Biashara gani zinazoingiza mamilioni kwa muda mfupi?

Biashara gani zinazoingiza mamilioni kwa muda mfupi?

Vizuri..Hili zao la mihogo shambani linachukua muda gani hadi kuvuna?
Linachukua sio chini ya miezi saba ndio maana nililima eka 5
niunganishe nao mkuu nilime muhogo kwa bei yao elekezi
Achana nao bei sasa hivi haillipi kabisa nisikudanganye. Uzuri wa mhogo ukishafunga juu majani hupalilii tena.

Ila nwanzoni kusafisha shamba na zile palizi 2 au 3 inakula, ingawa jamaa yangu mmoja alimwaga dawa ya magugu.

Ile kampuni ni ya Mhehe mmoja anaishi China. Alinikuta pale Mwenge vijana wake wamechambua mihogo yangu mengine wakaitupa alipofika aliirudisha yote kwenye viroba vikapimwa tena.

Nilipokaa nae mezani kuhusu bei alikataa kuongeza anadai ni mambo ya soko la dunia.

Hiyo Kampuni iko Mwenge hawajaweka bango nje sijui kwa nini ila ukitokea zile taa kuelekea cocacola mita 100 njia ya kwanza kulia unapita ya pili nadhani unaingia kulia halafu unaenda mita 40 au 50 kuna geti jeusi, mi mwaka mzima sijafika pale sijui kama bado wapo ila hapo ndio mhogo wangu uliwekwa halafu nikaitwa niupime tena katika kg 50 bags ili wanilipe, kuna viroba vingine vilizidi vingine vilipungua.

Naona kuna watu wanauliza mhogo unachukua muda gani. Haipungui miezi 7
Ila ili angalau kila shina lifike wastani kg 20 ni miezi 8 au 9.

Ndio maana inabidi ulime angalau eka 4 na kuendelea.

Hata wao ukiwaambia eka moja hawafuati mzigo ni hasara.

Eg:

18kg x 4000 miche kwa eka x ( bei) ya kununua x eka 5 ndio utaona matusi yake.

Ila mhogo mkavu unapungua uzito nusu
Achana na mhogo kwa sasa mpaka mazingira yakae vizuri.
 
Hongera Mkuu, pia umetoa somo zuri! Inaonekana unaweza kuzalisha muhogo kwa kwango cha kutosha, kabla hujaachana na kilimo cha muhogo je kwanini usitafte wanunuzi wengine? Jamani humu JF hakuna mnaofahamu wanunuzi wengine wa muhogo ndani na nje ya Dar?
Hakuna tena wengine wote tunagombaniana Buguruni, huu mhogo wachina sio wanakula wanafuata starch na kuna mbegu maalum yenye starch nyingi.
 
Mkuu hakuna biashara halali inayoingiza mamilioni ndani ya muda mfupi, hata hicho kilimo ili uweze kuzalisha pesa panahitahitaji uwekezaji mkubwa ndipo faida yake itaonekana!

Vivyo hivyo katika biashara yoyote, kadri mtaji utakavyokuwa mkubwa ndivyo kiwango cha faida kitakavyosoma!

Ila tu jambo la msingi ni soko la bidhaa unayokusudia kufanyia biashara, mfano kama kila ukichukua mzigo unamaliza ndani ya siku chache, hapo zidisha maarifa ni lazima utatoboa! Lakini kama Bidhaa inachukua muda mrefu kupata wateja, utajikuta unakula faida yote na si ajabu ukala hadi sehemu ya mtaji.
Biashara ikiwa namna hiyo ni kubadilisha haraka maana mtaji ni lazima utadidimia na hata kufilisika kabisa.

Hata hivyo katika biashara uvumilivu wa kufikia mafanikio nao pia unahitajika, historia ya mabilionea wa dunia kama kina Bill gates, inaonyesha mwanzoni mwa biashara zao walikula hasara mara kibao tu, lakini uvumilivu na maarifa vikawavusha mpaka kufikia records walizonazo!
 
Nimegundua wengi wanao comment hapa wanatumia "elimu" zao wanaogopa kuchafuka shambani. Wengine mashamba wanayaona kwenye picha tu.

Jambo la kumshukuru Mungu TZ unaweza kumiliki eka ardhi ya kutosha bila ubabaishaji.

Sasa hivi nina mkataba na kampuni nyingine na wameshaniuzia mbegu sio mhogo.

Mi napenda kutoa hoja kwa kitu nimepitia
Baada ya miezi 5 nitaanza kupiga hela
Nitarudi hapa
Na logg Off.
 
Nimegundua wengi wanao comment hapa wanatumia "elimu" zao wanaogopa kuchafuka shambani. Wengine mashamba wanayaona kwenye picha tu.

Jambo la kumshukuru Mungu TZ unaweza kumiliki eka ardhi ya kutosha bila ubabaishaji.

Sasa hivi nina mkataba na kampuni nyingine na wameshaniuzia mbegu sio mhogo.

Mi napenda kutoa hoja kwa kitu nimepitia
Baada ya miezi 5 nitaanza kupiga hela
Nitarudi hapa
Na logg Off.
Nataka niwekeze huko nipe elimu mkuu..

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Nimegundua wengi wanao comment hapa wanatumia "elimu" zao wanaogopa kuchafuka shambani. Wengine mashamba wanayaona kwenye picha tu.

Jambo la kumshukuru Mungu TZ unaweza kumiliki eka ardhi ya kutosha bila ubabaishaji.

Sasa hivi nina mkataba na kampuni nyingine na wameshaniuzia mbegu sio mhogo.

Mi napenda kutoa hoja kwa kitu nimepitia
Baada ya miezi 5 nitaanza kupiga hela
Nitarudi hapa
Na logg Off.
Kaka mie ni mkulima mwenzio, ni kampuni gani uliyoingia nao mkataba na mkataba wa kilimo gani? Najikita sana kwenye kilimo nimelima ufuta nahitaji kilimo cha mkataba nami nifaidike
 
Nataka niwekeze huko nipe elimu mkuu..

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Subiri mrejesho baada ya miezi 6 sasa hivi niko na maandalizi.
Kaka mie no mkulima mwenzio ni kampuni gani uliyoingia nao mkataba na mkataba wa kilimo gani? najikita sana kwenye kilimo nimelima ufuta naitaji kilimo cha mkataba nami nifaidike
Ndugu yangu niwe muwazi ngoja nifike hatua ya kuuza ndiyo tupeane akili.

Zisije tokea changamoto. Kwa mfano kampuni moja mnunuzi mmoja wa hiyo kitu alikufa kwa covid jamaa walisumbuka kidogo. Tuvute subra.

Waliniambia nitafute mwanasheria kabisa ausome mkataba kama uko sawa.

Tukiwa wengi ndio bora.

Hata mi nimenufaika na wadau kwa mambo mbali ua kilimo humu. Tuombe uhai.
 
Subiri mrejesho baada ya miezi 6 sasa hivi niko na maandalizi.

Ndugu yangu niwe muwazi ngoja nifike hatua ya kuuza ndiyo tupeane akili.

Zisije tokea changamoto. Kwa mfano kampuni moja mnunuzi mmoja wa hiyo kitu alikufa kwa covid jamaa walisumbuka kidogo. Tuvute subra.

Waliniambia nitafute mwanasheria kabisa ausome mkataba kama uko sawa.

Tukiwa wengi ndio bora.

Hata mi nimenufaika na wadau kwa mambo mbali ua kilimo humu. Tuombe uhai.
Kwaiyo tusubiri hadi mwezi wa tisa mkuu..?

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Taarifa za kufanikiwa katika biashara zinapatikana kila mahali lakini hakuna mahali wamoenyesha hizo biashara zinazosababisha hayo mafanikio ni biashara za aina gani hizoo?

Soko la mitaji likiwa katika hali ya kuzorota

Ni biashara gani inayoweza kukufanya kuwa milionea katika kipindi cha miaka michache ijayo?
Biashara ya mazao, ila kwanza lazima uwe na soko la uhakika!! Ndani ya muda mfupi sana, watu watakuhisi vingine!!
 
Taarifa za kufanikiwa katika biashara zinapatikana kila mahali lakini hakuna mahali wamoenyesha hizo biashara zinazosababisha hayo mafanikio ni biashara za aina gani hizoo?

Soko la mitaji likiwa katika hali ya kuzorota

Ni biashara gani inayoweza kukufanya kuwa milionea katika kipindi cha miaka michache ijayo?
 
Uwekezaji wa kilimo Tanzania ni biashara kichaaa, narudia ni biashara kichaa, ndio mana TRA hawahangaiki, ni umaskini mtupu, ili utoboe inahitaji uwe na capital nzito na kama mvua zikikubali inabidi utafute masoko nje kitu ambacho serikali sometyme inapiga ban... Ukivuka hapa mashalah

La sivyo ufanye usenge wa kusubiri bei ipande Kwa soko la ndani Jambo ambalo linategemea pia misimu miwili au mitatu ya kutokuwepo Kwa mvua, maana mvua ikikubali Tu mzigo unajaa tena au ufanye processing uzalishe end product na ufanye packaging (mtaji mzito kweli kweli) vinginevyo ulime kwenye scheme kipindi ambacho mvua sio za uhakika kwa maeneo mengine.....

Kwa projection hzo uwekezaji wa kilimo capital yake jamaa mwingine akiifanyia harakat zingine za mtaa lazima akuache mbali.....

Hata hivyo kilimo ni sehemu sahihi ya kutaftia mtaji .... Lakini kusema unaishi Kwa kutegemea kilimo Kwa bongo hii aisee kuna sku uta go down unaona hvi hvi ukiwa umechakaa na Sura kukunjamana ....
 
Kama ukipata taarifa sahihi na connection ya kutosha kwa wahusika wenyewe utajua ukweli wote. Ila kwa sasa na hali ilivyo naona ishu za dhahabu zina pesa. Ila mpaka upate ujuzi na connection sahihi. Narudia tena ni kuwa ishu za dhahabu zinapesa nyingi mno ila inabidi upate ujuzi na connection ya kutosha.

NB: Mimi sina connection wala ujuzi.
 
Aisee mkuu Acha Tu hii kitu , na bado mvua zimekubali ina maana mwezi wa nne Tu mwishoni mchele unamwagika tena sokoni , kupeleka nje ya nchi serikali wanazingua mpak uwe na connection na wakubwa , soko la ndani nalo ni extremely poor ...gharama za uendeshaji shambani ni nouma ....ni kulamba tope mwanzo mwisho, vibarua nao ni mtihani mwingine 😃😃...aaah kilimo hapana kabisa

Na kuna watu wanalima bado eka 1 ya mpunga...yaan hizo gharama zake sasa..alafu anakuambia ohh nahifadhi gunia ukipanda niuze .ss kaa naye chin mpigie hizo hesabu🤣🤣,hana anachofanya😶😶
 
Na kuna watu wanalima bado eka 1 ya mpunga...yaan hizo gharama zake sasa..alafu anakuambia ohh nahifadhi gunia ukipanda niuze .ss kaa naye chin mpigie hizo hesabu🤣🤣,hana anachofanya😶😶
Naona kuna mwamba hapo juu anawapa ABC za kilimo cha mihogo hata hvyo anatoa great warning wasijarbu Kwanza Hali haiko pouwa ...but naona Wana wameiva kweli kweli wanaforce awaunganishe na sponsor 😃😃 mi npo Tu hapa nawazoom huku nikiongeza 🍿 ...nawaza Tu Kwa nini asiwaruhusu wakajaa alaf kilimo chenyewe ndo kiwafurahishe 😀😋
 
Naona kuna mwamba hapo juu anawapa ABC za kilimo cha mihogo hata hvyo anatoa great warning wasijarbu Kwanza Hali haiko pouwa ...but naona Wana wameiva kweli kweli wanaforce awaunganishe na sponsor 😃😃 mi npo Tu hapa nawazoom huku nikiongeza 🍿 ...nawaza Tu Kwa nini asiwaruhusu wakajaa alaf kilimo chenyewe ndo kiwafurahishe 😀😋

Kuna kikampuni cha wachina 2016 walisema limeni mihogo kwa wingi tutanunua kilo 1000/= wana wakajaa wakaja moro kwa fujo wakalima hatari...mhogo ulipokomaa wakanunua kwa shilingi MIA...narudia..shilingi MIA..hahaa wapi shogangu Shoma...alidata balaa🤣🤣..cheza michezo yote sio mchezo wa soko la TZ
 
Back
Top Bottom