Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Bible Vs Science: Je ulimwengu una umri gani?

Kwa tafakari yangu, ni kuwa ulimwengu ulikuwako kabla ya hizo siku sita, LAKINI ULIKUWA HAUNA UHAI KWANI ULIKUWA HAUNA MWANGA, so siku sita za uumbaji ni siku ZA KUANDAA UHAI WA VIUMBE HAI WA MAJINI NA ARDHINI, MAANA Dunia ilikuwapo (Alishaiumba kwenye Mwanzo 1:1-3) so uumbaji wa kuanzia 1:3 ni kuandaa mazingira ya kuweka vimbe hai
Yes, Maana Neno linasema Mwanzo: 1:14 : Mungu akasema, na iwe mianga katika anga la Mbingu, ili itenge kat ya Mchana na Usiku, Nayo ndiyo iwe dalili na Majira na Siku na Miaka.
Hivyo basi, With this ni kwamba,Hapa ndipo tunaweza kuanza kuhesabia hizo siku, Miaka Etc, maana Ndiyo dalili ya Majira, Siku na Miaka.
Kwa kusema hivyo basi Umri wa Dunia, unachezea kwenye hiyo 6000 hapo.

Samahani: Naomba UfafanUzi kidogo kuhusu kutofautisha EARTH, WORLD and UNIVERSE
 
Kwa tafakari yangu, ni kuwa ulimwengu ulikuwako kabla ya hizo siku sita, LAKINI ULIKUWA HAUNA UHAI KWANI ULIKUWA HAUNA MWANGA, so siku sita za uumbaji ni siku ZA KUANDAA UHAI WA VIUMBE HAI WA MAJINI NA ARDHINI, MAANA Dunia ilikuwapo (Alishaiumba kwenye Mwanzo 1:1-3) so uumbaji wa kuanzia 1:3 ni kuandaa mazingira ya kuweka vimbe hai
mkuu unamaoni gani juu ya Kauli ya Bibilia kuwa Mungu mwenyewe anasema alifanya Yote kwa siku sita na siku ya saba akapumzika.
Je hapa alikuwa anawaficha nini waisrael?
Je hakujua kuwa vingine aliviumba kwa mamilioni ya miaka?
Je kuna code yoyote nyuma ya kauli hiyo ya moja kwa moja na iliyohitaji Practical obedience kwa wale jamaa huku akijua kabisa sio kweli wanachokifanya kuhusu siku sita za uumbaji.
Kumbuka tukio la uumbaji ndio lilimtenganisha Mungu wao na miungu mingine. Nadhani ni eneo ambalo Mungu Muumbaji aliwafunda vizuri wale jamaa ili wahifadhi hizo habari hadi kizazi hiki cha neema kwa wote waisrael wa kimwili na wakiroho.

unaweza kutia maarifa kidogo hapo mkuu.
 
Tuombe uzima Mkuu. Sina haja ya kuwa Gnostic hata siku moja. Gnostic ni hao akina John Ussher wanaotafsiri Biblia kinyumenyume.

Mambo haya nitayaeleza kadri muda utakavyo rafiki kwangu. Kwa sasa niko na series ya mambo ya kizushi katika Imani nayaonesha ili watu wafumbuliwe macho. Kisha sasa tutaanza kueleza hatua kwa hatua jinsi Biblia ilivyopatikana.
Natamani Kiranga angekuwa japo na busara ndogo ya kuwa realistic kama wewe angepata heshima humu jamvini.
Lakini ukimchunguza Akili yake iko below reasoning level.
Nadhani kaka Sanctus ulipitia kwenye Theolojia yenye kukupelekea kuwa gnostic bila kujitambua. Polepole u-gnostic utatoweka muda wa kuwa na Sisi tumo humu Jamvini.
 
Wamepima kuanzia Adam alipoumbwa!
Mbona tunasoma humu ndani Kuwa Dunia ilikuwa ina watu kabla ya Ujio wa Adamu?

Samahani kama nitakuwa sijaeleweka maana sipo vizuri kwenye hizi mambo.


Upo sahihi kabisa kuwa watu walikuwepo kabla ya Adam.
 
Yes, Maana Neno linasema Mwanzo: 1:14 : Mungu akasema, na iwe mianga katika anga la Mbingu, ili itenge kat ya Mchana na Usiku, Nayo ndiyo iwe dalili na Majira na Siku na Miaka.
Hivyo basi, With this ni kwamba,Hapa ndipo tunaweza kuanza kuhesabia hizo siku, Miaka Etc, maana Ndiyo dalili ya Majira, Siku na Miaka.
Kwa kusema hivyo basi Umri wa Dunia, unachezea kwenye hiyo 6000 hapo.

Samahani: Naomba UfafanUzi kidogo kuhusu kutofautisha EARTH, WORLD and UNIVERSE

ni kweli tunaanza kuhesabu siku, majira na Miaka baada ya uboreshaji wa Dunia kuwa sehemu sahihi ya kuishi, baada ya Dunia kupewa uhai na inawezekana ndio Hesabu ya hizo siku 6000 za uhai wa Dunia unapotoka, lakini Dunia bila uhai ilikuwepo kadiri ya Mwanzo 1:1-2
 
mkuu unamaoni gani juu ya Kauli ya Bibilia kuwa Mungu mwenyewe anasema alifanya Yote kwa siku sita na siku ya saba akapumzika.
Je hapa alikuwa anawaficha nini waisrael?
Je hakujua kuwa vingine aliviumba kwa mamilioni ya miaka?
Je kuna code yoyote nyuma ya kauli hiyo ya moja kwa moja na iliyohitaji Practical obedience kwa wale jamaa huku akijua kabisa sio kweli wanachokifanya kuhusu siku sita za uumbaji.
Kumbuka tukio la uumbaji ndio lilimtenganisha Mungu wao na miungu mingine. Nadhani ni eneo ambalo Mungu Muumbaji aliwafunda vizuri wale jamaa ili wahifadhi hizo habari hadi kizazi hiki cha neema kwa wote waisrael wa kimwili na wakiroho.

unaweza kutia maarifa kidogo hapo mkuu.

Dunia haikuumbwa kwa siku sita, Dunia ilikuwepo, ila ilikuwa Giza, Utupu na ukiwa, Yaani ilikuwa haina uhai Mwanzo 1:1-2, Mungu kwa muda wa siku sita akaitransform Dunia na kuiwekea mazingira ya kuweza kufanyika maisha kwa viumbe hai
Ukiangalia hakuna hata sehemu moja kwenye Biblia inapoonyesha kuwa Mungu anaumba maji, au Miamba, bali tunaona katika hizo siku sita anaitenga miamba na maji, yaani anavitenga vitu vilivyokuwepo, vitu alivyoviumba katika Mwanzo 1:1-2
 
Mjadala mzito huu ila mi najuwa kunamiaka mingi hata hiyo million inaweza kuwa ndogo kwani sisi tumetokea wapi tukijuwa mwanzo wetu tunaweza juwa kuwa Ulimwengu na Mtoto wake dunia waliumbwa miaka mingapi iliyopita.
 
Idea kama zile licha kuwa na mapungufu, zipingwe kwa maandiko aliyotumia, au wanayotumia pro-creation scientists kwamba dunia haina miaka mamilioni bali miaka kama angalau elfu sita based to biblical genealogy ya Adam.

Kosa ambalo unafanya wewe na alilofanya John Ussher ni kusoma Creation Accounts Chronologically. Kuelewa kwamba Biblia katika Kitabu cha Mwanzo inaelezea kwamba lilianza tukio hili na kisha likafuata hili na kisha lile. Unapokisoma Kitabu cha mwanzo kuna vitu lazima uvielewe kwanza. Mfano lazima uelewe Thinking ya Waebrania kuhusu Time and Space, uelewe Lugha yao na Culture yao.

Ukitaka kuelewa kwamba Kitabu cha Mwanzo hakitupatia uumbaji Chronologically,naomba ujiulize swali: Mwanga unatokana na Jua na kinyume. Je,kwa mjibu Wa Sura 1:3, mwanga ndio ulianza kuumbwa na kisha ndio Jua na Mwezi na Jua vikaumbwa( Mwa 1:16) . Je,kama mambo yalifanyika Chronologically, hali hiyo iliwezekana vipi? Kwamba Mwanga uanze na kisha ndio Jua liumbwe wakati Jua ndio linatoa Mwanga?

Kwanza:

" 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza."

Kisha:

"16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. 17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi."

Kwa hiyo, kwa nukuu hizo hapo utagundua kwamba Kitabu cha Mwanzo hakitupatii maelezo ya kisayansi jinsi Ulimwengu na Dunia vilivyoumbwa Chronologically Bali Kitabu kitabu hicho kinaeleza na kujibu Maswali yafuatayo: Who, Why and What juu ya Uumbaji.
 
jamvini.
Lakini ukimchunguza Akili yake iko below reasoning level.
Nadhani kaka Sanctus ulipitia kwenye Theolojia yenye kukupelekea kuwa gnostic bila kujitambua. Polepole u-gnostic utatoweka muda wa kuwa na Sisi tumo humu Jamvini

Usiwe na haraka ya kunihukumu hivyo. Mimi nitakuwa nawapeni Maswali ya kujiuliza na ukiona jibu au uelewa ulio nao una-contradict Facts za Kisayansi,Historia, Culture au thinking ya waandishi au audience kwa muda huo basi ujue hicho ulicho nacho ndio matangopori.

Hebu soma Mwa 1:3 na Mwa 1:16 halafu rudi hapa uniambie kama Logically inawezekana. Kama haiwezekani ndio ugutuke kwamba kumbe Kitabu cha Mwanzo hakielezi Uumbaji Chronologically.
 
Kaka mkubwa nakuelewa haya majibu yangemfikia pia

Cc@Nyabhingi
Usiwe na haraka ya kunihukumu hivyo. Mimi nitakuwa nawapeni Maswali ya kujiuliza na ukiona jibu au uelewa ulio nao una-contradict Facts za Kisayansi,Historia, Culture au thinking ya waandishi au audience kwa muda huo basi ujue hicho ulicho nacho ndio matangopori.

Hebu soma Mwa 1:3 na Mwa 1:16 halafu rudi hapa uniambie kama Logically inawezekana. Kama haiwezekani ndio ugutuke kwamba kumbe Kitabu cha Mwanzo hakielezi Uumbaji Chronologically.
Kosa ambalo unafanya wewe na alilofanya John Ussher ni kusoma Creation Accounts Chronologically. Kuelewa kwamba Biblia katika Kitabu cha Mwanzo inaelezea kwamba lilianza tukio hili na kisha likafuata hili na kisha lile. Unapokisoma Kitabu cha mwanzo kuna vitu lazima uvielewe kwanza. Mfano lazima uelewe Thinking ya Waebrania kuhusu Time and Space, uelewe Lugha yao na Culture yao.

Ukitaka kuelewa kwamba Kitabu cha Mwanzo hakitupatia uumbaji Chronologically,naomba ujiulize swali: Mwanga unatokana na Jua na kinyume. Je,kwa mjibu Wa Sura 1:3, mwanga ndio ulianza kuumbwa na kisha ndio Jua na Mwezi na Jua vikaumbwa( Mwa 1:16) . Je,kama mambo yalifanyika Chronologically, hali hiyo iliwezekana vipi? Kwamba Mwanga uanze na kisha ndio Jua liumbwe wakati Jua ndio linatoa Mwanga?

Kwanza:

" 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza."

Kisha:

"16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. 17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi."

Kwa hiyo, kwa nukuu hizo hapo utagundua kwamba Kitabu cha Mwanzo hakitupatii maelezo ya kisayansi jinsi Ulimwengu na Dunia vilivyoumbwa Chronologically Bali Kitabu kitabu hicho kinaeleza na kujibu Maswali yafuatayo: Who, Why and What juu ya Uumbaji.
 
Habari za mchana wakuu kama kawaida huwa nakuja na mada za kuchokoza fikra zetu hasa kwenye mambo ya kiimani hivyo mada hizi sio za kukosoa dini fulani au vitabu vya imani ila ni kuhoji tu ili tupanue fikra zetu kwenye masuala haya kwa faida yetu sote so sitegemei iibue mijadala ya kidini bali kuelimishana juu ya mambo haya baada ya kusema hayo twende moja kwa moja kwenye mada husika ya leo.
View attachment 948749
Biblia na umri wa Dunia
Mwaka 1650 professor wa masuala ya theologia na Askofu wa makanisa ya protestant wa Ireland John Ussher aliandaa maandiko yake kupitia mfululizo wa vitabu vyake kuanzia cha Annals of the Old Testament: Origins of the world ambacho ndani yake aliibua mjadala mpana sana wa karne nyingi sana. Ussher alipiga hesabu ya muda ulivyopita kati ya Adam kuumbwa hadi Yesu kuzaliwa na kugundua kwamba ni miaka 4000 imepita tokea Adam aumbwe hadi Yesu kuzaliwa hivyo kufanya dunia yetu ikiwa na wanadamu kuwa na miaka elfu 6 pekee mpaka sasa!!. Ussher alitumia maandiko kama chanzo cha nadharia yake alitumia nyaraka za masoretic zilizotumika kuandaa Biblia za agano la kale ili kuweza hesabu umri wa Adam hadi vizazi vya Abraham hadi kufikia Yesu na baada ya mnyambuliko huo alifanikiwa kugundua kwamba dunia iliumbwa usiku wa October 23 4004 kabla ya kristo.

Young Earth Creationists
Vuguvugu hili la YEC lilianza miaka ya 1960 ambapo iliasisiwa na wasomi 9 chini ya PhD wa theolojia na uhandisi Bwana Henry Morris wakijikita kwenye utafiti wa uhalisia wa umri wa dunia na uumbaji na wakahitimisha rasmi kuwa dunia tunayoishi iliumbwa ndani ya miaka elfu 10 pekee na sio zaidi ya hapo na wao pia walitumia maandiko ya Biblia ya kiebrania ili kufikia hitimisho hilo hivyo na wao wakaunga mkono hoja za hapo nyuma za Professor John Ussher na hata leo hii wameweza shawishi zaidi ya 40% ya wakazi wa marekani kwa takwimu za 2017 wanaamini nadharia hii kwamba uumbaji wa dunia ni kwa mujibu wa Biblia hauzidi miaka 10,000 iliopita.

View attachment 948751
SAYANSI inasemaje??
Baada ya sayansi na teknolojia kukua na kuongezeka vifaa vya kupima umri wa miamba,mazao na mifupa ya wanyama wakaibuka wasomi wa sayansi waliohoji kuhusu uhalali wa nadharia hizi na imeleta utata na mjadala mzito kwa miaka mingi sasa. Mwanasayansi wa karne ya 20 Clair Cameron Patterson baada ya tafiti kadhaa juu ya miamba akagundua ulimwengu toka uanze una miaka billion 4.5 na baadae wanasayansi mbalimbali wakaja na tafiti mbalimbali zikidai kwa usahidi wa kisayansi na kiacholojia kwamba uhai duniani umekuwepo miaka takriban 3.8 Billion iliopita hivyo kukinzana kabisa na nadharia hizo mbili za juu kuwa Biblia

Jinsi ya kupima
Kwa upande wa Young Earth wao wanalalia maandiko kwa kiasi kikubwa na kupiga hesabu miaka ya kibiblia tokea Adam hadi Yesu lakini wanasayansi wamepiga hesabu zao kwa ushahidi wa kushikika wakitumia mfumo unaitwa radiometric dating ambacho kinapima miamba hasa stage tofauti za jinsi miamba inavyooza na ambapo kila stage ina umri wake yake yaani miaka kadhaa ili ifike stage nyingine ya kuoza hivyo wanapiga hesabu kuanzia layer ya mwisho mpaka ya kwanza na kufikia hitimisho la umri wa mwamba huo na wakafanikiwa kugundua mwamba wa kwanza ulitokea miaka 3.8 Billioni iliyopita.
View attachment 948748
Utafiti wangu (Primary)
Binafsi nilichukua hatua kuonana na wanatheolojia kadhaa kutoka chuo fulani cha Biblia wenye ngazi ya PhD na wamenijuza kwamba Biblia haikuandikwa kwa maneno bali mafumbo hivyo isitafsiriwe kwa maana zetu bali kwa mafunuo na maana zilizo kwa Biblia... Mfano wanadai Dunia haikuumbwa kwa siku 7 kama zetu hizi bali miaka mamilion na wakaenda mbali kusema Biblia haikuanza kuandika matukio yote bali imeandika matukio juu ya watu waliochaguliwa tu hivyo wanakiri kuwa kweli dunia ina miaka mabillion na sio miaka elfu 6 pekee bali wanaotafsiri maandiko kwa akili zao ndio wanapotosha sababu wameitafsiri maneno kama yalivyo badala ya kutafuta maana ya hayo mafumbo na wakanipa mistari michache.

Yohana 16:25
25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.

Na wakaenda mbali kusema hata hayo mafumbo walioambiwa kuandika Biblia hawakuyaelewa sababu ni siri imewekewa hadi wakati muafaka yaani mwisho wa dunia ufike soma hapa kisa cha Daniel

Daniel 12:4
4 Lakini wewe, Ee Danieli, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.

Hapa tunaona kuna maandiko na nabii zimefichwa kwa uelewa wetu kabisa hata Daniel hakuelewa!!

Daniel 12:8-9
8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa
mwisho.

Hivyo kama hata Daniel kuna baadhi ya vitu alifichwa na mpaka anaandika hakuvijua basi hata sisi hatuwezi vijua mpaka siku ya mwisho hivyo wakahitimisha mjadala kwa kusema huenda ni kweli dunia ina 4.5 Billion years ila sio 6000 kama YEC inavyosema maana Biblia haielezi hicho kuwa ni miaka 6000 bali watu wanatafsiri maandiko kwa akili zao ilihali YAMEFICHWA!!
View attachment 948750
Hitimisho
Ukinzano huu kati ya maandiko na sayansi juu ya asili ya umri wa ulimwengu umezua mjadala mpana sana huku kila upande ukivutia kwake nikaona kwa kuwa JF ni kisima cha maarifa nilete hii mada ili tuweze kufikiria pamoja je umri wa dunia upi ni halisi

4.5 Billion ama 6000?

Naomba kuwasilisha

Ina maama Adamu aliumbwa wakati mmoja au muda sawa na ilivyoumbwa dunia au wewe una maanisha nini ?
 
umri wa dunia probably wanasayansi wako sawa 4.5 b years,vile vile hata upande wa bible maana kuna FUMBO KUBWA SANA KATIKA KITABU KINACHOELEZEA creations ya ulimwengu hasa MW 1:1 na Mw1;2 hizi ni dunia mbili tofauti,wachambuzi wanasema ile dunia ya MWZ 1:1 ilifall to entropy baada ya shetani kumuasi MUNGU,hivyo ya kwenye Mwz 1;2 ni matokeo ya ile ya kwanza kufa nahivyo basi kilichofanyika katika hii sio creation ni regenetions.
SOMA HAPA KUHUSU CREATIONS UTAELEWA MENGI www.kjvbibl The Bible, Genesis and Geology
 
Mkuu hiyo ya Adam kuwa wa kwanza au lah ni mada pana sana inayostahili uzi wake na ntakuja kuielezea siku nyingine ila kwa sasa tunajikita umri wa Dunia iwe na wanadamu ama lah kupitia hoja za hao YEC/Ussher Vs wanasayansi je nani mkweli juu ya umri wa dunia??
umri wa dunia probably wanasayansi wako sawa 4.5 b years,vile vile hata upande wa bible maana kuna FUMBO KUBWA SANA KATIKA KITABU KINACHOELEZEA creations ya ulimwengu hasa MW 1:1 na Mw1;2 hizi ni dunia mbili tofauti,wachambuzi wanasema ile dunia ya MWZ 1:1 ilifall to entropy baada ya shetani kumuasi MUNGU,hivyo ya kwenye Mwz 1;2 ni matokeo ya ile ya kwanza kufa nahivyo basi kilichofanyika katika hii sio creation ni regenetions.
SOMA HAPA KUHUSU CREATIONS UTAELEWA MENGI www.kjvbibl The Bible, Genesis and Geology

Tatizo wanasayansi kuna mambo wanashindwa kuyathibitisha juu ya suala la uumbaji.
 
Dunia haikuumbwa kwa siku sita, Dunia ilikuwepo, ila ilikuwa Giza, Utupu na ukiwa, Yaani ilikuwa haina uhai Mwanzo 1:1-2, Mungu kwa muda wa siku sita akaitransform Dunia na kuiwekea mazingira ya kuweza kufanyika maisha kwa viumbe hai
Ukiangalia hakuna hata sehemu moja kwenye Biblia inapoonyesha kuwa Mungu anaumba maji, au Miamba, bali tunaona katika hizo siku sita anaitenga miamba na maji, yaani anavitenga vitu vilivyokuwepo, vitu alivyoviumba katika Mwanzo 1:1-2
wakolosai 1:16
Yeye ndiye ali yeumba vitu vyote mbinguni na duniani; vitu vinavyoonekana na visivyoonekana; kama ni viti vya enzi au nguvu, au watawala au milki na mamlaka: vyote viliumbwa na yeye kwa ajili yake .

yohana 1:3
Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

isaya 66: 2
For My hand made all these things, Thus all these things came into being," declares the LORD "But to this one I will look, To him who is humble and contrite of spirit, and who trembles at My word.
waefeso 3:9 Mungu aliumba kila kitu.

Ukiona hapo kwa mujibu wa bibilia bila kujali mchanganyiko wowote unaoweza kujitokeza mwanzo 1/2
Mungu kaumba kila kitu hadi maji ambayo hayajatamkwa.

Oanisha ni Kauli ya Mungu akirefer matukio ya Mwanzo 1 na 2

Kutoka 20:11
For in six days the Lord made the heavens and the earth, the sea, and all that is in them, but he rested on the seventh day. Therefore the Lord blessed the Sabbath day and made it holy.

sasa naomba maoni yako hapa. Je Tupingeje hii kauli ya Mungu na bibilia au uchambuzi gani wa siri unabatilisha hili mkuu.

cc SANCTUS ANACLETUS
 
Hii mada mbona imekuwa mpya sana kichwani kwangu?sijawahi kufikiri hata siku moja kuhusu umri wa Dunia.......ila leo nimeanza rasmi japo sio kwa umuhimu lakini huu uzi iko siku ntaleta majibu sahihi hapa(mwaka wowote)nikifanikiwa kupa jibu
 
Kosa ambalo unafanya wewe na alilofanya John Ussher ni kusoma Creation Accounts Chronologically. Kuelewa kwamba Biblia katika Kitabu cha Mwanzo inaelezea kwamba lilianza tukio hili na kisha likafuata hili na kisha lile. Unapokisoma Kitabu cha mwanzo kuna vitu lazima uvielewe kwanza. Mfano lazima uelewe Thinking ya Waebrania kuhusu Time and Space, uelewe Lugha yao na Culture yao.

Ukitaka kuelewa kwamba Kitabu cha Mwanzo hakitupatia uumbaji Chronologically,naomba ujiulize swali: Mwanga unatokana na Jua na kinyume. Je,kwa mjibu Wa Sura 1:3, mwanga ndio ulianza kuumbwa na kisha ndio Jua na Mwezi na Jua vikaumbwa( Mwa 1:16) . Je,kama mambo yalifanyika Chronologically, hali hiyo iliwezekana vipi? Kwamba Mwanga uanze na kisha ndio Jua liumbwe wakati Jua ndio linatoa Mwanga?

Kwanza:

" 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
4 Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza."

Kisha:

"16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. 17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi."

Kwa hiyo, kwa nukuu hizo hapo utagundua kwamba Kitabu cha Mwanzo hakitupatii maelezo ya kisayansi jinsi Ulimwengu na Dunia vilivyoumbwa Chronologically Bali Kitabu kitabu hicho kinaeleza na kujibu Maswali yafuatayo: Who, Why and What juu ya Uumbaji.
nakupata kwa uzuri, kuna mambo kadhaa kwenye maelezo yako haya mkuu.

1:Hiyo thinking ya waebrania ni siri au, maana hujaitumia kuthibitisha Mungu ambaye sehemu zote anasema ameumba kila kitu duniani. Na Mungu huyohuyo akasema Ameyafanya Yote kwa siku Sita na Saba akapumzika.
Nyoosha maelezo ukipinga na maelezo niliyokupa huko juu Kuhusu uumbaji.

2: Hao waebrania ambao hata leo wapo japo hawamuamini Yesu, Unauhakika wanaamini Mungu hakuumba dunia kwa siku sita au sisi waebrania wa kisasa huku bongo tunauelewa mkubwa kuliko walengwa?

3:Kuhusu Jua na Mwanga, Sioni sababu ya Kumpangia Mungu mkuu. IKiwa alikuwa Workshop anatengenza Dunia anauhuru wa kutengeneza Mwanga kisha aweke system ya mianga maana hata mwezi sio kila siku upo usiku. Hivyo Kusema chanzo cha mwanga kilibidi kiwe jua tu hata kama lilikiwa halijaumbwa ni kumfanya Mungu kuwa na uwezo finyu katika uumbaji wake.

4: Kama aliumba Nuru, Na licha ya Nuru kuwepo giza likawepo hadi alipotenganisha huoni kulikiwa na shughuli ambayo inayoendelea beyond our finite imagination. Hapo panahitaji kuchukua kauli za Mungu kama zilivyo kwa Mujibu wa Ufafanuzi wa Bibilia Yote. Ule mtiririko uko sawa kabisa, na ufafanuzi wa mwanzo 2 pia uko sawa.

Katika Mwanzo mkuu kuna 5W zote na 1H
who - Mungu, Yohana 1 pia ikatia Muhuli yote hayakufanyika bila Yesu pia
What - Dunia
When - Hapo mwanzo kwa siku sita mfurulizo.
Why - Ili Mwanadamu atawale na kuvitiisha vyote vilivyomo.
Where - Kutoka katika "SI KITU" hadi Vitu au Dunia na Vitu Vilivyomo.

How
Kwa Kutamka na Vitu vikawa. Katengeneza na interdependent and self supporting system, Mmiliki Mwanadamu akamfanya kwa mavumbi ya ardhi, na akatengeneza system ya kuendeleza kizazi.
Hiyo chronological ni scientific kabisa mkuu. Na wapo wanasayansi wengi wanaoamini huo uumbaji wa siku sita hata kama sio wakristo lkn wanauchambua scientifically hadi raha. Jaribu kujifunza katika stream zote sio kwa wapinga Mungu tu.

Chanzo cha migogoro unayojitengenezea kilianza Amri ya nne IlipoNYOFOLEWA katika Amri Kumi sasa inabidi itafutwe justification ya kuungaunga kupinga matukio halisi ya Mwanzo. Nimekuqmbiq Bibilia Yote, inapoquote matukio yq Mwanzo inayareferer kama matukio halisi. Yesu aliyeumba anarefer matukio hayo kama yalivyo.
Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
mathayo 19:4-5.
Leo wafuasi wa Yesu wa Kisasa tunataka kuyafanya siri, mara hoo hadi tukawahoji waebrania, mara hadi twende vyuoni.

Hujaonyesha pia mkuu Kuwa Mungu aliyesema Kaumba kila Kitu, alifanya yote kwa siku sita kuwa alidanganya au hao waebrania hawakumuelewa miaka yote na hawajamuelewa hadi kesho ila waebrania wa ulaya au italy wamemuelewa zaidi.

karibu kwa maoni mkuu
 
For in six days the Lord made the heavens and the earth, the sea, and all that is in them, but he rested on the seventh day. Therefore the Lord blessed the Sabbath day and made it holy.

Hiyo bold siyo ushahidi kwamba kweli Dunia iliumbwa kwa siku Sita. Ulichofanya kuendelea tu kulieza wazo lako la uumbaji kwa muda Wa Siku. Hebu unaweza kurejea kwenye la Kiebrania "Yom" lenye maana ya siku uone lilipotumika muda ule lilimaanisha nini na " Bara" lenye maana ya Create lilikuwa na maana gani? Haya yatakusaidia kuanza kuelewa Ninachokiongelea.
 
Pia kama mkuu Sala na Kazi alivyotoa hoja, kwa sababu science ni progressive kila siku wanavumbua mapya wanaweza kuvumbua kile ambacho tunakisema pia, ingawa trend haionyeshi hilo.
Idea kama zile licha kuwa na mapungufu, zipingwe kwa maandiko aliyotumia, au wanayotumia pro-creation scientists kwamba dunia haina miaka mamilioni bali miaka kama angalau elfu sita based to biblical genealogy ya Adam.
sasa naomba ujenge hoja kutokea kwenye bibilia kudenounce idea kuwa Dunia ni kinda inamiaka maelfu na sio mamilioni ili akili zichekechwe vizuri.

Sasa hizi za kisayansi PingaMungu utaziaminije mkuu kuwa ziko sahihi kuliko ukokotozi wa kibibilia ikiwa hypothesis zake zinakana uwepo wa Mungu na Uumbaji wenyewe.
huoni kama unaingia mkenge ikiwa tutashindwa kujenga hoja biblically. Kama kusema kuna Ideas nje ya Bibilia sikatai ila lazima ziumane na Biblical truth au scriptural ideas ili zilete maana vinginevyo tutakuwa tunatembea kwenye sakafu potoshi.
mkuu mitale na midimu binafsi nimejaribu kusoma post zako kwa umakini. kuna baadhi ya maelezo yako nilitaka kukukanusha na pia nimefikiria kukuuliza maswali kadhaa kuhusu hoja na misimamo yako hasa juu matumizi ya sayansi, roho mtakatifu na biblia. lakini nimeona haina haja kwa sasa sababu post zako nyingi zinaonesha ni namna gani unavochanganya TAFITI ZA KISAYANSI NA BIBLIA. zinaonesha ni namna gani unavolazimisha TAFITI ZA KISAYANSI, ziwe poved na BIBLIA ilihali sayansi ina principle zake na bihlia ina principle zake kama kitabu cha KIIMANI na sio kitabu cha sayansi au philosophy. ndio maana kuna msemo unaosema kuwa "inapoishia sayansi ndipo imani inapoanzia"

kiujumla unalazimisha BIBLIA ithibitishe mambo ya kisayansi jambo ambalo nisawa na kulazimisha SAYANSI ithibishe mambo ya KIIMANI, imani na sayansi wapi na wapi mkuu.

kwenye sayansi na falsafa.hakuna neno IMANI/KUAMINI huko wanaongozwa na REASONING AND PRINCIPLES TU. hivyo mkuu kudai uthibitishoa wa masuala ya sayansi kwa kutumia biblia huko ni kuionea sayansi kwani sio kazi yake.

hivyo kwa muktadha huo niliokuonesha hapo juu binafsi ninaona huu mjadala unakuwa mgumu na haufiki mwisho zaidi ya kuzungukana tu. ndio maana kuna mchangiaji mmoja hapo juu unamdai uthibitisho wa mistari ya biblia katika hoja za kisayansi kitu ambacho kiukweli huwezi kikupata popote pale yaani kuprove hoja za kisayansi kwa mistari ya biblia hii haiwezani mkuu. uthibitisho wa kisayansi una formula na principle zake mkuu na sio mistari ya biblia.

mpendwa mitale na midimu binafsi ninafikiri kama Mungu angekusudia biblia kutufundisha sayansi/kutueleza kweli za kisayansi kinagaubaga kusingekuwa na haja ya wanasayansi, tafiti za kisayansi na sidhani kama Mungu angetuagiza tumpende kwa AKILI yetu yote nk kwani kila kitu, kila fomula na kila aina ya sayansi angetuwekea kwenye biblia na pia tusingekuwa tuna haja ya kusoma sayansi mashuleni nk cha msingi tunapaswa kumwomba roho mtakatifu atuongoze na kutusaidia kutambua pande POSITIVE na NEGATIVE za sayansi ilikulinda Imani yetu na mwisho kuufikia uzima wa milele.

wapendwa @zito junior SANCTUS ANACLETUS na mitale na midimu mtizamo wangu ni huu masuala mazima ya sayansi naamini katika tafiti za kisayansi na majibu ya kisayansi iwapo hayapingani na imani. na masuala mazima ya kiimani kuhusu Mungu na ulimwengu wa roho naamini katika biblia neno la Mungu. mapokeo matakatifu na mamlaka rasmi ya ufundishaji ya kanisa

vinginevyo kuendelea kuchanganya sayansi na biblia kitabu kielezeacho kweli za kiimani sidhani kama tunaweza kufika mwisho wa mjadala zaidi kulumbana.

hayo ni maoni yangu wapendwa.
 
Ina maama Adamu aliumbwa wakati mmoja au muda sawa na ilivyoumbwa dunia au wewe una maanisha nini ?
Hapana nachomaanisha je Dunia hii ina umri gani na sio VIUMBE vina umri gani maana obvious Dunia lazima iliumbwa kwanza kabla ya mwanadamu hivyo natamani nifahamu upi ni umri sahihi wa Dunia ni ipi maana Ussher alichosema ni kwamba Dunia iliumbwa siku sita kabla ya Adam kuletwa duniani na ndio maana nikaona nilete hii mada humu tusaidiane kujua nani mkweli kuhusu suala hili.
 
Back
Top Bottom