Biblia ndio kitabu pekee kinachojibu maswali Mengi kumuhusu binadamu na maisha yake

Vilaza hao achana nao, jitu linaamka huko lilikokuwa halina elimu yoyote ya maana zaid ya kukalili kitabu kilichoEditiwa na kila aina ya watu alafu jitu la hivi linataka Competition na watu waliosoma elimu ya vitabu vingi na ujuzi mwingi.

Mtu akishalogwa na dini ni ngumu kumkomboa zaid ya kutandikwa bakora akili irudi maala pake
 
Kilichoumbwa kwa mfano wa Mungu ni Roho, sio Mwili.
Mbona uzi huu umejibu swali lako.
(Natumfanye mtu kwa mfano wetu akatawale viumbe wa baharini, ardhini na angani) hapa hawakuongelea Roho bali mwili yaan ni mwili walioumba wakaupa maagizo ya kwenda kuucontrol ulimwengu, someni vzr hivyo vitabu vyenu vya uongo ili muelewe na sio kutumia hisia mlizolishwa makanisan.

Mtu alipoumbwa kwa mujibu wa biblia muonekano wake(physical appearence) walimaanisha inafanana na hao waumbaji sijui ndio akina nan, kiufupi biblia imedanganya, huwezi sema umuumbe kiumbe kwa mfano wako alafu huyo kiumbe awe tofauti na wew kimuonekano mpaka mfumo mzima wa muundo wa uumbwaji, mwanadamu ana mwili, nafsi na Roho, je hao waumbaji wana mwili? Wana nafsi? Wao wana Roho tu ambazo hatujui ziko vipi, kiufupi hapa biblia ilidanganya, waandishi wa hiki kipande walitakiwa kupigwa bakora akili ziwakae sawa
 
It is not a physical eyes, it is spiritual eye.


Understand it
Wapi Biblia imesema "spiritual eye"? Zaidi yako wewe kusema hayo?

Hilo sasa tatizo, labda unambie ni "metaphorical" tu, utamu wa lugha tu, na "kumuona" haimaanishi kumuona, na kupigana na Mungu haimaanishi "physically ni metaphorically"" unipe kinachoingia akilini, lakini "maneno ya Mungu" bila kuwa na mafundisho mema yoyote kwa maisha yetu ya kila siku yana faida gani kwetu?
 
Sijakuelewa, kwa hiyo unasema kuna maneno ya kwenye biblia yametokana na shetani?
 
Naujua zaidi kwa vile kaanzisha paulo .

Kwa mantiki haujajibu swali langu na nimetoa kweny bible.

Kiufupi wewe hujui bible kwa vile hauna elimu kwa vile unashindwa kujibu na ayah natoa kweny bible yako😂😂
 
😃😃😃 Ukiwa mlopolopo uwe na kumbukumbu.

Muanzilishi wa ukristo ni nani ?

Ukasema kama Yesu alianzisha Ukristo basi utaslimu.

Go ahead sasa
Sasa nionyeshe wapi yesu kaanzisha ? mimi nimekupata ayah kwamba Paul ndo kaanzisha.😂😂

Mjadala huru mlete kardinal wako hapo aonyeshe wapi yesu alianzisha ukristo maana wewe hujui kitu nakuonea tu.
 
Twende kwa maandiko kwanza ili uelewe vizuri.

Yohana 4:24
[24]Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Kwa hiyo, kinachoonekana hapa ni ROHO, na sio mwili wa damu na nyama.

Endelea kuangalia tena wakati wa uumbaji wa mbingu na dunia nini kilikuwepo kati ya roho na mwili;

Mwanzo 1:2
[2]Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Kwa hiyo hapo unaona, kilichokuwepo ni ROHO YA MUNGU na sio Mwili wa Mungu.

Kwa hiyo, Mungu aliposema "Na tumuumbe mtu kwa mfano wetu" alimaanisha kufanana ROHO (NAFSI) na sio MWILI.

Haya mambo ya waafrica, wazungu, waarabu n.k huo ni mwili ambao SIO MFANO WA MUNGU
 
Nionyesha katika adabu na taratibu za binadamu kama kula ,kulala, kutembea Na mambo ya kili siku kupitia bible?
Biblia haijaacha kitu ndugu yangu;
Tuanze na taratibu za kula;

Yohana 13:2
[2]Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskariote, moyo wa kumsaliti;

Point yangu hapo ni chakula cha jioni, hivyo kama kimeongelewa chakula cha jioni, basi kipo na cha mchana na asubuhi kadhalika.

Angalia tena hapa Mungu anawapangia waisraeli kuwa wale kitu gani kwa wakati gani;
Kutoka 16:12
[12]Nimeyasikia manung’uniko ya wana wa Israeli; haya sema nao, ukinena, Wakati wa jioni mtakula nyama, na wakati wa asubuhi mtashiba mkate; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Unaona hapo Mungu anaagiza asubuhi wale nini, mchana wale nini.

Tuendelee, hata jinsi ya kukaa wakati wa kula chakula, biblia haijanyamaza; angalia maandiko;
Mwanzo 43:32-33
[32]Wakamwandalia yeye peke yake, na wao peke yao, na wale Wamisri waliokula pamoja naye peke yao; maana Wamisri hawawezi kula pamoja na Waebrania, kwa kuwa ni chukizo kwa Wamisri.

[33]Wakaketi mbele yake, mzaliwa wa kwanza kwa cheo cha kuzaliwa kwake, na mdogo kwa udogo wake; watu hao wakastaajabu wao kwa wao.

Unaona hapo, waisraeli walikuwa wakitaka kula wanakaa kwa kufuata nafasi ya kuzaliwa, wa kwanza hadi wa mwisho.

Hivyo kuhusu taratibu za chakula biblia iko clear, lete hoja nyingine tu.
 
Mungu ni roho,alipomuumba mtu kwa mfano wake aliumba roho mwanadamu kabla hajaupata mwili alikuwa roho.mwili tuliupata pale Mungu alipotutaka tuje kuishi duniani.aliufanya mwili kwa mavumbi kisha akatuweka humo.
Mwanzo 3:7 7 Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Mwanzo 2:7. Kwahiyo wewe halisi sio mwili wewe ni Roho inayoishi ndani ya mwili.mwanadamu yeyote anayejitambua ni lazima alitambue hili ya kwamba she/he is a spirit living in a physical body
 
Jmani angalia point zangu nyingi hapa kama unafuatilia ...Cha kwanza inaathirika moja kwa na haiwezi kuwa ya kisasa kuhusu kuachana na ndoa kwa viongozi sa dini ,huoni kiuhalisia kwa sasa ni balaa.

Binadamu aliyekamilika ndo hao wanakuwa na watoto wa nje... Kwamba mfunge ndoa ila kuachana mpaka muende mahakamani kwamba biblia haijui kuhusu kuachana ? kwa nn binadamu kwa matakwa yao wanataka kuachana kwa hiyari yao ila hawana Muongozo kupitia bible😂.

Hayo mambo mwenzio alikuwa hajui mimi najua kuanzia kulaa nilale vip, kuamka,kuvaa viatu ,kutembea ,kusalimia mzunguko mzima mpaka jioni narudi huu ni utaratibu kamili.



 
Si kweli, katika Ukristo watu wanafundishwa kwenda kutafuta maarifa zaidi sehemu mbalimbali na mafundisho hayo yanatokana na Biblia.

Kingine, Biblia haisomwi wala kuenezwa kishabiki kama ufanyavyo.
Hiyo si Kati ya misingi na mafundisho ya Biblia. Unaweza ukatafuta watu ambao misingi yao ni kujiinua na kujiona wao ni bora kwenye kila kitu na ukajiunga nao hao, lakini usihamishie hayo kwenye bible na Ukristo.
 
Kuhusu ibada za kikriso maandiko yanasema Yohana 4:24 kwamba Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu yeye katika roho na kweli. hivi ndivyo wakristo tunamuabudu Mungu,ndivyo tufanyavyo ibada. Sisi tunasali Rohoni wakati wote 24/7 tuwe kazini barabarani shambani vitani usingizini tunasali rohoni.kwa mtu mwingine huwezi kujua kama tunasali kwasababu hatuongei kwa mdomo wa mwili na nyama bali rohoni . Sisi tunafanya makutaniko kama tulivyoagizwa ,Ebrania 10:2525 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Na kuhusu ndoa maandiko yanatufumdisha ndoa ya mke na mume mmoja Mathayo 19:4 .na kuhusu hili ukristo unatambua ndoa za kimira kiselikali au kanisani kwasababu ndoa ni agano la mtu/watu na Mungu. Tunamuona rebeka katki biblia wazazi walimuuliza kama yupo tayari kwenda na mumuwe alipojibu yupo tayari walimtakia safari njema.

Na kuhusu kuzika wakristo tunazika tunayo mifano mingi katika bible ya waliokufa .sijui hapa unataka kujua nini. Kama ni wanawake kuzika then yes ukisoma yohana 11 martha alimzika kaka yake lazaro. Lakini ukristo haujishughulishi sana na mambo ya mwilini ndio maana kuna andiko pia Yesu anasema acheni wafu wawazike wafu wenzao.
NB. Mambo haya ni according to christian na hiyo haimaanishi we are superior or inferior. Dini ni mpango wa mwanadamu kumfikia Mungu lakini wokovu ni mpango wa Mungu kwa aliowaandaa kuwa wake regardless dini.ndio maana kuna waislamu wanaoa mke mmoja na ni msimamo hataki kuoa wengi,na kuna wakristo wanaovalia mavazi kama ya kiislamu and so on. Hatutakiwi kuwa na vikwazo vya sisi kwa sisi kisa dini popote ulipo shika shikilia wokovu ni wa Bwana
 
Kwanza kabisa neno la Mungu ni lilelile juzi leo na milele hakuna kitu kama ukisasa kwenye neno.Mungu hafuati matakwa ya mwanadamu bali mwanadamu afuate matakwa ya Mungu. Kinachopingana na Mungu kinatoka upande wa pili. Biblia haiwezi kukinzana yenyewe yaani mtu aoe then iwe na option ya kuachana, Yesu anasema isipokuwa kwa dhambi ya uzinzi tena anasema hata kwa hiyo dhambi hawa wawili wakiachana atakaye muoa yule aliyeachwa kwa kuzini nae anazini nae atakae olewa na yule aliyeacha kwa kuzini nae anazini kwahiyo inshort hakuna kuachana, Mungu anaendelea kuiona hiyo ni ndoa mpaka mmoja wao afe sasa kwanini viongozi wa dini waachanishe kitu ambacho wanajua fika mbinguni bado kinasoma?! Ndio maana ni mahakama isiyo na dini bali itakayo amani ya dunia hii ndio huachanisha watu ila ndoa ya hawa watu huendelea kusoma mpaka mmoja afe.
Kuhusu utaratibu wa kula kuvaa nk wakristo haitushughlishi sana tunafanya inavyompendeza Mungu .ukisoma math 15 mafarisayo walimuuliza yesu mbona wanafunzi wako hawanawi mikono wakati wa kula kama tulivyopokea kutoka kwa mababu zetu.kwahiyo unaona hata kunawa walikuwa hawanawi. Utaratibu upo kwaajili yangu mimi sio mimi kwaajili ya utaratibu. kutembea kila mtu ana miondo yake hatuwezi kukubaliana ati tuwe tunatembea hivi.kulala sisi wakristo hatulali ni miili yetu tu ndo inalala ila sisi tuko macho 24/7 kwahiyo mwili hata kwenye mawe utalala🤣 .sisi tunasafisha ndani ili nje kuwe kusafi.
 
Accumen Mo apata darasa hapo juu kwanza, kisha twende taratibu.

Nimekwambia Amri kuu tuliopewa wakristo ipi.
Na Mungu wetu hutoa Hekima na Maarifa kwa watu wake jinsi ya kuishi.
Suleimani aliomba Hekima akapewa na akaweza kufanya hukumu akiwa kama mfalme.
Kaandika vitu vingi kwenye biblia, ila wewe huoni.
Tumepewa uhuru wakristo na hatufati sheria za mwilini, kwamba ukivaa kanzu Mungu anafurahi zaidi kuliko ukivaa suruali na sharti.

Tuenende kiroho.

Ukristo ulitufikia tukiwa na kawaida yetu ya mambo mengi kwasababu tunaufahamu ambao tunao na akili ya kidunia tunayo kila binadamu.

sasa ukilazimisha ufundishwe, kula, kuvaa, kupaka mafuta, kusalimia naomba ufungue da care tutakuja kijiunga kindergarten 😃😃🤣
 
Kama jibu ni hapana what next?

Hiyo ndiyo inafanya mungu awepo?

Unaweza thibitisha haya madai yako,

Unaeeza kuthibitisha uwepo wa Mungu!?
Ndio. Utawezaje kushindana na mtu ambaye haumuwezi?
Let alone haumjui?

Yaani mwanadamu nii sawa na sisimizi kumchunguza mwanadamu. Kisa mnaishi kwenye ulimwengu mmoja...

Au mwanadamu na Bacteria..yes...bacteria anaishi kwenye ulimwengu wa mwanadamu, ndani ya mwili wa mwanadamu, lakini hayajui mengine ambayo mwanadamu anaishi nje ya mwili wake.

Mungu yupo kwenye ulimwengu huu lakini hatumuoni, kwa sababu yeye makazi yake ni ulimwengu wa milele...na huu ulimwengu tunaoishi ni sehemu tuu, ya muda mfupi kwenye ulimwengu wa milele.

Sasa utajuaje habari za Mungu kwenye ulimwengu huu?? Jibu ni hapana, hautajua chochote. Utakosoa hivi vyote vilivyoumbwa kwa hoja ndogondogo, ila hoja kubwa za uwepo wa Mungu zipo kiroho zaidi, na hauwezi elewa maana yake haujui chochote kwenye ulimwengu wa roho...ila ukishajua tuu, ndio utaelewa zaidi
 
Wasiojua wanaachwa wasijue maana wataleta vurugu kwa wanaojua, na wasiojua siku zote wapo wengi[emoji3][emoji3]

Na wanaojua siku zote huwa wachache na wanaendelea kujua zaidi na kutumia elimu hii kunufaika na kufika mbali zaidi na zaidi...

That's the law. Of nature.

Unadhani watu ni wajinga wanapopiga kampeni ya uchaguzi na kuzunguka maeneo yote ya nchi nzima? Kila jimbo, kila utawala?

Sipendelei siasa, ila Ndio maana nawaambiaga wanasiasa kuwa Upinzani hapa nchini haitokaa itawale nchi hata kidogo kwa sababu they're too weak on almost everything.

Wanataka kujua lakini at the same time hawataki kujua.

Chama tawala kinawatazama tuu, na kuwanyamazia kimya...kimetega mitego mingi sana na masimiko mengi mno ya kuitawala nchi milele, na hakuna hata chama, au serikali au nchi ingine inayoweza kutikisa chama tawala nchini...hata marekani wenyewe. (Rejelea kipindi cha Magu, mambo aliyoyafanya kibabe na nchi zingine, na kila mtu alimtii, kuitisha mkutano wa nchi masikini kusema ni matajiri, kumuita yule kigogo wa madini ikulu, kuichomolea nje korona, na kadhalika.)

Serikali ya Tanzania nadhani ipo vizuri na fit mno katika kuilinda na kuitunza jamii yake kuliko serikali ingine yoyote ile duniani kwa sasa...na pia inafulea watanzania kama watoto wadogo yaani..tunadekadeka tuu ujinga

Hata marekani wenyewe wapo so vulnerable kuliko Tanzania. Na hii yote tunamshukuru sana Nyerere aliyoyafanya..baba wa taifa was a little genius, mjanja, na sawa na malaika wa kisiasa kwa ajili ya eneo lake la kazi ambalo ni Tanzania.

Kama hauwezi kuelewa, usijali. Kajifunze, ukiwa sawa ndio uje usome tena hii post.[emoji2][emoji2]
 
Kwa mantiki hiyo biblia haiwezi kuamua na kuendana na maisha ya sasa😂😂mbona watu wanaachana kwa hiyari yao mfano Marehemu Mengi.

Mfano watu wanamichepuko ni sawa ila kuongeza mke hapana ,kwa mantik ya uumbaji biblia ni batili hapa tunajua maumbile ya mwanaume...So nakuonyesha bible ni batili😂😂kabisa na ninayo mifano lukuki
 
😂😂unachekesha sana ibada mnafanya rohoni ? kelele za siku ya ibada zimetoka wapi?
Ibada ikiambatanishwa na nia ni rohoni hili ni popote pale.

Nakula hapa nimeanza kwa jina la Mungu kimoyo moyo ila mkristo aliopo karibu yangu naona anazungusha mikono kweny mabega mpaka kweny paji la uso.


Mliambiwa mwili wa binadamu ni hekalu la Mungu ina maana kila tendo lazima liambatane na ibada kwamba lazima ufanye kwa kufuata sheria za Mungu...
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…