Biashara Tanzania ni pasua kichwa. Ukiondolewa kwenye reli, kurudi na kukaa sawa si rahisi

Biashara Tanzania ni pasua kichwa. Ukiondolewa kwenye reli, kurudi na kukaa sawa si rahisi

Wabongo mkiona mtu amefanya reshuffle ya biashara mnasema kafirisika, Sumry kafirisika lini?
Mfano Mohamed Trans alifirisikaje wakati alikufa mali wakagawana familia sasa mitoto imeleta ubishi kuendesha biashara ikashindwa ikapiga bei mabasi na miundombinu yake na kuhamia mambo mengine. Hapo founder kafirisika?

Kwa mtazamo huu mtasema Siemens walifirisika kisa walikuwa wanatoa simu ila hawatoi siku hizi, wao waliona simu ni vitu kila mwaka unaumiza kichwa utoe products mpya wakaamua wakomae na mitambo ya energy kama gas turbines na mifumo mikubwa ya umeme duniani.
Kuna watu biashara ikileta changamoto wanahamia kwingine, au profitability ikipungua au threats of new intrants au akifika threshold fulani anaona kukua hakupo tena anahamia kwingine au utaalamu ukipungua labda alikuwa ni mhasibu ila uzoefu wa miaka 30 anaona kwa sasa vijana wanakuja na mambo ya computerized accounting yanamchanganya na hawezi kuwa master tena anabadili service kutoka kuwa mhasibu na kuwa agent. Au mtu kuanzia miaka ya 90 alipata hela sana kwenye clearing & forwarding alikuwa giant ila siku hizi anaona imevamiwa anahamia kwenye betting.

Kuna watu hawakazi kichwa kwenye biashara fulani tu, akisoma mchezo anahama. Badala yake kuna wengine wanakomaa anakopa anafanya ili na lile biashara hiyo hiyo.
Umeelezea kitaalamu sana. Kuna mama mmoja wa Arusha alikuwa na vibanda kibao vya simu mwanzoni mwa miaka ya 2000 na pia alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kuuza simu za kutoka Dubai ila baada tu ya watu kuwa wengi akahamia kwenye mambo mengine na kuachana kabisa na ishu za kuuza simu. Watu walidhani maza kalost mara kaibukia kwenye malori ya mchanga na kuanza kuwa muuza matofali (blocks) maarufu. Kuna watu wana vipaji hadi wanatisha..
 
Watu wanasema mohamed trans kafirisika!! Hivi mtu akifa anafirisika?

Mfano leo mzee tashrifu kafariki kaacha Bus zinapiga kazi mwakani kampuni ife utasema tashrifu kafirisika?

Ukweli ni kwamba waarabu au watu wenye asili ya Asia wanajua sana biashara kwa hapa bongo.

Mfano yule mwarabu wa shinyanga alivuma sana na kampuni ya allys sport bus miaka ya 2009 baadae akawa kimya amekuja kurudi upya na kampuni ya mpya ally star bus na ndo kaishikilia njia ya dar mwanza anatoa gari nyingi kwenda na kurudi kila siku kwenye njia hiyo.

Mtu anachukua nauli 120k dar to mwanza na gari inajaa kila siku hata ukienda kukata tickets unaambiwa kesho VVIP Bus imejaa!! Gari yenyewe sasa hata sio VVIP
 
Watu wanasema mohamed trans kafirisika!! Hivi mtu akifa anafirisika?

Mfano leo mzee tashrifu kafariki kaacha Bus zinapiga kazi mwakani kampuni ife utasema tashrifu kafirisika?

Ukweli ni kwamba waarabu au watu wenye asili ya Asia wanajua sana biashara kwa hapa bongo.

Mfano yule mwarabu wa shinyanga alivuma sana na kampuni ya allys sport bus miaka ya 2009 baadae akawa kimya amekuja kurudi upya na kampuni ya mpya ally star bus na ndo kaishikilia njia ya dar mwanza anatoa gari nyingi kwenda na kurudi kila siku kwenye njia hiyo.

Mtu anachukua nauli 120k dar to mwanza na gari inajaa kila siku hata ukienda kukata tickets unaambiwa kesho VVIP Bus imejaa!! Gari yenyewe sasa hata sio VVIP
huyu Allys alifariki hizo basi pia zikagawanwya mke mkubwa na watoto wake na mke mdogo na watoto wake, ila wengine wamashafilisika yule allys star ndo kabaki peke yaje, na watoto wa Muhammad transi wengi wamefilisika mpaka kuuza migodi ya halmasi. Kwa ufupi na waarabu wengi wanafilisika ila wanafichiana siri hawasemane kama sisi wa makonde, wengi walisha filisika kokoo ni omba omba ila huwezi kugundua jinsi wanavo fichana siri.
 
tatizo la wengi tukishafanikiwa kwa aina fulani ya biashara tunaona kama hiyo biashara tutadumu nayo milele.
hatuwazi kabisa kutengeneza binary za kibiashara, kwamba biashara moja ni mtaji wa biashara nyingine.

na tunajisahau sana kwenye starehe sera za TRA ni kwa uchache sana zitakuathiri ila tatizo kubwa lipo kwetu.

kwa mfano unamiliki bus dar moro then unaona kabisa SGR inapita route yako, si upeleke gari mbeya. Mchawi wa biashara ni wewe mwenyewe.
 
Zamani nilikua najiuuliza kwanini wafanya biashara wengi wana punguza mitaji yao na kujenga majumba, kumbe ni security yao biashara hapa kwetu ni unpredictable, kwa sera moja ya TRA mtaji unakatika kwa siku moja
Ni kweli biashara Ina badilika lazima uwe na assets za kutosha.
Sor nje ya mada hivi mkiwa mnastorisha mkafikia kwenye gari hiyo harrier na upo na mtu unamuheshimu utamwambia " harrier Tako la nyani" Kwa mfano baba mkwe
 
Leri = reli.
Ni kweli boss inahitaji uvumilivu na akili ya ziada kurudi kwenye mstari ukianguka. Muhimu ni kumwomba sana Mungu kukupa utulivu wa akili unapopatwa na majanga kwenye biashara. Yaani hata kama umeanguka kabisa muhimu ni kuhakikisha àkili yako ipo sawa na huendeshwi na mihemko.

Cha kwanza kubali kabisa kwamba tayari maji yamezidi unga inahitaji muda na mbinu kurudi relini. Katika mikakati mipya pambana sana kukwepa kuchukua mkopo. Bora kama una cheti kutafuta ajira ukapiga kwanza huku ukitunza pesa. Kama ajira hakuna anza na ulicho nacho mkononi. Hata kama ni uchinga bora uanzie hapo.

Tatizo wengi wakianguka wanaanza kuwa na presha na kutokukubaliana na hali. Watakurupuka kuuza vitu na kuchukua mikopo na kujikuta kwenye majanga zaidi. KUANGUKA KWENYE BIASHARA ni kawaida ila kurudi tena relini ni wachache wanaoweza.
Sijamaliza kusoma ila hapo kwenye MUNGU yaani Mungu ndo Kila kitu
 
Ni kweli biashara Ina badilika lazima uwe na assets za kutosha.
Sor nje ya mada hivi mkiwa mnastorisha mkafikia kwenye gari hiyo harrier na upo na mtu unamuheshimu utamwambia " harrier Tako la nyani" Kwa mfano baba mkwe
Neno tako kwa mswahili sio tusi hata mama mkwe hulitamia bila aibu........labda kwa watu wa bara baadhi
 
Jamani wafanya biashara wenzangu nilicho gundua hapa nchini kila siku mambo hubadilika katika biashara na soko.

Kuna marafiki zangu wawili walipata setback kwenye biashara zao moja alikua na mtaji kati ya 70-80m masuala ya ndoa ya kugawana mali na mke akamuondoa kwenye leri ya biashara mgine alikua ana capital base150-200m aliondolewa kwenye leri ya biashara kwa sera mbovu za uchumi za jpm 2016 Ni lidhani baada ya mda mfupi mwaka au miaka miwili watarudi lerini lakini wapi.

Leo ni meenda kuwajulia hali zao kumbe mambo bado wana jikongoja hawajarudi full kwenye biashara moja gari hana anatumia daladala mgine anatumia gari number 'A' kaipata kwa milioni 6 baada yakuuza harrier tako la nyani aongezee kwenye mtaji wake ilio bakia ndo kanunua hiyo no A.

Jamani kama una mtaji wako utunze kwa makini usiigii kwenye biashara usio jua na huna wakika nao mtaji ukikata kurudusha sio rahisi. Mambo ya meshabadilika sio kama zamani.

Goodwill ya Biashara ia built with time na inakuwa recovered kwa time kama nilipotea, sasa ukitoka kwenye Biashara, kurudi ni Ngumu maana mifumo, mabadiliko etc hubadilika, lazima uwe mbunifu sana, Capital can be recovered, not Goodwill au wateja, wanakuwa wamemove on!

Ukivurugikiwa na Biashara wakati umeoa, kuinuka kunaitaji roho ngumu sana na determination ya hali ya juu, sio rahisi, na ndo mda wa kutosikiliza mtu zaidi ya determination zako.

Kama unaweza, hudumia watoto na mke na kaa mbali kabisa ili iwe rahisi kuanza upya kufanya bidii, hao wanaweza wasiinuke milele, Amina, Haleluya! Wanaweza ishia kufa na sonona.
 
Muhamed trans hajafilisika.. mpaka leo bado ni tajiri..

Waarabu huwa wanabadilisha biashara. Kama sumry alivyoua ma bus na kwenda kwenye large scale agliculture.

Mohammed trans mpaka leo wana malori kibao. Na sheli wanazo za kutosha tu
Yah story ya mohamed trans niliisikia nasikia alichukua mkopo wa pesa nyingi akaweka bond baadhi ya mali kumbe ilikua ni trick yale mabasi yalipigwa mnada na pesa ya mkopo ameinvest,naskia sku iz amehamia mwanza ?
 
Mkuu ulishawahi kupitia hiyo hali au unatoa tu ushauri kwa kutumia uzoefu wako?
Jamaa alichokiongea ni sahihi na kina uhalisia.
Unapojikuta umeanguka tumia hicho hicho kidogo ulichonacho kujikongoja hadi ufikie level unayotaka,shida iliyopo wengi huwa wanaona aibu kushuka chini kutokana na status waliyojiwekea.
Wewe huoni wale wachina wamekwea pipa kutoka kwao kuja TZ kisha wanauza viatu kwenye meza sasa wale ndio real enterpreneur wala hawana muda wa kuwaza kwamba watachekwa as long as their plan is to be a future millionaires/billionaires.
Pia usisahau ya kwamba mtaji namba moja ni ideas ulizonazo kichwani.
 
Afadhali hao Ndugu zako mitaji yao ilikuwa inapukutika kidogo kidogo, mimi rafiki yangu alienda kuchukua nguruwe 200 mbeya wenyewe thamani ya mil 50,kumbe homa ya nguruwe ilikuwa imeanza kuingia kimya kimya anafika dar anawaswaga zizini kesho yake asubuhi anakuta nguruwe zote zimekufa.
Napewa taarifa rafiki yako amepoteza fahamu yupo rabinisia baada kupata fahamu akasema mapambano yanaendelea😄
 
Back
Top Bottom