Boniface Jacob adaiwa kukamatwa na watu waliokuja na gari aina ya defender. Kamanda Kitwinkwi asema hana taarifa hizo

Boniface Jacob adaiwa kukamatwa na watu waliokuja na gari aina ya defender. Kamanda Kitwinkwi asema hana taarifa hizo

Nikiona mambo kama haya najitia moyo sana kwa maneno ya faraja kutoka kwa wafuasi wa CHADEMA kweye miezi ya mwanzo ya mwaka 2021 maneno hayo ni kama "mama anaupiga mwingi,mama anawanyoosha sukuma gang,mama hataki dhulma,mama ameamua kutupa jongoo na mti wake,mama anaelewana na Mbowe kuliko anvyoelewana na Majaliwa,mama hana baya"🤣🤣🤣🤣
Chadema wamebugi wenyewe,maza alikua fair,sasa hivi wameanza eti 'samia must go'..hata ungekua wewe unaona watu wanapanga kupeleka moto mpaka uachie madaraka utafanyaje!?
 

Watu waliokua na silaha ambao wamejitambulisha kuwa ni Polisi, wamemvamia Meya wa Zamani wa Ubungo @exmayor_bonifacejacob maeneo ya Golden Fork, Sinza alipokua akipata chakula na kumkamata. Bonny amepambana kujitetea lakini wamemzidi nguvu kwa kuwa wapo wengi na wana silaha. Wamefanikiwa kuondoka nae.

Baadhi ya watu wamefuatilia gari hilo na kuona likielekea kituo cha Polisi Oysterbay. Viongozi mbalimbali wa chama pamoja na Wanasheria wanaelekea kituoni hapo kujua sababu ya kukamatwa kwake. Taarifa zaidi zitawajia.!
Aisee.
 
Kupitia Mtandao wa X, Askofu Mwamakula amesema Kuna taarifa kuwa aliyekuwa Meya wa Ubungo, Boniface Jacob amenyakuliwa na defenda akiwa kikaoni Sinza, Dar es Salaam na haijulikani kapelekwa wapi. Sisi Askofu Mwamakula tunatoa wito kama ni Polisi wamemchukua waseme maana huyo ni kiongozi wa jamii hawezi kunyakuliwa kama mwizi.

Soma Pia: Meya wa Manispaa ya Ubungo, Ndg. Boniface Jacob akamatwa na Polisi kwa mahojiano

Wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikisema kada wake aliyekuwa meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob 'Boni Yai' amekamatwa na Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi wa Kinondoni, Mtatiro Kitwinkwi amesema hana taarifa.

Akizungumza na Mwananchi kamanda Kitwinkwi kuhusu sakata hilo amesema: “Hapana, sina taarifa.”

Taarifa za Jacob kukamatwa, zimeanza kusambaa mitandaoni dakika chache zilizopita leo Jumatano, Septemba 18, 2024 na kwamba amekamatiwa Sinza, jijini Dar es Salaam.

Mwananchi limemtafuta, Wakili wa Chadema, Hekima Mwasipu ambaye amesema yupo njiani kuelekea Kituo cha Polisi cha Osterbay.

“Ni kweli amekamatwa na polisi waliovalia sare na wengine wamevalia kiraia maeneo ya Sinza. Walikuwa na defender na tuna taarifa kuwa amepelekwa Osterbay polisi na mimi niko njiani nakwenda.”

===

Saa 12:07 Jioni: Ameandika Yericko Nyerere
View attachment 3099699

Kwa mjibu wa Wakili Hekima Mwasipu, nikwamba Mhe. Bon Yai amekanatwa na Polisi na yuko Ostabei ofisi ya RCO, kwasasa simu zake zinachukuliwa kisheria kisha ataanza kuandikwa maelezo yake! Mliokaribu fikeni Obei fasta na barua za dhamana mkononi ili mahojiano yakiisha iwe rahisi kumwekea dhamana! Makosa anayotuhumiwa ni kusambaza taarifa za Uongo
Kesi itaenda mahakamani ni ukweli utajulikana.
 
Ila itafikia hatua watu watatembea na pinde na mishale ya sumu, mapanga n.k maana hii hali inatisha
Halafu mtu akichomekwa mshale kwisha habari . Nimewaza tu hivyo
 
Back
Top Bottom