Bila Upelelezi kukamilika hakuna kukamata, ukiachiwa na Mahakama hakuna kukamatwa tena

Bila Upelelezi kukamilika hakuna kukamata, ukiachiwa na Mahakama hakuna kukamatwa tena

Hapo nimeelewa baada ya kuona aina ya makosa ambayo haya husiki nahiyo sheria.

Chakuangalia hapo ni jinsi ya kuzuiya ubambikaji wa kesi maana mtu akiwa na chuki anaweza kukubambikia kesi ambayo haihusiani na hayo mabadiliko sheria na msoto wa rumande unabaki palepale, otherwise nampongeza mama kwa hili.
 
Mama anaupiga Mwingi ila asije kubadili gia angani kama umeme wa 27,000/=
 
Tunaposema kila Mtanzania amuunge mkono Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan tunamaanisha mambo kama haya, Niwe mkweli tu tangu Uhuru Mama huyu ni watofauti sana hebu ona alichofanya kwenye magazeti na hii,
===
Bunge limepitisha Mabadiliko muhimu ya Sheria kupitia muswada wa mabadiliko ya Sheria mbalimbali Na. 7 wa mwaka 2021 ambapo kifungu cha 131 cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kimefanyiwa mabadiliko.

Kifungu hiki kipya cha 131A kinamkataza Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP), Polisi, au yeyote mwenye mamlaka ya kushitaki, kutokupeleka kesi mahakamani pasipo upelelezi kukamilika. Hii ilipelekea mtu kukaa na kesi kwa miaka mingi huku kila siku akiambiwa na waendesha mashitaka kuwa upelelezi haujakamilika.

Pia kwenye mabadiliko haya, ikiwa utashitakiwa na mahakama kukuachia huru, basi polisi hana mamlaka ya kukukamata tena na kukufungulia kesi upya. Kitendo hiki kilikuwa kinawafanya watu watoke mbio sana mahakamani mara baada tu ya kuachiwa huru.

Kwa msingi huu Mwendesha mashtaka wa serikali, Polisi, na wengine wote wenye mamlaka ya kushitaki, ikiwa hajakamilisha upelelezi hana haki ya kufungua kesi mahakamani hadi pale atakapokamilisha upepelezi na pia hawezi kukukamata ikiwa umepatikana huna hatia na mahakama.

Unaweza ukaniuliza ikiwa wamekatazwa kupeleka kesi mahakamani kabla upelelezi haujakamilika, ina maana sasa watuhumiwa watasota sana selo mpaka polisi wakamilishe upepelezi wa makosa yao?

Jibu ni hapana, mabadiliko hayo hayo kifungu cha 131A (2) kinasema kuwa ikiwa upelelezi haujakamilika na hivyo kutomwezesha mtu kupelekwa mahakamani basi anatakiwa aachiwe kwa kupewa dhamana wakati polisi ama mamlaka nyingine ikiendelea kukamilisha upelelezi wa makosa yake. Hautakiwi kuwekwa selo au kukaa polisi ikiwa upepelezi wa kosa lako haujakamilika.

Hata hivyo, katazo hili la kutopeleka kesi mahakamani bila upelelezi kukamilika linahusu makosa yote isipokuwa makosa ya kubaka (rape), wizi wa kutumia silaha (armed robnery), kumiliki silaha kinyume cha sheria, kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria, makosa ya kujeruhi sana (grievious harm), kosa la kuhatarisha usalama wa taifa, usafirishaji dawa za kulevya, na jinai nyingine ambazo hadhi yake husikilizwa tu na mahakama kuu. Kama kesi yako imefunguliwa mahakama kuu basi kosa hilo haliguswi na mabadiliko haya, utaratibu wa kawaida wa mashauri ya jinai utafuatwa.

Kifungu cha 131A(3) cha mabadiliko haya kinatoa msisitizo kwenye kifungu cha 170(6) cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kwamba kama makosa ambayo adhabu zake kama mtu angekuwa anahukumiwa na mahakama angehukumiwa kulipa faini ya Tshs 200,000/= basi mtu huyo anatakiwa akiri kosa kwa maandishi, kisha alipe faini hiyo kwenye akaunti za serikali, na aachiwe huru.
Vyema! Lakini haikua haki ya mtanzania kuondolewa kwa vifungu kandamiz vya sheria?
 
Bado haija solve tatizo effectively ikiwa uwepo mahabusu za Polisi nao hautaangaliwa. Usishangae watu wakakaa kwenye mahabusu za Polisi miaka na miaka wakisubiri kufikishwa Mahakamani.
mahabusu za polisi mwisho kukaa ni siku 14
 
Hapo naona kama unafuu mdogo sana coz kama wakiwa na Nia mbaya na wewe watakushtaki kwa hayo makosa mengine yasiyokuwa na dhamana na blabla nyingine
 
Tunaposema kila Mtanzania amuunge mkono Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan tunamaanisha mambo kama haya, Niwe mkweli tu tangu Uhuru Mama huyu ni watofauti sana hebu ona alichofanya kwenye magazeti na hii,
===
Bunge limepitisha Mabadiliko muhimu ya Sheria kupitia muswada wa mabadiliko ya Sheria mbalimbali Na. 7 wa mwaka 2021 ambapo kifungu cha 131 cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kimefanyiwa mabadiliko.

Kifungu hiki kipya cha 131A kinamkataza Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP), Polisi, au yeyote mwenye mamlaka ya kushitaki, kutokupeleka kesi mahakamani pasipo upelelezi kukamilika. Hii ilipelekea mtu kukaa na kesi kwa miaka mingi huku kila siku akiambiwa na waendesha mashitaka kuwa upelelezi haujakamilika.

Pia kwenye mabadiliko haya, ikiwa utashitakiwa na mahakama kukuachia huru, basi polisi hana mamlaka ya kukukamata tena na kukufungulia kesi upya. Kitendo hiki kilikuwa kinawafanya watu watoke mbio sana mahakamani mara baada tu ya kuachiwa huru.

Kwa msingi huu Mwendesha mashtaka wa serikali, Polisi, na wengine wote wenye mamlaka ya kushitaki, ikiwa hajakamilisha upelelezi hana haki ya kufungua kesi mahakamani hadi pale atakapokamilisha upepelezi na pia hawezi kukukamata ikiwa umepatikana huna hatia na mahakama.

Unaweza ukaniuliza ikiwa wamekatazwa kupeleka kesi mahakamani kabla upelelezi haujakamilika, ina maana sasa watuhumiwa watasota sana selo mpaka polisi wakamilishe upepelezi wa makosa yao?

Jibu ni hapana, mabadiliko hayo hayo kifungu cha 131A (2) kinasema kuwa ikiwa upelelezi haujakamilika na hivyo kutomwezesha mtu kupelekwa mahakamani basi anatakiwa aachiwe kwa kupewa dhamana wakati polisi ama mamlaka nyingine ikiendelea kukamilisha upelelezi wa makosa yake. Hautakiwi kuwekwa selo au kukaa polisi ikiwa upepelezi wa kosa lako haujakamilika.

Hata hivyo, katazo hili la kutopeleka kesi mahakamani bila upelelezi kukamilika linahusu makosa yote isipokuwa makosa ya kubaka (rape), wizi wa kutumia silaha (armed robnery), kumiliki silaha kinyume cha sheria, kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria, makosa ya kujeruhi sana (grievious harm), kosa la kuhatarisha usalama wa taifa, usafirishaji dawa za kulevya, na jinai nyingine ambazo hadhi yake husikilizwa tu na mahakama kuu. Kama kesi yako imefunguliwa mahakama kuu basi kosa hilo haliguswi na mabadiliko haya, utaratibu wa kawaida wa mashauri ya jinai utafuatwa.

Kifungu cha 131A(3) cha mabadiliko haya kinatoa msisitizo kwenye kifungu cha 170(6) cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kwamba kama makosa ambayo adhabu zake kama mtu angekuwa anahukumiwa na mahakama angehukumiwa kulipa faini ya Tshs 200,000/= basi mtu huyo anatakiwa akiri kosa kwa maandishi, kisha alipe faini hiyo kwenye akaunti za serikali, na aachiwe huru.
Bado kuna shida, maana wata weka watu mahabusu miaka tele bila kufikishwa mahakamani
 
Shika adabu yako wewe,Una maana sisi Sukuma Gang ni vichaa?
A self confessed SKM Gang member(na sio lazima awe msukuma), is a mad mad killer of sorts.
Wengine hata kwa sura zao tu!
1644577426475.png
 
Wanaompinga Mama ni vichaa na watu wabaya tu,

Wasiopenda kuona WATANZANIA wakiwa wamoja wakati wote,

Wasiopenda watu waishi kwa raha mstalehe kwenye nchi yao,

Tunayo nafasi ya kujenga Taifa bora sana tukiwa na Mama Samia,
Bado kwenye muungano hakujakaa sawa kabisa..katiba bado inapwaya..tume ya uchaguzi ina pwaya pakubwa.

Kwa hili nalipongeza bunge


#MaendeleoHayanaChama
 
Akikosea atakosolewa,akifanya vizuri atasifiwa.......tupunguze unafiki wa kisiasa
 
Hapo naona kama unafuu mdogo sana coz kama wakiwa na Nia mbaya na wewe watakushtaki kwa hayo makosa mengine yasiyokuwa na dhamana na blabla nyingine
Tena wakati wa mwendaake hata ukimpasha ukweli kiongozi kwa mapungufu yake, unatafutiwa kesi ya uhujumu uchumi.
Kuna waliofia jela kwa kubambikwa kesi, mfano mzee Shamte wa TPSF.
 
Huyu ndo rais aliyetumwa na MUNGU,inchi Ina visheria vidogo vidogo ambayo vinaumiza Sana,mama take them off
 
Serikali hii hii ya ccm ndiyo iliyotunga nakutumia sheria mbovu miaka na miaka alafu serikali hii hii inakuja kurekebisha hiyo sheria alafu unataka tushangilie.Kwa akili za ovyo hizi tuna safari ndefu sana zakufikia kuiwajibisha serikali inapotenda isivyo stahili.Kwasababu siamini kua tunapaswa kutenda mabaya kwanza kisha badae ndo tuyarekebishe baada ya wananchi wengi kuumia.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom