Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Uzi unahusu biblical and scientific knowledge sasa uchawi sioni kama unaingia hapo..
Mtazamo wangu ni kwamba the Bible dont provide the math kuonyesha exactly dunia ina umri gani (hesabu zinazofanyika hapa ni fake guesses tu) lakini the same bible haijatoa limitations za kutafuta ukweli kwa kutumia njia za kisayansi, na sayansi inaprovide proven facts (unless proven wrong by another scientific fact)ambayo ni miaka 4.6b..
Everthing is knowledge acha kukaza ubongo

Uligusia kuhusu suala la elimu na manufaa,sasa nimekuonyesha ya kuwa zipo elimi zisizo na manufaa.

Inaonekana ulikuwa hujui kama Uchawi nayo ni elimu.
 
Uzi unahusu biblical and scientific knowledge sasa uchawi sioni kama unaingia hapo..
Mtazamo wangu ni kwamba the Bible dont provide the math kuonyesha exactly dunia ina umri gani (hesabu zinazofanyika hapa ni fake guesses tu) lakini the same bible haijatoa limitations za kutafuta ukweli kwa kutumia njia za kisayansi, na sayansi inaprovide proven facts (unless proven wrong by another scientific fact)ambayo ni miaka 4.6b..
Everthing is knowledge acha kukaza ubongo

Ubongo wangu uko salama salimini Master !

Unapokea ya haki na unayatupilia mbali ya batili.

Nipo ....!
 
Uligusia kuhusu suala la elimu na manufaa,sasa nimekuonyesha ya kuwa zipo elimi zisizo na manufaa.

Inaonekana ulikuwa hujui kama Uchawi nayo ni elimu.
ukisoma dictionary yeyote kigezo cha kwanza knowledge lazima iwe ni fact... kwa kigezo icho kwangu sioni kama uchawi ni knowlege
 
Hatukuangalii wewe sisi tuna angalia ukweli ulivyo.

Sasa kuanzia leo unatakiwa kusafisha ufahamu wako juu ya UCHAWI.

Nipo ....!
Watu hatuko sawa, ndio maana kuna wengine rangi nyekundu wanaona kijani na kijani ndio fact kwa upande wao....
 
Biblia haisemi chochote juu ya umri wa Dunia ila imetaja kuwepo kwa maji, uumbaji wa mimea na watu
Mimi ni mjiolojia na ningependa kuchangia kwa perspective ya kisayansi hasa tulivyofundishwa na kusoma paper na vitabu mbalimbali za kijiolojia

Kuna dhana mbili za evolution ambazo ndizo zinazoelea juu ya umri wa dunia
Dhana ya Organic evolution na Crustal Evolution
Hii ya Crustal evolution ndio hasa itaelezea vizuri umri wa dunia
Katika Crustal evolution inaanzia kwenye kuumbwa kwa dunia ambako kuna theories nyingi sana zinazoelezea juu ya kuumbwa kwa Ulimwengu (dunia ikiwemo) yaani The Creation of the Universe
Theory iliyoungwa mkono na wanasayansi wengi kwa sababu inaweza kufanyiwa majaribio ya kifizikia kwenye maabara ni ile ya Galaxy Theory ambayo inadai kulikuwepo na vumbi kubwa kwenye space na hilo vumbi ilikuwa na composition kubwa ya Hydrogen, Oxygen, Nitrogen, Iron, Nikel na aina zinginezo. Hili vumbi linaaminika kujikusanya taratibu takribani miaka bilioni 13/14 iliyopita na ilipotimu miaka bilioni 4.5 iliyopita hilo vumbi likaanza kujizungusha yenyewe kwa kasi kubwa na kutengeneza nguvu mbili za uvutano yaani Centrifugal force (nguvu inayosukuma mada kwenda mbali na katikati ya mzunguko) na centripetal force (Nguvu inayovuta mada kwenda katikati ya mzunguko). Vumbi hili ilipozunguka ikazidiwa na kuanza kukatika na kuzaa mikia ambayo ndiyo sayari zinazoizunguka Jua. Kiini cha katikati la hilo vumbi ndio Jua ambalo imezishikilia hizo sayari zote zilizomeguka wakati vumbi hilo linajizungusha kwa kasi. Umri wa kila sayari uanweza kutofautiana kwa sababu hazikumeguka kwa wakati mmoja
Mwezi ulitumika kupima umri wa Dunia kwa sababu ndio miamba inayopimika ambayo iko karibu na Dunia na kwa hiyo umri wa mwezi ni sawa na umri wa dunia kwa makadirio.
Vipimo vilivyopimwa kwenye miamba kutoka mwezini zinaonyesha kuwa ina miaka kati ya 4.4 mpaka 4.5 billion. Hii imefanyika kwa sababu kupata sample sahihi katika uso wa dunia ni ngumu kwa sababu miamba mingi yamefunikwa wakati miamba ya mwezini hayajafunikwa. Kipimio cha Radiometric Dating ndio inayoweza kuleta usahihi wa vipimo kwa sabau inatumia half-life concept ambayo inaleta majibu consistence kila inapotumika
 
Vimethibitishwa na uwezo wake wa kutambua mfano ukilifukia fuvu lako leo kwa siri mpaka mwaka 2020 wakilichimbua wakipima wanagundua lina miaka miwili tu hivyo baada ya kutumika kupima miamba mingi na elementa zingine kwa mafanikio na kuweza kuthibitisha umri wake basi ndipo ilipopata credibility
Hiko kipimo ndo kilisema binadamu wa kwanza aliishi miaka milioni 3?
 
wakolosai 1:16
Yeye ndiye ali yeumba vitu vyote mbinguni na duniani; vitu vinavyoonekana na visivyoonekana; kama ni viti vya enzi au nguvu, au watawala au milki na mamlaka: vyote viliumbwa na yeye kwa ajili yake .

yohana 1:3
Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

isaya 66: 2
For My hand made all these things, Thus all these things came into being," declares the LORD "But to this one I will look, To him who is humble and contrite of spirit, and who trembles at My word.
waefeso 3:9 Mungu aliumba kila kitu.

Ukiona hapo kwa mujibu wa bibilia bila kujali mchanganyiko wowote unaoweza kujitokeza mwanzo 1/2
Mungu kaumba kila kitu hadi maji ambayo hayajatamkwa.

Oanisha ni Kauli ya Mungu akirefer matukio ya Mwanzo 1 na 2

Kutoka 20:11
For in six days the Lord made the heavens and the earth, the sea, and all that is in them, but he rested on the seventh day. Therefore the Lord blessed the Sabbath day and made it holy.

sasa naomba maoni yako hapa. Je Tupingeje hii kauli ya Mungu na bibilia au uchambuzi gani wa siri unabatilisha hili mkuu.

cc SANCTUS ANACLETUS

Kaka Hakuna mtu anayekataa kuwa Mungu hakuumba vitu vyote, unajua Kitabu cha Mwanzo ukikisoma vizuri kina kila kitu unachokiitaji kwenye hii Dunia, Kuna sayansi kubwa sana pale, kuna elimu nzito kabisa
sasa twende polepole
Mwanzo 1:1-2 Mungu alifanya nini?
1. Aliumba mbingu na nchi (Ardhi)
2.Nchi ilikuwa Giza, ukiwa na utupu
3. kulikuwa pia na vilindi vya maji
so hivyo vyote viliumbwa nje ya zile siku sita, je baada ya kuumbwa hivi vilikaa siku ngapi kabla ya zile siku sita ?

umetoa andiko la Kutoka 20:11, ni kweli ndani ya siku SITA mUNGU ALIUMBA BAHARI kwa kutenganisha maji na ardhi, Mwanzo 1:6 Mungu akasema na liwe anga katikati ya maji LIKAYATENGE MAJI NA MAJI, Mwanzo 1:9 naMaji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja ili pakavu paonekane.........

Kaka mitale na midimu ,
maandiko yote ya kuanzia Mwanzo 1.3-10 kitu kipya alichokiumba mungu kutoka vile vilivyokuwa awali Mwanzo 1:1-2 ni NURU pekee, lakini vingine kama Maji , Nchi, Giza alishaviumba kabla
Baada ya Mungu kukamilisha kuitransform Dunia iwe na mazingira ya kusupport uhai ndio kuanzia Mwanzo 1:11 na kuendelea anaanza kuweka Mimea na viumbe hai

MIMI NINACHOAMINI MUNGU ALIIUMBA DUNIA MIAMBA NA MAJI NA ILIKUWEPO KWA MUDA MREFU SANA, KISHA AKAPANGA MIPANGO YA KUWEKA VIUMBE HAI, LAKINI ILIBIDI LAZIMA AANDAE MAZINGIRA YA KUWAWEZESHA HAO VIUMBE HAI NA MIMEA IWEZE KUKUA NA KUSTAWI KWA UZURI, NDIO SASA MUNGU NDANI YA SIKU SITA ANAITRANSFORM DUNIA NA KUIPA MAZINGIRA YA KUWEZA KUTUNZA VITU HIVYO VYOTE

KITABU CHA MWANZO NI KITABU KIZURI SANA, NDIO MWANZO WA DUNIA NA NDIO MWANZO WA SAYANSI
 
Hiko kipimo ndo kilisema binadamu wa kwanza aliishi miaka milioni 3?
Mkuu unachotakiwa kujua methodology inafuata principles mfano inafahamika kuwa layer moja inabadilika kuingia layer ingine baada ya muda fulani unaoitwa half life lets say kutoka half life ya layer moja kwenda ingine inachukua miaka million 50 sasa si utahesabu tu layer zipo ngapi na utapata jibu na ndio maana hizo tafiti zao zinakubalika na wasomi ssa nyie mkiletewa mnapinga bila kuuliza methodology kisa tu imani zenu hazikubaliani na hilo. Ila cha kushangaza wanasayansi hao hao wakitoa tafiti mfano kuthibitisha Yesu/Issa au Mfalme Daudi waliwahi exist basi tafiti zao mnazikubali.

Tuache double standards tafiti hujibiwa kwa tafiti tafuta mfumo mwingine hesabu umr wa hiyo miamba ukipata no below 6000 ndio object ila kama hakuna mfumo mwingine credible zaidi kwanini mnapinga bila alternative?? Maana jibu lako lipo sarcastic sana
 
MIMI NINACHOAMINI MUNGU ALIIUMBA DUNIA MIAMBA NA MAJI NA ILIKUWEPO KWA MUDA MREFU SANA, KISHA AKAPANGA MIPANGO YA KUWEKA VIUMBE HAI, LAKINI ILIBIDI LAZIMA AANDAE MAZINGIRA YA KUWAWEZESHA HAO VIUMBE HAI NA MIMEA IWEZE KUKUA NA KUSTAWI KWA UZURI, NDIO SASA MUNGU NDANI YA SIKU SITA ANAITRANSFORM DUNIA NA KUIPA MAZINGIRA YA KUWEZA KUTUNZA VITU HIVYO VYOTE

Dhana ya siku SITA tuliyo nayo sio ile iliyomaanishwa na Waebrania wakati ule. Jaribu kuangalia Istilahi "YOM" (neno la Kiebrania lenye maana ya Sita) linabeba maana gani. Ndio Waebrania waliposema Sita walikuwa na maana gani? Namba hiyo ina maana ya picha kumaanisha MUDA MREFU.Kwa mfano,mimi nikisema nina Watoto "KIBAO". Haimaanishi kwamba nina watoto wanaoitwa Kibao Bali wengi. Kwa hiyo,kwa Waebrani kila namba ilikuwa na maana yake.
 
Habari za mchana wakuu kama kawaida huwa nakuja na mada za kuchokoza fikra zetu hasa kwenye mambo ya kiimani hivyo mada hizi sio za kukosoa dini fulani au vitabu vya imani ila ni kuhoji tu ili tupanue fikra zetu kwenye masuala haya kwa faida yetu sote so sitegemei iibue mijadala ya kidini bali kuelimishana juu ya mambo haya baada ya kusema hayo twende moja kwa moja kwenye mada husika ya leo.
View attachment 948749
Biblia na umri wa Dunia
Mwaka 1650 professor wa masuala ya theologia na Askofu wa makanisa ya protestant wa Ireland John Ussher aliandaa maandiko yake kupitia mfululizo wa vitabu vyake kuanzia cha Annals of the Old Testament: Origins of the world ambacho ndani yake aliibua mjadala mpana sana wa karne nyingi sana. Ussher alipiga hesabu ya muda ulivyopita kati ya Adam kuumbwa hadi Yesu kuzaliwa na kugundua kwamba ni miaka 4000 imepita tokea Adam aumbwe hadi Yesu kuzaliwa hivyo kufanya dunia yetu ikiwa na wanadamu kuwa na miaka elfu 6 pekee mpaka sasa!!. Ussher alitumia maandiko kama chanzo cha nadharia yake alitumia nyaraka za masoretic zilizotumika kuandaa Biblia za agano la kale ili kuweza hesabu umri wa Adam hadi vizazi vya Abraham hadi kufikia Yesu na baada ya mnyambuliko huo alifanikiwa kugundua kwamba dunia iliumbwa usiku wa October 23 4004 kabla ya kristo.

Young Earth Creationists
Vuguvugu hili la YEC lilianza miaka ya 1960 ambapo iliasisiwa na wasomi 9 chini ya PhD wa theolojia na uhandisi Bwana Henry Morris wakijikita kwenye utafiti wa uhalisia wa umri wa dunia na uumbaji na wakahitimisha rasmi kuwa dunia tunayoishi iliumbwa ndani ya miaka elfu 10 pekee na sio zaidi ya hapo na wao pia walitumia maandiko ya Biblia ya kiebrania ili kufikia hitimisho hilo hivyo na wao wakaunga mkono hoja za hapo nyuma za Professor John Ussher na hata leo hii wameweza shawishi zaidi ya 40% ya wakazi wa marekani kwa takwimu za 2017 wanaamini nadharia hii kwamba uumbaji wa dunia ni kwa mujibu wa Biblia hauzidi miaka 10,000 iliopita.

View attachment 948751
SAYANSI inasemaje??
Baada ya sayansi na teknolojia kukua na kuongezeka vifaa vya kupima umri wa miamba,mazao na mifupa ya wanyama wakaibuka wasomi wa sayansi waliohoji kuhusu uhalali wa nadharia hizi na imeleta utata na mjadala mzito kwa miaka mingi sasa. Mwanasayansi wa karne ya 20 Clair Cameron Patterson baada ya tafiti kadhaa juu ya miamba akagundua ulimwengu toka uanze una miaka billion 4.5 na baadae wanasayansi mbalimbali wakaja na tafiti mbalimbali zikidai kwa usahidi wa kisayansi na kiacholojia kwamba uhai duniani umekuwepo miaka takriban 3.8 Billion iliopita hivyo kukinzana kabisa na nadharia hizo mbili za juu kuwa Biblia

Jinsi ya kupima
Kwa upande wa Young Earth wao wanalalia maandiko kwa kiasi kikubwa na kupiga hesabu miaka ya kibiblia tokea Adam hadi Yesu lakini wanasayansi wamepiga hesabu zao kwa ushahidi wa kushikika wakitumia mfumo unaitwa radiometric dating ambacho kinapima miamba hasa stage tofauti za jinsi miamba inavyooza na ambapo kila stage ina umri wake yake yaani miaka kadhaa ili ifike stage nyingine ya kuoza hivyo wanapiga hesabu kuanzia layer ya mwisho mpaka ya kwanza na kufikia hitimisho la umri wa mwamba huo na wakafanikiwa kugundua mwamba wa kwanza ulitokea miaka 3.8 Billioni iliyopita.
View attachment 948748
Utafiti wangu (Primary)
Binafsi nilichukua hatua kuonana na wanatheolojia kadhaa kutoka chuo fulani cha Biblia wenye ngazi ya PhD na wamenijuza kwamba Biblia haikuandikwa kwa maneno bali mafumbo hivyo isitafsiriwe kwa maana zetu bali kwa mafunuo na maana zilizo kwa Biblia... Mfano wanadai Dunia haikuumbwa kwa siku 7 kama zetu hizi bali miaka mamilion na wakaenda mbali kusema Biblia haikuanza kuandika matukio yote bali imeandika matukio juu ya watu waliochaguliwa tu hivyo wanakiri kuwa kweli dunia ina miaka mabillion na sio miaka elfu 6 pekee bali wanaotafsiri maandiko kwa akili zao ndio wanapotosha sababu wameitafsiri maneno kama yalivyo badala ya kutafuta maana ya hayo mafumbo na wakanipa mistari michache.

Yohana 16:25
25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.

Na wakaenda mbali kusema hata hayo mafumbo walioambiwa kuandika Biblia hawakuyaelewa sababu ni siri imewekewa hadi wakati muafaka yaani mwisho wa dunia ufike soma hapa kisa cha Daniel

Daniel 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.

Hapa tunaona kuna maandiko na nabii zimefichwa kwa uelewa wetu kabisa hata Daniel hakuelewa!!

Daniel 12:8-9
8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa
mwisho.

Hivyo kama hata Daniel kuna baadhi ya vitu alifichwa na mpaka anaandika hakuvijua basi hata sisi hatuwezi vijua mpaka siku ya mwisho hivyo wakahitimisha mjadala kwa kusema huenda ni kweli dunia ina 4.5 Billion years ila sio 6000 kama YEC inavyosema maana Biblia haielezi hicho kuwa ni miaka 6000 bali watu wanatafsiri maandiko kwa akili zao ilihali YAMEFICHWA!!
View attachment 948750
Hitimisho
Ukinzano huu kati ya maandiko na sayansi juu ya asili ya umri wa ulimwengu umezua mjadala mpana sana huku kila upande ukivutia kwake nikaona kwa kuwa JF ni kisima cha maarifa nilete hii mada ili tuweze kufikiria pamoja je umri wa dunia upi ni halisi

4.5 Billion ama 6000?

Naomba kuwasilisha

Ukisoma biblia utagundua kulikuwa na maangamizi kabla ya maangamizi ya noah
Af biblia inaongelea historia ua binadam tuu na si vinginevyo
 
Kingine ni wanascience wanasema binadam alianza kutokea kama zinjathropus miaka laki2 iliopita
Homosapien(moden man) alitokea miaka elf50 iliyopita
 
Ila cha kushangaza wanasayansi hao hao wakitoa tafiti mfano kuthibitisha Yesu/Issa au Mfalme Daudi waliwahi exist basi tafiti zao mnazikubali.

Tatizo kuna wakristu wana mtizamo kama Wa Kiislamu kwamba Biblia ilipatikana kama Kurani inavyodaiwa kupatikana!

Biblia ni neno la Mungu kwa mtizamo kwamba tu Yale maudhui ni divinely authored. Lakini Lugha, Staili ya Uandishi, Utamaduni, ni vitu vya kiuandishi tu. Mungu hakuwa ana-detect uandishi wa neno kwa neno. Kwa Mfano, Magufuli akimuagiza Msigwa atoe press Release atamueleza mambo ya ku-communicate lakini Lugha na misamiati vitakuwa vya Msigwa mwenyewe na Release ile itaitwa ya Ikulu au Ujumbe Wa Raisi.
 
Mada yako ilipo anza ulikataa maswala ya udini lakini wewe umeleta udini hiyo sehemu apo ya 500 baada ya Yesu hapo a yupo mtume Muhammad lakini hujaandika umeacha wazi
 
"Uchawi" upi ni Elimu? Unaelewa maana ya Elimu? Kunyofoa viungo vya Albino ni Elimu? Kupasulia Nazi kwenye Kaburi nako ni Elimu?

Tuliza kichwa,nilicho kiona humu watu wanajadili mambo ya kielimu bila kujua elimu ni nini ?

Naendelea...

1. Kusonga ugali elimu au sio elimu ?

2. Kuendesha gari ni elimu au si elimu ?

3. Kusimama kwenye zebra kwa mwenye kupisha wavukaji wa miguu ni elimu sio elimu ?

4. Kula ni elimu au sio elimu ?

5. Kuruka kamba elimu au sio elimu ?

Nipo....
 
Mada yako ilipo anza ulikataa maswala ya udini lakini wewe umeleta udini hiyo sehemu apo ya 500 baada ya Yesu hapo a yupo mtume Muhammad lakini hujaandika umeacha wazi
Tofautisha udini na historia..... Udini naopinga ni ule kuja na kukashifu dini za watu mfano kusema Biblia ni feki au Mtume sijui alitokewa na mapepo sio malaika n.k hayo ndio udini ila sijakataza kuongelea viongozi wa hizo dini kwa minajili ya kujengea hoja tu na sio kuwakashifu.
 
Back
Top Bottom