BoT yakataza rasmi kampuni za mikopo mitandaoni kuchukua mawasiliano ya wateja ili kuwadhalilisha. Yatoa mwongozo mpya!

BoT yakataza rasmi kampuni za mikopo mitandaoni kuchukua mawasiliano ya wateja ili kuwadhalilisha. Yatoa mwongozo mpya!

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Kwa muda mrefu sasa, wakopaji wengi wa mitandaoni wamekuwa wakilalamika kuhusu kitendo cha baadhi ya apps za mikopo ku-access list ya mawasiliano ya wateja na kisha kuwatumia message baadhi ya contacts iwapo mteja ameshindwa kulipa.

Soma pia: Serikali ipitie upya Sheria ya 'Mikopo ya Mtandaoni (Online)'

Tabia hiyo ilifika hatua mbaya zaidi kiasi cha baadhi ya kampuni kuanzisha magroup ya Whatsap na kuadd baadhi ya contacts unaowaheshimu na kuweka picha za wadeni wao ili kuwapa presha za kulipa madeni wanayodaiwa.

BOT 2.png


Siku ya jana BOT walitoa muongozo rasmi kujibu vilio vya wananchi ambapo katika muongozo huo, BOT umeweka miongozo ifuatayo (Nime-summarize)
  • Hairuhusiwi kwa kampuni moja kumiliki apps mbili au zaidi za mikopo
  • Kampuni za mikopo haziruhusiwi kushare taarifa za mteja kwa watu au makampuni za nje ya nchi
  • Hairuhusiwi kwa kampuni za mikopo mitandaoni kukusanya namba za simu, meseji, picha, email au taarifa nyingine zozote kwenye simu yako
  • Mdhamini wa mteja ni lazima afahamishwe kuwa amechaguliwa kuwa mdhamini na akubali
  • Watu wa huduma kwa wateja hawaruhusiwi kutumia lugha chafu na kejeli kwa wateja
  • Ni marufuku kuchapisha taarifa za mteja mtandaoni iwapo atafeli kulipa deni
  • Ni marufuku kwa kampuni kumtaka mteja kulipa riba au pesa yote anayodaiwa kabla ya tarehe ya makubaliano
  • Ni marufuku kutuma meseji kwa contacts za mteja ili kumuonesha kuwa anadaiwa
Hayo ni machache tu wakuu.

Ningependa kuwapongeza BOT kwa kusikiliza kilio cha watanzania wengi.

Unaweza kupata taarifa zaidi kupitia website ya BOT

Nawasilisha
 

Attachments

Benki Kuu ya Tanzania imetoa muongozo kwa wakopeshaji wa kidigitali ambapo pamoja na mambo mengine muongozo huo umepiga marufuku wakopeshaji mtandaoni kutumia lugha za kudhalilisha, kuchapisha taarifa za waliokopeshwa mtandaoni au kutuma jumbe kwenye namba zilizopo katika simu ya aliyekopeshwa.

Muongozo huo uliosainiwa Agosti 2024, unakuja katika kipindi ambapo kumekuwa na ongezeko kubwa la taasisi mbalimbali zinazotengeneza App za kukopesha. Kampuni hizi zimekuwa zikitupiwa lawama juu ya utendaji wao usiofaa.

Mfano Juni 04,2024, baadhi ya Wabunge walilamika juu ya kuungwa kwenye makundi ya WhatsApp ambapo vitambulisho vya watu wanaosemwa kuwa na madeni vimekuwa vikitumwa.

“Wanafedheshesha watu. Wanarusha vitambulisho vya watu kwenye makundi, kwa hiyo watu wanadhalilishwa,” alieleza Mbunge Jang’ombe Ali Hassan King.

Muongozo huo wa Benki Kuu unataka mkopeshaji kidigitali kwanza kusajiliwa na Benki Kuu na pia mfumo wa kidigiti anaoutumia lazima uwe salama katika utumiaji. Baadhi ya mambo ambayo muongozo umeyakataza ni pamoja na:

1. Kutumia vitisho, vurugu au njia zingine za kumuumiza aliyekopeshwa katika marejesho

2. Kutumia lugha za matusi kwa mteja au wadhamini wa mteja au namba zingine kwenye simu yake kwa nia ya kumdhalilisha

3. Kuangalia katika simu ya mteja namba zingine za simu kwa ajili ya kuwatumia meseji mteja anaposhindwa kulipa katika muda au asipolipa.

4. Kutuma taarifa binafsi za mteja katika mitandao kwa ajili ya kumdhalilisha.
 
Benki kuu pia waoredheshe namba zote rasmi za hizo kampuni za mikopo isiruhusu namba ambayo hawajairodhesha kutumika katika kuwasiliana na wateja na pia ofisi za hizo kampuni zinazotoa mikopo zijulikane na zitangazwe hadharani zilipo na benki kuu waende kukagua ofisi hizo wasiruhusu biashara hii ikaenda kienyeji Iili mteja anapolalamika iwe rahisi kuwafuatilia na pia APP zao zisajililiwe na BOT na TRA pia wawe na access ya APP hizo ili malipo stahili ya kodi ya lipwe na riba zenye mwongozo wa BOT zitumike na kuthibitishwa na BOT
 
Back
Top Bottom