Binti wa miaka 17 ajinyonga baada ya kuachika mara tatu kwenye ndoa

Binti wa miaka 17 ajinyonga baada ya kuachika mara tatu kwenye ndoa

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amesema Rebecca Benjamini Mkazi wa Kata ya Izunya Wilaya ya Nyang'hwale mwenye umri wa miaka 17 amefariki dunia kwa kujinyonga kutokana na msongo wa mawazo baada ya kuwa anaachwa kila anapoolewa "Ameachika mara tatu kwenye ndoa"

Mwaibambe amesema hayo alipokutana na Kamati ya Amani na Maadili ya Mkoa wa Geita, ambapo amesema chanzo cha kifo cha Rebecca ni msongo wa mawazo ambao ulikuwa ukisababishwa na yeye kuolewa na kuachika mara kwa mara.

"Rebecca amefariki dunia baada ya kujinyonga hadi kupoteza maisha kwa kutumia kamba iliyosukwa kwa chandarua kwenye kenchi ya nyumba yake, chanzo alikuwa akilalamika kwamba kwanini kila akiolewa anaachika na tayari alikuwa ameshaachika mara tatu"

Baadhi ya Viongozi wa Dini aliokutana nao leo kutoka katika Madhehebu mbalimbali ili kutokomeza matukio ya Watu kuua na kujiua, wamesema Wananchi wanatakiwa kuwa na hofu ya Mungu.

Millard
Miaka 17 ndoa 3? Huyu kuna roho mbaya ilikuwa inamuwinda kupitia mapenzi na imefanikiwa.
 
Uko sahihi kabisa Dada
Wazazi tujifundishe kuwakaribisha watoto wetu nyumbani baada ya divorce.

A divorced daughter is better than a dead daughter.

Jamii zetu za kiafrika zina shida sana mwanamke anapoachika sasa mabinti wanaweza kujikuta wanaingia kwenye ndoa ilmradi tu waonekane wameolewa.
Nashkuru nimepata mzazi (baba tofauti kidogo)ananiambiaga hivi ndoa ni mapenzj na huruma kama hakuna usiruhusu kunyanyasika sikukusomesha uwe mjinga na kukubali kua mtumwa be responsible woman but not stupid!
 
Kuna kitu hakipo sawa kwenye jamii ambacho ndio kimepelekea maamuzi ya kujitoa uhai.

Miaka 17 mtu kuwa ameolewa mara tatu nalo ni jambo linafikirisha sana, kuwa ndoa zinyewe zinadumu kwa muda gani? Ni ndoa zinazotambulika kimila/kidini/kiserikali? Changamoto ya ndoa hizo kuvunjika ni ipi?

Ni mambo jamii yote kwa ujumla inapaswa kukaa chini na kuyatafakari vinginevyo tutakuwa tunapambana na matokeo kila siku badala ya kutatua mzizi wa shida yenyewe.
Wasukuma wanaolewa na miaka 12 mbona
 
Kuna mama kaolewa mara 5 zote kaachika sasa anataka ndoa ya sita sasa mtu mara zote hizo si bora utulie ufanye mambo yako, kuna watu hawawezi kabisa kuishi wenyewe inasikitisha
 
please say u r joking
Wala sitanii ni ukweli kabisa! Nina uzoefu nishafundisha usukumani kule mtoto wa kike akiwa mweupe kusoma atakusikia kwenye bomba tu, nishawahi ishi na watoto wawili wa kike Shinyanga hukoo walitelekezwa na wazazi wao kwa kuwa wamefaulu std 7 na waliambiwa wasifaulu std 7 wakafaulu hivyo wazazi wakasusa kusomesha maana walikuwa washakula mahari za ng'ombe tayari..nawakumbuka mpk majina!

Kinachosaidia sasa hivi ni hii kuwa mtoto akifaulu lazima aende shule la sivyo mzazi unashtakiwa ila mwanzo hali ilikua mbaya mnooo!!
 
Miaka 17 ameolewa mara tatu huku akiachika mara tatu, tuseme alianza kuolewa na miaka mingapi,

Sema kijijini inaleta maswali huku mjini ni sawa tu
 
Wasukuma wanaolewa wakiwa na miaka 12 wengine hata period inakuwa bado, anapata akiwa ndoani.
 
Wazazi tujifundishe kuwakaribisha watoto wetu nyumbani baada ya divorce.

A divorced daughter is better than a dead daughter.

Jamii zetu za kiafrika zina shida sana mwanamke anapoachika sasa mabinti wanaweza kujikuta wanaingia kwenye ndoa ilmradi tu waonekane wameolewa.
Sasa katika tukio hili jamii imehusikaje?! Yaani mtu awe depressed kwasababu zake binafsi lawama tupewe wanajamii?!

Hebu mtupumzishe muda mwingine wanajamii tunalaumiwa hata na vitu visivyotuhusu. Miaka kumi na saba sio umri wa kulaumiwa kwa kukosa ndoa baada ya kutalikiwa.
 
Sasa katika tukio hili jamii imehusikaje?! Yaani mtu awe depressed kwasababu zake binafsi lawama tupewe wanajamii?!

Hebu mtupumzishe muda mwingine wanajamii tunalaumiwa hata na vitu visivyotuhusu. Miaka kumi na saba sio umri wa kulaumiwa kwa kukosa ndoa baada ya kutalikiwa.
Bila shaka umeamka na marue rue ukakimbilia kujibu bila kutafakari.

Mnaambiwa muamke kwanza japo mpige mswaki akili zikae sawa mnabana pua, bando letu wenyewe.
 
Ukoa sahihi kabisa DadaNashkuru nimepata mzazi (baba tofauti kidogo)ananiambiaga hivi ndoa ni mapenzj na huruma kama hakuna usiruhusu kunyanyasika sikukusomesha uwe mjinga na kukubali kua mtumwa be responsible woman but not stupid!
Usione anakusaidia hapo anakuandaa kuwa kiburi kwenye ndoa mwisho wake utaishia kuwa single mama, ndoa ni utumwa huru.
 
Back
Top Bottom