Binadamu: Kiumbe chenye chanzo kisichojulikana, yupoyupo tu hana mwanzo wala mwisho

Binadamu: Kiumbe chenye chanzo kisichojulikana, yupoyupo tu hana mwanzo wala mwisho

Absolutely yes.

Binafsi naamini kwamba Binadamu hana mwanzo wala mwisho, Yupo tu.

Ukianza kuweka ulazima wa kwamba kila kitu kilichopo lazima kiwe na chanzo, Basi hata
"chanzo cha vyanzo" lazima kiwe na chanzo chake,

Ili muundo ule ule wa ulazima huo ufuatwe. Pasiwepo kitu chochote kitakacho kwenda kinyume na ulazima huu kwa kujitokeza chenyewe tu pasipo mwanzo,

Maana kitavuruga muundo mzima wa ulazima huu na kuzua maswali mengi ya kimewezaje kuwepo bila chanzo.
Kwani unajua chanzo cha punda na kusudi la kuwepo?
 
Sifahamu chochote kuhusu chanzo chake.

Kama una kifahamu tueleze.

Si lazima binadamu wa kwanza awe na chanzo.
Umeanza kwa kusema haufahamu chochote kuhusu chanzo cha binadamu, mwishoni umemaliza kwa kusema....

"sio lazima kuwe na chanzo" Hapa naona unachanganya mambo mno,
Hii inanipa picha kuwa najadili na mtu mwenye upeo wa kifikra wa namna gani


Lakini pia umesema kama nafahamu nkueleze, Lakini nkikueleza pia unapinga...Kwanini upinge kitu ambacho umekiri wazi kuwa haufahamu ?

Kwanini usifanye tafiti kuhusu ambayo huwa tunakwambia ? Lakini unapinga papo kwa hapo kuonyesha kuwa hauwezi kuwa na mtazamo tofauti na ulionao

Nasema hivi kwasababu tumekutana kwenye uzi mwingine huko.
 
Na chanzo cha jua ni kipi?

Jua hilo, lilitokea tu from nothing?
Sasa hapo jua ndilo lenye majibu sahihi.

Mimi naamini hii dunia ni kipande kilichopasuka kutoka juani. Kikaenda masafa marefu ambako kilibahatika kupoa kwakua kilikua mbali na jua ambalo lina moto wa hatari.

Baada ya kupoa, wale bakteria ambao wanaishi ndani ya hicho kipande, wakaanza kuchomoza kwakua hakuna joto la kuwaunguza. Hapa maana yangu ni, mazingira ambapo dunia ilienda kutulia yanaruhusu uwepo wa bakteria ambao sisi tunaita viumbe hai hawa ambao wanaonekana.

Nasema hivi kwakua nipo huku mashambani. Sehemu zilizochomwa moto hata pasipowekwa mbegu ya aina yoyote, pakimwagiliwa maji, panaota majani/mimea.

Hili linatosha kunithibitishia kuwa dunia ni kipande cha jua kilichopoa na bakteria ambao ni sisi viumbe hai, tukachomoza na kuendelea na maisha kwakua hakuna kikwazo cha kutuangamiza tukapotea.

Huu ni mtizamo wangu
 
Mwanza ipo tayari kwenye uhalisia.

Huwezi kuota kitu ambacho Hakipo kwa namna yoyote ile ya kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika.

Vitu vyote vinavyo otwa kwenye ndoto angalau vipo kwa kuonekana, kushikika, kusikika au kuhisika.

Huwezi kuota nje ya hapo.

Taarifa zote zilizomo kwenye ubongo ambazo unaweza kuziota ndotoni, Ni zile tu ambazo Angalau umeshawahi kuziona, kuzisoma, kuzishika, kuzisikia mahali fulani, na kuhadithiwa.

Huwezi kuota kitu kisicho kuwepo (Nothing) lazima uote "something" ambacho kwa namna fulani ubongo wako una taarifa nacho.
Kwa hiyo kumbe ndoto ni michezo ya ubongo tu[emoji1][emoji1][emoji1]basi ubongo una ujinga mwingi sana
 
Umeanza kwa kusema haufahamu chochote kuhusu chanzo cha binadamu, mwishoni umemaliza kwa kusema....

"sio lazima kuwe na chanzo" Hapa naona unachanganya mambo mno,
Hii inanipa picha kuwa najadili na mtu mwenye upeo wa kifikra wa namna gani


Lakini pia umesema kama nafahamu nkueleze, Lakini nkikueleza pia unapinga...Kwanini upinge kitu ambacho umekiri wazi kuwa haufahamu ?

Kwanini usifanye tafiti kuhusu ambayo huwa tunakwambia ? Lakini unapinga papo kwa hapo kuonyesha kuwa hauwezi kuwa na mtazamo tofauti na ulionao

Nasema hivi kwasababu tumekutana kwenye uzi mwingine huko.
Mkuu kutokufahamu jibu la jambo fulani hakukufanyi uamini tu chochote unachoambiwa bila uthibitisho, hivi unafahamu kwamba si lazima mtu ajue jibu la 1÷0 ili ajue kwamba jibu haliwezi kuwa 1, yeye akisema ni Undefined maana yake hakuna jibu hivyo hahitaji kuthibitisha chochote ila wewe ukisema jibu ni 1 basi utatakiwa ulete uthibitisho wa hilo jibu

Au vile vile pia haihitaji mtu amjue rais wa marekani ili ajue kwamba rais wa marekani hawezi kuwa John Magufuli, sasa huwezi kusema eti kwa sababu humjui rais wa marekani basi uwaamini hata wanaokuambia kuwa ni John Magufuli, wakati hakuna uthibitisho na unaona kabisa ni kitu ambacho hakiwezekani

So vivyo hivyo haihitaji mtu kujua chanzo halisi au sahihi cha Ulimwengu ili ajue kwamba chanzo chake siyo Mungu, sasa huwezi kusema eti kwa vile hujui chanzo cha Ulimwengu basi wanaosema kuwa chanzo chake ni Mungu ndio wako sahihi wakati nao hawajathibitisha, by the way mimi naamini Mungu yupo ila nilikuwa namsaidia tu Jamaa kujibu
 
Umeanza kwa kusema haufahamu chochote kuhusu chanzo cha binadamu, mwishoni umemaliza kwa kusema....

"sio lazima kuwe na chanzo" Hapa naona unachanganya mambo mno,
Hii inanipa picha kuwa najadili na mtu mwenye upeo wa kifikra wa namna gani


Lakini pia umesema kama nafahamu nkueleze, Lakini nkikueleza pia unapinga...Kwanini upinge kitu ambacho umekiri wazi kuwa haufahamu ?
Napinga, Kwa vile Mnashindwa kuthibitisha uwepo wa hicho chanzo.

Mnaishia kusema tu kipo, Na mnafahamu kipo ila kukithibitisha Hamuwezi.

Sifahamu chanzo cha dunia, ila mnapo anza kusema kitu fulani ndicho chanzo Halafu ninyi wenyewe Hamuwezi kukithibitisha hata na ninyi hamfahamu vilevile.

Mnacho jaribu kufanya ni kuhalalisha mawazo yenu yaonekane yana ukweli bila uthibitisho.


Kwanini usifanye tafiti kuhusu ambayo huwa tunakwambia ? Lakini unapinga papo kwa hapo kuonyesha kuwa hauwezi kuwa na mtazamo tofauti na ulionao
Nimefanya tafiti na kubaini hakuna chanzo chochote kile cha ulimwengu na Binadamu.
Nasema hivi kwasababu tumekutana kwenye uzi mwingine huko.
 
Naona tumo kwenye njia yenye tanuri la fikra pofu na kutoka humo ni Lazima watu wakubali kujitoa kwenye ugoto wa fahamu zao Kwa kuukubali ukweli wenye kweli ndani yake?
 
Nimefanya tafiti na kubaini hakuna chanzo chochote kile cha ulimwengu na Binadamu.
Kwanza kumbuka kuwa hoja hapa tunazungumzia binadamu na siyo kitu kingine chochote.

Hebu elezea huo utafiti uliufanya kwa kutumia mbinu zipi za kiutafiti??
 
Mkuu kutokufahamu jibu la jambo fulani hakukufanyi uamini tu chochote unachoambiwa bila uthibitisho, hivi unafahamu kwamba si lazima mtu ajue jibu la 1÷0 ili ajue kwamba jibu haliwezi kuwa 1, yeye akisema ni Undefined maana yake hakuna jibu hivyo hahitaji kuthibitisha chochote ila wewe ukisema jibu ni 1 basi utatakiwa ulete uthibitisho wa hilo jibu

Au vile vile pia haihitaji mtu amjue rais wa marekani ili ajue kwamba rais wa marekani hawezi kuwa John Magufuli, sasa huwezi kusema eti kwa sababu humjui rais wa marekani basi uwaamini hata wanaokuambia kuwa ni John Magufuli, wakati hakuna uthibitisho na unaona kabisa ni kitu ambacho hakiwezekani

So vivyo hivyo haihitaji mtu kujua chanzo halisi au sahihi cha Ulimwengu ili ajue kwamba chanzo chake siyo Mungu, sasa huwezi kusema eti kwa vile hujui chanzo cha Ulimwengu basi wanaosema kuwa chanzo chake ni Mungu ndio wako sahihi wakati nao hawajathibitisha, by the way mimi naamini Mungu yupo ila nilikuwa namsaidia tu Jamaa kujibu
Kwahiyo nkikupa njia za kufuata ili upate uthibitisho upo tayari ?
 
Nikiangalia maumbile ya binadamu na jinsi anavyoishi kwenye hii dunia, najiuliza imekuwaje amekuwa alivyo na jinsi hakuna kiumbe kingine kinachofanana na Binadamu kiutendaji wake.

Ukiangalia Kwa mfano, hivi kweli hakuna mbunifu wa binadamu ambaye ndiye aliyebuni uke ukae kwa mfumo ambao unaweza kuingiliwa na uume.

Hakuna mbunifu aliyebuni mji wa uzazi Kwa mwanamke na kuweka mbegu Kwa mwanaume? Kisha ukifanyika uingilianaji mimba inatungwa.

Baada ya binadamu kuzaliwa ukiangalia kwa makini unaanza kujiuliza, hakuna kweli mbunifu aliyejua kuwa binadamu Ili aishi atahitaji kula hivyo akamuumba akiwa na mdomo?

Mfumo wa kula mpaka kupata haja hakuna mbunifu wake kweli? Yaani mfumo wa mmeng'enyo wa chakula upo tu Wala haukukusudiwa kuwepo ila upo tu. Kweli?

Fikiria macho, masikio, ngozi, na viungo vingine vya binadamu vinavyofanya kazi. Waza kuwa hapa unaposoma hii mada macho, masikio yako yaache kufanya kazi itakuwaje?

Bado nawaza imekuwaje binadamu hana Mwanzo Wala mwisho??
Uliyotaja kwa nyani pia yapo mkuu
 
Naona tumo kwenye njia yenye tanuri la fikra pofu na kutoka humo ni Lazima watu wakubali kujitoa kwenye ugoto wa fahamu zao Kwa kuukubali ukweli wenye kweli ndani yake?

Mkuu unge uweka huo ukweli hapa
 
Back
Top Bottom