Mwenyezi Mungu anazidi kutupatia uzima?!

Hivi mnazani peke yenu ni rahisi kiivyo?!

Inahitaji akili kubwa kuelewa hili jambo kwa mapana yake!
 
Mkuu kuna kila dalili kuwa ww ni mzee, au kama ni kijana ni wale wavuvi wa kusoma. Hujaona kuwa chanzo ni BBC? Hata hivyo Membe ni tapeli wa kisiasa kama alivyo tapeli mwenzake Lowassa. Na iwapo wapinzani watampa nafasi tutawapa ukweli wao live bila kuuma maneno.


Kumbe mnamchukulia Lowasa kama Tapeli ?!

Inamaana hamtambui mchango mkubwa alofanya wa kuja na hamasa ya wanachama wapya pamoja na kuwa boost kuweza kupata wabunge wengi na madiwani?

Mnazani bila Lowasa mngeweza kufika pale?

Ama kweli shukrani za Punda mateke!
 
Membe usitake kuvuna usipopanda


2020 iache haikuhusu kisha tengeneza 2025 uingie ikulu si kuchallange

Binafsi nashauri urais tumwachie magu kisha ubunge tukapigane tupate wabunge wenye sense of duty. Honour and. Justice
 
Hahahahaha wapinzani mjiandae tena, mmeletewa tena mtu, hahahaha, akishashindwa uchaguzi 2020, taaratibu atarejea CCM huku akiwa mpole na kuomba msamaha hahahaha, wapinzani wa Tanzania itawachukua muda sana kuuelewa huu mchezo!


Kama atasaidia kuongeza idadi ya wanachama, wabunge na madiwani hata akirudi CCM wala haitadhuru kama ilivyokuwa kwa Lowasa.
 
EL alikiletea Chama chetu wabunge na madiwani feki ambao baadaye walirudi hukooo lumumba so EL HASTAHILI SHUKRANI KTK MAGEUZI bali anapaswa kuhukumiwa na wananchi wenyewe aliowaaminisha na wakamwamini kwa kumpa kura kama mwana mageuzi halisi kumbe ni pandikizi la CCM yeye na madiwani na wabunge wote waliorudi lumumba

Kwa kifupi EL alitudharirisha ss wapiga kura, atapokea malipo yake kwa mnyazi Mungu inshallah
Kumbe mnamchukulia Lowasa kama Tapeli ?!

Inamaana hamtambui mchango mkubwa alofanya wa kuja na hamasa ya wanachama wapya pamoja na kuwa boost kuweza kupata wabunge wengi na madiwani?

Mnazani bila Lowasa mngeweza kufika pale?

Ama kweli shukrani za Punda mateke!
 
Mkuu kuna kila dalili kuwa ww ni mzee, au kama ni kijana ni wale wavuvi wa kusoma. Hujaona kuwa chanzo ni BBC? Hata hivyo Membe ni tapeli wa kisiasa kama alivyo tapeli mwenzake Lowassa. Na iwapo wapinzani watampa nafasi tutawapa ukweli wao live bila kuuma maneno.
Mkuu naona umekimbilia kuni attack bila sababu, kwa tulioiona thread dakika chache baada ya kupostiwa aliandika ile haya moja tu. Kaongezea maelezo baadae, anyway huyo Membe Kuna watu wa mataifa ya mbali waliwekeza kwake pesa nyingi sana akiwaaminisha atapindisha meza. Sasa CCM wamemwekea ngumu kibabe, Sasa kaa mkao ukisikia anakuja CDM style ya Lowassa usishangae, hakuna kinachoshindikana kwenye shilingi. Zamu hii ndo mtaelewa kuwa hakuna upinzani wa maana Tanzania.
 
Mimi nawashauri ACT Wazalendo wamchukue mheshimiwa Membe aili agombee urais kupitia chama chao. Mimi naamini Membe ana watu wengi kumwezesha kupata kura za kutosha na wabunge wengine wanaweza kushinda baadhi ya majimbo kwa kupitia Membe (namaanisha watu wanaweza kumpenda Membe mpaka wakampa zawadi ya wabunge kama ilivyokuwa kwa Lowassa na Chadema). Ikiwa itatokea hivi wanaweza kubahatisha na wabunge wa viti maalumu. Japo kushinda Urais sidhani kama inawezekana.
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa Tanzania na kada wa chama tawala cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa miongo mingi Bernard Membe anasema ikiwa vyama vya upinzani vitaungana na kumpa ridhaa ya kugombea nafasi ya Urais, basi atakuwa tayari kupambana na Rais John Magufuli katika uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Oktoba mwaka huu.

Membe amesifia sehemu ya utendaji kazi wa Magufuli, lakini ameyataja baadhi ya mambo ambayo anasema ikiwa hayatabadilishwa, basi yataitumbukiza nchi matatani. Katika mahojiano haya maalum na mwandishi wa BBC Sammy Awami kutoka nyumbani kwake, katika kijiji alichozaliwa Membe alianza kwa kutoa tathmini ya uongozi wa Rais Magufuli.



Chanzo: BBC

nimem disqualify kabisa aliposema eti corruption imekuwa curbed under this regime.
he's a joke!
 
Muacheni Membe buana apeperushe bendera yenu wapinzani ili mshindwe vizuri, then Membe ataendelea kuwa wa kwetu

Labda kama kuna wanaomtaka, ila ukweli ni kuwa Membe ni zao la siasa za mbeleko, na hana uwezo wowote wa kufanya siasa za upinzani. Mimi siamini kwenye hao wazee wa ccm, kama ambavyo sikuwahi kuwa na imani na Lowassa.

ACT hawana namna, maana chama chako kiliundwa na kundi la JK,Membe, Mwigulu, Nape, January nk, ili kuwa backup ya ccm katika kupambana na cdm. Hivyo piga ua, lazima Membe aende ACT maana ana mkono wake huko. Lakini haitatokea kwangu kusupport hayo mazee yaliyochoka ya ccm.
 
Mkuu kuna kila dalili kuwa ww ni mzee, au kama ni kijana ni wale wavuvi wa kusoma. Hujaona kuwa chanzo ni BBC? Hata hivyo Membe ni tapeli wa kisiasa kama alivyo tapeli mwenzake Lowassa. Na iwapo wapinzani watampa nafasi tutawapa ukweli wao live bila kuuma maneno.
Mkuu hitaki democrasia itawale?

Membe ataenda ACT na lengo la zito si kushinda urais bali awape nguvu ya kushinda viti viwili vitatu vya ubunge kwa ajili ya ruzuku ya kuwawezesha Seif na Zitto wasife njaa
 
Safari hii hampati kitu tunaye mgombea wetu TAL
Wala siyo shetani wala nini!

Nakwambia mkimkataa Membe hali yenu ya matokeo ya Uchaguzi mtajuuta hamtoamini si tupo hapo Mwenyezi Mungu anazidi kutupatia uzima?!

Hivi mnazani peke yenu ni rahisi kiivyo?!

Inahitaji akili kubwa kuelewa hili jambo kwa mapana yake!
 
Back
Top Bottom