Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Acheni ujinga watanzania wengi mnakawaida ya kutopenda vya kwenu inawezekana kweli kuna mapungufu kwenye bongo movie lakini si kwa ukubwa uo mnaoongela hapa,,,,,
Mtoa mada unaponda bongo movie alfu unakuja kusifia movie ya kihindi wewe ndo Bogaz kabisa wahindi wale mtu anapigwa ngumi anarushwa mita50 had anabomoa ukuta ule ndo uhalisia,,,[emoji15]

Mkuu umeongea yote!

Kuna kipindi ilikuwa ukisema mi sisikilizagi bongo fleva nasikiliza mziki wa nje unaonekana mjanja sana. Sasa hiyo hali ndo inatokea kwa bongo movie sa hiii.

Yaani ili uonekane modern ni lazima useme "siangaliagi bongo movie".

Siangalii bongo movie alafu hapo hapo anatoa makosa kibao yaliyotokea kwenye filamu. Sasa unajiuliza kama haangaalii amejuaje hayo makosa.

Tuna safari ndefu sana.
 
Soko lenu mnaangalia wapi, mbona watu wa comedy kama mizengwe wanafanya vizuri, tatizo lenu mkiona mwanamke ana mvuto mnalazimisha aigize hata kama hana uwezo.
Chuo cha sanaa bagamoyo kuna watu waliofundishwa sanaa ya uigizaji vizuri ila mnawaacha mnakimbilia vilaza matokeo yake filamu zinakosa uhalisia

Comedy inafanya vipi vizuri? Kwa mwaka 2020 nitajie filamu tano za comedy zilizouza sana Tanzania?

Yaaani mizengwe unaweza kufananisha na Huba au Shilingi ya dstv

Ringo na Pembe wameingiza how much kutokana na filamu walizotoa mwaka jana?
Filamu gani ya comedy kutokea Tanzania kwa sababu ya ubora wake imeingia NETFLIX, HULU, DISNEY + au any major streaming platform.

Na unamaanisha nini watu wa comedy wanafanya vizuri? Au kwa sababu unacheka?

Alafu mbona hayo mambo ya wadada warembo mlikuwa hamyasemi kipindi cha kanumba? Wema sikatokea huko huko? Priyanka hajasomea filamu alikuwa ni miss world mbona ni muigizaji mzuri tu? Ebu nijibu mkuu nikuelewe
 
BONGO MOVIE WENGI NI VILAZA, SIO AJABU WAMEILAZA SANAA YA UIGIZAJI.

Anaandika, Robert Heriel.

Hapana shaka sanaa ya Uigizaji kwa sasa imelala Usingizi wa Pono, imelala fofofo na waigizaji wake wanakoroma. Wapo kwenye ndoto za majinamizi wabaya wanaowakimbiza kwenye mitaro huko usingizini. Tangu kifo cha Marehemu Kanumba miaka zaidi ya tisa iliyopita Tasnia ya Bongo Movie imelala fofofo.

Hakuna Tasnia inayoongozwa na Vilaza isilale, sijawahi kuona popote pale duniani. Bongo Movie imejaa wasanii vilaza kwa kiwango kikubwa sana, watu waliokimbia shule ndio wamekimbilia huko kwenye tasnia ya filamu. Embu fikiria mtu amekimbia shule kwa kushindwa somo hata la kiswahili unafikiri atatuambia nini kwenye suala la kuelimisha jamii kupitia fani ya uigizaji.

Kilaza ni kilaza tuu, uwezo wake wa kufikiri ni mdogo alafu anakuwa Director wa filamu, unafikiri filamu yake itakuwaje kama sio Utopolo. Kilaza hufikiri mambo chini ya kiwango, ukiwaangalia wasanii wengi wa bongo movie wakiigiza kwanza hawawezi kuuvaa uhusika, wanachojua ni kutoa macho, kukenua, kubinua makalio, kuvaa nguo fupi, wakati kwa upande wa wasanii wa kiume wanachjua ni kupaka piko sijui waves nywele zao, kutoboa masikio au kubandika stiker masikioni, na kulamba lamba midomo kama sio kusuka nywele. Kwa mambo haya wamefuzu kwani mambo haya hufanywa kwa sehemu kubwa na vilaza, kwani hata mtu asiye msanii anaweza kufanya mambo hayo. Vilaza hufanya mambo ambayo mtu yeyote anaweza kufanya.

i/ Muongoza Filamu alifeli shule, akaunga unga wee akapata cheti, huyo akajiingiza kwenye Tasnia ya Filamu, haya embu niambie atatupa kipi cha maana hapo?
ii/ Mtayarishaji alifeli shule, akaunga unga wee, embu niambie ataleta jambo gani katika ulimwengu huu wa elimu, sayansi na teknolojia?
iii/Mchukua Kamera alipata sifuri au four ya mwisho kabisa, hivi unategemea atakuwa na ubunifu gani kwenye masuala ya kurekodi picha na video na kamera?
iv/ Mtia sauti, aliishia kidato cha nne, embu niambie anauelewa gani na mambo ya sauti, muziki na ala? Sio ajabu sauti nyingi zinazoingizwa kwenye movies nyingi ni zile zile haziendani na uhalisia,
v/ Mtu wa Makeup aliishia darasa la pili, hivi anajua nini kuhusu urembo? Kama utabisha angalia filamu zetu kisha angalia za wenzetu kama wanaijeria utaelewa.
vi/ Mtu wa simulizi, aliishia darasa la saba, hivi unafikiri uwezo wake wa kufikiri, na uelewa wa mambo ataandika script ipi yenye kufanya kizazi cha sasa kukubali kisa chake

Shida kubwa ya Wasanii wa Bongo Movie ni elimu ni ndogo sana kwa wengi wao, wengi ni Slow Learner, wachache sana wanauwezo mkubwa wa kiakili, kufikiri na kuchambua mambo. Wengi wao ni bora liende nao wawemo.

Ukitaka kujua kuwa Wasanii wetu wengi wao ni Vilaza basi angalia Role Model wao waliopo ughaibuni kama Marekani, bado ni wale wale waliokimbia shule, watu wenye Skendo, wavaa uchi, watumiaji wa madawa ya kulevya, na wahuni walioshindikana.

Bongo Movie ikataka iinuke iache kuchukua Vilaza, slow Learner watu waliokimbia shule ambao kimsingi lazima wawe na akili finyu na kazi zao lazima ziwe duni.

Waigizaji wengi wa Nigeria, Ghana, South Afrika wana elimu Degree moja kuendelea, yaani ambao hawajasoma ni wachache sana ukilinganisha na wenye shahada. Ndio maana wanajua kile wafanyacho. Embu angalia filamu na tamthilia za Kikorea ambazo kwa sasa zinateka soko hapa nchini, waigizaji karibu wote wa Kikorea ni Wasomi wa elimu ya juu kabisa kuanzia Degree tena nyingine ni zile za moto. Njoo kwa Wahindi, wafilipino, na kule Amerika ya kusini, waigizaji karibu wote ni wasome wa elimu ya juu kabisa.

Mtu mwenye elimu ya uhakika sio ile elimu ya kuunga unga kwenye vyuo visivyoeleweka hawezi kutoa kazi mbovu.

Naipongeza serikali kwa kuanzisha michepuo mipya itakayoendana na mambo ya sanaa na Lugha ili kufufua Tasnia ya Filamu hapa nchini.

Mtu kaishia Darasa la saba au kidato cha nne, atajuaje na kuigizaje mambo ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi yaani ataanzia wapi?
Mtu madarasa hayamtoshi, ataweza kuigiza filamu za kisiasa, ugaidi, na masuala ya demokrasia? Atawezaje ikiwa hajui hata historia ya hiyo demokrasia yenyewe zaidi ya maneno ya mtaani na vijiweni.
Mtu kaishia kidato cha nne atawezaje kufikiria kuandaa scripts ya mambo ya Mpango wa dunia wa milleniam, atawezaje kuigiza Umuhimu wa vyama vingi vya siasa ndani ya nchi?
Mtu kaishia kidato cha nne kwa kulazimishwa, atawezaje kuigiza filamu ya masuala ya sheria na haki za binadamu, hajui hata katiba ya nchi yake, mtu kama huyo huoni ni jipu?

Mtu kaishia kidato cha nne, atawezaje kuandaa filamu ya athari ya udikteta na ukosefu wa uhuru wa kujieleza ndani ya jamii,lini atawaza hayo, yeye kama sio kuwaza mapenzi tuu muda wote?

Mtu kaishia darasa la saba au kidato cha nne, atawezaje kufikiri hata kuigiza filamu inayopromoti utalii wa nchi yetu, utashangaa licha ya nchi yetu kuwa na Mbuga na vivutio vingi lakini tangu tupate uhuru hakuna filamu ya wanyama iliyochezwa na wabongo, utashangaa. Ndio shida ya vilaza hiyo. Wenyewe watakuambia uchumi mgumu.

Mtu anaelimu ya kuunga unga, atawezaje kuigiza inayozungumzia masuala ya fani za kitaalamu kama vile Ualimu wenyewe sio ule wa kuigiza kama wanaoigiza watoto kibaba baba na kimama mama. Au udaktari, au sheria, au injinia, utawezaje igiza kitu hukijui na huna akili ya ku-master kwa upesi.

Mimi nawashauri wenye nafasi na wanaotaka Bongo Movie iamke basi wafanye haya;
Wasajili watu wenye vipaji Fresh from the School, waende shule zenye vipaji huko, Vyuo vikuu vinavyotambulika wachukue watu huko.
Wasaniii wawekewe sheria kuwa ili uwe mwigizaji basi yakubidi uwe na elimu isiyochini ya Diploma. Na uwe umefaulu vizuri kidato cha nne

Tasnia inapoongozwa na Kilaza kamwe haiwezi kuzaa matunda chanya kwenye jamii.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Sumbawanga
Mkuu umeongea ukweli mtupu hawa watu lazima wawe na utaalamu kuhusu fani husika.

Kama mtu anaigiza udaktari basi aigize kweli aelewe mambo muhimu ya udaktari juu ya script anayocheza.

Sio unaigiza daktari alafu umevaa nguo za nesi.

Kama mtu anaigiza polisi kweli awe na taaluma kuhusu upolisi,sio polisi wa kituoni na nguo zake za kaki ati ana ndevu wakati polisi wale hawatakiwi kufuga ndevu.

Sio polisi wawili wameenda kukamata kila polisi anamwita mwenzie afande wakati kijeshi lazima kuna mmoja atakuwa senior na mwingine mdogo

Sio mtu anaigiza movie ya kijeshi ati private wa jeshi anampigia saluti coplo wa jeshi jambo ambalo halipo na ni upuuzi.

Kiufupi wanaigiza kama watoto wadogo vile wakati wenzetu huko nje unajiuliza ni kweli ama maigizo wakati huo hapa bongo unaona kabisa hapa ni changa la macho.

Wanachofanya bongo movie ni kutudanganya hata juu ya wanachoigiza,yaani huwezi kujifunza kitu cha ukweli kwenye movie za bongo

Coplo kumpigia saluti coplo ni uongo kiuhalisia haipo hivyo kwa hiyo movie zetu wanatudanganya na ndo wanazidisha ujinga kwenye jamii kwa kuwaigizia watu jambo ambalo silo.

Kwenye mapenzi oooooh wanajua kuigiza sana hasa ukikuta mwanaume the way anareact akiona demu mwenye chura utaona kabisa ni kama wamekuona wewe lakini wapii they are experts katika hiyo sector ya mapenzi na ngono.

Nilishawahi kuwaza na mimi nije kuwa muigizaji ili nielimishe jamii juu ya mambo mbali mbali ya Nchi hii kwa kuigiza kitu cha ukweli kutokana na wao kuharibu tasnia hii lakini ndo nina malengo mengine tofauti na uigizaji.
 
Sasa mkuu ushasema bajeti ni ndogo watafanyaje kitu kizuri? Ushawahi kufanya production? Unajua Episode Moja ya SALAMANA ilikuwa inacost how much? Na ile show tu sembuse Movie?

Alafu unahisi leo wakaungana wolper, JB, Aunty Ezekiel, Rammy gallis, Ray na Gabo wakachukua bank loan wakachukua DIRECTOR WA KICHINA kuongoza na wakatengeneza bonge la BLOCK BUSTER ACTION film kama ile ya james Bond wanashindwa?

Ishu ni kuwa WATAUZIA WAPI? NA WATARUDISHAJE COST? Hayo masuala sijui ya madirector kukosa elimu ni propaganda tu . Huwezi kuniambia bongo hamna director mzuri na hata kama hayupo wameshindwa kukodi kutokea nje?

Ishu imekaa kimfumo mkuu. Yaaani nchi hata local theatres hamna na CCM ipo tu alafu mnataka muwalaumu wasanii?
Hizo ndizo fikra zenu za kimaskini, unauliza watamuuzia nani, Kuna mtu haangalii kitu kizuri?, hebu fanyeni hivyo muone kama hamtopata wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi,

Kama mnaweza kukopeshana pesa hadi kufikia hatua ya kutukanana matusi ya nguoni kwanini msiungane mkachukua mkopo bank na kufanya mambo makubwa?

Angalieni wenzenu wa Bongo flavor wanavyojitahidi, sasa hivi hadi Wamarekani wameanza kufanya collabo na Waafrica baada ya kuona hatusikilizi tena miziki yao tupo busy na ya kwetu, kwanini Bongo movies msibadilike kama Bongo flavor? Na kama hamuwezi basi mtuachie fursa sie wapya tufanye mapinduzi lakini bado mnatubania,

Aibu yenu.
 
Acheni ujinga watanzania wengi mnakawaida ya kutopenda vya kwenu inawezekana kweli kuna mapungufu kwenye bongo movie lakini si kwa ukubwa uo mnaoongela hapa,,,,,
Mtoa mada unaponda bongo movie alfu unakuja kusifia movie ya kihindi wewe ndo Bogaz kabisa wahindi wale mtu anapigwa ngumi anarushwa mita50 had anabomoa ukuta ule ndo uhalisia,,,[emoji15]
Vionjo kama hivyo havikosi,wabongo wanataka sana kufanya hivyo lakini hata teknolojia hiyo hawana watababaisha babaisha.

Wabongo wanataka sana wawe na utaalamu ule lakini hawawezi.

Vile vionjo vinanogesha movie hapa bongo ovyo kaka,tusijifiche kwenye kivuli cha kupenda vya kwetu wakati ni vya ovyo.

Ili tuvipende lazima tuvikosoe
 
Mkuu umeongea ukweli mtupu hawa watu lazima wawe na utaalamu kuhusu fani husika.

Kama mtu anaigiza udaktari basi aigize kweli aelewe mambo muhimu ya udaktari juu ya script anayocheza.

Sio unaigiza daktari alafu umevaa nguo za nesi.

Kama mtu anaigiza polisi kweli awe na taaluma kuhusu upolisi,sio polisi wa kituoni na nguo zake za kaki ati ana ndevu wakati polisi wale hawatakiwi kufuga ndevu.

Sio polisi wawili wameenda kukamata kila polisi anamwita mwenzie afande wakati kijeshi lazima kuna mmoja atakuwa senior na mwingine mdogo

Sio mtu anaigiza movie ya kijeshi ati private wa jeshi anampigia saluti coplo wa jeshi jambo ambalo halipo na ni upuuzi.

Kiufupi wanaigiza kama watoto wadogo vile wakati wenzetu huko nje unajiuliza ni kweli ama maigizo wakati huo hapa bongo unaona kabisa hapa ni changa la macho.

Wanachofanya bongo movie ni kutudanganya hata juu ya wanachoigiza,yaani huwezi kujifunza kitu cha ukweli kwenye movie za bongo

Coplo kumpigia saluti coplo ni uongo kiuhalisia haipo hivyo kwa hiyo movie zetu wanatudanganya na ndo wanazidisha ujinga kwenye jamii kwa kuwaigizia watu jambo ambalo silo.

Kwenye mapenzi oooooh wanajua kuigiza sana hasa ukikuta mwanaume the way anareact akiona demu mwenye chura utaona kabisa ni kama wamekuona wewe lakini wapii they are experts katika hiyo sector ya mapenzi na ngono.

Nilishawahi kuwaza na mimi nije kuwa muigizaji ili nielimishe jamii juu ya mambo mbali mbali ya Nchi hii kwa kuigiza kitu cha ukweli kutokana na wao kuharibu tasnia hii lakini ndo nina malengo mengine tofauti na uigizaji.


Mkuu naomba unitajie jina la hiyo muvi ambayo koplo anampigia saluti koplo au ni mwigizaji gani aliigiza kwa hiyo movie ili niitafute.

Tusije tukawa tunaongelea vitu ambavyo havipo ili tu tufurahishe umma
 
But kila kitu kina mwisho wake, Zama zinabadilika tunataka wasomi kwenye industry ya bongo movie , we have been entertaining non sense for so long , we want changes kwa kweli

Nikiangalia tamthilia zao Sijui jua Kali , Mimi Naona bado safar ni ndefu , uigizaji wa kishamba sana
Kuna yule mama anaact kama waziri, khaa yale ndio maisha ya waziri kweli? Si bora hata wangesema ni mfanyabiashara mkubwa basi ikatosha,

Wanasingizia bajeti, lakini wanakopeshana pesa hadi kutukanana matusi mazito mazito,
Hayo madanga wanayopasiana wanashindwa kuwaomba wawafadhili wafanye movie moja matata yenye story nzuri ya kusisimua,

Shida directors wao, producers wao, Editors wao, halafu ushikaji mwingi wanafanya kazi kimazoea sana.
 
Sasa kama hauna huo muda mchafu na hujawahi kuangalia umejuaje hawana ubunifu na movie zao zote wanaigiza mapenzi?

Unaijua movie ya safari ya Gwalu ya Gabo? Kuna mapenzi mule?

Yaaani umejuaje ka huangalii?
Oi dingi usinichoshe na mautopolo yenu. Kiujumla hamna ubunifu yani hamna jambo jipya yani mmefulia.
 
Comedy inafanya vipi vizuri? Kwa mwaka 2020 nitajie filamu tano za comedy zilizouza sana Tanzania?

Yaaani mizengwe unaweza kufananisha na Huba au Shilingi ya dstv

Ringo na Pembe wameingiza how much kutokana na filamu walizotoa mwaka jana?
Filamu gani ya comedy kutokea Tanzania kwa sababu ya ubora wake imeingia NETFLIX, HULU, DISNEY + au any major streaming platform.

Na unamaanisha nini watu wa comedy wanafanya vizuri? Au kwa sababu unacheka?

Alafu mbona hayo mambo ya wadada warembo mlikuwa hamyasemi kipindi cha kanumba? Wema sikatokea huko huko? Priyanka hajasomea filamu alikuwa ni miss world mbona ni muigizaji mzuri tu? Ebu nijibu mkuu nikuelewe
Wenzako wamesomea sanaa unajua elimu ya Priyanka au unacomment tu, unajua elimu ya madirector wao
 
Hizo ndizo fikra zenu za kimaskini, unauliza watamuuzia nani, Kuna mtu haangalii kitu kizuri?, hebu fanyeni hivyo muone kama hamtopata wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi,

Kama mnaweza kukopeshana pesa hadi kufikia hatua ya kutukanana matusi ya nguoni kwanini msiungane mkachukua mkopo bank na kufanya mambo makubwa?

Angalieni wenzenu wa Bongo flavor wanavyojitahidi, sasa hivi hadi Wamarekani wameanza kufanya collabo na Waafrica baada ya kuona hatusikilizi tena miziki yao tupo busy na ya kwetu, kwanini Bongo movies msibadilike kama Bongo flavor? Na kama hamuwezi basi mtuachie fursa sie wapya tufanye mapinduzi lakini bado mnatubania,

Aibu yenu.

Hao wanunuzi wa ndani na nje ya nchi wanapatikana vipi? Kwenye nchi zilizoendelea hamna anayeuza physical copies tena KAMA STEPS kwa sababu ya uharamia.
Movie duniani kote zinauzwa kwa kutumia MOVIE TICKETS kwenye Cinemas. Bongo kuna cinemas ngapi? Unataka JB ajengee sinema?

Hollywood, Bollywood, Nollywood na Han Cinema ya Korea kila sehemu kuna Cinemas kuonyesha movie. Enheeee bongo unatengeneza movie ya 1 B umechukua mkopo bank hela yako unarudishaje?

Na kamwe usifananishe bongo fleva na bongo movie.

Bongo fleva wamepata mkombozi mtu ana uhakika akitoa album ANAUZIA WAPI Youtube, audio mack apple music na march hapa spotify amekuja bongo kuuza kazi za wasanii?
Niambie Unatengeneza big budget movie utaweka youtube? Hela yako itarudi?

Mnalamika bure. Ishu ni mfumo na CCM.

Acha kulalamika.
 
Comedy inafanya vipi vizuri? Kwa mwaka 2020 nitajie filamu tano za comedy zilizouza sana Tanzania?

Yaaani mizengwe unaweza kufananisha na Huba au Shilingi ya dstv

Ringo na Pembe wameingiza how much kutokana na filamu walizotoa mwaka jana?
Filamu gani ya comedy kutokea Tanzania kwa sababu ya ubora wake imeingia NETFLIX, HULU, DISNEY + au any major streaming platform.

Na unamaanisha nini watu wa comedy wanafanya vizuri? Au kwa sababu unacheka?

Alafu mbona hayo mambo ya wadada warembo mlikuwa hamyasemi kipindi cha kanumba? Wema sikatokea huko huko? Priyanka hajasomea filamu alikuwa ni miss world mbona ni muigizaji mzuri tu? Ebu nijibu mkuu nikuelewe
Tatizo hamjui halafu hamtaki kukosolewa, mnasingizia bajeti wakati kila mara mnatoa moviee wenzenu movie moja wanaweza kutoa baada ya miaka mitatu wakati nyinyi mwaka mmoja mmeshatoa movies zaidi ya nne.
Muda wa kufanya research hamna wala kutathimini namna gani movie imefanyaje kwenye soko.
 
Hao wanunuzi wa ndani na nje ya nchi wanapatikana vipi? Kwenye nchi zilizoendelea hamna anayeuza physical copies tena KAMA STEPS kwa sababu ya uharamia.
Movie duniani kote zinauzwa kwa kutumia MOVIE TICKETS kwenye Cinemas. Bongo kuna cinemas ngapi? Unataka JB ajengee sinema?

Hollywood, Bollywood, Nollywood na Han Cinema ya Korea kila sehemu kuna Cinemas kuonyesha movie. Enheeee bongo unatengeneza movie ya 1 B umechukua mkopo bank hela yako unarudishaje?

Na kamwe usifananishe bongo fleva na bongo movie.

Bongo fleva wamepata mkombozi mtu ana uhakika akitoa album ANAUZIA WAPI Youtube, audio mack apple music na march hapa spotify amekuja bongo kuuza kazi za wasanii?
Niambie Unatengeneza big budget movie utaweka youtube? Hela yako itarudi?

Mnalamika bure. Ishu ni mfumo na CCM.

Acha kulalamika.
Toeni basi movie ya kuonyesha mfumo na ccm wanavyowaatiri vinginevyo mtabaki kuchangishana rambirambi na kuibiana maana hicho ndio mnakiweza
 
Wenzako wamesomea sanaa unajua elimu ya Priyanka au unacomment tu, unajua elimu ya madirector wao


Daaah yaaani wewe wa kuniuliza mimi elimu ya priyanka chopra? Wenzio hayo mambo ndo tunafanyia presentation.

Priyanka hajasomea film. Alikuwa mrembo na baada ya kushinda tu miss world Abbas akumuita kufanya nae movie 2002. Yaaani infact hakwenda ata chuo.
 
Mkuu umeongea yote!

Kuna kipindi ilikuwa ukisema mi sisikilizagi bongo fleva nasikiliza mziki wa nje unaonekana mjanja sana. Sasa hiyo hali ndo inatokea kwa bongo movie sa hiii.

Yaani ili uonekane modern ni lazima useme "siangaliagi bongo movie".

Siangalii bongo movie alafu hapo hapo anatoa makosa kibao yaliyotokea kwenye filamu. Sasa unajiuliza kama haangaalii amejuaje hayo makosa.

Tuna safari ndefu sana.
Yees ni unafki tu nakufata mkumbo wengi wao humu kujifanya wako educated sana ,,etii ooh ulaya hakuna muigizaji asie na degreee,,.

ooh me kwangu nimepiga marufuku bongo movie, lakini wasanii wote wa bongo movie anawajua sa sijui amewajulia wapi[emoji23][emoji23]
 
Daaah yaaani wewe wa kuniuliza mimi elimu ya priyanka chopra? Wenzio hayo mambo ndo tunafanyia presentation.

Priyanka hajasomea film. Alikuwa mrembo na baada ya kushinda tu miss world Abbas akumuita kufanya nae movie 2002. Yaaani infact hakwenda ata chuo.
Umeulizwa elimu yake unaleta maneno mengine kumbe na wewe ni walewale
 
Hao wanunuzi wa ndani na nje ya nchi wanapatikana vipi? Kwenye nchi zilizoendelea hamna anayeuza physical copies tena KAMA STEPS kwa sababu ya uharamia.
Movie duniani kote zinauzwa kwa kutumia MOVIE TICKETS kwenye Cinemas. Bongo kuna cinemas ngapi? Unataka JB ajengee sinema?

Hollywood, Bollywood, Nollywood na Han Cinema ya Korea kila sehemu kuna Cinemas kuonyesha movie. Enheeee bongo unatengeneza movie ya 1 B umechukua mkopo bank hela yako unarudishaje?

Na kamwe usifananishe bongo fleva na bongo movie.

Bongo fleva wamepata mkombozi mtu ana uhakika akitoa album ANAUZIA WAPI Youtube, audio mack apple music na march hapa spotify amekuja bongo kuuza kazi za wasanii?
Niambie Unatengeneza big budget movie utaweka youtube? Hela yako itarudi?

Mnalamika bure. Ishu ni mfumo na CCM.

Acha kulalamika.
CCM ndio wanawafundisha nyie kuigiza? Mbona ngono mnazipatia? Nchi hii ni kubwa sana yaan mmeshaizunguka koooote mkatafuta hata stories za makabila flan mkaigiza? Kuna locations chungu nzima mnashindwa kwenda huko mkaigiza muachane na locations za mahotelini? Big budget gani, watu wanasema hamna ubunifu, stories zenu ni zile zile za mapenzi na uchawi, waigizaji hawana viwango, mnajali makalio na hereni za kuning'inia na make ups kama clowns,

Mpishe wasomi waliosomea tasnia hiyo wapige kazi na wao, sura zenu haziuziki tena.

Tunalalamika sie au nyie? Mngekua mnafanya kitu cha kuonekana hata serikali ingewekeza.
 
Nafikiri hoja yako sijui kama ina maana la zaidi ni post ya udhalilishaji. Kuna vitu ni talent. Kuwa akili ya kujibu physics hakukupi talent ya kuwa muigizaji nzuri. Nafikiri unashindwa kuheshimu kwamba uigizaji unahitaji kipaji na sio kila mtu.
 
Back
Top Bottom