Binadamu: Kiumbe chenye chanzo kisichojulikana, yupoyupo tu hana mwanzo wala mwisho

Binadamu: Kiumbe chenye chanzo kisichojulikana, yupoyupo tu hana mwanzo wala mwisho

Kwahiyo nkikupa njia za kufuata ili upate uthibitisho upo tayari ?
Yaani wao wamejenga ukuta wasihojiwe kuhusu dhana na nadharia zao, lakini kila wakati wanataka uthibitisho toka kwenye nadharia na dhana wasizoziamini.
 
Nilivoiangalia hii ni KANUNI. Kama ni kanuni ni Lazima iwe na misingi yake.

ULAZIMA kuwa Kila chenye Mwanzo ni Lazima kiwe kina chanzo chake na hicho chanzo kinatakiwa kiwe na chanzo kingine na hali iendele hivyo unatokana na nini?

Hebu elezea kwa kina msingi Wa kanuni hii na uweke ithibati yake.
Unaambiwa hata aliyeipendekeza hajulikani.. yani ni uchawi-uchawi mtupu
 
Hili ndilo tatizo la mijadala ya humu JF. Kuna watu wanatakatifusha Kanuni zao bila ya sababu!!

“Kila kitu lazima kina chanzo chake”

In ver simple logic ina maana sentensi hii itatengeneza series ya infinity.... yaani kila kilichopo kimeundwa na aliyeunda kaundwa na yeye kaundwa pia.... infinity
Sentensi yenyewe ni KANUNI tayari

Labda sasa mtuambie maana ya hiyo sentensi

Unapaswa kujua kwamba kiini cha mgogoro wa “infinity” kilianzia hapa.
Ni tabia ya kibinadamu kutaka kujua kila kitu kwa kujiuliza maswali...... it called intelligence

Kitambo sana kabla yetu watu walianza kujiuliza haya mswali ya nani kaumba binadamu na mpangilio huu, nani kaumba dunia na mpangilio huu, nani kaumba ulimwengu na mpangilio huu nk nk?...... yaani inaonekana haiwezekani vikajipangilia vyenyewe tu kwa mpangilio huu wa ufanisi na complexity ya hali ya juu kabisa(hapa kanuni ikaanza kuibuka kwamba “LAZIMA” kuna aliyeumba na HAIWEZEKANI vikajiumba)

Jawabu likawa ni Mungu maana fikra(kanuni) zilikua zinakataa kwamba hayupo ambaye kaumba vyote

Lakini baada ya dhana ya Mungu muumba wa vyote kuibuka lakini bado binadamu akaanza kupata maswali mapya...... sasa na huyu Mungu mwenye uwezo mkubwa namna hii katokea wapi? Nani kamuumba na yeye?(muendelezo wa kanuni)

Ukiangalia hiyo series ya maswali inajengwa na kanuni ya swali la kwanza ambalo lilitokana na kwamba “haiwezekani” huu ulimwengu ukawa ulitokea tu “LAZIMA” kuna aliyeutengeneza
Alipopatikana aliyeutengeneza kanuni ikamuhusu na yeye pia...... kwamba “haiwezekani” huyu mungu akawa ametokea tu from no where kama ilivyokuwa haiwezekani ulimwengu ukatokea from no where

Ukweli ni kwamba BINADAMU HAJUI KILA KITU na hana majibu ya maswali yoko

Binadamu anachofanya kwa mambo asiyo yajua huwa anatengeneza theories mbali mbali kama big bang theory
Au anamtengeneza “mungu” ili kupata majibu rahisi kwa mswali yaliomshinda

KILA KITU LAZIMA KINA CHANZO ni KANUNI na ndio maana hata wewe unauliza kwanini watu tuamini eti binadamu hajulikani alipotokea wala hajulikani aliyempangilia?
Ni kanuni ya ndio ina kusukuma kutokubaliana na wanaotuaminisha binadamu hajulikani alipotoka
 
Kanuni hii ni ya kwangu binafsi, Si kwamba ni kanuni ya watu wote.

Kanuni hii ni kutokana na kwamba watu wanaodai Mungu ni chanzo cha ulimwengu hawana UTHIBITISHO wa madai yao.
(Ni mawazo yao ya kufikirika tu)

Watu wengi wana amini Mungu Hana chanzo kwamba alitokea tu, Pia wana amini Mungu huyohuyo hana mwisho.

Watu wengi wameweza kuamini Mungu wasiyemjua Hana chanzo Lakini wana lazimisha kwamba Dunia ina chanzo, Na chanzo hicho wanadai ni "Mungu" Kwamba wana amini Haiwezekani Dunia iwe imetokea tu yenyewe Pasipo chanzo.

Sasa ni hivi[emoji116]

Kama "Haiwezekani" Dunia isiwe na muumbaji, kwamba lazima awepo aliye iumba "Imewezekana" vipi Mungu asiwe na Muumbaji?

Kama Mungu hana mwanzo, Inashindikana vipi kwa Dunia kutokuwa na mwanzo?

Huu ulazima wa kwamba Dunia lazima iwe na chanzo, ila Mungu yeye Hana chanzo uliwekwa na nani?

Hapa sasa ndipo,Kanuni hii inapo tumika kwamba,

Kama ni lazima kila kitu kilichopo kiwe na chanzo, Basi hata Mungu lazima awe na chanzo. Maana Mungu huyo bado "HAJATHIBITIKA" rasmi kwamba yeye ndio chanzo halisi cha ulimwengu.
( Bado ni mawazo na mafikirio ya watu tu)

Sasa kama bado Mungu HAJATHIBITIKA kuwa chanzo halisi cha Dunia, Hakuna ulazima wa kwamba Dunia imeumbwa na ina mwanzo.

Ila mtu akianza kuweka ulazima wa kwamba Dunia lazima iwe imeumbwa, Lazima athibitishe kwamba chanzo cha Dunia hakina mwanzo.

Na aeleze na kuthibitisha chanzo hicho cha Dunia, kimewezaje kuwepo bila chanzo kingine.
Wewe ni kiumbe mwenye uwezo wa kibinadamu usilazimishe kufahamu yasiyo uwezo wako utachanganikiwa memory yako na ramu gb 4 unataka kichwa Chalo kihifadhi vitu vya gb 1000 hiko ni kichekesho
 
Wewe ni kiumbe mwenye uwezo wa kibinadamu usilazimishe kufahamu yasiyo uwezo wako utachanganikiwa memory yako na ramu gb 4 unataka kichwa Chalo kihifadhi vitu vya gb 1000 hiko ni kichekesho
Unajuaje kwamba kuna uwezo mwingine tofauti na huu wa kibinadamu?

Uthibitishe huo "uwezo mwingine" ulio zaidi na uwezo wa mwanadamu.
 
Nikiangalia maumbile ya binadamu na jinsi anavyoishi kwenye hii dunia, najiuliza imekuwaje amekuwa alivyo na jinsi hakuna kiumbe kingine kinachofanana na Binadamu kiutendaji wake.

Ukiangalia Kwa mfano, hivi kweli hakuna mbunifu wa binadamu ambaye ndiye aliyebuni uke ukae kwa mfumo ambao unaweza kuingiliwa na uume.

Hakuna mbunifu aliyebuni mji wa uzazi Kwa mwanamke na kuweka mbegu Kwa mwanaume? Kisha ukifanyika uingilianaji mimba inatungwa.

Baada ya binadamu kuzaliwa ukiangalia kwa makini unaanza kujiuliza, hakuna kweli mbunifu aliyejua kuwa binadamu Ili aishi atahitaji kula hivyo akamuumba akiwa na mdomo?

Mfumo wa kula mpaka kupata haja hakuna mbunifu wake kweli? Yaani mfumo wa mmeng'enyo wa chakula upo tu Wala haukukusudiwa kuwepo ila upo tu. Kweli?

Fikiria macho, masikio, ngozi, na viungo vingine vya binadamu vinavyofanya kazi. Waza kuwa hapa unaposoma hii mada macho, masikio yako yaache kufanya kazi itakuwaje?

Bado nawaza imekuwaje binadamu hana Mwanzo Wala mwisho??
Mwanadamu ni mnyama sawa tu na wanyama wengine. Tena ukimlinganisha na miamba mingine iliyoko huko porini kimaumbile ni kiumbe dhaifu sana! Hebu fikiria umpambanishe Homo Sapiens kimaumbile na dubu au mfalme wa pori mwenyewe!

Kitu pekee kina/lichomfanya binadamu awe kileleni katika msimbo wa kimaumbile na chakula ni ubongo wake mkubwa. Ubongo ndiyo umemuwezesha kuunda silaha mbalimbali ambazo zimemuwezesha siyo tu kuwatawala wanyama wengine bali hata kufikia hatua ya kutaka kujiangamiza mwenyewe na kujifuta kutoka katika uso wa dunia akitaka.

Wanaanthrolopolojia ya kimaumbile wana uthibitisho kwamba ubongo wa binadamu ulianza kukua kwa ghafla mara tu alipogundua moto na kuanza kula nyama zilizopikwa na kuchomwa. Chakula hiki muhimu kilimpatia protini ya kutosha ambayo ilifanya ukuaji wa ubongo uwezekane, jambo ambalo pengine lisingetokea kama angeendelea kula majani na nyama mbichi. Ndiyo maana kuna wanaoamini kuwa ugunduzi wa moto pengine ndiyo ugunduzi wa muhimu zaidi kuwahi kufanywa na binadamu kwa sababu ndiyo hasa ulimuwezesha kuianza safari ya kutoka huko kwenye "unyani" na kuingia kwenye "u Homo Sapiens".

Unaongelea sijui mdomo na mmeng'enyo wa chakula kaka vile hizo ndiyo sifa pambanuzi zinazomtofautisha binadamu na viumbe wengine.

Hoja yako, ili iwe na mashiko, ni lazima ijikite katika sifa bainifu zinazomtenga binadamu na wanyama wengine. Na sifa mojawapo kuu ni ukubwa wa ubongo wake (akili) uliompa mpaka lugha tata inayomuwezesha mpaka kufikiri kidhahnia; na hata kuunda lugha maalum ili kuhuisha fikra zake dhahnia (mf. Hisabati) ili kuweza kuuelewa na kuufafanua Ulimwengu (The Universe) uliomzunguka.

Bila uwezo huu wa kutumia akili binadamu si lo lote, si cho chote hata mbele ya siafu au manyigu tu...na kama alivyoonya sana Steve Hawking kabla hajafa, si ajabu katika miaka 100 ijayo akili hizi hizi zilizompa binadamu utawala wa kimaumbile hapa duniani ndiyo hizo hizo zitaweza kumfanya ajiangamize mwenyewe. Steve Hawking amekufa huku akisisitiza sana kuwa juhudi za haraka na kidharula zifanyike ili kuhakikisha kuwa mwanadamu anatafuta mahali pengine pa kukimbilia kama anayo hamu ya kuendelea kuishi. Ndiyo maana leo hii unaona kuna mvuvumko mpya wa kwenda mwezini japo lengo hasa ni kuanzisha makazi ya kudumu katika sayari ya Mars.

E = MC² (Adui mmojawapo wa binadamu; na kama kuna siku itatokea akajiangamiza, si ajabu kifomyula hiki cha Albert Einstein kitakuja kulaumiwa sana 😭) 🚶🏿‍♂️🚶🏿‍♂️
 
Shimba ya Buyenze umetoa maelezo mazuri sana Lakini hujajibu swali la Msingi. Nini chanzo cha binadamu?

Watu kama kina Infropreneur Wanasema hata nadharia za wanasayansi kuhusu uasili na chanzo cha uwepo wa binadamu hazina majibu ni nini hasa chanzo cha binadamu.

Kwa ivo leo hii nyani wakianza kula nyama nao pia ubongo wao utakua na kuanza kuwa kama binadamu??
 
Unasema vipi hakuna mwisho ?

Mwisho wako wewe na kiumbe chochote hai ni kwamba utakufa, what is alive must die.... Kuhusu mwanzo viumbe vyote hai mbona kuna plausible theories zinazosema ulipotokea..., kama unaweza kuamini kina plasmodium au species fulani hapo zamani zilikuwa hazipo na sasa hivi zipo au nyingine kupotea unashindwa kuamini vipi chanzo cha hivyo vingine ni sawa na chanzo cha hivi vingine..... (What's so special about homo-sapiens) ?

Take time na fuatilia kiumbe ambacho kinachokua masaa kupass generations kadhaa jambo ambalo linachukua miaka kwa binadamu alafu utagundua maybe its not magical at all....
 
Shimba ya Buyenze umetoa maelezo mazuri sana Lakini hujajibu swali la Msingi. Nini chanzo cha binadamu?

Watu kama kina Infropreneur Wanasema hata nadharia za wanasayansi kuhusu uasili na chanzo cha uwepo wa binadamu hazina majibu ni nini hasa chanzo cha binadamu.

Kwa ivo leo hii nyani wakianza kula nyama nao pia ubongo wao utakua na kuanza kuwa kama binadamu??
Kama umenisoma vizuri, ninachopinga ni wewe kumuona binadamu kuwa ni kiumbe wa pekee sana tofauti na wanyama wengine. Ndicho nilichokuwa najaribu kufafanua kwa kuelezea sifa mojawapo kuu inayompambanua na viumbe wengine.

Na hapa bado unanirudisha kule kule kwa kuuliza nini chanzo cha binadamu. Kwa nini isiwe nini chanzo cha bakteria, ngamia au mbu na iwe binadamu? Binadamu ana upekee gani kwako mpaka umtafutie chanzo cha peke yake tofauti na tembo, kwa mfano? Lazima kuna kitu na jibu unalolitafuta. Weka sababu zako wazi.

Hilo la uhusiano kati ya ugunduzi wa moto na ukuaji wa ubongo wa binadamu limefanyiwa utafiti na hao Wanaanthropolojia ya kimaumbile. Na wamechapisha tafiti zao. Pengine walidanganya sina uhakika. Njia nzuri ya kuhakikisha kama utafiti wao ni wa kweli pengine ingekuwa, kama unavyodokeza hapa, kuwapa nyani protini kwa wingi na kuona kama kutakuwa na madiliko katika ubongo wao. Tatizo ni kwamba, you guessed it, utaambiwa kuwa matokeo haya ni ya pole pole (evolutionary) na yanachukua maelfu ya miaka...kama tu tunavyoaminishwa katika nadharia ya Evolution.
 
Ukiangalia maisha ya kenge na kuku unaweza kuuliza hili swali kweli???
Swali lake ni valid sana kwa sababu wote ni viumbe na kama unaamini katika sayansi, wote wametokana na kitu kile kile; na wamekuja kutofautiana huku mbele ya safari. Kama unauliza chanzo cha binadamu, basi ni valid pia ujiulize kenge na kuku wametoka wapi maana chanzo cha uhai ni kimoja kulingana na wanasayansi japo ni wazi hawana uhakika.

Kwa nini binadamu kwako ni so special? Ni kwa vile aliumbwa na Mungu? Tapo lako la kifikra katika mjadala huu ni lipi ili tujikite huko?
 
Shimba ya Buyenze umejibu vema. Lakini kwenye kujenga hoja huwezi kuweka Kila kitu.

Kwa mfano unataka kujadili ni kwanini watu wanakunywa Pombe aina ya gongo, haiwezekani ukauliza ni kwa nini watu wanakunywa Pombe. Swali kama hili litafanya uwanda uwe mpana sana.
 
Back
Top Bottom