Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Bongo Movies wengi ni vilaza, si ajabu wameilaza sanaa ya uigizaji. Wasomi ingieni huko

Mkuu I said it in their CONTEXT course wanafanyaga reference ya kile kipindi cha Kanumba wanasema the market was good.

Pia kiukweli uwezi ukafananisha hali ya kipindi kile na sasa hivi when it comes to sales of movies. Kipindi kile movie zilikuwa mbaya but soko lilikuwa zuri kipindi hiki ubora vumeongezeka compared to zamani lakini soko hamna kabisa

Sasa tunaenda sawa.

Movie zilikuwa mbaya na zilikuwa zinapendwa kwa sababu ya jamii kuwa gizani, elimu duni, na mitandao ilikuwa bado haijachanganya.

Wasanii walipaswa wabadilike kulingana na nyakati, waligundue hili mapema kabla haijala kwao, wao wakazubaa.

Kipindi kile ishu sio kuigiza, ishu ilikuwa ni kuonekana kwenye TV bila kujali unaongea nini, nchi ilikuwa ushambani, sasa kila mtu ni mjanja kasoro tuu waigizaji ambao wanadhani jamii yao ni ile ile.
 
Huwezi fananisha Bongo Flavor na Bongo movie, Movie industry ni tasnia inayohitaji taaluma na uekezaji mkubwa, tofauti na masuala ya music.

Mkuu tunachozungumzia hapa, ni kuwa hata huo uwekezaji mdogo uliofanywa mbona hatuoni la maana?
Ndio nikasema shida shule ndogo kwa wasanii wengi na wahusika wa filamu.

Filamu nyingi zimelenga mambo ya kitoto.

Yaani Watu wazima wanaigiza kama watoto, kimama mama na kibaba baba bhana!!!!!!!!!!!!
 
Hao wanunuzi wa ndani na nje ya nchi wanapatikana vipi? Kwenye nchi zilizoendelea hamna anayeuza physical copies tena KAMA STEPS kwa sababu ya uharamia.
Movie duniani kote zinauzwa kwa kutumia MOVIE TICKETS kwenye Cinemas. Bongo kuna cinemas ngapi? Unataka JB ajengee sinema?

Hollywood, Bollywood, Nollywood na Han Cinema ya Korea kila sehemu kuna Cinemas kuonyesha movie. Enheeee bongo unatengeneza movie ya 1 B umechukua mkopo bank hela yako unarudishaje?

Na kamwe usifananishe bongo fleva na bongo movie.

Bongo fleva wamepata mkombozi mtu ana uhakika akitoa album ANAUZIA WAPI Youtube, audio mack apple music na march hapa spotify amekuja bongo kuuza kazi za wasanii?
Niambie Unatengeneza big budget movie utaweka youtube? Hela yako itarudi?

Mnalamika bure. Ishu ni mfumo na CCM.

Acha kulalamika.
Serekali haijawahi kuwa serious na masuala ya filamu, hawaelewi kama ni moja ya sehemu inayoweza kuwaingizia kipato kikubwa tu, India film Industry inachangia asilimia 12 ya pato la nchi kila mwaka.
 
Serikali yenu ijifunze kudeal na MABEPARI huko korea SAMSUNG kuna kipindi 2017 ilikumbwa na kesi ya rushwa. Kiongozi wa samsung akaenda jela kampuni imebaki salama inachangia pato la nchi.

Unafungia STEPS major distributor alafu HUJI NA SOLUTION ndo unasolve nini sasa? Aliyehusika na hiyo issue ni nani kwanini asifungwe yeye?

Serikali ingekuja na solution kwamba STEPS AKIONDOKSA ITENGENEZWE MODEL NYINGINE YA WASANII KUUZA KAZI ZAO.

Wamefuta Steps MAJOR distributor industry imekufa movie hazitengenezwi sababu hamna namna ya kuuza movie na nyie mlivyo wa ajabu mnaanza kusema eti kisa wasanii hawana vipaji. Movie za ngono mbona hata marekani zipo?

Hii nchi inahitaji redemption. Ujinga ni mwingi.
Steps hakufungiwa bali aliondoka mwenyewe baada ya kuona amebanwa kodi
 
Mkuu tunachozungumzia hapa, ni kuwa hata huo uwekezaji mdogo uliofanywa mbona hatuoni la maana?
Ndio nikasema shida shule ndogo kwa wasanii wengi na wahusika wa filamu.

Filamu nyingi zimelenga mambo ya kitoto.

Yaani Watu wazima wanaigiza kama watoto, kimama mama na kibaba baba bhana!!!!!!!!!!!!

Mambo ya maana yanahitaji bajet kubwa. Vipaji vipo. Madairekta wapo mnaweza kukodi hata nje. Mbona wakina Campos na Ogopa videos wamekula sana mipunga ya kina AY?

Yaaani serikali waanze kuichukulia hii industry seriously uone kama movie za mkwawa hazijatengenezwa.
 
Serekali haijawahi kuwa serious na masuala ya filamu, hawaelewi kama ni moja ya sehemu inayoweza kuwaingizia kipato kikubwa tu, India film Industry inachangia asilimia 12 ya pato la nchi kila mwaka.

Serikali unataka iwe sirius ili watu wapoteze vitumbua vyao?

Serikali ikiitambua Fani ya uigizaji itaweka vigezo lazima uwe na Diploma au degree moja unafikiri wangapi watabaki hapo?
Kisha watu wapewe leseni
 
Mambo ya maana yanahitaji bajet kubwa. Vipaji vipo. Madairekta wapo mnaweza kukodi hata nje. Mbona wakina Campos na Ogopa videos wamekula sana mipunga ya kina AY?

Yaaani serikali waanze kuichukulia hii industry seriously uone kama movie za mkwawa hazijatengenezwa.

Wamekula mpunga kwenye Filamu ipi?
Au unazungumzia hizi video za muziki boss?

Hizi hiz movie wanazoigiza za bajeti ndogo mbona ni kama wanaigiza kimama mama na kibaba baba. Mtu na akili zake hawezi ketisha masaburi yake akaangalia

Watunzi wana stori za kitoto toto, yaani filamu haina hata sehemu ya kutafakarisha, sehemu ya Watch part 2 ndio vituko vituko
 
Daaah yaaani wewe wa kuniuliza mimi elimu ya priyanka chopra? Wenzio hayo mambo ndo tunafanyia presentation.

Priyanka hajasomea film. Alikuwa mrembo na baada ya kushinda tu miss world Abbas akumuita kufanya nae movie 2002. Yaaani infact hakwenda ata chuo.

Sio Priyanka tu, Aishwarya Rai, Sushmita Sen, Juhi Chawla wote waliingia Bollywood kwa njia hiyo hiyo, kuna wengi walikua ni mamodel wakatisua pia, akina Arjun Rampal, Deepika.
Kareena Kapoor aliishia darasa la 12 tu, hata college hajafika, hivi sasa ni katika Most Successful FIlm Actress ever pale Bollywood.
 
Steps hakufungiwa bali aliondoka mwenyewe baada ya kuona amebanwa kodi

Mkuu ni kwamba hujui au free market works? Ushasema walibanwa kodi sasa ulitegemea wangeendelea kufanya biashara?

Okay fine walikuja na mechanism gani kuhakikisha the movie industry inapata distributor mwengine?

Serikali yenu imeshindwa hata kuita kampuni kama SILVER BIRD ya nigeria itengeneze sinemas watu wauze movie? JB angepata faida si ndo angeendelea kutengeneza movie nzuri zaidi?.

Sasa JB atatengenezaje movie nzuri kama hana hata sehemu ya kuuzia movie zake
 
Anzeni kutengeneza movies nzuri hizo foleni zitakuwepo sasa mwataka tupange foleni kuangalia vile mnavyongonoka?
Mpo serious kweli na kazi? Mbona tunapanga foleni kuingia kwenye shows za Music?
point umeshindwa kuifahamu, Rome haikujengwa kwa siku moja, Leo Bollywood wanatengeneza filamu zenye ubora wakukaribiana na Hollywood , hili halikuja kirahisi, ni support waliokua wanaipata kutoka kwa watu ndio iliwawezesha wao kuweza kusogea kiubora.
Ni ngumu kujitokeza kwa financers wakaekeza fedha zao bila ya kuwa na Imani alau ya kurudi fedha zao achilia kupata faida, hivi mtu aje atoe milioni zake 200, aekeze kwenye filamu zitarudi kwa njia gani hapa bongo?
 
Sasa mkuu ushasema bajeti ni ndogo watafanyaje kitu kizuri? Ushawahi kufanya production? Unajua Episode Moja ya SALAMANA ilikuwa inacost how much? Na ile show tu sembuse Movie?

Alafu unahisi leo wakaungana wolper, JB, Aunty Ezekiel, Rammy gallis, Ray na Gabo wakachukua bank loan wakachukua DIRECTOR WA KICHINA kuongoza na wakatengeneza bonge la BLOCK BUSTER ACTION film kama ile ya james Bond wanashindwa?

Ishu ni kuwa WATAUZIA WAPI? NA WATARUDISHAJE COST? Hayo masuala sijui ya madirector kukosa elimu ni propaganda tu . Huwezi kuniambia bongo hamna director mzuri na hata kama hayupo wameshindwa kukodi kutokea nje?

Ishu imekaa kimfumo mkuu. Yaaani nchi hata local theatres hamna na CCM ipo tu alafu mnataka muwalaumu wasanii?
Kizuri hujiuza ndo maana wakina Vandame wanaweza kuwa hawajui hata kuna nchi inaitwa TANZANIA ila huku ana ma role model kibao ukiacha mashabiki.TUACHENI VISINGIZIO SASA WE LI MTU(JENGUA)LINAIGIZA LINAPENDWA KICHIZI MPAKA DEMU ANAJIUA UKIANGALIA SURA YA JENGUA KAMA PALAMAGAMBA KABUDI JUMLISHA NA MIJICHO YAO we unaona watu wa TASNIA YA BONGO MOVIES WAPO SERIOUS
 
Sio Priyanka tu, Aishwarya Rai, Sushmita Sen, Juhi Chawla wote waliingia Bollywood kwa njia hiyo hiyo, kuna wengi walikua ni mamodel wakatisua pia, akina Arjun Rampal, Deepika.
Kareena Kapoor aliishia darasa la 12 tu, hata college hajafika, hivi sasa ni katika Most Successful FIlm Actress ever pale Bollywood.

Mkuu umeelezea vizuri sana. Watu hawaelewi haya mambo. Na sio india tu korea kuna dada mmoja anaitwa IU ameigiza series ya Hotel De Luna as leading actress . Yule ni mwimbaji pure hakuingia darasani ila alikuwa na kipaji na mapenzi lakini namna anavyofanya vitu vyake ndani yacile series ni hatari.

Bongo badala tuangalie mzizi wa tatizo ni nini tunaanza kusema kisa wasanii hawajasoma, mara sijui kuna majungu sana, hivi kweli kuna industry ambayo hamna chokochoko na mabifu?

Kiukweli Tuna safari ndefu sana mkuu.
 
Tatizo hamjui halafu hamtaki kukosolewa, mnasingizia bajeti wakati kila mara mnatoa moviee wenzenu movie moja wanaweza kutoa baada ya miaka mitatu wakati nyinyi mwaka mmoja mmeshatoa movies zaidi ya nne.
Muda wa kufanya research hamna wala kutathimini namna gani movie imefanyaje kwenye soko.
Hiyo sio hoja mkuu, hatua inayokua refu kwenye kutengeneza filamu ni script writing, ila ukishakua na script mkononi shooting na post production hata miezi mitatu yaweza tosha inategemea na scale ya filamu yenyewe, filamu zinazochukua mda ni zile za science fiction, lakini drama na romance hazina shida kabisa.
 
Comedy inafanya vipi vizuri? Kwa mwaka 2020 nitajie filamu tano za comedy zilizouza sana Tanzania?

Yaaani mizengwe unaweza kufananisha na Huba au Shilingi ya dstv

Ringo na Pembe wameingiza how much kutokana na filamu walizotoa mwaka jana?
Filamu gani ya comedy kutokea Tanzania kwa sababu ya ubora wake imeingia NETFLIX, HULU, DISNEY + au any major streaming platform.

Na unamaanisha nini watu wa comedy wanafanya vizuri? Au kwa sababu unacheka?

Alafu mbona hayo mambo ya wadada warembo mlikuwa hamyasemi kipindi cha kanumba? Wema sikatokea huko huko? Priyanka hajasomea filamu alikuwa ni miss world mbona ni muigizaji mzuri tu? Ebu nijibu mkuu nikuelewe
Bro VICENT KIGOSI mbona umekuja juu hivyo
 
Mkuu ni kwamba hujui au free market works? Ushasema walibanwa kodi sasa ulitegemea wangeendelea kufanya biashara?

Okay fine walikuja na mechanism gani kuhakikisha the movie industry inapata distributor mwengine?

Serikali yenu imeshindwa hata kuita kampuni kama SILVER BIRD ya nigeria itengeneze sinemas watu wauze movie? JB angepata faida si ndo angeendelea kutengeneza movie nzuri zaidi?.

Sasa JB atatengenezaje movie nzuri kama hana hata sehemu ya kuuzia movie zake
Nyinyi kila kitu mnasema serikali, serikali ndio inawaambia mtengeneze filamu za ovyo, kuna filamu kama Neria ya Zimbabwe, sinema kama hizo mnaweza kupata hata sponsor US aid na taasisi nyingine kutokana na maudhui yake
 
Kweli hii n fursa kwa vijana. Wakaka wanachibua tu badala ya kupiga kazi. Wadada wapo sokoni nao.
 
Hiyo sio hoja mkuu, hatua inayokua refu kwenye kutengeneza filamu ni script writing, ila ukishakua na script mkononi shooting na post production hata miezi mitatu yaweza tosha inategemea na scale ya filamu yenyewe, filamu zinazochukua mda ni zile za science fiction, lakini drama na romance hazina shida kabisa.
Hapo ndio mnakosea, kuna muda sinema inatakiwa ikae sokoni lakini wewe kila miezi 3 unatoa filamu hapo unategemea nini
 
Kizuri hujiuza ndo maana wakina Vandame wanaweza kuwa hawajui hata kuna nchi inaitwa TANZANIA ila huku ana ma role model kibao ukiacha mashabiki.TUACHENI VISINGIZIO SASA WE LI MTU(JENGUA)LINAIGIZA LINAPENDWA KICHIZI MPAKA DEMU ANAJIUA UKIANGALIA SURA YA JENGUA KAMA PALAMAGAMBA KABUDI JUMLISHA NA MIJICHO YAO we unaona watu wa TASNIA YA BONGO MOVIES WAPO SERIOUS

Unaninisikitisha sana mkuu. Kuna kitu kinaitwa GLOBALIZATION.

Sasa hivi watu mnataka movie za kibongo ziwe na quality za hollywood ndio muangalie. Foreign movies ziko everywhere ni mb tu unashusha. Mkiangalia mnafananisha na movie zetu huku bongo mnaconclude tuna movie zisizo na kiwango (which is true)

Mnachosahau ni kuwa kipindi kile soko lilikuwa ni la bongo movie tu hivyo ni lazima uangalie tu. Hakukuwa na netflix wala youtube.
 
eti watu kwenye bongo flavor wanaongea muda wote wanafoka najiulizaga maisha ndo yalivyo hivyo kweli
 
Nyinyi kila kitu mnasema serikali, serikali ndio inawaambia mtengeneze filamu za ovyo, kuna filamu kama Neria ya Zimbabwe, sinema kama hizo mnaweza kupata hata sponsor US aid na taasisi nyingine kutokana na maudhui yake

Hamna aliyesema serikali idairekt movie au ifanye recruitment ya actors. Kwanini wasanii wakitaka msaada wa serikali mnashangaa?, kwani wao hawahitaji usimamizi kwenye kazi zao?

Ishu ni kuwa hujawahi kuwa kwenye kiwanda cha filamu. Swali dogo tu tumetengeneza movie hiyo tumeita sponsors n.k JE BONGO.... FILAMU INAUZWA VIPI? HATUNA SINEMAZ. WEWE UNAWEZA KUSTREAM FILAMU NETFLIX? na bando lako buku jero mkuu?

Its not about quality au waigizaji au sponsors ao wapo tu. Kwani sponsors hawapo? Faida inarudi vipi? Mna sinemaz? Mna stream?

Mkuu naomba ukasome how film industry works ndo tuje kuendelea na mjadala.
 
Back
Top Bottom