BoT yakataza rasmi kampuni za mikopo mitandaoni kuchukua mawasiliano ya wateja ili kuwadhalilisha. Yatoa mwongozo mpya!

Hiyo riba ni zaidi ya 80%
BOT wasicheze na akili za Watanzania.
Inakuwaje deni la wiki moja lizae riba ya 40-90%?
Maana app nyingi mkopo ni wa wiki ambapo siku ya 4 tu wanadai pesa yao
Hawa waondoshwe nchini.
Wamekiuka Sheria miaka mingi
BOT wakishafanya hivi ndio imetoka. Hawafuatilii kabisa wala kuchukua hatua.
 
Kwanini ukakope vikampuni uchwara?

Una shida Ela ya chap, kakope kwenye mabenki na taasisi zinazoeleweka

Juzi kati nmevuta laki 5 na 55 benki ya nmb, riba elfu 68 Kwa siku 14

Deadline Yao tar 5 mwezi huu na sijapigiwa simu au sms yoyote ya vitisho.
 
cc: Dr. Mwigulu Nchemba
 
Aiseee jamaa walitumia nguvu kubwa sana kunisaka niwalipe mamilioni yao lakini wamenyoosha mkono.
It's like a movie
 
Hiyo kali mzee. Kwanza hadi kukupa pesa zote hizo ilikuaje maana wanatoaga vimikopo vidogovidogo sana ila unalipa nyingi
Nilipojaza profile niliwatamanisha . Najaza hatua ya mwisho simalizii nawapigia simu ile customer service kuwa nilitaka kukopa milioni 1 kumbe mnakopesha vihela vidogo. Naomba wafute account yangu au wanipe milioni hapo hamna hamna wananipa laki 5
 
Nadhani hujaelewa dhumni la uzi na kile walichokikataa BOT, Tatizo watanzania wengi sifa ndo zinawasumbua na kujifanya kujua kila kitu. Binafsi mimi napongeza hatua walizochockua BOT hizi App zilikuwa na ujinga mwingi sana. Unakuta mtu alikopa huko wewe hajui unshangaa uapigiwa simu eti wewe ni mtu wake wa karibu na fulani ametutapeli na alikuweka wewe kama mdhamini, ukijaribu kuhoji kidogo huo udhamini ni wa aina gani unaishia kutukanwa na hawaishii hapo watabadilisha line na kuendelea kukughasi kila siku. UPPUZI MTUPU.
 
Na hii ndo kero kubwa aisee. Unakuta mtu uliwahi wasiliana nae mara moja ukasevu namba yake unashangaa unaambiwa ulimdhamini. Mi hadi mmoja nilikua simkumbuki kumbe namba niliwahi kuisevu wakati tunabargain biashara flani tu mtandaoni
 
Ndivyo wafanyavyo kumbe?
 
Jaribu ku summarize ili tupate muda wa kusoma na comment za wenzako. Muda ni mali.
 
ujalazimishwa kukopa boss kama si rafiki achana nayo
Kwani nyie mumelazimishwa kukopesha, kama sio shobo zenu ni nini? Munawapelekea watu matangazo kuanzia kwenye mitandao ya kijamii, sms na mpaka majumbani chumba Hadi chumba, sa kwa nini watu wasichukue hela za bure kama hizo? Mkikopwa tulizeni makalio ofisini kwenu watu wanakula bata musiwasumbue.
 
Kampuni ya Otaimo Financial Service, ilinidhalilisha Sana sms kibao za matusi. Ushahidi ninao
 

Attachments

  • Screenshot_20241021-115131.png
    511.6 KB · Views: 10
  • Screenshot_20241021-115607.png
    143.1 KB · Views: 16
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…