Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Nitagombea Urais Upinzani ukinipa ridhaa

Uchaguzi 2020 Bernard Membe: Nitagombea Urais Upinzani ukinipa ridhaa

Wapinzani walivyo hawajielewi watampa ridhaa waliwe Kichwa kama 2015
 
Wao ACT sio kumpokea tu Membe, hata wakitaka wahamie nyumbani kwake kabisa, lakini sisi wapiga kura wa upinzani tunaojitambua, hatuko tayari kurudia kosa la Lowassa. Na sana sana hatuko tayari kujitokeza kupiga kura kwa tume hii ya kihuni.
Mkuu naomba nikuulize swali na naomba unijibu toka moyoni., Ikitokea CHADEMA na muungano wa vyama vya upinzani wakakubali kumsimamisha Membe Kama mgombea wao wa uraisi reaction yako itakuwa ni nini!?
NB:. Assume imekuwa hivyo ili jibu lako lisiegemee kuniambia haiwezekani, hata 2015 watu walijiapiza kwa kila namna Lowassa hawezi kuja CHADEMA.
 
C
Uchaguzi ulopita CDM walipata wabunge na madiwani wengi sababu ya uwepo wa Ukawa na Lowasa.

Mkaribesheni Membe faida mtazopata ni nyingi kuliko hasara.
Mkaribisheni huko huko Ccm ashindane Mwenyekiti wenu.
 
Haya mambo yananichanganya sana / au tumpe Membe au Lissu kiukweli mimi sijausoma mchezo vzr
 
Mkuu siku zote unafikra nzuri sana Ila sio kila mtu anafikiri kama wewe. Kwa mfano 2015 ulikuwa unapinga ujio wa Lowassa na kupewa nafasi Kama mgombea, Ila uliona umati uliochukuliwa na upepo wa ""Mabadilikooo Lowassa., Lowassa Mabadilikooo"" huku wakizungusha mikono?????, Najaribu kukupa picha ya wapiga kura wa TZ ambao wengi wao thinking capacity is very low. Kwahiyo unaposema sisi tuliowengi sielewi unamaanisha wananchi hawahawa au wa kutoka bara jingine??!?

Nakueleza waliopiga kura 2015 hawakupata muda wa kujiuliza maana wakibadilishwa gia angani na Mbowe na genge lake. Hali ile ilikuwa kama unapiga hizi nyimbo za injili zenye midundo ya bolingo, mara ghafla unaweka wa Koffi olomide, ni wazi watu wataendelea kucheza, lakini baada ya muda watajua mashairi sio ya Yesu. Kilichoendelea kwenye chaguzi zetu za marudio, uchaguzi wa serikali za mitaa, na Lowassa kurudi ccm, kumewafanya watu kujiuliza mara mbili mbili hizi siasa za kihuni. Ndio maana unaona kwa sasa, wapiga kura wengi wa upinzani, hao uliiwaona 2015, wakigoma kushiriki uchaguzi.

Nakuhakikishia bila tume huru ya uchaguzi, tegemea wapiga kura wachache sana, kwani ccm haina mvuto zaidi ya kushurutisha kukubalika, na iwapo wapinzani hasa cdm wataweka mgombea asiye na mvuto nje ya Tundu Lissu, hamasa itakuwa chini sana. Hilo litapelekea wapiga kura kuwa wachache, au wa wastani lakini wasio na hamasa, kwani kiu yao ya mabadiliko itakuwa haijatimia.
 
Haya mambo yananichanganya sana / au tumpe Membe au Lissu kiukweli mimi sijausoma mchezo vzr
Membe ni kama Lowassa tu,atashindwa uchaguzi then atarudi zake kwao CCM mchezo umeisha.

Pandikizi tu hilo.
 
Nakueleza waliopiga kura 2015 hawakupata muda wa kujiuliza maana wakibadilishwa gia angani na Mbowe na genge lake. Hali ile ilikuwa kama unapiga hizi nyimbo za injili zenye midundo ya bolingo, mara ghafla unaweka wa Koffi olomide, ni wazi watu wataendelea kucheza, lakini baada ya muda watajua mashairi sio ya Yesu. Kilichoendelea kwenye chaguzi zetu za marudio, uchaguzi wa serikali za mitaa, na Lowassa kurudi ccm, kumewafanya watu kujiuliza mara mbili mbili hizi siasa za kihuni. Ndio maana unaona kwa sasa, wapiga kura wengi wa upinzani, hao uliiwaona 2015, wakigoma kushiriki uchaguzi.

Nakuhakikishia bila tume huru ya uchaguzi, tegemea wapiga kura wachache sana, kwani ccm haina mvuto zaidi ya kushurutisha kukubalika, na iwapo wapinzani hasa cdm wataweka mgombea asiye na mvuto nje ya Tundu Lissu, hamasa itakuwa chini sana. Hilo litapelekea wapiga kura kuwa wachache, au wa wastani lakini wasio na hamasa, kwani kiu yao ya mabadiliko itakuwa haijatimia.


Absolute Mbowe na Zitto na lipumba na maalimu seif wanatumia akili ndogo hawezi kuipindua ccm,

Naomba membe akagombee kwao ccm
Lissu chadema tofauti na hapo kura yangu nampa Magufuli au sipigi kura.
 
Mkuu naomba nikuulize swali na naomba unijibu toka moyoni., Ikitokea CHADEMA na muungano wa vyama vya upinzani wakakubali kumsimamisha Membe Kama mgombea wao wa uraisi reaction yako itakuwa ni nini!?
NB:. Assume imekuwa hivyo ili jibu lako lisiegemee kuniambia haiwezekani, hata 2015 watu walijiapiza kwa kila namna Lowassa hawezi kuja CHADEMA.
Kwangu mimi wakifanya hivyo sitapiga kura na nitawaona wapinzani ni mataahira kwa 100%.
 
We muache Mbowe aje alete utopolo tutamvunja mguu wa pili.
Akiruhusu upuuzi wa Membe kugombea kupitia Chadema nita-confirm Rasmi Mbowe ni pandikizi la CCM na hana tofauti na wakina Mbatia,Mrema,Cheyo,Shibuda etc.
 
Membe angepata heshima kubwa kama angejitokeza kuwa mbele kuleta mapinduzi bila ya kuweka masharti ya kupewa nafasi ya uongozi katika chama chochote au sehemu yoyote.

Hii ingewaonyesha watu kwamba anachukizwa na yaliyopo huko CCM, kwa hiyo yeye atachangia kwa vyovyote iwezekanavyo kuyaondoa.

Huo ndio ungekuwa msisitizo wake.

Na baada ya kufanya hivyo kazi na kuleta mafanikio, basi, angefikiriwa kupewa nafasi yoyote ya uongozi mbali ya hiyo ya urais.

Kauli mbiu iwe: "Kazi Kwanza, Malipo ni Baada ya Kazi."
 
Nakueleza waliopiga kura 2015 hawakupata muda wa kujiuliza maana wakibadilishwa gia angani na Mbowe na genge lake. Hali ile ilikuwa kama unapiga hizi nyimbo za injili zenye midundo ya bolingo, mara ghafla unaweka wa Koffi olomide, ni wazi watu wataendelea kucheza, lakini baada ya muda watajua mashairi sio ya Yesu. Kilichoendelea kwenye chaguzi zetu za marudio, uchaguzi wa serikali za mitaa, na Lowassa kurudi ccm, kumewafanya watu kujiuliza mara mbili mbili hizi siasa za kihuni. Ndio maana unaona kwa sasa, wapiga kura wengi wa upinzani, hao uliiwaona 2015, wakigoma kushiriki uchaguzi.

Nakuhakikishia bila tume huru ya uchaguzi, tegemea wapiga kura wachache sana, kwani ccm haina mvuto zaidi ya kushurutisha kukubalika, na iwapo wapinzani hasa cdm wataweka mgombea asiye na mvuto nje ya Tundu Lissu, hamasa itakuwa chini sana. Hilo litapelekea wapiga kura kuwa wachache, au wa wastani lakini wasio na hamasa, kwani kiu yao ya mabadiliko itakuwa haijatimia.
Ni vigumu kunielewa maana umeamua kuvutia upande wako. Na una Imani na uelewa wa wapiga kura as if wanajitambua. Okay., Tume haiko huru kama unavyodai, Ila wapinzani watashiriki Kama kawa bila kujali. Wapiga kura watakuwa wachache Kama unavyodai Ila uchaguzi utafanyika, unadhani wapinzani wanategemea nini kushiriki?, Na matokeo yatakuwaje kwa mtazamo wako!?
 
Mkuu naomba nikuulize swali na naomba unijibu toka moyoni., Ikitokea CHADEMA na muungano wa vyama vya upinzani wakakubali kumsimamisha Membe Kama mgombea wao wa uraisi reaction yako itakuwa ni nini!?
NB:. Assume imekuwa hivyo ili jibu lako lisiegemee kuniambia haiwezekani, hata 2015 watu walijiapiza kwa kila namna Lowassa hawezi kuja CHADEMA.

Kwanza mkuu mimi sio mwanachama wa cdm, bali ni shabiki wa kutupwa wa cdm. Hivyo sina maamuzi yoyote ndani ya cdm. Kama wapinzani kwa muungano wao wataamua kumsimamisha Membe, hilo siwezi kuwazuia, lakini mimi sintokuwa mmoja ya watakaounga mkono uamuzi huo. Nitahakikisha natumia ushawishi wangu mitaani, na huku jukwaani kupinga uamuzi huo wa kurudia kosa kama la Lowassa.

Tutakuwepo watu ambao tutafanya siasa za kuikataa ccm, bila kutegemea wala kukiunga mkono chama chochote cha siasa, au kwa umoja wao kumsimamisha huyo muhuni. Bora wapinzani wapate kura 10 za mapambano, kuliko kura millioni kutoka kwa wazee wahuni wa ccm. Mimi bado msimamo wangu ni kudai tume huru ya uchaguzi, kuliko kushiriki uchaguzi wa kihuni.
 
Membe angepata heshima kubwa kama angejitokeza kuwa mbele kuleta mapinduzi bila ya kuweka masharti ya kupewa nafasi ya uongozi katika chama chochote au sehemu yoyote.

Hii ingewaonyesha watu kwamba anachukizwa na yaliyopo huko CCM, kwa hiyo yeye atachangia kwa vyovyote iwezekanavyo kuyaondoa.

Huo ndio ungekuwa msisitizo wake.

Na baada ya kufanya hivyo kazi na kuleta mafanikio, basi, angefikiriwa kupewa nafasi yoyote ya uongozi mbali ya hiyo ya urais.

Kauli mbiu iwe: "Kazi Kwanza, Malipo ni Baada ya Kazi."

Hapa nakuunga mkono kwa asilimia mia moja. Haiwezekani mtu akae kwenye chama chake muda wote, kisha akikosa nafasi ndio aje upinzani, halafu atake nafasi ya juu. Wakati huo huo wapinzani tukiwa hatujasahau maumivu ya Lowassa, na wabunge wengine waliokuwa ccm kabla ya uchaguzi 2015, na walipopata ubunge kupitia upinzani, wakaribuniwa warudi ccm kwa gharama za kuuchafua upinzani. Tulipofikia panatosha.
 
Mkurupukaji ni wewe, hujaona chanzo

BBC hapo???
Umekuja Sasa hivi saa 8, unajua saa 5 wakati anapost thread aliishia wapi?, Hujui watu JF wanaletaga habari nusunusu waonekane wa kwanza kupost baadae wanaongezea story?., Mimi sio mjinga kumwambia hivyo, alileta story robo mwanzoni.
 
Ni vigumu kunielewa maana umeamua kuvutia upande wako. Na una Imani na uelewa wa wapiga kura as if wanajitambua. Okay., Tume haiko huru kama unavyodai, Ila wapinzani watashiriki Kama kawa bila kujali. Wapiga kura watakuwa wachache Kama unavyodai Ila uchaguzi utafanyika, unadhani wapinzani wanategemea nini kushiriki?, Na matokeo yatakuwaje kwa mtazamo wako!?

Vyama vya upinzani kama vyama, kuamua kushiriki huo ni uamuzi wao. Lakini sisi wapiga kura hasa wa upinzani tunaojitambua, hatuko tayari kwenda kupiga kura ambazo Magufuli anaamua nani atangazwe mshindi. Hao wapinzani wa kweli kushiriki kwenye uchaguzi huu, ni kubariki hujuma kuendelea kufanyika miaka na miaka kwenye chaguzi zetu.

Wapinzani wanaamua kushiriki ili kupata baadhi ya viti kwa minajili ya kupata ruzuku ya kuendeshea vyama, lakini matokeo watakayopata baada ya kushiriki hilo zoezi haramu, litawaharibia haiba yao, na mvuto kwa wafuasi wao. Ni bora kutokushiriki na kupaza sauti ya tume huru ya uchaguzi, kwani wataharamisha huo uchaguzi, na hata kama ccm watakaa madarakani kibabe, basi itakuwa ni bila ridhaa ya umma. Hili litawaacha wapinzani na base yao ya wafuasi.
 
Ohooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo.
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa Tanzania na kada wa chama tawala cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa miongo mingi Bernard Membe anasema ikiwa Vyama vya Upinzani vitaungana na kumpa ridhaa ya kugombea nafasi ya Urais, basi atakuwa tayari kupambana na Rais John Magufuli katika uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Oktoba mwaka huu.

Membe amesifia sehemu ya utendaji kazi wa Magufuli, lakini ameyataja baadhi ya mambo ambayo anasema ikiwa hayatabadilishwa, basi yataitumbukiza nchi matatani. Katika mahojiano haya maalum na mwandishi wa BBC Sammy Awami kutoka nyumbani kwake, katika kijiji alichozaliwa Membe alianza kwa kutoa tathmini ya uongozi wa Rais Magufuli.



Chanzo: BBC
Hahaha, yaleyale ya Lowassa kukubaliana na mshindi wa CCM.

Ushauri wa bure;

Ni bora wapinzani wasishiriki uchaguzi mgombea wa ccm apite kuliko kupokea masalia kutoka ccm wanaokuja kudhoofisha Ari ya Upinzani
 
Back
Top Bottom