Bilioni 11 za Rais Samia zamtetemesha RC Shinyanga, afanya maamuzi magumu

Bilioni 11 za Rais Samia zamtetemesha RC Shinyanga, afanya maamuzi magumu

RC anasema hivi kwa sababu yeye sio " accounting officer" wa mkoa. Hata hayo ya kumuondoa afisa ni maneno ya jukwaani. Mwenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Katibu Tawala wa Mkoa. RC hapitishi matumizi yeyote mkoani na ha saini hundi yeyote. Wenye mamlaka hayo ni makatibu tawala na wakurugenzi. Hapa ameingilia kazi za wenzake.
Amemuacha mkurugenzi kwa sababu anajua kuwa bila yeye hakinunuliwi kitu hata afanye nini. Wanachoweza kufanya watendaji wakipata amri kama hizi ni kuzipeleka kwa madiwani ili watoe baraka zao. Minutes za kikao cha madiwani na kibali cha Katibu Mkuu wa Tamisemi kitamchomoa kwenye tundu la sindano. Kama alivyo chomoka yule wa Vieiti. Wakimkatalia nayo ni vizuri. Hata wakikaa kimya, ataweza kuchomoka kwa kusema anangoja maelekezo kutoka wizarani. Akitekeleza tu mzigo wote utakuwa wake hasa itakapogundulika kuwa vifaa alivyonunua havina viwango.
Wanasiasa wabaki kwenye siasa na waheshimu wenye taaluma zao.

Amandla...
 
Rc Shy kachemka nahoji uhalali was vyeti vyake na vetting itakuwa ina chenga chenga procedures za manunuzi hazikwepeki hiyo siyo pesa ya mtu binafsi aache mihemko
 
Utawala bora ni Upi?
Watoto wasiende shule kwa wakati?
Mkuu, unaweza ukaona ni heri akatafutwa mzabuni au mkandarasi kwa njia ya mkato ili watoto waende shule, lakini siku ikibainika kuna shaka katika matumizi ya fedha, huyo huyo afisa manunuzi anayelazimishwa atumie njia za mkato ndiye atakayeswekwa ndani kwa kile watakachokiita 'kukiuka taratibu za manunuzi ya umma'

Mbaya zaidi mahakamani huwa hakuna utetezi kwamba ulitumia busara mradi ukamilike haraka watoto waende shule, sana sana huwa kuna mashtaka kwamba ulivunja sheria za manunuzi, na atafungwa afisa manunuzi, sio mkuu wa mkoa. Na tena sisi wenyewe huwa tunakuja kusaga kunguni kwamba afisa manunuzi alileta kampuni za ndugu zake!
 
Huyo RC kelele tuu na kama alifuata utaratibu hana ujanja wa kumfukuza kazi atarudishwa na atalipwa haki zake zote
 
Peleka vyako mkuu,
Mimi vyangu genuine vipo chini ya mchago kitambo ila kwa kauli ya Rc Shy kwakweli kaonyesha kupwaya Sana even if wanatumia force ac/ single source lakini PPA zifuatwe ninaongea by experience ni hili
 
Mkuu, unaweza ukaona ni heri akatafutwa mzabuni au mkandarasi kwa njia ya mkato ili watoto waende shule, lakini siku ikibainika kuna shaka katika matumizi ya fedha, huyo huyo afisa manunuzi anayelazimishwa atumie njia za mkato ndiye atakayeswekwa ndani kwa kile watakachokiita 'kukiuka taratibu za manunuzi ya umma'

Mbaya zaidi mahakamani huwa hakuna utetezi kwamba ulitumia busara mradi ukamilike haraka watoto waende shule, sana sana huwa kuna mashtaka kwamba ulivunja sheria za manunuzi, na atafungwa afisa manunuzi, sio mkuu wa mkoa. Na tena sisi wenyewe huwa tunakuja kusaga kunguni kwamba afisa manunuzi alileta kampuni za ndugu zake!
Acha kutia watu hofu,Nia njema lazima ionekane hata kama itachelewa
 
Mkuu mpya wa Mkoa wa Shinyanga Bi Sophia Edward Mjema amefanya maamuzi magumu ya kumsimamisha kazi afisa manunuzi mzembe wa Wilaya ya Kishapu Ili kupisha Ujenzi wa madarasa kwa dharula kama ilivyoelekezwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Mkuu huyo wa Mkoa amemshangaa afisa huyo mzembe kwa kuendeleza urasimu kwenye fedha za Rais Samia zinazotaka madarasa yajengwe kila sehemu yanapohitajika kwa dharula ili ifikapo trh 06|01|2022 wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza waanze mwaka wa masomo maramoja kwa pamoja.

Mtakumbuka Rais Samia alitoa Jumla ya madarasa elfu 15 kwa shule za Sekondari na madarasa elfu 3 kwa Shule shikizi za msingi huku akitoa Jumla ya madawati 462,795 sawa na Wastani wa madawati 120 na madarasa 4 katika Kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima yaani mjini na vijijini.

Mkoa wa Shinyanga ulitengewa na kupatiwa Jumla ya TZS 11BL ambazo leo kwa mujibu wa RC watu wazembe wanaziangalia tu kwenye akaunti kama mapambo badala ya kuchangamkia Ujenzi ili ifikapo trh 06|01|2022 ahadi ya Rais Samia kwamba kwenye mwaka wake watoto wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha Kwanza wataanza shule tarehe moja nchi nzima yaani trh 06|01|2022 saa moja kamili asubuhi.

Wakati huohuo Rais Samia Suluhu Hassan tayari ameshapeleka kwenye halmashauri zote 184 nchini Jumla ya TZS 62.4BL kwaajili ya elimu bure, Hivyo watoto hawa anaowapambania leo Bi Sophia Mjema tayari ada yao ilishalipwa,Wazazi|walezi wao watanunua uniform pamoja na madaftari tu,Huyu ndio Samia Suluhu Hassan Rais wa awamu ya Sita na hizi ndio kazi zake.

Hongera Rais Samia mimi nichadema ila nakukubali Sana
 
Mkuu mpya wa Mkoa wa Shinyanga Bi Sophia Edward Mjema amefanya maamuzi magumu ya kumsimamisha kazi afisa manunuzi mzembe wa Wilaya ya Kishapu Ili kupisha Ujenzi wa madarasa kwa dharula kama ilivyoelekezwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Mkuu huyo wa Mkoa amemshangaa afisa huyo mzembe kwa kuendeleza urasimu kwenye fedha za Rais Samia zinazotaka madarasa yajengwe kila sehemu yanapohitajika kwa dharula ili ifikapo trh 06|01|2022 wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza waanze mwaka wa masomo maramoja kwa pamoja.

Mtakumbuka Rais Samia alitoa Jumla ya madarasa elfu 15 kwa shule za Sekondari na madarasa elfu 3 kwa Shule shikizi za msingi huku akitoa Jumla ya madawati 462,795 sawa na Wastani wa madawati 120 na madarasa 4 katika Kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima yaani mjini na vijijini.

Mkoa wa Shinyanga ulitengewa na kupatiwa Jumla ya TZS 11BL ambazo leo kwa mujibu wa RC watu wazembe wanaziangalia tu kwenye akaunti kama mapambo badala ya kuchangamkia Ujenzi ili ifikapo trh 06|01|2022 ahadi ya Rais Samia kwamba kwenye mwaka wake watoto wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha Kwanza wataanza shule tarehe moja nchi nzima yaani trh 06|01|2022 saa moja kamili asubuhi.

Wakati huohuo Rais Samia Suluhu Hassan tayari ameshapeleka kwenye halmashauri zote 184 nchini Jumla ya TZS 62.4BL kwaajili ya elimu bure, Hivyo watoto hawa anaowapambania leo Bi Sophia Mjema tayari ada yao ilishalipwa,Wazazi|walezi wao watanunua uniform pamoja na madaftari tu,Huyu ndio Samia Suluhu Hassan Rais wa awamu ya Sita na hizi ndio kazi zake.

Safi Sana
 
Mimi vyangu genuine vipo chini ya mchago kitambo ila kwa kauli ya Rc Shy kwakweli kaonyesha kupwaya Sana even if wanatumia force ac/ single source lakini PPA zifuatwe ninaongea by experience ni hili
Hizo regulation lazima ziakisi malengo ya mradi,
 
Hizo fedha siyo za rais Samia !

Hizo fedha ni za watanzania rais hana fedha hapa nchini.

Fedha zake ni zile za mshahara wake muache kupotosha watu kwa makusudi.

Kama zimekopwa basi zitalipwa kwa kodi za watanzania na kama zimetolewa kama zawadi basi zimetolewa kwa jina la JMT.

Rais ni taasisi na ndiye anayeunda serikali; amechaguliwa na wananchi anaongea na kutenda kwa niaba ya wananchi kwa hiyo tukisema Rais Samia ametoa fedha ni sahihi tu kwa kuwa hatuzungumzi Rais kama mtu binafsi bali ni taasisi.
 
Rais ni taasisi na ndiye anayeunda serikali; amechaguliwa na wananchi anaongea na kutenda kwa niaba ya wananchi kwa hiyo tukisema Rais Samia ametoa fedha ni sahihi tu kwa kuwa hatuzungumzi Rais kama mtu binafsi bali ni taasisi.
Hana fedha za kugawa kwa wananchi msilazumishe kufurahisha nafsi zenu.
 
Back
Top Bottom