Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake

Biashara ya Daladala: Ushauri na Mbinu za Uendeshaji Wake

images

Hii biashara ni pasua kichwa sana! nilinunua coaster 2 mpya hzo hapo juu nilizifuatilia mwenyewe kutoka Japan nilichokutana nacho siyo kabisa! nilipata rout ya moro dar madereva hesabu siiyoni mara unapigiwa simu gari imedakwa hata wiki haijaisha natoa hela nyingi zaidi ya zinazoingia nakaisaliti hyo biashara! nikajaribu tena njia nyingine ya kubeba watalili bahati nzuri nikafanikiwa kupata rout ya Arusha gari kule zilitakiwa zikae huko wiki 2 sijakaa vizuri simu ikaingia ujumbe mfupi kuwa gari zimeharibika kwenye engine matengenezo ni Million 120 hapo ndipo nilipo pata hasara ya ajabu hela sikuipata ya kukodi gari maana watu niliowachukua walitakiwa warudi ndipo nichukue changu hawakurudi walikodishiwa gari nyingne! Ndiyo ikawa mwisho wa hii biashara! gari zote nimeuza! Tena niliweka hadi bandiko hapa jf gari aina ya coaster inauzwa! Biashara ya kichaa sifanyi!

Matengenezo ya injini ni mil.120!!!!!!! Halafu ziliharibika zote kwa pamoja?
 
Nakushauri hiyo gari bebea watoto wa shule nursery wala hutoona haya wanayokufanyia hawa madereva kwani utakuwa umeingia mkataba na wenye shule ambayo utakuwa umeingia tenda nayo

achana na kubeba abiria wa kawaida fanya hii ndo nzuiri kwako haitkupa stress za hovyo
nilipopata vicent nilishauriwa kuchukua daladala (hiace) ili ifanye kazi kigamboni. Kupitia jf nilifaninikiwa kuipata. Lakini kilichofuata hapo ni sawa na ndoto ya kutisha!... Ukiamka hutamani usinzie tena.
Leo dereva anakwambia center-ruber imeisha, kwa hiyo badala ya tsh 40,000 unapata 15.kesho asbh ndo kwanza unaingia ofisini anakwambia timing belt imekatika...inatumika pesa ya jana na haitoshi inabidi utoe yako mfukoni.

Siku ya tatu na ya nne akikuhurumia ukakusanya 80 basi siku inayofuata unaambiwa nimepigwa bao na majembe. Ilikuwa nilipe 250,000 so nimewapoza 35,000. So hesabu yako mkuu hii hapa elfu tano! Gosh!!!

Picha hizo zimeendelea mpaka nikatia shaka, akipiga dereva wkt mwingine nachomoka kuthibitisha tatizo. Ajabu! Mara kadhaa ni uongo kunakuwa hakuna cha majembe wala mashoka! Bse of that nimewatimua kila nikigundua usanii huo, ndani ya mwezi 1 madereva wanne! Sasa naanza kuhisi kuwa they are probably all the same!! Na inanipunguzia concetration yangu kazini.

Baadhi ya watu wanasema ningeweza kuitumia vizuri kama nikitafuta tenda ya kubeba watoto (nursery) na kuwa hiyo haina longolongo nyingi. Naomba ushauri wenu wakuu! Pse, pse!!
 
Mkuu sijakuelewa kabisa labda uandike kwa ufupi kidogo nielewe
biashara ya daladala inalipa vizuri sana

nimepitia uzi huuu kurasa zooote na nimejifunza mengi sana, aidha mengine nimekutana nayo sana katika biashara hiii ya daladala, ambayo mpaka sasa ninaifanya.

Kwasababu nina hamu ya ku share nanyi uzoefu wangu basi nitaomba mnivumilie kidogo ili niweze kuandaaa notes kidogo, kama mnavyojua kudonyoa donyoa hizi computer sio vipaji vyetu ila ingekuwa kuongea fasta tungemaliza.


[font=&amp]tatizo wengi wanaoanza biashara hiii wanafanyia kazi pesa badala ya pesa kuwafanyia kazi wao "they work for money" instead of "their money work for them". [/font]

naandaa notes kidogo na nitakuja hapa na uzoefu wangu, jinsi biashara ya daladala nlivyoanza, changamoto nilizopitia mapa hapa nlipofika.

La msingi hapa ni kuwa watu wanahamu sana ya kuwa matajiri bila kupitia changamoto, wanafanya hesabu za mezani wanataka kuziweke kwenye uhalisai. Theory na practicle vina tofauti kubwa sana. Hii pia nilifanya mimi kwa miaka miwili.

Unapowaona matajiri waliofanikiwa ndani na nje ya nchi ujue wamepitia changamoto nyingi na kubwa sana.na pengine ilifika pahala wakafilisika kabisa, wakajiiinua na wakaanza tena.

Nikisikia mmmoja wetu kuwa kapata/kakusanya hela kanunua hiace/daladala then kafanya miezi 3 kakutana na changamoto, na kaamua kuuza na kuachana na biashara hiyo, napata picha iliyonikumba mimi, na namwona huyo bwana kama mimi.

Hapa kuna mambo kadhaa huwa yanasabasha;

1. Wengi tunaingia kwenye biashara kama kubahatisha kwasababu unahisi ina hela au fulani anafanya, hatui- study biashara japo kidunchuuu

2.wengi waliochangia hapa inonekana ni watumishi/waajiriwa (kama mimi) kwahiyo wanalo tawi la kushika na kumsitisri mambo yakiharibika, nayo ni kazi,

3.wengi wanaogopa changamoto au hawakuzitarajia ama hawataki kukutana nazo, na wakikutana nazo wanachanganyikiwa kabisaaa.

Kubwa kuliko yoote wengi kama nlivyokuwa mimi tunafanyia kazi pesa badala pesa zangu zinifanyie kazi

tukisikia hesabu ya hiace ni 30,000-50,000 mathalani, baaasi tunapiga hesabu haraka haraka kuwa mwezi unajiona una 900,000/-1,5000,000/, kama tumefanikiwa kupata mtaji basi huo mtaji utufanyie sisi kazi ili tupate pesa na sio tuna mtaji halafu tena tuufanyie kazi huo mtaji.

Naweza kuwa sieleweki wadau ila taratiiibu tutaelewana; hata mimi sijafanikiwa saaana lakini i see the way, na mambo yanaenda smooth na hela sasa naziona zikitengenezwa na mtaji nilioutafuta.

Nawasilisha wakuu, ngoja sasa niweze kuwaandalia ka notes kidogo, nitakuja tena hapa sooon tuendeleze huuu uzi.

Thanx
 
Mm pia nipo kwenye biashara hii ya Daladala,kwa kifupi ukiogopa changamoto biashara hii utaona ni chungu sana,Ngoja ni share nanyi changamoto nilizopitia katika biashara hii,mara ya kwanza kabisa kununua hiace nikafanya taratibu zote vya vibali kisha nikaingiza barabarani gari ikafanya kazi siku mbili ya tatu ikapata ajali mbaya sana na baada ya hapo ikakaa gereji mwezi mzima niligharimu kama 1m kunyoosha bodi na mambo mengine,baada ya hapo gari ikaingia tena barabarani ikafanya kazi miezi mitatu ikaanza kula oil nikaifanyia overhaul ikagharimu kama Laki7,baada ya hapo gari ikaingia tena mzigoni ikafanya kazi miezi miwili ikanok engine ni mengi tu nayoweza kushare na ninyi lkn kwasababu ya muda naachia hapo,lkn hadi sasa nipo kwenye hii biashara ya Daladala
 
Mkuu mimi binafsi nakushauri uchukue toyota hiace naona kama itadumu kuliko nissan
 
gongo la mboto chanika gari zote zinafanya kazi ila inabidi ubate nissan caravan qd, nissan caravan td27 haziwezi moto mwingi ni za safari za kila siku. Suka atalalamika sana kama ukimpa td maana watampita njiani vituo vyote hasa najua chanika kuna gari vijana wanasema mnyama yaani toyota 5l inakimbia coaster haifati.
Kwa gharama maana hiace about 22M and nisaan qd about 16M but hesabu sawa ya tajiri.
Ila lifetime ya hiace is about 7-10 years, wakati nissan ni 2-5 years kwa uzoefu wangu hasa kwa high way.
Ninayo ilikua inaenda Arusha karatu, hiace 5l na Nisan Qd

Una maelezo mazuri sana ila hapo kwa Nissan ungetia Rz ungekuja na maelezo tofauti mkuu. . . . Uliza madereva wako kama njia yao ina Petrol engines watakueleza
 
Natumaini ni wazima wa afya,

Naomba mwenye uzoefu wa biashara ya daladala anipe japo mawli matatu ya kuanzia na wapi ntaweza kupata Gari zuri kwa bei nzuri. Me mfukoni ninayo Milioni 6 kesho.
 
Duu Mkuu hiyo pesa ndogo sana utapata Hiace iliyochoka sana maana hata Noah huwezi pata maana ni bora ungeiongeza ukanunua Noah ukaifanya Daladala ukala 50 kwa siku sio mbaya ngoja waje wataalam
 
Dah! Mistake kubwa watu wanayofanya katika business ni kuingia kichwakichwa kwny biashara(bila experience) na kutoinvest muda wako ktk hiyo business
Kama wewe ndo utakuwa kinda/dereva wa hiyo gari na kila gereji upo am sure itakutoa
Otherwise its a waste of ur money and time, Fanya mengine sio busness
 
Dah! Mistake kubwa watu wanayofanya katika business ni kuingia kichwakichwa kwny biashara(bila experience) na kutoinvest muda wako ktk hiyo business
Kama wewe ndo utakuwa kinda/dereva wa hiyo gari na kila gereji upo am sure itakutoa
Otherwise its a waste of ur money and time, Fanya mengine sio busness

Ndio mahna nimekuja huku nipate mawli matatu mkuu tuangalie tunafanyaje
 
Duu Mkuu hiyo pesa ndogo sana utapata Hiace iliyochoka sana maana hata Noah huwezi pata maana ni bora ungeiongeza ukanunua Noah ukaifanya Daladala ukala 50 kwa siku sio mbaya ngoja waje wataalam

Noah yaweza kunitoa kweli mkuu
 
Kwanza nakupongeza kwa kuweza kuzichanga pesa kufikia hadi hapo na kuwa na ndoto yako. Bei ya gari haiangalii mkoa uliopo,maana unapoongelea gari lolote lazima lihusiane na Dar es Salaam.

Sasa kwa bei hiyo huwezi kupata gari,jipange uongeze pesa kiasi. Halafu ukubali changamoto za Magari,maana ukijua kupokea pesa ujue na kuitoa pesa.
Wengi wanalaza magari kwa kuona wanapokea pesa na muda fulani ikitakiwa kutoa pesa basi mtu anaona kwamba biashara ngum na haifai.Lakini ukweli ni jinsi utakavyojipanga ndio utakavyoiweza hii biashara.

Wengi wanakatishana tamaa ya biashara za magari ni wale wenye mentality za kwamba Magari sio biashara ya kufanya,maana presha tupu,lakini mie nakumbuka hii kauli ipo tangu Baba yangu yupo kijana na mpaka uzee tumempeleka kaburini bado watu wanakauli ya kwamba sio bisahara nzuri.
Tatizo lililojitokeza enzi hizo na wale wenye mentality hizo ni kwamba,wengi wetu tunaopata gari hizi ni vijana,Sasa ukipata gari lazima watu wakukome na madem wakujue kwamba wewe ndio mwenye mali,na masifa tele na matumizi makubwa sana kuliko kipato.

Mwisho wa siku unakwama,na unaweza kukuta ghalfa siku moja gari inakuambia inahitaji milioni moja kutatua tatizo hapo ndio wengie wanaona bora waache.
Kama ni mara ya mwanzo kumiliki gari fanya hivi;

a) Kama ni mwaka wa mwanzo wa gari, Ukipata 50,000, basi weka akiba 30,000

b) Kama ni mwaka wa pili wa biashara, Ukipata 50,000 basi weka akiba 20,000

Hapo utakuwa umeweza kuvuka maana hata likitokea tatizo kubwa vipi basi uwezo wa pesa unakuwa nao.

Muhimu: Kuwa makini na ununuzi wa magari,mtafute fundi mzuri ndio umtumie akushauri,na pia ongeza pesa. Hata 10m bado huwezi kupata gari ya biashara kama ndio mara ya mwanzo.

Kwa wale wazoefu ndio wanaweza kuanza kwa pesa hiyo,maana wapo watu hata huku Zanzibar,anaweze kukuuzia gari bodi ipo safi sana kwa 10m hadi 8,ila Engine utajua pa kuipata,sasa wajanja wanaungaunga hadi gari inatoka.Ila ni wale ambao tayari wanauzoefu wa magari na pia wanayo magari kama hayo kwenye mzunguuko wao wa biashara.

Maana nikitizama wewe ni lazima uanzie na Dungu,ambapo Dungu used kibongo ni ghali pia.
 
Mm nipo kwenye hii biashara kitambo lkn sio sana kihivyo! Wengi wanadhani kununua gari bei kubwa ndio uzima wa gari wakati sio! unaweza ukanunua hiace 25ml na bado ikawa kimeo! Ngoja ni share jinsi mm navyoendesha biashara hii.

Kwa kifupi mm huwa sinunui hiace mpya ila nachofanya huwa nanunua bodi nzuri ya hiace kisha nafunga engine mpya pamoja na gear box yake kisha matairi mapya na service za bodi gari inasimamia 10-12ml, miezi sita tu kishaeleweka,kwa uzoefu wangu sitanunua Hiace mpya milele! Kama gari ni engine na engine complete ni 7.5ml, je ukinunua hiace 25ml ukitoa 7.5ml bodi utakuwa umenunua bei gani?

Japokuwa wapo wataoponda mchango huu lkn mm kila mwaka naona mambo yanajipa.....ni hayo2
 
Mm nipo kwenye hii biashara kitambo lkn sio sana kihivyo! Wengi wanadhani kununua gari bei kubwa ndio uzima wa gari wakati sio! unaweza ukanunua hiace 25ml na bado ikawa kimeo! Ngoja ni share jinsi mm navyoendesha biashara hii.

Kwa kifupi mm huwa sinunui hiace mpya ila nachofanya huwa nanunua bodi nzuri ya hiace kisha nafunga engine mpya pamoja na gear box yake kisha matairi mapya na service za bodi gari inasimamia 10-12ml, miezi sita tu kishaeleweka,kwa uzoefu wangu sitanunua Hiace mpya milele! Kama gari ni engine na engine complete ni 7.5ml, je ukinunua hiace 25ml ukitoa 7.5ml bodi utakuwa umenunua bei gani?

Japokuwa wapo wataoponda mchango huu lkn mm kila mwaka naona mambo yanajipa.....ni hayo2
Mtoto Tajiri,
Hii point yako ni ya msingi sana.
Maana mie mdogo wangu nae pia aliwahi kununua gari kimeo ikamtesa sana ndio watu wakampa njia.
Uimara wa gari ni engine na mfumo wake na bodi.Kuna gari bodi zake ni nzuri sana ila Engine ndio tatizo.
Na unakuta tajiri imeishamlipa na anaona kununuea Engine bora anunue jipya,hapo ndio unakuta mtu unapenyea.
Ni Idea nzuri,nakubaliana na wewe
 
Shukrani kaka kwa kunielewa!kwa kifupi biashara hii ukishapata uzoefu wa kutosha huwezi kuimba tena ule wimbo wa kuwa biashara ya magari ni pasua kichwa,wapo wanaopenda biashara lkn wanachukia changamoto!,jua ya kwamba biashara ni kama shule kuna test,mitihani na n.k,Juhudi,uvumilivu,maarifa yatakufikisha hadi kwenye ndoto yako na ndoto yako kuwa kwenye hali ya Uhasilia!
 
Kwanza nakupongeza kwa kuweza kuzichanga pesa kufikia hadi hapo na kuwa na ndoto yako. Bei ya gari haiangalii mkoa uliopo,maana unapoongelea gari lolote lazima lihusiane na Dar es Salaam.

Sasa kwa bei hiyo huwezi kupata gari,jipange uongeze pesa kiasi. Halafu ukubali changamoto za Magari,maana ukijua kupokea pesa ujue na kuitoa pesa.
Wengi wanalaza magari kwa kuona wanapokea pesa na muda fulani ikitakiwa kutoa pesa basi mtu anaona kwamba biashara ngum na haifai.Lakini ukweli ni jinsi utakavyojipanga ndio utakavyoiweza hii biashara.

Wengi wanakatishana tamaa ya biashara za magari ni wale wenye mentality za kwamba Magari sio biashara ya kufanya,maana presha tupu,lakini mie nakumbuka hii kauli ipo tangu Baba yangu yupo kijana na mpaka uzee tumempeleka kaburini bado watu wanakauli ya kwamba sio bisahara nzuri.
Tatizo lililojitokeza enzi hizo na wale wenye mentality hizo ni kwamba,wengi wetu tunaopata gari hizi ni vijana,Sasa ukipata gari lazima watu wakukome na madem wakujue kwamba wewe ndio mwenye mali,na masifa tele na matumizi makubwa sana kuliko kipato.

Mwisho wa siku unakwama,na unaweza kukuta ghalfa siku moja gari inakuambia inahitaji milioni moja kutatua tatizo hapo ndio wengie wanaona bora waache.
Kama ni mara ya mwanzo kumiliki gari fanya hivi;

a) Kama ni mwaka wa mwanzo wa gari, Ukipata 50,000, basi weka akiba 30,000

b) Kama ni mwaka wa pili wa biashara, Ukipata 50,000 basi weka akiba 20,000

Hapo utakuwa umeweza kuvuka maana hata likitokea tatizo kubwa vipi basi uwezo wa pesa unakuwa nao.

Muhimu: Kuwa makini na ununuzi wa magari,mtafute fundi mzuri ndio umtumie akushauri,na pia ongeza pesa. Hata 10m bado huwezi kupata gari ya biashara kama ndio mara ya mwanzo.

Kwa wale wazoefu ndio wanaweza kuanza kwa pesa hiyo,maana wapo watu hata huku Zanzibar,anaweze kukuuzia gari bodi ipo safi sana kwa 10m hadi 8,ila Engine utajua pa kuipata,sasa wajanja wanaungaunga hadi gari inatoka.Ila ni wale ambao tayari wanauzoefu wa magari na pia wanayo magari kama hayo kwenye mzunguuko wao wa biashara.

Maana nikitizama wewe ni lazima uanzie na Dungu,ambapo Dungu used kibongo ni ghali pia.

Asante kwa ushauri me nawaza bas ninunue maindi na maharage kwa mara y mwsho naweza pata zaidi y m 10 then ntakutafuta mkuu
 
Back
Top Bottom